Kocha wa Taifa Stars Amunike ameidhalilisha sana Simba SC katika Uteuzi wake hivyo siishangilii tena Taifa Stars hadi akiondoka / akifukuzwa

Kocha wa Taifa Stars Amunike ameidhalilisha sana Simba SC katika Uteuzi wake hivyo siishangilii tena Taifa Stars hadi akiondoka / akifukuzwa

Halafu Tanzania Simba na Yanga hata Azam na Mtibwa zinatamba sababu zina uwezo wa kifedha kulinganisha na timu nyingine.Nyingine ni ile hali kwamba mtu anakuwa either Simba ay Yanga hata kama anajihusisha na timu nyingine.Rais wetu mpendwa Magufuli kama unasomaga hizi thread nakuomba sana Futa hizi Timu mbili za Yanga na Simba.Hakutakuwapo maendeleo ya kweli kama hizi timu zikiendelea kuwepo.Kenya walijaribu na kuzishusha daraja afc leopards na for mahi na matokeo yake sasa yanaonekana.Tuwe kama Uingereza kila mtu anapenda timu ya kitongoji chake.
 
Huwezi ukaita Wachezaji Watatu ( 3 ) wa Simba SC halafu ukawaita Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC. Kuanzia leo namchukia rasmi huyu Kocha na naomba Mungu tufungwe mechi zote kuanzia sasa. Na huwa nikimchukia Mtu huwa namchukia kweli. Nilikuwa namvumilia sana huyu Kocha na Mbichwa wake mkubwa pamoja na Pua lake ila naona kwa alichokifanya leo ni ' dhihaka ' kubwa kwa Klabu yangu pendwa ya Simba SC.

Kwahiyo ndani ya Simba SC amewaona Wachezaji Watatu tu Kipa Aishi Manula, Kiungo Mdogo wangu Kipenzi Jonas Gerald Mkude a.k.a Xavi Hernandez wa Tanzania na John Raphael Boko tu pekee? Ina maana Mohammed Hussein Zimbwe Jr ' Tshabalala ' hakumuona? Ina maana Kiungo ' Fundi ' kabisa Hassan Dilunga hakumuona? Ina maana Beki mwenye Roho Mbaya Paul Bukaba hakumuona?

Kuanzia le siishangilii tena Taifa Stars na naomba ifungwe kila mechi itakazocheza hasa inayoanza hii na Uganda Cranes wiki chache tu zijazo. Kama Kocha huyu mwenye Chuki za wazi wazi na Simba SC na mwenye Mahaba mazito na Yanga SC akiondoka au akifukuzwa nitarejea Kuishangilia ila siyo kwa sasa. Kocha ' Mnafiki ' sana huyu na niwaambieni mapema tu TFF kwamba huyu Kocha Emanuel Amunike hatufai kabisa na mfukuzeni mapema kabla hatujamfukuza kwa ' Bakora ' pale Kwa Mchina ( Mama yangu Samahani ) pale Kwa Mkapa kama tulivyohimizwa tuuite.

Popote pale duniani Timu ya Taifa yoyote ile huwa inajazwa Kwanza na Wachezaji ama wa Timu iliyokuwa Bingwa katika Ligi husika ya hiyo nchi au inashiriki Michuano ya Kimataifa sasa huyu Bichwa Kubwa, Mimacho Kutumbua wenu na Pua Andazi Amunike ameita hao Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC kwa ' Vigezo ' gani? Yanga SC ndiyo Bingwa Mtetezi wa VPL ( sasa TPL ) hii inayoendelea? Yanga SC inashiriki Michuano ya Kimataifa kwa sasa?

Ameshaniharibia kabisa Siku yangu!

Nawasilisha.
Kiongozi, leo umeteleza kidogo.

Usually, huwa unafanya uchambuzi wa issues zako kisayansi. Lakini leo mahaba ya timu yako pendwa yamefunika your usual reasoning.

Nilitegemea uzungumzie merits za walioachwa against waliochaguliwa. Kigezo hakiwezi kuwa idadi toka timu fulani. Je Bukaba ni bora kuliko waliochaguliwa kwenye nafasi yake? Ni mfano tu. Anaweza kuwa mzuri, lakini kama hachezi mechi nyingi kwenye timu yake, makocha wengi wa national team huwaacha wachezaji wa aina hiyo.
 
Ninapowaambia kuwa hapo hakuna Kocha muwe mnanielewa. Ukiona Mimi GENTAMYCINE namuwekea wasiwasi Mtu fulani tu jua kuwa 99.9% ana matatizo na hafai. Nadhani Tanzania haijawahi kupata Kocha wa Timu ya Taifa Taifa Stars ' Mpumbavu ' kama huyu. Utamuachaje nje Mohammed Hussein Zimbwe Jr ' Tshabalala, Paul Bukaba na Hassan Dilung HD?
Wewe mbumbumbu tu tena huna madhara yyte hata usiposhangilia, kocha ndo ameshachagua sasa kama roho inakuuma hama nchi, ulisikia wapi timu ya taifa ikawa simba au Yanga? Kweli wewe mbumbumbu la mambumbumbu na mbumbumbu wenzio wanakuunga mkono. Hiyo simba yenu ni timu ya uwanja wa mkapa tu nje ya hapo ni tano tano tu, na Leo hii muandae kapu LA kubebea magoli maana mtatwanga mrudi na manundu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu Tanzania Simba na Yanga hata Azam na Mtibwa zinatamba sababu zina uwezo wa kifedha kulinganisha na timu nyingine.Nyingine ni ile hali kwamba mtu anakuwa either Simba ay Yanga hata kama anajihusisha na timu nyingine.Rais wetu mpendwa Magufuli kama unasomaga hizi thread nakuomba sana Futa hizi Timu mbili za Yanga na Simba.Hakutakuwapo maendeleo ya kweli kama hizi timu zikiendelea kuwepo.Kenya walijaribu na kuzishusha daraja afc leopards na for mahi na matokeo yake sasa yanaonekana.Tuwe kama Uingereza kila mtu anapenda timu ya kitongoji chake.
Umeongea upupu ungemshauri aifute kwanza ccm maana miaka kenda miaka rudi maendeleo sifuri
 
We kweli shabiki maandazi
Hebu nitajie first eleven ya Simba itakayocheza leo

1. Aishi Manula
2. Zana Coulibally
3. Mohammed Hussein Tshabalala
4. Paul Bukaba
5. Pascal Serge Wawa ' Sultani '
6. James Kotei
7. Clatous Chota Chama ' Tripple C '
8. Mdogo wangu mwenyewe Kinondoni, Mwananyamala na Kawe Jonas Gerald Mkude a.k.a Xavi Hernandez wa Tanzania
9. Mohammed Kagere ' Kijicho '
10. John Raphael Boko
11. Rashid Juma

Matokeo ni kama haya yafuatayo: Ama Simba 2 - JS Saoura 1 au Simba 1 - JS Saoura 0 au Simba 1 - JS Saoura 1

Je una jingine?
 
Walitaka waitwe kina Zana, Wawa, Chama Gyan, Kotei na wengineo. Wanashindwa kuelewa kuwa Simba bila hao Mapro si lolote si chochote. Imagine timu first Eleven wote ni Mapro isipokuwa hao tu aliowaita kina Manura, Boko na Mkude, hao wengine kama hawatumiki ipasavyo mlitaka kocha awaite tu kwa kusikia kwamba ni wachezaji wazuri wakati hajawahi kuwashuhudia wakicheza uwanjani, acheni hizoo.

Huyu Mchezaji uliyemtaja hapo ' Manura ' ni wa Simba SC hii hii au labda ni wa Timu yako huko Kijijini Kwenu / Kwako?
 
Mara nyingi first eleven yake ina Watanzania wanne Mkude,Boko, Manura na Zimbwe. Kiukweli Zimbwe hakustahili kuachwa kuitwa timu ya taifa. Huku ni kutolitendea haki taifa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Jamani huyu Mtu mnayemuita ' Manura ' anacheza Timu gani? Naona Wewe ni Mtu wa Pili Kumuita hivyo.
 
Huwezi ukaita Wachezaji Watatu ( 3 ) wa Simba SC halafu ukawaita Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC. Kuanzia leo namchukia rasmi huyu Kocha na naomba Mungu tufungwe mechi zote kuanzia sasa. Na huwa nikimchukia Mtu huwa namchukia kweli. Nilikuwa namvumilia sana huyu Kocha na Mbichwa wake mkubwa pamoja na Pua lake ila naona kwa alichokifanya leo ni ' dhihaka ' kubwa kwa Klabu yangu pendwa ya Simba SC.

Kwahiyo ndani ya Simba SC amewaona Wachezaji Watatu tu Kipa Aishi Manula, Kiungo Mdogo wangu Kipenzi Jonas Gerald Mkude a.k.a Xavi Hernandez wa Tanzania na John Raphael Boko tu pekee? Ina maana Mohammed Hussein Zimbwe Jr ' Tshabalala ' hakumuona? Ina maana Kiungo ' Fundi ' kabisa Hassan Dilunga hakumuona? Ina maana Beki mwenye Roho Mbaya Paul Bukaba hakumuona?

Kuanzia le siishangilii tena Taifa Stars na naomba ifungwe kila mechi itakazocheza hasa inayoanza hii na Uganda Cranes wiki chache tu zijazo. Kama Kocha huyu mwenye Chuki za wazi wazi na Simba SC na mwenye Mahaba mazito na Yanga SC akiondoka au akifukuzwa nitarejea Kuishangilia ila siyo kwa sasa. Kocha ' Mnafiki ' sana huyu na niwaambieni mapema tu TFF kwamba huyu Kocha Emanuel Amunike hatufai kabisa na mfukuzeni mapema kabla hatujamfukuza kwa ' Bakora ' pale Kwa Mchina ( Mama yangu Samahani ) pale Kwa Mkapa kama tulivyohimizwa tuuite.

Popote pale duniani Timu ya Taifa yoyote ile huwa inajazwa Kwanza na Wachezaji ama wa Timu iliyokuwa Bingwa katika Ligi husika ya hiyo nchi au inashiriki Michuano ya Kimataifa sasa huyu Bichwa Kubwa, Mimacho Kutumbua wenu na Pua Andazi Amunike ameita hao Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC kwa ' Vigezo ' gani? Yanga SC ndiyo Bingwa Mtetezi wa VPL ( sasa TPL ) hii inayoendelea? Yanga SC inashiriki Michuano ya Kimataifa kwa sasa?

Ameshaniharibia kabisa Siku yangu!

Nawasilisha.
Kaka badilisha font zako unazotimia kuandika uzi zinachosha
 
Kaka badilisha font zako unazotimia kuandika uzi zinachosha

Sina huo mpango halafu sijakulazimisha uwe unasoma ' Threads ' zangu na unaweza ukasoma ' Threads ' za wengine sawa? Usinichoshe na kama una matatizo ya ' Macho ' wahi pale CCBRT Msasani kamwone Dada yangu niliyesoma nae ' Primary School ' Brenda Msangi ( ambaye ni Boss wa juu tu pale ) akusaidie ili upatiwe Tiba na uwe unaona vizuri.
 
Nilikuwa naheshimu sana IQ yako sasa naanza kuhisi post unazoletaga humu zinazohitaji kufikiria labda unaandikiwa pale Lumumba then unaleta.
 
Huwezi ukaita Wachezaji Watatu ( 3 ) wa Simba SC halafu ukawaita Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC. Kuanzia leo namchukia rasmi huyu Kocha na naomba Mungu tufungwe mechi zote kuanzia sasa. Na huwa nikimchukia Mtu huwa namchukia kweli. Nilikuwa namvumilia sana huyu Kocha na Mbichwa wake mkubwa pamoja na Pua lake ila naona kwa alichokifanya leo ni ' dhihaka ' kubwa kwa Klabu yangu pendwa ya Simba SC.

Kwahiyo ndani ya Simba SC amewaona Wachezaji Watatu tu Kipa Aishi Manula, Kiungo Mdogo wangu Kipenzi Jonas Gerald Mkude a.k.a Xavi Hernandez wa Tanzania na John Raphael Boko tu pekee? Ina maana Mohammed Hussein Zimbwe Jr ' Tshabalala ' hakumuona? Ina maana Kiungo ' Fundi ' kabisa Hassan Dilunga hakumuona? Ina maana Beki mwenye Roho Mbaya Paul Bukaba hakumuona?

Kuanzia le siishangilii tena Taifa Stars na naomba ifungwe kila mechi itakazocheza hasa inayoanza hii na Uganda Cranes wiki chache tu zijazo. Kama Kocha huyu mwenye Chuki za wazi wazi na Simba SC na mwenye Mahaba mazito na Yanga SC akiondoka au akifukuzwa nitarejea Kuishangilia ila siyo kwa sasa. Kocha ' Mnafiki ' sana huyu na niwaambieni mapema tu TFF kwamba huyu Kocha Emanuel Amunike hatufai kabisa na mfukuzeni mapema kabla hatujamfukuza kwa ' Bakora ' pale Kwa Mchina ( Mama yangu Samahani ) pale Kwa Mkapa kama tulivyohimizwa tuuite.

Popote pale duniani Timu ya Taifa yoyote ile huwa inajazwa Kwanza na Wachezaji ama wa Timu iliyokuwa Bingwa katika Ligi husika ya hiyo nchi au inashiriki Michuano ya Kimataifa sasa huyu Bichwa Kubwa, Mimacho Kutumbua wenu na Pua Andazi Amunike ameita hao Wachezaji Wanne ( 4 ) wa Yanga SC kwa ' Vigezo ' gani? Yanga SC ndiyo Bingwa Mtetezi wa VPL ( sasa TPL ) hii inayoendelea? Yanga SC inashiriki Michuano ya Kimataifa kwa sasa?

Ameshaniharibia kabisa Siku yangu!

Nawasilisha.
Mara nyingi nafurahishwa sana na mada zako nyingi maana nikisoma naona unafikri kwa kina na kimantiki kabla ya kuziandika. Binadamu ana vitu vingi sana anafanana na wanyama ila tofauti kubwa ipo kwenye kufikiri, kiwango cha wanyama katika kufikiri ni kidogo sana ingawa wanayo akili. Binadamu wote wanafanana kwa kiwango kikubwa sana bila kujali rangi na maumbile yao mfano uwezo wa akili wa binadamu mmoja na mwingine havitofautiani sana ila tofauti inakuja katika matumizi ya akili, wanaotumia akili kwa kiwango kikubwa na wengine kwa kiwango kidogo. Kutumia akili ni jambo watu wanafundishwa na ndio maana ya shule tunakwenda shule sio kuongeza akili ila tunakwenda kujifunza jinsi ya kutumia akili ili kujiletea maisha bora na jamii inayokuzunguka. Taifa letu shida yake kubwa ni kufundisha watu wake jinsi ya kutumia akili inawezekana katika mifumo yetu ya elimu kuna shida ndio maana tunavyoangalia mambo tunaona tofauti na wenzetu ndio maana tumekuwa watumiaji wa vifaa wanavyounda kutokana na matumizi makubwa ya akili zao kuliko sisi wanavyotumia vyetu, ata soccer wanalocheza linaonekana lina utofauti mkubwa na soccer tunalocheza sisi leo. Matumizi ya akili hayawezi kujificha kabisa utaweza kuona katika hoja na maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa mtu mmoja mmoja kwa familia na taifa kwa ujumla wake. Hoja yangu Amulike ni mchezaji katika wakati wake kwa kiwango kikubwa cha kimataifa lakini anatokea katika nchi yenye maendeleo makubwa ya soccer kwa maana wanavyoona soccer ni tofauti na sisi na kasomea elimu ya soccer jinsi ya kuona wachezaji bora na jinsi ya kuwaunganisha wachezeji kuwa timu lakini sio Mtanzania mpaka awe na mapenzi na Yanga na Kuichukia simba sasa wakati tunajenga hoja ya kumlaumu kwa kutumia kigenzo cha hisia ya mapenzi tunaweza kuwa tunakosea tunatakiwa kujiuliza maswali kwa maana ya taaluma akili yako ina taarifa kiasi gani katika elimu ya soccer mpaka wakati wa kufikiri nipate majibu kuwa Mwalimu ni mbaguzi. Binadamu kwa kiwango kikubwa sana anajifunza kwa kusikia na kuona sasa nikitoa hoja ambayo itawapotosha watu wengine natengeneza tatizo katika akili za wengine wanaoniamini kuwa sifanyi makosa ktk hoja zangu. Katika mchakato wa kufikiria kuna hatua kuu tatu ya kwanza kunakuwa na taarifa katika hifadhi ya akili yako(subconscious) ambayo baada ya kupokea taarifa jipya zinakwennda kutafuta ktk hifadhi kuna taarifa gani inafanana na hiyo mpya zinaanza kutengeneza uhusiano ndipo suala la kufikria linaanza uelewa unaanza kuja unatengenza hisia hasi au chanya ambazo zinakusukuma kufanya maamuzi mfano wewe una mapenzi makubwa sana na simba hiyo ni taarifa ambayo imeifadhiwa katika subconscious yako sasa unasikia Amulike katangaza kikosi hiyo ni taarifa mpya imeingia inakwenda kukutana na ile taarifa ambayo ipo tayari katika akili yako ya kuwa na mapenzi na simba zinakufanya kufikiri baada ya kupata jibu kuwa mwalimu kawadhalilisha simba inatengeneza hisia ya chuki dhidi ya mwalimu ambazo zinakusukuma kufanya maamuzi kama ulivyofanya kumlaumu Mwalimu Amulike bila kujiuliza lawama zako zitakuwa na athari kwa kiwango gani kwako na kwa wengine. Chochote cha kusaidia kupiga hatua mara nyingi lazima kiwe chanya kuliko hasi, ndio maana narudia tena kuna uwezekano mkubwa sana akili zetu zinaandaliwa vibaya tokea utotoni maana mitazamo yetu katika mambo mengi hazipo sawa(mindset) mimi sikulaumu wewe ila nachoona ni tatizo la kimfumo katika vitu vingi sana iwe siasa, elimu, kutumia au kuendeleza resource n.k kuna shida ya msingi ktk jamii yetu na hii hoja yako ni mfano jinsi gani watanzania tutachukuwa muda mrefu kuwa na maendeleo, fahamu zetu zinajengwa kimakosa kwa hiyo tunakuwa tunalishana na kuridhishana sumu katika akili zetu, hiki kikiondoka kinakuja kizazi kingine kibovu kuliko cha mwanzo kuna elimu kubwa katika hili nalosema kama unaweza kuwa humble na positive unaweza kuona sense ndani yake. Kila jambo kabla ya kuchukuwa hatua tunatakiwa kufikiri kwa kina na kama tunakosa majibu katika hisia chanya bora kuwa na subira na kufanya angalau utafiti kidogo kabla ya kuchukuwa hatua yoyote maana kugeuza hatua kurudi mwanzo ni kitu kigumu inakuwa tayari imeshaleta athari umakini katika kila jambo linapunguza kufanya makosa.
 
Back
Top Bottom