Korea Kaskazini na Iran ni nchi salama kwa Mtanzania?

Korea Kaskazini na Iran ni nchi salama kwa Mtanzania?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Kwa jinsi Iran inavyosigana na mataifa makubwa kama Marekani, inaweza kuleta picha kuwa ni nchi hatari kuishi. Lakini ukifuatilia taarifa za hapa Tanzania, ni wazi kuwa nchi ya Tanzania na Iran hazijawahi kuhasimiana. Hata kipindi fulani, Iran iliipatia Tanzania msaada wa matrekta madogo 100. Imeshatoa na misaada mingine pia.

Rais wa Korea Kaskazini anadaiwa kuwa ndiye dikteta katili duniani. Lakini nchi yake haina ugomvi na Tanzania. Baba wa Taifa hilo alikuwa rafiki wa hayati Nyerere.

Nchi zote hizo mbili zina mabalozi Tanzania, lakini nafikiri Tanzania haina mabalozi kwenye nchi zao.

Kwa muktadha huo, hizo nchi ni salama kwa Mtanzania?
1. Mtanzania anaweza kuishi huko na kufanya shughuli zake halali kwa amani bila kubaguliwa?

2. Kutokana na hizo nchi kutokuwa na uhusiano mzuri na mataifa ya Kimagharibi, hatuwezi kutumia huo mwanya kama fursa ya kiuchumi kwa kufanya nao biashara?
 
Wakati wa Mwalimu Tanzania ilikuwa mwanachama wa nchi zisifungamana na upande wo wote wakati wa vita baridi kati ya kambi ya nchi za magharibi zilizoongozwa na US na zile za mashariki zilizokuwa zikiongozwa na Urusi.
Kwa muktadha huo Tanzania ilikuwa na uhusiano na nchi yo yote bila kujali ni ya upande gani.
Kwa hiyo Iran na NKZ zina uhusiano mzuri tu na nchi yetu.
Hata hivyo baada ya NKZ kuwekewa vikwazo na UN kuhusu progarame yake ya silaha za kinuklea Tanzania ilianza kupunguza uhusiano wa kibiashara na nchi hiyo kwa shinikizo la UN.
 
Wakati wa Mwalimu Tanzania ilikuwa mwanachama wa nchi zisifungamana na upande wo wote wakati wa vita baridi kati ya kambi ya nchi za magharibi zilizoongozwa na US na zile za mashariki zilizokuwa zikiongozwa na Urusi.
Kwa muktadha huo Tanzania ilikuwa na uhusiano na nchi yo yote bila kujali ni ya upande gani.
Kwa hiyo Iran na NKZ zina uhusiano mzuri tu na nchi yetu.
Hata hivyo baada ya NKZ kuwekewa vikwazo na UN kuhusu progarame yake ya silaha za kinuklea Tanzania ilianza kupunguza uhusiano wa kibiashara na nchi hiyo kwa shinikizo la UN.
Hili limekaaje?
Kwa mfano, nikaenda huko kuanzisha makazi na kisha Kusajili kampuni huko huko kwao, na mtu mwingine akawa na kampuni yake hapa Tanzania, na akawa anaagiza bidhaa toka nchi za Magharibi kwa jina la kampuni yake iliyopo hapa Tanzania, kisha na mimi niliyeko huko NK au Iran nikanunua kupitia hiyo kampuni iliyopo Tanzania na kuipeleka huko nilikotaka.

Serikali ya Tanzania itaweza kutuhumiwa katika hilo hasa ikizingatiwa kuwa biashara zimefanywa na makampuni ya watu binafsi, moja iliyopo Tanzania na nyingine iliyopo Korea/Iran?
 
kama tu jpm alianza kuwekewa vikwazo kisa aliikataa chanjo ya Corona vipi kuhusu mtata kiduku mzee wa nyuklya watakubali.
 
Back
Top Bottom