Kodi ya miamala ya simu ifutwe ama ipunguzwe; itaongeza umaskini na kupunguza ajira

Kodi ya miamala ya simu ifutwe ama ipunguzwe; itaongeza umaskini na kupunguza ajira

Doctor Ngariba

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2020
Posts
588
Reaction score
951
Habari JF members,

Naomba turejee kauli ya Rais wetu Samia alipokuwa anazungumza na wahariri wa vyombo vya habari alipoulizwa kuhusu katiba mpya na siasa za majukwaa. Simple tu alijibu dhamira yake kubwa ni kuifungua nchi kiuchumi japo katiba ni muhimu pia.

Lakini kwa hali ilivyo inaonekana kwa namna fulani dhamira hii yaweza kuyeyuka kutokana na kuwepo kwa baadhi ya kodi na tozo zilizoletwa na serikali yake kupitia bajeti ya serikali iliyosomwa hivi karibuni bungeni.

Kwa kuwa mheshimiwa Rais alikubali kukosolewa na kushauriwa serikali yake, naomba pia kupitia jukwaa hili (ambalo naamini na yeye yumo) tumshauri katika kodi/tozo hizi labda atapokea ushauri wetu na kuufanyia kazi.

1. Kodi kwenye miamala ya simu
2. Kodi kwenye mafuta

Kwa kuanza mimi nashauri hii kodi ya kwenye miamala ya simu ifutwe ama ikishindikana kabisa basi ipunguzwe maana itaongeza umaskini na kupunguza ajira za watu waliojiajiri katika utoaji wa huduma ya mobile money.
 
Kumbe ulipoona sisiem imeshinda takribani viti vyote vya ubunge, ulielewa nini mkuu?
Kwani CCM walishinda au walibaka uchaguzi, mimi naamini walioshinda ni wachache mno hata hivyo naomba maoni yako mkuu kwa serikali yetu maana nahofia nitafunga kibanda changu cha Tigopesa.
 
Lipa kodi kwa maendeleo ya taifa. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewee. Itakua aibu ya mwaka kama watu takribani milion 60 bado tuwe tunatembeza bakuri kuomba misada kwenye nchi zenye watu milion tano.

Watanzania tulipe kodi ilitutunishe mfuko wa fedha zetu kisha tujenge mifumo ya kimaendeleo. Hata huko kwa wenzetu nako maendeleo huletwa na wao wenyeree. Tumtangulize mungu tutafika watanzania wenzangu
 
Kuna mambo ambayo ni kandamizi kwa wananchi na serikali haiko tayari kutoa hivyo vikwazo kwasababu kwake kuna maslahi inapata.

Mbinu wanayotumia serikali ni kuongeza zaidi hicho kikwazo ili kuwafanya wanachi walalamike nakuona wameonewa zaidi, ili baadaye serikali ikija kusolve hilo tatizo inarudisha mfumo ule ule wa mwanzo ambao kwa kipindi hicho bado zilikua zinamuumiza mwananchi na zilifaa kupunguzwa zaidi

Baada ya hapo kila mtu ataona serikali imetatua tatizo na hakutakua tena na mtu atakayejadili kua serikali ipunguze kodi au tozo kwasababu kila mmoja ataona hali ya sasa ni nafuu kulikohizi gharama zilizowekwa na kuondolewa baada ya wao kulalamika
 
Mimi nnachoona ni tax class imehamishwa, jua tu kuna segment ya watu fulani wamepata ahueni kwa sasa, mzigo wa kodi wanaenda kuubeba watu wa aina nyingine.
 
Lipa kodi kwa maendeleo ya taifa. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewee. Itakua aibu ya mwaka kama watu takribani milion 60 bado tuwe tunatembeza bakuri kuomba misada kwenye nchi zenye watu milion tano.

Watanzania tulipe kodi ilitutunishe mfuko wa fedha zetu kisha tujenge mifumo ya kimaendeleo. Hata huko kwa wenzetu nako maendeleo huletwa na wao wenyeree. Tumtangulize mungu tutafika watanzania wenzangu
Ni kweli mkuu kodi ndio msingi wa maendeleo ya nchi hata hivyo kodi ziwekwe kwa kuangalia kipato cha wananchi. Hebu fikiria na walio chini yenu msijiangalie nyie tu.

Hii ni nchi yetu sote.
 
Lipa kodi kwa maendeleo ya taifa. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewee. Itakua aibu ya mwaka kama watu takribani milion 60 bado tuwe tunatembeza bakuri kuomba misada kwenye nchi zenye watu milion tano.

Watanzania tulipe kodi ilitutunishe mfuko wa fedha zetu kisha tujenge mifumo ya kimaendeleo. Hata huko kwa wenzetu nako maendeleo huletwa na wao wenyeree. Tumtangulize mungu tutafika watanzania wenzangu
Dah jiwe
 
Kuna mambo ambayo ni kandamizi kwa wananchi na serikali haiko tayari kutoa hivyo vikwazo kwasababu kwake kuna maslahi inapata...
Sidhani kama wana dhamira hiyo maana hata kwenye vifurushi vya muda wa maongezi na data wamechemka kurejesha nyuma kama ilivyokuwa kabla.

Hebu tuangalie kama watanzania waliopo Tunduma wanavuka kwenda Nakonde-Zambia kununua mafuta wakati mzigo unapitia bandari ya DSM.

Hawa viongozi wetu ni wabinafsi kwa sababu hawaathiriki na mabadiliko haya ndo maana wanaona fresh tu.
 
Tatizo kubwa ni akili ya wataalamu wetu wa uchumi imefikia kikomo katika kutafuta vyanzo vipya vya mapato yatokanayo na kodi. Hawapendi kufanya R&D kwa kwa malengo ya kukwepa gharama ya moja kwa moja.

Hawatambui ya kwamba kupata matunda ya mambo yenye tija hayana njia ya mkato, bali inawapasa kuchesha bongo barabara. Badala ya vyanzo vipya vya kodi kuwa rahisi na rafiki zinageuka kuwa kero na mzigo mkubwa kwa mwananchi wa kawaida.
 
Swali ninalojiuliza kwann hiz tozo iwe kiasi kikubwa kama hiki hizi huduma zinafanywa na karbia kila mtu kulikua na haja gan kuweka kiwango kikubwa kama haki ikizingatiwa tayari kod wanachukua mbona tunazalauliana kias iki jaman ata kama ndio kisa maendeleo hii nchi imeanzwa kujengwa kabla ya ata hii mitandao na imeendelea kujengwa na itajengwa ya nin kuumizana.

Mfano ukinunua umeme kuna ela inakatwa na maendeleo ya umeme kwel yanaonekana na pia hiz tozo zingezingatia kiwango fulan mfano ata kama kile cha rea au kuzid kidogo apa hakuna kusema maendeleo wala nin ni uonevu kwa sababu tutalalamika yataisha hulka ya mtanzania ni unyonge na uoga wanaoona sawa hiz tozo weng wana unafuu wa maisha kwao si kitu
 
Tatizo kubwa ni akili ya wataalamu wetu wa uchumi imefikia kikomo katika kutafuta vyanzo vipya vya mapato yatokanayo na kodi. Hawapendi kufanya R&D kwa kwa malengo ya kukwepa gharama ya moja kwa moja..
Ni hatari sana kuwa na wataalamu wa namna hii au labda wanaogopa kumshauri vizuri Rais na serikali yake au uchumi wanaoutaka ni ule wa wachache!!!
 
Lipa kodi kwa maendeleo ya taifa. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewee. Itakua aibu ya mwaka kama watu takribani milion 60 bado tuwe tunatembeza bakuri kuomba misada kwenye nchi zenye watu milion tano..
Hakuna mtanzania ambaye halipi kodi, unaweza kumtaja hapa km yupo.
Tangu Benjamin afute Kodi ya kichwa (direct tax) Kodi ile ilihamishiwa kwenye bidhaa na huduma.
Kila ununuapo bidhaa au huduma, unalipa 18% ya gharama ya hiyo bidhaa au huduma. Sasa unasemaje watu hatutaki kulipa kodi???

Swali linaloumiza na naamini hata wew unaujiuliza ni "hilo ongezeko la tozo juu ya 18% VAT linatokana na nin? Kwanini ulipie Kodi mbili kwa huduma moja? Kwa faida gani unayoipata ya zaidi ya ile 18%?

Lakini niseme tu, hakuna mtu anayefurahia hii, hata wewe mwenyew, unless uwe hufanyi miamala yako kwa simu.

Tuache ushenzi
 
Sidhani kama wana dhamira hiyo maana hata kwenye vifurushi vya muda wa maongezi na data wamechemka kurejesha nyuma kama ilivyokuwa kabla.

Hebu tuangalie kama watanzania waliopo Tunduma wanavuka kwenda Nakonde-Zambia kununua mafuta wakati mzigo unapitia bandari ya DSM.

Hawa viongozi wetu ni wabinafsi kwa sababu hawaathiriki na mabadiliko haya ndo maana wanaona fresh tu.
Nachukua hiyo fact ya mwisho kua wao sio waathirika lakini pia bado hoja yangu ya wao kucheza na mindset za watz naiona bado haiepukiki kwa namna series matatizo kama haya si mageni

Serikali haitatui tatizo, inaliongeza maradufu ili watu walioongelee sana, kisha tukilalamika linarudisha katika hali ile ya mwanzo na hapo tutaona kama tumesaidiwa

Na ndio maana saizi hakuna anayelalamika kuhusu gharama za vifurushi japo kua kuna baadhi ya vifurushi vimezimwa
 
Lipa kodi kwa maendeleo ya taifa. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewee. Itakua aibu ya mwaka kama watu takribani milion 60 bado tuwe tunatembeza bakuri kuomba misada kwenye nchi zenye watu milion tano...
Nami naunga mkono hili la kulipa kodi lkn ili liwe na uzito na lipokelewe vizuri na Wananchi, nashauri viongozi wetu watumie busara ndogo tu, waonyeshe uzalendo kwa vitendo, kila mtanzania anafahamu kwamba viongozi wa kisiasa wanalipwa pesa nyingi ambayo haiendeni na hali halisi ya uchumi wetu.

Waonyeshe uungwana kwa kujipunguzia mishahara na marupurupu mengine ili anangalau yalingane na yale wanalipwa wataalamu wetu mfano madaktari, wahandisi, wanasheria nk, hapo watakuwa wametutendea haki.

Kubaki na posho zao sijui kukarabati nyumba, mawasiliano, posho za vikao posho za mafuta huku wakitumia gari za serikali ni kejeri kubwa kwa wananzengo
 
Yaani ilikuwa imetoa ajira kwa watu wengi Sana Kama bodaboda ilivyoshikilia vijana
 
Swali ninalojiuliza kwann hiz tozo iwe kiasi kikubwa kama hiki hizi huduma zinafanywa na karbia kila mtu kulikua na haja gan kuweka kiwango kikubwa kama haki ikizingatiwa tayari kod wanachukua mbona tunazalauliana kias iki jaman ata kama ndio kisa maendeleo hii nchi imeanzwa kujengwa kabla ya ata hii mitandao na imeendelea kujengwa na itajengwa ya nin kuumizana...
Wao miamala yao wanafanyia bank, na ndio maana hawajaweka tozo huko.

Jiulize kwan bank ile sio miamala? Kwann kusiwekwe tozo na huko ili tulipe sote?

Wakati mwingine napenda tukamuliwe zaid ya hapa ili akili zitusogee tusiende kuchagua viongozi kwa kufuata nyimbo na fulana
 
Nami naunga mkono hili la kulipa kodi lkn ili liwe na uzito na lipokelewe vizuri na Wananchi, nashauri viongozi wetu watumie busara ndogo tu, waonyeshe uzalendo kwa vitendo...
Siasa ya Afrika hasa Tz n biashara.

Unafikiri kama mtu aliwekeza 200mil kuupata ubunge, atakubali vip kupunguza posho na malipo yake!?

Dawa ya hawa inachemshwa na wao wenyewe, na ipo siku watainywa wao wenyewe.

Siku hizi kila maisha yanavyozidi kubana, hakuna mwanaccm wala Chadema anayefurahia, sasa hiyo ndio itayowaua hapo mbeleni
 
Back
Top Bottom