Tetesi: Kodi ya kibali cha harusi, birthday, send off, ubatizo, kumtoa mwali kufutwa mapema na Rais Magufuli

Tetesi: Kodi ya kibali cha harusi, birthday, send off, ubatizo, kumtoa mwali kufutwa mapema na Rais Magufuli

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Kwenu jukwaani.

Hivi karibuni kila halmashauri humu nchini imekuwa ikibuni vyanzo vya mapato. Baadhi zimeenda mbali kwa kupendekeza tozo ya Tsh 50,000 kwa kibali cha sherehe kama harusi, birthday/bethidei, send off nk.

Habari kutoka chanzo changu cha uhakika jikoni kabisa serikalini, kimedai Rais Magufuli ataibuka mapema mwezi ujao wa February na kukataza kodi hizi.

Chanzo hiki kimedai kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu kote nchini umekuwa chanzo cha kufutwa kwa kodi hii iliyobuniwa na watendaji ili kukuza mapato ktk halmashauri.

Chanzo hicho jikoni serikalini kimedai CCM na serikali hawataki na hawapo tayari kwa mzozo wowote na wananchi mwaka huu na hata vitendo vya bomoabomoa huenda nazo zikakomeshwa kwa muda.
 
Kwa ninavyomjua Jiwe atapita humo humo ulipoandika, wewe ngoja tuendelee kupiga kelele halafu yule jamaa kwa kupenda sifa atakuja na kuifuta hiyo kodi ili aonekane ni shujaa na mtetezi.
Hili ni suala la muda tu, tusubiri tuone.
 
Kama kawaida yao, wanatengeza tatizo alafu wanakuja kulitatua te. te .te te te te sema siku izi watanzania wamesha wastukia ndiyo mana habar zao hazichukui hata dakika kumi kupotea
 
Wana tengeneza Tatizo halafu wanajifanya kulitatua ,kweli #Hapa Kazi tu#
 
Kwenu jukwaani.

Hivi karibuni kila halmashauri humu nchini imekuwa ikibuni vyanzo vya mapato. Baadhi zimeenda mbali kwa kupendekeza tozo ya Tsh 50,000 kwa kibali cha sherehe kama harusi, birthday/bethidei, send off nk.

Habari kutoka chanzo changu cha uhakika jikoni kabisa serikalini, kimedai Rais Magufuli ataibuka mapema mwezi ujao wa February na kukataza kodi hizi.

Chanzo hiki kimedai kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu kote nchini umekuwa chanzo cha kufutwa kwa kodi hii iliyobuniwa na watendaji ili kukuza mapato ktk halmashauri.

Chanzo hicho jikoni serikalini kimedai CCM na serikali hawataki na hawapo tayari kwa mzozo wowote na wananchi mwaka huu na hata vitendo vya bomoabomoa huenda nazo zikakomeshwa kwa muda.
Siku ya kuzaliwa CCM tarehe 5/2 ina kuja, huenda ndio siku ya tamko.
 
Katika siasa za Inji hii, ukitaka kupata umaarufu ghafulale; tengeneza tatizo kaa kimya kisha uibuke upya na kulitatua, aaaah magoli; mpaka maandamano na public holiday kupongezana! Likitokea hilo, wengi hatutashangaa!
 
Kwa ninavyomjua Jiwe atapita humo humo ulipoandika, wewe ngoja tuendelee kupiga kelele halafu yule jamaa kwa kupenda sifa atakuja na kuifuta hiyo kodi ili aonekane ni shujaa na mtetezi.
Na kwasababu watanzania ni wajinga watamsifia makofi na kumtungia wimbo wa kumsifia.
Kutawala Tanzania ni rahisi kuliko kutawala nchi yoyote Duniani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji16][emoji16][emoji16]
FB_IMG_1546009134332.jpeg
 
Hii kodi kama ingebuniwa na Jiwe - Tz nzima ingelipuka nakupongeza kwa uboni lakini kwa sababu imeanzishwa na subordinates wake - ataifuta mapema tu!
 
Back
Top Bottom