Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amempa saa 24 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Vijijini, Khalfani Magani kujieleza kwa nini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa madai ya kuficha fedha za mfadhili za ujenzi wa shule.
Agizo hilo amelitoa jana Alhamisi Septemba Mosi 2022 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Mgwashi iliyopo wilayani Korogwe, akimtaka kiongozi huyo ajieleze kwa nini asiondolewe kwenye nafasi yake hiyo.
Mgumba amesema kuwa ameamua kutoa maagizo hayo baada ya mkurugenzi huyo kuchelewesha ujenzi wa shule ya sekondari Mgwashi uliokuwa ukamilike Juni mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa huyo amesema shule hiyo ilipatiwa mgao na Serikali wa Sh600 milioni ambapo awali walipokea Sh470 milioni huku mfadhili alishatoa zaidi ya Sh100 milioni kwaajili ya ujenzi huo lakini Mkurugenzi huyo hakutaka kueleza taarifa hiyo ya Mfadhili kwenye kikao chochote.
"Umeletewa fedha mwezi wa 12 (Desemba) na huu mradi ulitakiwa ukamilike mwezi wa nne (Aprili), kuna watu walikuwa na nia ovu ya kumchonganisha Rais (Samia Suluhu Hassan) na wananchi wa Mgwashi hatutawavumilia na hawana nafasi kwenye utawala huu," amesisitiza Mgumba.
Ameongeza kuwa, “Mkurugenzi nataka ujieleze ndani ya masa 24 kwanini umechelewesha mradi na kwamba majibu yake kama yatanidhisha ndiyo nitamshauri Rais au Waziri hatua gani za kufanya na tabia ya kuchelewesha mradi iwe mwanzo na mwisho.”
Agizo hilo amelitoa jana Alhamisi Septemba Mosi 2022 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Mgwashi iliyopo wilayani Korogwe, akimtaka kiongozi huyo ajieleze kwa nini asiondolewe kwenye nafasi yake hiyo.
Mgumba amesema kuwa ameamua kutoa maagizo hayo baada ya mkurugenzi huyo kuchelewesha ujenzi wa shule ya sekondari Mgwashi uliokuwa ukamilike Juni mwaka huu.
Mkuu wa Mkoa huyo amesema shule hiyo ilipatiwa mgao na Serikali wa Sh600 milioni ambapo awali walipokea Sh470 milioni huku mfadhili alishatoa zaidi ya Sh100 milioni kwaajili ya ujenzi huo lakini Mkurugenzi huyo hakutaka kueleza taarifa hiyo ya Mfadhili kwenye kikao chochote.
"Umeletewa fedha mwezi wa 12 (Desemba) na huu mradi ulitakiwa ukamilike mwezi wa nne (Aprili), kuna watu walikuwa na nia ovu ya kumchonganisha Rais (Samia Suluhu Hassan) na wananchi wa Mgwashi hatutawavumilia na hawana nafasi kwenye utawala huu," amesisitiza Mgumba.
Ameongeza kuwa, “Mkurugenzi nataka ujieleze ndani ya masa 24 kwanini umechelewesha mradi na kwamba majibu yake kama yatanidhisha ndiyo nitamshauri Rais au Waziri hatua gani za kufanya na tabia ya kuchelewesha mradi iwe mwanzo na mwisho.”