Kosa gani ulimfanyia mama yako hadi likasababisha akuchape au kukuadhibu?

Kosa gani ulimfanyia mama yako hadi likasababisha akuchape au kukuadhibu?

Blank page

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2015
Posts
5,487
Reaction score
4,817
Happy mother's day!!!
Shkamooni akina MAMA wote mliopo JF tunawapenda sana,
leo kwa kuenzi siku ya kina mama duniani napenda tukumbuke mambo mawili matatu ambayo yashawah kutokd huko nyuma enzi tunakua na kulelewa na mama zetu...embu sema ni kosa au kitu gani ulifanya mpaka ikapelekea mama yako,mlezi au mzazi akakuchapa ama kukuadhibu au ulimkasirisha??
mi nakumbuka nimefanya mambo meng sana..ya makosa mara nyngne nliadhbiwa na mama mfano.nishawai kutoroka nyumbani na kwenda kwenye sherehe,kwa watu kula chakula..nikawa naingia hadi kweny makombo ya vyakula vilivyobakishw na watu,ase mama yangu akapata taarifa nivofika home mbna nilikoma kwa kipigo ase...nkaambiwa wew nyumban huli wali?? sikuwa na lakusema,ila chapo iliningia ase.
[HASHTAG]#nakupendasanamamayangu[/HASHTAG]
 
hata. mimi sikumbuki Kama nimewahi kuchapwa. maana tokea nimeanza kujitambua. sijawahi kuchapwa. I love you mumy. na kina mama wote.
ukiwa mtoto,kipind hujitambui ilikuaje aukuwa ukimuudh mama?
 
Kwa kweli Mimi sikumbuki kama niliwahi chapwa na Mama kwa sababu ni mpole mno.
Kweli nilikuwa nafanya makosa lakini alikuwa akinisamehe.

Ila kina mama ni watu wa kipekee sana.
Kuna siku moja mama alinituma nikawashe moto kwenye jiko la kuni yeye alikuwa akimenya viazi.
Sasa nilipofika jikoni nikakuta moto kidogo, nikachukua kuni nikaweka jikoni nikaanza kupuliza ili moto uwake sasa kila nilipopuliza moto haukuwaka badala yake ni moshi tu ndo ulitawala.

Moshi uliniwasha machoni hadi michozi ikanitoka, kwa kweli hasira zikanishika nikachukua zile kuni nikazivurumisha kwenye majivu pale jikoni, nikaenda nje nikachukua michanga nikaja kufukia pale jikoni kabisa hadi moto wote ukazimika.

Nikaenda kukaa nyuma ya nyumba huku nikilia macho yamenivimba hatari.

Mama akaanza kuita sikuitika, alipoenda jikoni alichokiona huko ilibidi aniite tena kwa hasira na hapo nikaitika ila sauti ilionyesha nilikuwa nalia.

Basi akaja kule nyuma, kakasirika kweli kweli lakini aliponikuta na hali ile hasira zikamuisha ghafla na kuanza kunibembeleza ninyamaze. Nilipotulia nikamueleza kilichotokea.

Doh!
Sikuwa kumuona mama akicheka kama siku hiyo.
Hadi leo hua akikumbuka hilo ananicheka sana.

Hili ni tukioa ambalo kamwe sitalisahau.
 
Happy mother's day!!!
Shkamooni akina MAMA wote mliopo JF tunawapenda sana,
leo kwa kuenzi siku ya kina mama duniani napenda tukumbuke mambo mawili matatu ambayo yashawah kutokd huko nyuma enzi tunakua na kulelewa na mama zetu...embu sema ni kosa au kitu gani ulifanya mpaka ikapelekea mama yako,mlezi au mzazi akakuchapa ama kukuadhibu au ulimkasirisha??
mi nakumbuka nimefanya mambo meng sana..ya makosa mara nyngne nliadhbiwa na mama mfano.nishawai kutoroka nyumbani na kwenda kwenye sherehe,kwa watu kula chakula..nikawa naingia hadi kweny makombo ya vyakula vilivyobakishw na watu,ase mama yangu akapata taarifa nivofika home mbna nilikoma kwa kipigo ase...nkaambiwa wew nyumban huli wali?? sikuwa na lakusema,ila chapo iliningia ase.
[HASHTAG]#nakupendasanamamayangu[/HASHTAG]
Team makombo kumbe tupo kibao
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Nilioga mtoni akanifuma alinitandika yaani ...halafu adhabu zake ni za series Leo episode ya kwanza kesho tena akitoka kazini nyingine kwa siku tano....hahaahah nikikumbuka nacheka sana ...kuna siku nyingine nilimpiga mdogo wangu teke la tumbo alinizaba kofi mpaka niliona nyota .......ukisikia mtu kaona nyota its literary stars sio utani niliona vinyota viwili vidogo na limoja likubwaaa halafu linang'araaa sana..Niliadhibiwa sana na mama sababu ya utundu wangu nlivokua mdogo ila all in all nampenda sana na ni kati ya binadamu walioniinfluence mimi kuwa hivi nilivyo Leo...Nimekumbuka nyingine hahahahaha kuna siku asubuhi sana kama 12 ivi nliamka halafu nikawnda jikoni direct nkachukua sukari na chumvi nikachanganya halafu nikalamba (haka kamchezo alinionya mara nyingii sanaaaaaaa) sasa akanifuma bana heheeeh kulikua na pikipiki nje akanizamisha chini ya pikipiki huku kisampa kimeinuka juujuu hivi [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] alinitandika kila nikitaka kuinuka najigonga kwenye pikipiki natulia ...alitia fimbo kwenye kisampa mpka hamu yote ya sukari ikaisha... Siku nyingine nilimpiga house girl bna sasa ili mama asionyeshe upendeleo akanitandika fimbo 3 trust me zile fimbo nazikumbuka mpaka Leo I LOVE YOU MAMA
 
Back
Top Bottom