Kondoo mwenye korani azaliwa

Waislamu ache ujinga! Hakuna maandishi yoyote hapo hilo ni baka la rangi nyeupe sio mchoro! Hivi mkienda umasaini si mtarudi na hadidu za maneno kibao maana kule wana michoro sio baka kama hilo!

Kama huna cha kuchangia kaa kimya!!!
 
Yasin ni Sura ya 36 katika Quran Tukufu, inasema;

SURA 36. SURAT YA-SIN

 
Yasin ni Sura ya 36 katika Quran Tukufu, inasema;

SURA 36. SURAT YA-SIN


sasa ndugu Mkunga.......tuwekee basi mistari ya Surat Ya-Sin.......nimeomba kweli lakini naona kama inakuwa ngumu vile.......au kuna tatizo ikiwekwa hapa?
 
Hiyo ni rangi tu ya tofauti yaani doa, haina uhusiano wowote, hata kama hilo neno ni la kiarabu itakuwa imetokea coincidence tu...msikauwe bure ka mwana kondoo ka watu, punguzeni ushirikina kiimani.(mwenye kujua imeandikwa nini atujuze)
Na hata hakujuzi mtu, maana umeshaanza kwa dharau na kashfa, sasa unataka ujuzwe uli uendeleze maneno yako ya shombo au.
 
Kondoo huyo ni shetani anawakilisha muslim

Mtu kama huna cha kuchangia bora unyamaze kimya kuliko kutoa maneno ya shombo shombo, Mngeambiwa huyo kondoo mkojo wake dawa ya ukimwi umgekopa mpk hela muende mkapange foleni, vitu visivyo na msingi wala uthibitisho ndio mnakimbilia.
 

Lete ushahidi ndugu, acha kuongea vitu visivyo na uthibitisho. weka ushahidi hapa jamvini kila mtu apate kushuhudia sio maneno matupu.
 
SURA 36. SURAT YA-SIN
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
1. Ya-Sin (Y.S.).
2. Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!
3. Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
4. Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
5. Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
6. Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa , basi wao wamekuwa wenye
kughafilika.
7. Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo
hawaamini.
8. Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao
viko juu tu.
9. Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao;
kwa hivyo hawaoni.
10. Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
11. Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi
wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
12. Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo
yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
13. Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
14. Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine
wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
15. Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema
hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
16. Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
17. Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
18. Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa
yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
19. Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama
nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
20. Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu
wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
21. Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
22. NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
23. Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema,
akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
24. Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
25. Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
26. Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
27. Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio
hishimiwa.
28. Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si
wenye kuteremsha.
29. Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
30. Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
31. Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei
tena kwao.
32. Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
33. Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani
yake nafaka, wakawa wanazila!
34. Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua
chemchem ndani yake,
35. Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je,
hawashukuru?
36. Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea
katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
37. Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
38. Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu,
Mwenye kujua.
39. Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
40. Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea
katika njia zao.
41. Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio
sheheni.
42. Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
43. Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
44. Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
45. Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili
mpate kurehemewa...
46. Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni
wenye kuipuuza.
47. Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru
huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli
walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
48. Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
49. Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
50. Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
51. Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao
Mlezi.
52. Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo
yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
53. Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.
54. Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo
kuwa mkiyatenda.
55. Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.
56. Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.
57. Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.
58. "Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
59. Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
60. Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet'ani? Hakika yeye
ni adui dhaahiri kwenu.
61. Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
62. Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je,
hamkuwa mkifikiri?
63. Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.
64. Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
65. Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu
yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
66. Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia.
Lakini wange ionaje?
67. Na tungeli taka tunge wageuza SURA hapo hapo
walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.
68. Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?
69. Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo.
Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha.
70. Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
71. Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama
wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
72. Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao
wanawala.
73. Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
74. Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate
kusaidiwa!
75. Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao
hudhurishwa.
76. Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na
wanayo yatangaza.
77. Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la
manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!
78. Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo
atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?
79. Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi
wa kila kuumba.
80. Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo
mnawasha.
81. Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye
ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.
82. Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
83. Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake
Yeye mtarejeshwa.
 
ndo mana nikasema hii thread siiwezi.unaona sasa!!?kristu......tumaini letu.
 

kama kila hata hayo madoa kwenye kondoo mnalinganisha na aya-haya mawingu mbona yana taswira lakini hakuna mwenye mpango nayo
 
Mtu kama huna cha kuchangia bora unyamaze kimya kuliko kutoa maneno ya shombo shombo, Mngeambiwa huyo kondoo mkojo wake dawa ya ukimwi umgekopa mpk hela muende mkapange foleni, vitu visivyo na msingi wala uthibitisho ndio mnakimbilia.
<br />

Mkulu DK

He he he he he ,nimekusoma ha ha ha ha!
Mkojo ungekuwa wa dawa sio he he he he
<br />
 
Kweli waislam mna kazi kubwa sana mbele yenu? Yaani hilo baka jeupe ndo linawafanya muanze hija? Poleni sana, Yasin kwa kiarabu haiandikwi hivyo, hapo mme forge. Yasin inaandikwa:


&#65168;&#65208;&#65227;
 
<br />
<br />
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…