Mzee FD,
Heshima yako mkuu, katika society yoyote ile lazima kuwa na viongozi au kiongozi, sio kila wakati ni lazima kiongozi awahusishe wananchi katika maamuzi muhimu kwa ajili ya their future, Mimi sio kabisa fan wa JKN, lakini kwenye hili la Wachina ni lazima kumpa heshima yake kuwa alikuwa na vision ambayo ni moja kati ya important skill kiongozi anapaswa kuwa nayo,
kuwashirikisha wananchi alijitahidi, tena afadhali yeye wabishi aliwaweka kizuizini Mao aliwaua wote waliopinga, baada ya Mao kufa kuna waliojaribu kugeuza muelekeo wa China, guess what? Wote walifungwa au kuuliwa na wengine walipigwa marufuku kushiriki siasa tena! Lakini angalia kwetu, hata kabla Mwalimu hajafariki tayari wakaua Azimio La Arusha, wakapitisha IPTL, wakabinafsisha kila kitu, sasa Mwalimu hayupo niambie wamefanya mangapi maovu?
Mwalimu aliwashirikisha wananchi na viongozi, tatizo ni wananchi wasio kuwa na mwamko wa kisiasa, elimu ndogo ya kuelewa faida na hasara ya maamuzi makubwa au ya kitaifa kisiasa, na viongozi waongo na wanafiki tena nitakutajia kwa majina viongozi waliokuwa karibu na Mwalimu ambao walipaswa kufa kabla ya kukubali kuona mambo ya Mwalimu yanaharibiwa,
Kingunge, Nsa Kaisi, Warioba, Butiku, Salimin, Natepe, Mwakanjuki, Makame, Nassoro Moyo, Lusinde, Sozigwa, Mnauye, Anna Abdallah, Kawawa, Jumbe, Salim, Msekwa, Musuguri, Mongella, Tandau, Mwakawago, Makweta, Siovelwa, Sozigwa, Ndejembi, Sarakikya, Mbita, Munanka, Bomani, Kahama, Mwangoka, Kisumo, Mama Swai, Mungai
hao juu ndio viongozi waliokuwa karibu na Mwalimu, na mpaka leo hawa bado wana influence kali katika siasa za bongo kwani hata JK mwenyewe asingeenda kokote katika uchaguzi bila ya kukubaliwa na 75% ya hawa wazee, hawa ndio waliopaswa kuweka mguu chini na kuwakatalia hawa kina BM maamuzi yao machafu. BM hayumo kwenye hilo kundi juu kwani he was never close to Mwalimu kabla ya uchaguzi wa 1995, BM siku zote alikuwa karibu na Butiku lakini sio Mwalimu kwa sababu elewa kwamba kabla ya kuwa rais BM hakuwahi kuchaguliwa hata NEC, kila alipogombea alikuwa akishindwa, kule Uchina kuna viongozi kama hao juu waliobaki katika chama hawayumbi hata siku moja katika kusimamia misimamo ya maendeleo ya nchi yao iliyowekwa china na Mao na mzee DeoPing!
Mzee FD Mwalimu alifanya ya kutosha, somebody had to take it to another level, badala ya kuvunja misingi yake bila kuwa na cha ku-replace, China ni mfano mkubwa wa kuigwa na sisi kwani kama walivyosema waliotangulia, ni kwamba at one point sisi na wao tulikuwa tunawekwa meza moja nao na wakubwa wa West!