Komredi Mizengo Pinda yuko wapi?

Komredi Mizengo Pinda yuko wapi?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
21,113
Reaction score
65,124
Wasalaam,

Nimetokea ghafla kumkumbuka sana huyu komredi wangu wa ukweli mzee wa "Piga Tuu"
Huyu ndugu yangu baada tu ya kuisha kwa uchaguzi na awamu hii ya tano kuingia madarakani tumekuwa hatumsikii kabisa.

Mawaziri wakuu wastaafu wengine kama Mzee Malecela, Mzee Warioba, Mzee Msuya na Mzee Sumaye walikuwa wanaunguruma hata baada ya vipindi vyao kuisha. Lakini komredi Mizengo Pinda amekuwa adimu sana kwenye masikio na macho yetu, ni kama yupo lakini hayupo.

Binafsi nimekukumbuka sana komredi wangu mzee wa "hisia kali" na maamuzi mazito lakini yenye busara ya aina yake.

Popote pale ulipo komredi, Malcom Lumumba anakusalimu sana sana. Angepata nauli na wasaa wa kufahamu ulipo kwasasa angefunga hata safari kuja kukusalimia.

NB: Pia hizi salamu zimfikie ndugu yetu Former Minister Plenipotentiary Mheshimiwa sana Bwana Benard Kamilius Membe ambaye naye sijamtia machoni kwa muda mrefu sana.
 
Mzee yupo zake shamba Dodoma analima kisasa na kutoa ushauri...mtembelee kwenye shamba lake la horticulture pale Dodoma,Yuko welcoming Sana huyu senior citizen

Daaah Shukrani sana Mkuu,
Vipi huyu mwenzake Mzee wetu mwingine niliyemtaja anapatikana wapi ???
 
Membe nadhani kajichimbia huko Kusini last time nimemwona hivi juzi kwenye maziko nadhani ni ya alhaj mtopa...wapo hawa wazee wamechagua kukaa kimya

Anafanya biashara ya Mafuta au Gesi huko makwao ??, Kwanini ajichimbie wakati siyo kawaida yake yule jamaa aisee!
 
Ndo ujue kuna jambo...kimya kingi kina mshindo wanasema
Kwanini hawa jamaa wasiende hata kufundisha pale Mlimani mbona wanaweza kufanya hizo kazi ??? Tena wana uelewa mkubwa sana kuhusu dunia kuliko hata walimu wa pale.
 
Kwanini hawa jamaa wasiende hata kufundisha pale Mlimani mbona wanaweza kufanya hizo kazi ??? Tena wana uelewa mkubwa sana kuhusu dunia kuliko hata walimu wa pale.
Nadhani tofauti kubwa ya kipato ndiyo hasa inasababisha wanasiasa wakistaafu wasirudie tena white board...nafahamu Prof Msola amevumilia akarudi Ila wabobevu kv kina mwandosya, & co wamekacha... tofauti ya kipato nahisi inawasuta wanaona Bora wale mafao Tu...sanasana hapo wanakuwa na ndoto za kurudi tena kwenye siasa wanasubiri upepo utulie
 
Nadhani tofauti kubwa ya kipato ndiyo hasa inasababisha wanasiasa wakistaafu wasirudie tena white board...nafahamu Prof Msola amevumilia akarudi Ila wabobevu kv kina mwandosya, & co wamekacha... tofauti ya kipato nahisi inawasuta wanaona Bora wale mafao Tu...sanasana hapo wanakuwa na ndoto za kurudi tena kwenye siasa wanasubiri upepo utulie

Aiseeh aiseeh! Basi wafanye hata kitu cha maana ili kusaidia nchi, maana mtu kama Prof. Mwandosya akisubiria SIASA haitasaidia kabisa kwasasa. Inabudi Serikali iandae Mkakati Madhubuti wa kuweza kuhakikisha kwamba hawa wataalamu wanakuwa wanatoa sauti ambazo zinaweza kutoa mwelekeo kwa nchi yetu. Maana kuna wengine wana uwezo mzuri bado lakini ndiyo vile sasa wapo wapo tu....
 
Nadhani tofauti kubwa ya kipato ndiyo hasa inasababisha wanasiasa wakistaafu wasirudie tena white board...nafahamu Prof Msola amevumilia akarudi Ila wabobevu kv kina mwandosya, & co wamekacha... tofauti ya kipato nahisi inawasuta wanaona Bora wale mafao Tu...sanasana hapo wanakuwa na ndoto za kurudi tena kwenye siasa wanasubiri upepo utulie
Professor Mwandosya anaendelea kufundisha kama kawaida ila makaazi yake kwa sasa hivi muda mwungi huwa huki Kijijini kwake, Lufilyo, Tukuyu .
 
Comrade wangu Mizengo ooh Mizengo!
[emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]
 
Mzee yupo zake shamba Dodoma analima kisasa na kutoa ushauri...mtembelee kwenye shamba lake la horticulture pale Dodoma,Yuko welcoming Sana huyu senior citizen
Bado analima Dodoma ???
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Once a Cheka, Always a Cheka.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
20230313_183303.jpg
 
Back
Top Bottom