Kosa gani ulimfanyia mama yako hadi likasababisha akuchape au kukuadhibu?

Aiseee mi nimezichezea mnooo... makosa daily.. mara nimechokoza mbwa ... mara tumechangia mtoto wa jirani tukampa kisago... mara nimekutwa nachezea moto kupika pika.. mradi nilikua naharibu balaa..
 
Aiseee mi nimezichezea mnooo... makosa daily.. mara nimechokoza mbwa ... mara tumechangia mtoto wa jirani tukampa kisago... mara nimekutwa nachezea moto kupika pika.. mradi nilikua naharibu balaa..
doh hatar iyo,so mama alikuwa akikshush kipgo tu ase.
 
Nakumbuka Kuna siku Mama aliondoka kwenda kwenye Sherehe zile za ucku Banah,Ila wakati anaondoka aliniachia maagizo kuwa usiondoke ubaki na ulale na mdogo wako,usije mwacha alale peke yake,
Apo tayari nilishamuomba kwenda kwenye Maurid Ya chuoni kwetu (Madrasa),Akagoma"Hakuna kwenda kokote Ubaki na Mdogo wako" Dooh!!! Nikawaza nikasema Leo Nalikosa lile pilau,Aitokuja tokea..
Basi Banah! Nikasubiri aondoke,Alivyomalizia Tuh Nikaingia ndani nakuvaa vazi langu la Kimadrasa,Nikampanga dogo Wewe Leo utaenda kulala kwa jirani Sawa ,dogo akaitikia kwa shingo upande,Nami Nikajua naweza Wahi rudi Bi Mdash atoshtukia ..
Mauridi Yakaisha Usiku sana, Ikabidi tulale chuo(Madrasa),Asubuh yake ndo turudi Home

We!! Nililala uku nakiwaza kipigo,Sababu Bi Mkubwa alikuwa akikuambia jambo Alafu ukufatisha ana Maneno ye Bakoraaa Tuh..
Nikarudi Asubuh Nyumbani Namkuta Mama Kalala Mlangoni fimbo Pembeni..Nilivyomsalimia Tuh Kilichofata Sitosahau Mpka leo ...Nilipigika Mpka Nikachukia Kurudi Tena Chuo(Madrasa), Lol!!!! Love U Maaa
 
Kwa experience niliyo nayo makosa nilokua napigwa yalikua yale madogo sana lakini kuna yale makubwa MF: kukutwa tunagegedana na watoto wa majirani, kukutwa na mipira ya wakubwa , kuangalia porno yale kusema kweli niliwekwa kikao sikuwahi pigwa na ndo yalinipa woga kurudia fanya sasa!!..
 
Mimi nilikuwa kikojozi, aiseee kuna siku mama alinipiga hadi niliugua siku 2, ikawa mwisho wa kunipiga japo niliendelea kukojoa, nakupenda sana mama yangu
 
Hahhahaha umenikumbusha nilimshawishi pacha wangu kuiba khanga za bimkubwa tuende maulidini... mbona tulifurahia shoo alivyorudi maana alisafiri... !!!
 
Nilitumwa kwenda mashine kusaga mahindi nikaiba shilingi tano ili nikanunue nayo pipi, kosa nililofanya nikaiweka kwenye mfuko wa tishet wakati mama ananitwisha mahindi akawa ameiona timbwili likaanzia hapo kwa nini nimeiba pesa na sijaomba nilipata stick na mashine nikaenda
 
Mie.nilifanya mchezo.mbayaa haa haaa, Bi mkubwa alikuwa na mkanda wake wa JKT enzi hizo wacha anikung'ute nikaingia uvungu wa Kitanda hapo ikawa salam yangu
 
Mama yangu ni mpole sanaaa! Ata kumfanyia kosa utaona aibu. Ila kuna siku aliniudhi nikamnunia... Nikaenda kwenye migomba na kukaa huko mpaka giza likaingia. Baba aliporudi mama akanisemelea eti nimemnunia sababu amenisema (ata sikumbuki alinisema nini)... Baba akaja kunisema zaidi. [emoji1][emoji1] eti kwa nini unamliza mama yako? Akanitaka nikaombe msamaha. Nikaenda kishingo upande na kweli nikamkuta mama macho mekunduu huku anajishughulisha jikoni. Akawa hanitumi kumsaidia chochote... Nikapiga magoti kumuomba msamaha, na kujiliza juu ndo akarudi katika hali ya kawaida.
 
Ulikuwa unadekaa kumbeee enzi haa haaa mie Bi mkubwa wala asingekukopesha huko huko migombani angekufirigisa na bakora za kutosha na mshua akirudi anamalizia na risala nzito juu ya kitendo chako huku akimpa Bi mkubwa Big up ya nguvu
 
Ulikuwa unadekaa kumbeee enzi haa haaa mie Bi mkubwa wala asingekukopesha huko huko migombani angekufirigisa na bakora za kutosha na mshua akirudi anamalizia na risala nzito juu ya kitendo chako huku akimpa Bi mkubwa Big up ya nguvu
Hahaha! Mama alikua anaumia sana ukimnunia.
 
Mama yangu hajawahi kunichapa.maana mimi nilikuwa mtoto wake wa pekee.lakini hajanilea nikiwa na miaka 3.nikachukuliwa na baba nikaenda kulelewa na mama wa kufikia.huko ndo kulikuwa na shughuli.
Najua mnajua mama wa kambo walivyo.ila namshukuru sanaaaaaa.maana alinifundisha mengi.
Leo yananisaidia.mungu amrehemu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…