Kofia zake zaanza kushuka thamani , Aliyeimba "Chura "naye avalishwa! walioziweka makabatini kama ukumbusho wazitoa

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Siku za hivi karibuni mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya ccm Mh Magufuli amewatunukia nishani mpya ya Kofia baadhi ya wasanii kama ishara ya kuthamini mchango wao kwenye jukwaa la kampeni zake , baadhi ya wasanii wakazithamini kofia hizo na kwenda kuzihifadhi kwenye makabati yao ya kumbukumbu , huku wadau wakiamini hiyo ni tuzo ya heshima .

lakini sasa baada ya Snura naye kupewa , tuzo hiyo imeanza kupoteza thamani yake , Snura mwimbaji wa chura , wimbo usiyo na maadili ulioleta utata hana hadhi ya kupewa tuzo yoyote achilia mbali kofia ya Magufuli


Maadili ya wimbo wake hayakuwa sawa ndio maana alipigwa marufuku na BASATA
 
Kwani Diamond aliyevalishwa kofia hajawahi kuimba nyimbo AMBAZO hazina maadili?
Au Kuna binadamu NI Bora zaidi na wengine hawana thamani?
Hata Kama alimbaa wimbo ambao hauna maadili aliomba radhi watanzania
Na isitoshe watu tunabadilika tabia na Itunajifunza kila siku tunaacha mabaya na tunasonga mbele
Ndio maana hata mbele ya Mungu wote tuna thamani sawa
 
kura 1 ina thamani kubwa sana, kama coca cola wanavyohangaika kutompoteza mteja hata mmoja kwa Pepsi! Asante mkuu kwa kudhihilisha kuwa kofia hizo zina thamani kubwa!
 
Mdee na Bulaya kulala kitanda kimoja kimaadili ni sawa?
 
Nimeiona mkuu anaongea na mlinzi wake pale kuna jambo letu pale
 
Yani yule aliyeimba chura ananesa nesa chura anaimba imba chura, wakicheza uchi baharini, ndio wanapewa kofia ? watanzania maskini wanakuja kusikiliza sera za kuondokkana na changamoto kwenye maeneo yao, kumbe wanakuja kuona aliyeimba chura ananesa nesa chura akivalishwa kofia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…