The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 747
- 2,112
Afisa Manunuzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Mussa Kimwaga amemlalamikia Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kwa kutukana na kuwa mbabe kwa watumishi.
Bw. Kimwaga akitema cheche
Tuna ubunifu mwingi sana na ushauri mwingi lakini hatupewi nafasi ya kutoa ushauri mzuri. Ubabe ni mkubwa sana kwa Mkurugenzi wetu.
Binafsi hata mimi natamani niondoke Kondoa; nashindwa tu sina mtu wa kunihamisha. Ulikuwa unamtamka hapa Muweka Hazina, Muweka Hazina amekimbia – ameondoka Kondoa si kwa mapenzi ni kwasababu ya kusemwa vibaya na Mkurugenzi.
Sawa, mtumishi kuna kukosea lakini pia kuna namna ya kumuonya mtumishi, lakini unatukanwa matusi ya nguoni. Binafsi nimetukanwa kwenye site. Unafanya kazi wakati mwingine tunatumia resources zetu za mshahara tunajua Halmashauri yetu ya Kondoa wakati mwingine mambo ni magumu. Unatoa hela yako binafsi unafanya kazi lakini no appreciation kwa Mkurugenzi. Inafika mahali inavunja moyo!
Binafsi, Mkuu wa Mkoa mimi natamani niondoke hata kesho kwenye hii Halmashauri. Mimi nimechoka!
Sijaanzia hapa kufanya kazi; nimefanya kazi Muheza (miaka minne), Handeni (miaka minne) Shinyanga Manispaa… Nimefanya kazi sina rekodi ya ubadhirifu, sijawahi kupelekwa Takukuru, lakini kwa Kondoa nimekata tamaa. Na Mkurugenzi naye hanitaki! Amesema “Wewe sikutaki!” Hata kwenye hii miradi inayoendelea amesema “Wewe sikutumii!” Ubabe umezidi!
Hawaongei hao. Wanakaa kimya Wakuu wa Idara lakini wanaugua …
Bw. Kimwaga akitema cheche
Tuna ubunifu mwingi sana na ushauri mwingi lakini hatupewi nafasi ya kutoa ushauri mzuri. Ubabe ni mkubwa sana kwa Mkurugenzi wetu.
Binafsi hata mimi natamani niondoke Kondoa; nashindwa tu sina mtu wa kunihamisha. Ulikuwa unamtamka hapa Muweka Hazina, Muweka Hazina amekimbia – ameondoka Kondoa si kwa mapenzi ni kwasababu ya kusemwa vibaya na Mkurugenzi.
Sawa, mtumishi kuna kukosea lakini pia kuna namna ya kumuonya mtumishi, lakini unatukanwa matusi ya nguoni. Binafsi nimetukanwa kwenye site. Unafanya kazi wakati mwingine tunatumia resources zetu za mshahara tunajua Halmashauri yetu ya Kondoa wakati mwingine mambo ni magumu. Unatoa hela yako binafsi unafanya kazi lakini no appreciation kwa Mkurugenzi. Inafika mahali inavunja moyo!
Binafsi, Mkuu wa Mkoa mimi natamani niondoke hata kesho kwenye hii Halmashauri. Mimi nimechoka!
Sijaanzia hapa kufanya kazi; nimefanya kazi Muheza (miaka minne), Handeni (miaka minne) Shinyanga Manispaa… Nimefanya kazi sina rekodi ya ubadhirifu, sijawahi kupelekwa Takukuru, lakini kwa Kondoa nimekata tamaa. Na Mkurugenzi naye hanitaki! Amesema “Wewe sikutaki!” Hata kwenye hii miradi inayoendelea amesema “Wewe sikutumii!” Ubabe umezidi!
Hawaongei hao. Wanakaa kimya Wakuu wa Idara lakini wanaugua …