Kodi za maskini nchi hii zinatumiwa na matajiri

Kodi za maskini nchi hii zinatumiwa na matajiri

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Nimekutana na andiko hili la ndugu yetu, nikaona si vibaya tukashea pamoja, maana naona kaandika vitu vingi vya msingi kwa mtazamo wangu, japo sikulazimishi kuamini kama ni kweli au la, msome ndugu Mushi....


88888888888888
b4b865cb-8b5d-4f45-9479-89a3e1c01646.jpg

Na Thadei Ole Mushi

Kama kuna jambo ambalo nitasimama kidete kulitetea hapa nchini bila kuogopa ni maslahi ya masikini wa nchi hii. Unawaona hao watoto hapo pichani?

Hii ni Shule ya Msingi Olgira, Kata ya Sunya, Kiteto mkoani Manyara. Shule hii ina madarasa matano na wanafunzi 600 na walimu watano. Kwenye Shule hii kuna watoto wanatokea Kitongoji cha Natushi Km 12 kufika Shuleni anafika anaanza kupambana na mazingira kama haya, wakati huo kuna kiongozi anatumia V8 la Serikali kupeleka mwanawe pale Feza.

9ca08e84-961e-4116-8d68-2b27fd0fa148.jpg


Kuna wakati Masikini wanatakiwa kuhoji ipo hivi....
Serikali imetoa Scholarship za wanafunzi waliofanya vizuri masomo ya Sayansi kwenda kusoma nje ya nchi. Nimepitia majina ya wanafunzi wanaolengwa na mpango huo nikakuta asilimia 95 wanatokea Shule za Private ambazo ada yake si chini ya milioni tatu. Kwa kuwa watoto hawa wa matajiri walipata mazingira mazuri na shule bora basi wamefanikiwa kufikia ufaulu wa juu.

Mtoto wa masikini kama hawa unaowaona hapa Pichani ni ngumu kuja kukutana na kodi ya wazazi wake akaitumia kusoma. Hata hivyo mimi naamini mtoto aliyetoka shule ya serikali ya kawaida akapata hata two ana uwezo mkubwa kuliko hawa wanaolishwa kila kitu pale St. Mary's. Mtoto anayetembea kwa miguu KM 12 shule haina walimu, chakula ni shida, Mzazi wake kauza kila kitu mtoto asome halafu anapata two huyu ndiye anayetakiwa kusaidiwa.

Nilikuwa nina fikiri
1. Fedha zilizolenga kupeleka wanafunzi kusoma nje ya nchi kwa mwaka huu ziende zikajenge hii shule ya Olgira na nyingine zenye hali kama hii.

2. Jambo la Pili vitengenezwe vigezo ambavyo vitasaidia kodi ya nchi hii kukutana na mtoto wa maskini, mathalan hii scholarship iliyopewa jina la Rais Samia inaendeleza ubaguzi na tabaka la elimu lililopo nchini. Nadhani wanafunzi waliopata one za sayansi toka shule za Serikali za kawaida ndio wapewe hii fursa.

3. Wanafunzi waliosoma Private kwa kuwa wazazi wao wana unafuu wa maisha basi Serikali inaweza kuwasaidia kutafuta vyuo huko nje na kuwasaidia nauli lakini issue ya ada wazazi wawalipie wenyewe.

Inauma sana haya yanayoendelea...... Watoto wa maskini watabaki kuwa wapiga kura wa watoto wa viongozi na wenye fedha. Niwaombe vijana kuacha kushinda kuangalia vichekesho Tiktok na kutafuta Connections badala yake washiriki kwenye siasa za nchi hii. Niwaombe vijana kujadili mustakabali wa taifa lao. Niwaombe vijana kuachakujadili vitu vya kijinga jinga na kufuatilia mambo ya msingi ya taifa lao.

Nisaidie kushare kama umekubaliana na mtizamo huu.

a1b55913-5dff-4a89-856b-6f8eecec2f9c.jpg
Ole Mushi.
0712702602.
 
Naona hapo unazungumziwa mzigo wa boss ulio kwenye punda ila punda mwenyewe hazungumziwi anaeubeba mzigo

Punda haijulikani kuwa anakula nini anakunywa nini analala wapi na mahitaji yake muhimu

Lakini mzigo ndio unazungumzwa kweli na kila mtu anapata na huzuni na simanzi

Punda (Mnyama kazi) hapo ndio mwenye kazi na lawama. Mazingira ya mnyamakazi huyu ni duni sana mshahara wake mdogo sana marupurupi hamna nyumba wala allowance ya nyumba HAKUNA ila wengine wanamarupurupu mpaka yanataka kuwatokea puani

Hili nalo mkaliangalie
 
Masikini wanafyatua tuu vitoto bila kujali watasoma wapi. Hicho ndiyo chanzo cha matatizo.
 
Umeongea mengi uenye ukweli na uwazi,

Katika mishe zangu nipo huwa napata nafasi ya kukutana na shule na wanafunzi hawa.Ukweli inatia huruma!

Inafika hatua mwalimu anachagua pa kufundisha,mengine yenye kumzungusha anayapotezea kutokana na uchache wao ofisini,bado mtoto mwenyewe ananjaa na bado haipendi shule kwa jinsi shule ilivyo!

Watoto hupoteza hali ya kujifunza na hata mwalimu akifundisha mtoto asiyependa masomo naye hivyo hivyo huichukia kazi yake!!

Cha kusitajabisha shule hizi ni nyingi mnoo kuliko zile zenye hali bora.Mwisho tutegemee watu wasio na uelewa!
Kinachoshangaza zaidi ni kuona viongozi wanapigania mitaala mipya bila kuboresha kwanza shule zote ziwe katika mfanano mmoja!
 
Viongozi wenyewe ndio hawa kina zitto kabwe wanafiki,wazandiki na waongo

Kwa viongozi aina ya zito ni bora kupigia kura kina samia tu
Usihamishe magoli! Zito ni kiongozi tu wa upinzani. Hahusiki na ukusanyaji wa kodi na tozo ambazo kila siku tunadanganywa zinaenda kujengea madarasa! Na wakati zinaenda kununulia magari ya kifahari, na kulipana posho. Hata uduni wa hayo madarasa kwenye picha, ni matokeo ya sera mbovu za serikali ya ccm!

Viongozi wanaishi maisha ya kifahari, watoto wao wanasoma shule za gharama! Halafu watoto wa walipa kodi, wanasoma katika mazingira duni. Jambo hili halikubaliki hata kidogo.
 
Nimekutana na andiko hili la ndugu yetu, nikaona si vibaya tukashea pamoja, maana naona kaandika vitu vingi vya msingi kwa mtazamo wangu, japo sikulazimishi kuamini kama ni kweli au la, msome ndugu Mushi....


88888888888888
View attachment 2375400
Na Thadei Ole Mushi

Kama kuna jambo ambalo nitasimama kidete kulitetea hapa nchini bila kuogopa ni maslahi ya masikini wa nchi hii. Unawaona hao watoto hapo pichani?

Hii ni Shule ya Msingi Olgira, Kata ya Sunya, Kiteto mkoani Manyara. Shule hii ina madarasa matano na wanafunzi 600 na walimu watano. Kwenye Shule hii kuna watoto wanatokea Kitongoji cha Natushi Km 12 kufika Shuleni anafika anaanza kupambana na mazingira kama haya, wakati huo kuna kiongozi anatumia V8 la Serikali kupeleka mwanawe pale Feza.

View attachment 2375403

Kuna wakati Masikini wanatakiwa kuhoji ipo hivi....
Serikali imetoa Scholarship za wanafunzi waliofanya vizuri masomo ya Sayansi kwenda kusoma nje ya nchi. Nimepitia majina ya wanafunzi wanaolengwa na mpango huo nikakuta asilimia 95 wanatokea Shule za Private ambazo ada yake si chini ya milioni tatu. Kwa kuwa watoto hawa wa matajiri walipata mazingira mazuri na shule bora basi wamefanikiwa kufikia ufaulu wa juu.

Mtoto wa masikini kama hawa unaowaona hapa Pichani ni ngumu kuja kukutana na kodi ya wazazi wake akaitumia kusoma. Hata hivyo mimi naamini mtoto aliyetoka shule ya serikali ya kawaida akapata hata two ana uwezo mkubwa kuliko hawa wanaolishwa kila kitu pale St. Mary's. Mtoto anayetembea kwa miguu KM 12 shule haina walimu, chakula ni shida, Mzazi wake kauza kila kitu mtoto asome halafu anapata two huyu ndiye anayetakiwa kusaidiwa.

Nilikuwa nina fikiri
1. Fedha zilizolenga kupeleka wanafunzi kusoma nje ya nchi kwa mwaka huu ziende zikajenge hii shule ya Olgira na nyingine zenye hali kama hii.

2. Jambo la Pili vitengenezwe vigezo ambavyo vitasaidia kodi ya nchi hii kukutana na mtoto wa maskini, mathalan hii scholarship iliyopewa jina la Rais Samia inaendeleza ubaguzi na tabaka la elimu lililopo nchini. Nadhani wanafunzi waliopata one za sayansi toka shule za Serikali za kawaida ndio wapewe hii fursa.

3. Wanafunzi waliosoma Private kwa kuwa wazazi wao wana unafuu wa maisha basi Serikali inaweza kuwasaidia kutafuta vyuo huko nje na kuwasaidia nauli lakini issue ya ada wazazi wawalipie wenyewe.

Inauma sana haya yanayoendelea...... Watoto wa maskini watabaki kuwa wapiga kura wa watoto wa viongozi na wenye fedha. Niwaombe vijana kuacha kushinda kuangalia vichekesho Tiktok na kutafuta Connections badala yake washiriki kwenye siasa za nchi hii. Niwaombe vijana kujadili mustakabali wa taifa lao. Niwaombe vijana kuachakujadili vitu vya kijinga jinga na kufuatilia mambo ya msingi ya taifa lao.

Nisaidie kushare kama umekubaliana na mtizamo huu.

Ole Mushi.
0712702602.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]UCHUMI UMEKUA SANA
 
Back
Top Bottom