Kodi ya majengo kuanza kukatwa kwenye Luku kuanzia Agosti 20, 2021. Je, Serikali imekosa Dira, mbinu zimewaishia?

wewe na huyo ndezi mwenzio alietangulia wote shwain
 
Nanunua umeme hapa naambiwa ujumbe huu hapa chini. Ina maana serikali tayari imeshaingiza makato ya kodi ya nyumba kwenye kila mita?
Ujumbe huu naupata sababu ya tatizo la mtandao au ndiyo serikali ishafanya yake? Maana mchana nilinunua umeme ulikubali safi, ila sasa hivi nanunua tena, napata ujumbe huo. Vipi na nyinyi wenzangu mnapata ujumbe huo mnaponunua umeme?
 
Ndio mkuu.. effective from today..
 
Kama Mwanaume nikichangia 12000 Kwa mwaka ili serikali ilete maendelo sioni tatizo ,tuache kulia lia Kama watoto, 12000 ni kitu gani
Mkuu kinacho niuma nikulipia jengo ambo silimiliki mimi yanii hapa nalaani mpaka kiama sisi wapangaji serikali aitu tendei haki, MBOMBONGAFU
 
Mkuu kinacho niuma nikulipia jengo ambo silimiliki mimi yanii hapa nalaani mpaka kiama sisi wapangaji serikali aitu tendei haki, MBOMBONGAFU
Ndio ukasirike ili na wewe ujenge lako Mkuu,huu ni ulimwengu wa kibepari, only the fittest will survive, aliye na moja atanyang'anywa apewe yule mwenye mbili.
Binafsi napenda serikali au mtu anaponitia hasira ya kuniamsha
 
Shida sio kuchangia serikali, ila kulipa kodi isiyokuhusu hasa kwetu sisi wapangaji.
Unatakiwa umdai mwenye nyumba, hata Kama anazingua sio ishu kubwa hiyo 1000 Kwa mwezi Na Labda mko wapangaji 5 maana yake sh 200 tu ili tujenge hospital, barabara nk ndio ikutoe povu Mkuu?
 
Hili la kodi ya majengo naliunga mkono.Kama umepanga kaa chini na mwenye nyumba muweke mambo sawa.
 
Kwani wanaomiliki majengo wote ni wanaume ndugu...?
Aliyeandika Mada ni Mwanaume ndio maana nikasema hivo Mkuu, jinsia yeyote iwayo kuchangia 1000 sio ishu ya kutolea povu, halafu unakuta hiyo 1000 Kwa mwezi inachangiwa na wapangaji kibao kwenye nyumba moja.
Tuache kelele za kijinga
 
Nilisema sifa kwasababu.... Haiwezekani ulipe kodi ya nyumba kwa mwenye nyumba na ulipie kodi ya jengo ambalo sio lako!!! Hii unaona ni sawa kwann? Na kwann tozo sio sawa?
Sasa Mkuu wewe kulipa 1000 Kwa mwezi unaona ni kitu ya kutanua mishipa ya Shingo Kwa kupiga kelele kweli? Na pengine hiyo 1000 mko wapangaji kibao.
Hii chukulia kama ni changamoto ya kukufanya na wewe uwe baba /mama mwenye nyumba ili ufaidi huo mteremko
 
Aliyeandika Mada ni Mwanaume ndio maana nikasema hivo Mkuu, jinsia yeyote iwayo kuchangia 1000 sio ishu ya kutolea povu, halafu unakuta hiyo 1000 Kwa mwezi inachangiwa na wapangaji kibao kwenye nyumba moja.
Tuache kelele za kijinga
TSHS. 1000 KWA MWEZI,WAPANGAJI 2=500@1
3=333@1

ALAFU MTU MZIMA NA NDEVU ZAKO UNALETA MALALAMIKO!!
MIMI NAONA HILI LA KODI ZA MAJENGO TULIACHE ILI SERIKALI IPUMUE.
 
Mimi sijiongelei mimi kama mimi mkuu najaribu kuona mzigo wataobeba wapangaji mkuu!! Note mimi naishi kwangu sijapanga.... So sijiongelei mimi naongelea walio wengi hili litawaumiza!!! Kuhusu mishipa ya shingo ilo nakuachia wewe maana mipasho sio mambo yangu
 
Watavuka, mfano mita za umeme nchini ni million 10, 10,000,000*2000=20,000,000,000 wamekusanya 20b, kwa hiyo watakusanya b120 kwa mwaka hiyo nimechukulia kwa 1000, hivyo watakusanya zaidi ya b200 kwa mwaka
 
hii imenitokea leo na cha ajabu tunaambiwa deni ni laki moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…