Koffi Olomide ndio msanii bora wa muda wote kutoka Congo

Koffi Olomide ndio msanii bora wa muda wote kutoka Congo

Leo acha niseme ukweli wakuu,watu wanapenda kutompa mtu sifa zake mpaka afe.
Toka kizazi cha kina Lwambo mpaka sasa kina ferre na fally hakuna msanii wa kumlinganisha na koffi kimuziki apo Congo.Sema watu wanapenda kutukuza vitu vya kale kama kwenye mpira wanavyompaisha Pele na Maradonna wakati messi na Ronaldo wamefanya mengi makubwa tu.

Sasa basi hata kwenye mziki,utasikia sijui Madilu,Papa wemba sijui nani.Ndio wametoa nyimbo kali sana lakini hakuna aliefanya consistency ya nyimbo nyingi kuwa juu kama koffi.
Hata huyo Werrason bado anapaishwa tu kwa nyimbo chache ukifananisha na Koffi.

Tukubali tu wakuu hakuna kama Koffi kwenye muziki wa boringo.
Ushasema koffi ni msAnii bora ukitoa generation ya kina luambo
Hujui madilu naye ni generation ya luambo ?
Anyway kwa kizazi kipya koffi olomide na fally ipupa de carpe ya mervele ndio wasanii bora wa muda wote
 
Mimi huwa nikisikia huu wimbo wa Koffi olomide-Loi aisee nitakurupuka hatakama nilikuwa bafuni,huu wimbo huwa unanibamba sana,

Mwanzoni mwa video ya loi manati kubwa inavutwaaaa sanaa.

Hili jamaa inaonekana gemu limelihimili toka miaka na miaka.

Loi.... loi.... loi.... loi.
Isikilize Album nzima utapenda zaidi kuna ngoma inaitwa micko
 
Mkuu wewe furahia tu mziki wa Koffi. Kwa sisi wa enzi hizo tunajua huwezi kuwaweka chungu kimoja hao ulio wataja na Luambo. Franco Luambo Makiadi ni habari nyingine kabisa-ukiongelea muziki wake unaongelea muziki wa TP OK Jazz huenda ikawa bendi bora zaidi kutokea CONGO na Africa kwa ujumla. Hiyo ndio bendi ya Vicky Longomba, Poete Lutumba Simaro, Commandant de Bord Josky Kiambikuta, Ntessa Dalienst, Ndombe Pepe, Sam Mangwana, Madilu System, Djo Mpoy, Kiwakana Aime, Checain Lola Djangi kukutajia wachache. Miaka ya 1980 kwa mfano TP OK Jazz ilikuwa na wapiga solo (5) Franco, Papa Noel, Thierry Mantuika Kobi, Gerry Dialungana Kasia, Dizzy Mandeku-sikiliza nyimbo za wakati huo au wasome hao jamaa kwani wote ni who is who kwenye muziki wa Zaire. Luambo ni mwanamuziki wa kwanza kujengewa SANAMU "monument" huko CONGO miaka 26 bada ya kufariki na kufanyiwa international conference ya kujadili muziki wake. Luambo ana kitu inaitwa "OK Jazz School of Music". Kabla ya Tchacho ujuwe kulikuwa na Rhumba Odemba ambayo bado ipo ndani na nje ya Congo. Kuhusu gitaa ya Franco check hii youtube na pia google "Syran Mbenza & Ensemble Rumba Kongo: Immortal Franco: Africa's Unrivalled Guitar Legend" Kuhusu maisha ya Franco check hiki "Congo Colossus: The Life and Legacy of Franco & OK Jazz Paperback – January 4, 1994 by Graeme Ewens (Author)"
Wikipedia wanasema "

François Luambo Luanzo Makiadi (6 July 1938 – 12 October 1989) was a major figure in 20th-century Congolese music, and African music in general. He is widely referred to as Franco Luambo or, simply, Franco. Known for his mastery of rumba, he was nicknamed the "Sorcerer of the Guitar" for his seemingly effortless fluid playing. As a founder of the seminal group OK Jazz, he is counted as one of the originators of the modern Congolese sound." Sikatai Koffi yuko vizuri sana lakini ukimuweka yeye na Luambo ni sawa na mzee Mwinyi alivyosema "Nyerere ni Kilimanjaro na yeye ni kichuguu". Mkuu furahia Tchacho.
Heshima kwako.mkuu
 
Massiya natamani nikualike home halafu tusikilize miziki ya Franco aka L'a okanga la ndju pene. Tena kwenye saturi zile mziki wake unatoka bomba vibaya mnoo. Fikiria unasikiliza bisalela au freins a man au Mario. Baba hawamjui Franco hawa.
 
Massiya natamani nikualike home halafu tusikilize miziki ya Franco aka L'a okanga la ndju pene. Tena kwenye saturi zile mziki wake unatoka bomba vibaya mnoo. Fikiria unasikiliza bisalela au freins a man au Mario. Baba hawamjui Franco hawa.

Mkuu ahsante. Kutaja Bisalela umenikumbusha wimbo maridhawa waimbaji wakiwa na Micheal Boyibanda, Kiambukuta Josky na Wuta Mayi wakiongozwa na Youlou Mabiala (Mwana wa OK Jazz au Mwana Luambo). Solo ya Luambo na Mtunzi /rythm gitaa akiwa Papa Lutumba. Kutokana na wimbo wa Simaro mwingine uitawao Mabele ulioimbwa na Sam Mangwana ambao ulikaa juu ya charts kwa muda mrefu Mzee Luambo aliwaita wapigaji wake viongozi machweo na kuwaambia kwa muda wa miezi sita ijayo ni tungo zangu tu ndio zitapigwa live. Huu ndiyo mwimbo uliyofanya Simaro kupachikwa title ya Le Poete (mwanamashairi). Balaa nyingine ilitokea kati ya Maya mtunzi Simaro mwimbaji Carlyto Lassa na Mario mtunzi Luambo waimbaji Luambo na Madillu-Carlyto akachaguliwa kuwa mwimbaji bora Zaire wa Mwaka na Lutumba Simaro mtunzi bora, Mario ikapigwa chini (Luambo aliwashangaa waandishi wale waliopiga kura). Wakati huu TP OK Jazz ilikuwa na makundi mawili la ndani DRC chini ya Simaro na la nje Europe chini ya Franco. Stori hizi zinaonyesha ndani ya TP OK Jazz kulikuwa na miamba ilito tukuka na sifa moja wapo ya Luambo ni kukubali kufanya kazi na mafundi hawa na kuwa ongoza kupata kikosi ambacho huenda aina yake isitokee tena.

 
Ila Likoffi Jamani Linajua toka mdogo mpaka leo nasikiliza na kuzicheza nyimbo zake,huyu mtu anajua bwana
 
Massiya natamani nikualike home halafu tusikilize miziki ya Franco aka L'a okanga la ndju pene. Tena kwenye saturi zile mziki wake unatoka bomba vibaya mnoo. Fikiria unasikiliza bisalela au freins a man au Mario. Baba hawamjui Franco hawa.
sebene lipo?gitaa maana raha ya congo man hata nyimbo ikiwa ya taratibu unacheza kiboss boss hapo ndo koffi alipotuwin
 
Back
Top Bottom