Kosa la karne kwa CCM ni kujitenga na hoja ya Katiba na kuwaacha upinzani watambe nayo

Kosa la karne kwa CCM ni kujitenga na hoja ya Katiba na kuwaacha upinzani watambe nayo

Naanto Mushi

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
6,236
Reaction score
15,677
Kwasababu bado sina chama cha siasa, nataka kuwashauri viongozi wakuu wa CCM. 'Msijitenge na hoja ya katiba na kuwaachia upinzani pekee, mnafanya kosa kubwa'.

Nimeangalia trend mpaka sasa huko mitandaoni, nimesikitika kuona kwamba kila mwana CCM ambaye ataongea kuhusu katiba mpya, basi ataongelea kwa kusema kwamba nchi haihitaji katiba mpya kwa sasa. Hili ni kosa kubwa sana, nadhani ambacho CCM wangepaswa kufanya kwa sasa ni kufanya utafiti wa kisayansi wa kujiridhisha ni kwa asilimia ngapi wananchi milioni 60 wana kiu ya katiba mpya.

Baada ya kujiridhisha ndipo haswa wanatakiwa kuja na hoja ama za kupinga katiba mpya ama na wao wajiingize moja kwa moja kwenye ajenda ya katiba mpya.

Kufuatia miaka mitano ya 'stress' ni wazi kwamba upepo uliopo sasahivi ni upepo wa mabadiliko, na wala CCM wasidhani kwamba upepo huu wakudai mabadiliko ni hoja ya CHADEMA, la hasha, kuna wana CCM wengi tu sasahivi nao wanahisi kwamba kuna mabadiliko yanahitajika kufanyika.

Sasa ukiwa kwenye hali hiyo ya uchu wa watu kutaka kubadilika, kama chama cha siasa na wewe itabidi uone namna gani uta flow na mawimbi, na hii itakuwa na matokeo makubwa sana kwenye umaarufu wa chama cha mapinduzi chenyewe, hatari kubwa na ya mapema ya CCM ni kuanza kuonesha eti wanapinga katiba mpya.

Ningeshauri uongozi mpya wa CCM waone namna ya wao kuikumbatia hii ajenda ya kuwa na katiba mpya, wasiwaachie upinzani peke yao, kama kweli wanamipango ya CCM kuendelea kuonekana kwenye uso wa Tanzania miaka 20 inayokuja. Hakuna namna CCM itataka kupinga katiba mpya na kuendelea kutawala kwa miaka 20 inayokuja, sidhani kama taifa hili la vijana wenye uchu wa mabadiliko wataacha hichi kitu kitokee.

Sidhani kama ndani ya miaka 10 hadi 20 ijayo ambapo nchi itakuwa na watu kati ya milioni 70 au 80, asilimia zaidi ya 65% wakiwa vijana ambao wengi watakuwa wamesoma na hawana ajira, hapo hapo kiwango cha umasikini bado ni kikubwa, halafu hapo hapo nchi bado inaishi bila katiba mpya, hichi kitu kitakuwa kigumu sana kuwezekana, na kama kuna watu huwa wanafanya analysis ya kutabiri matukio ya miongo miwili ijayo, ni wazi kwamba kwa dunia ya sasa inavokwenda, CCM hawatakiwi kabisa kufikiria kwamba wataendelea ku exist salama bila nchi kuwa na sheria na katiba ya kueleweka.

Na itakuwa ngumu sana ku guarantee Tanzania isiyomwaga damu kama hakuta kuwa na katiba na sheria za kueleweka ndani ya miaka 10 mpaka 20 inayokuja maana ni kipindi ambacho kiwango cha subira na uvumilivi kwa watanzania walio wengi kitakuwa kimefika ukomo.

So mi nachukulia huu utawala wa mama kuwa ni kipindi cha muhimu na cha mpito kwa mustakabali wa utulivu wa nchi ya Tanzania kwa miaka 10 na 20 inayokuja. Hili suala lisichukuliwe ki uwepesi, watanzania wengi hawapo tayari kwa 'another Magufuli' ndo mana hili vugu vugu la katiba mpya ni tofauti na vugu vugu la katiba kwenye enzi ya Kikwete. Completely different atmosphere.

So kwa mtizamo wangu, katiba mpya ni damu na moyo wa CCM kama kweli itataka kusalia madarakani.
 
Waikubali kwanza halafu waone kitakacho wakuta kwenye uchaguzi mkuu wa 2025! Yaani wakubali Katiba Mpya, na yenye Tume Huru ya Uchaguzi ndani yake!

Hakuna polisi wa kuingiza masanduku ya kura bandia, au kutimua mbio na kura za wapinzani!! Hakuna uvccm wanaoruhusiwa kuwatisha wapiga kura, huku wakijifanya eti ni tiss!!

Kudadek, saa mbili tu asubuhi!! Ccm chali!!!
 
Tatizo sio mama tatizo ni mfumo mzima wa CCM ni kama wamejitenga kabisa na mama kuna ambao bado wana maumivu ya meko yaani bado hawaamini.
 
Iko wazi kwa katiba hii tutakuja kupata dikteta uchwara mwingine ni suala la muda tu.

Hivi akina Kabudi hadi wanajikanyaga kwenye hotuba kumuita dikteta mheshimiwa mungu mnafikiri ilitokea bahati mbaya??


Rais amepewa mamlaka makubwa sana na hakuna control ya kumbana akikiuka
 
Waikubali kwanza halafu waone kitakacho wakuta kwenye uchaguzi mkuu wa 2025! Yaani wakubali Katiba Mpya, na yenye Tume Huru ya Uchaguzi ndani yake!...
Na hii ndo naona pia ni tatizo kwa CCM na viongozi wake, kitendo cha wao kuhisi kwamba CCM kama chama ni ideology ambayo inapaswa kulindwa ndo ambacho kinadumaza hii nchi. Mi kwa mawazo yangu, CCM has to die ili hii nchi itoke hapa ilipo. Kama ilivotokea Kenya kwa chama cha KANU, for good reason, na manufaa ya hii nchi.

Inatakiwa tufike mahali mtu kama NAPE yupo kwenye chama chake na mtu kama January yupo kwenye chama chake na wanapambana kwa hoja, hatutaki watu waendelee kujificha kwenye koti la U CCM hapo ndipo hii nchi itaamka.

Ingalikuwa nina say kwenye deep state ya hii nchi ningefanya namna CCM kama chama kife, kwa manufaa ya Tanzania
 
Tatizo sio mama tatizo ni mfumo mzima wa ccm ni kama wamejitenga kabisa na mama kuna ambao bado wana maumivu ya meko yaani bado hawaamini
Ndo mana mi huwa nahisi kama CCM imeshajeuka 'Doctrine' au 'Ideology' kitu ambacho sio sawa na ndo chanzo cha hii nchi kubaki nyuma.

'CCM has to die for this nation to rise' huu ndo ukweli mchungu ambao unatakiwa kuwa kweli
 
Tunadhani tunamsaidia Mama kumtamkia kuwa chama kinampongeza.Hali huku nje kuna gape kubwa sana.

KOSA KUBWA nikuanza kukutana na makundi yasiyounganisha Taifa.
Angeanza na vyama vya upinzani then makundi mengine,kwani kwenye makundi mengine kuna mchanganyiko.

Mwinyi Zanzibar alijua donda liko wapi,hakuangalia ukada.Ndio maana hakuna kelele kama huku bara.
 
Kikwete alikua anaona mbali sana legacy yake ya kuanzisha mchakato wa katiba itabaki kwenye kumbukumbu za nchi hii
 
Iko wazi kwa katiba hii tutakuja kupata dikteta uchwara mwingine ni suala la muda tu.

Hivi akina Kabudi hadi wanajikanyaga kwenye hotuba kumuita dikteta mheshimiwa mungu mnafikiri ilitokea bahati mbaya??


Rais amepewa mamlaka makubwa sana na hakuna control ya kumbana akikiuka
Nakubaliana na wewe, ila kwa namna mambo yanavoenda, kama katiba mpya haitapatikana ndani ya hii nchi ndani ya miaka 10 ijayo, ni ngumu sana ku guarantee kwamba hii nchi haitamwaga damu.

Fikiria taifa sasa lina watu karibu milioni 60, miaka 10 ijayo tunaweza fika milioni 70 au 80, hapo hapo kiwango cha umasikini bado ni kikubwa, halafu sehemu kubwa ya population ni vijana chini ya 30 years ambao wengi hawana ajira.... mimi naona kabisa kuna bomu ndani ya muongo mmoja unaokuja, wala sina shaka kuhusu hili.

Na triggers mojawapo ni suala la sheria na katiba mbovu, itakuwa ngumu sana kwa watanzania kuvumilia utawala mwingine wa mabavu. Never
 
Kikwete alikua anaona mbali sana legacy yake ya kuanzisha mchakato wa katiba itabaki kwenye kumbukumbu za nchi hii
Aliona mbali sana Kikwete sema bado ntamlaumu hakuwa imara kuhakikisha utawala wake katiba mpya inapatikana, naamini angeweza kushawishi lile kwa sababu hata ndani ya CCM kuna watu wana uchu wa mabadiliko ya kikatiba na kisheria. Mwana CCM gani anatamani atokee mungu mtu mwingine kama Jiwe? No-one
 
Hapana, lakini ukweli CCM wanakosa golden chance ya kuwa pioneer wa katiba mpya. Kuna baadhi wanaona umuhimu wa katiba mpya lakini wanakosa platform ya kusemea wanabaki kuwatumia watu wawasemee!
Tena kama kuna kipindi kizuri cha CCM ku pioneer katiba mpya, ni kipindi hichi ambacho Rais Mama Samia ameonekana kuungwa mkono na watanzania wengi, hii ndo ilikuwa point ya CCM ku win popularity ambayo its obvious imepotea lakini naona wao wenyewe wanajirudisha kwenye tope la kwamba CCM ni 'Doctrine na Ideology' ambayo lazima ilindwe.. kosa kubwa
 
Kikosi cha usalama wa chama ndio chanzo chakumharibia Mama
Nani ndo kiongozi wa hichi kikosi? anadhani kukataa katiba mpya Tanzania ndo kutasaidia CCM? Je, kwa miaka 10 ijayo ambayo nchi itakuwa na watu karibu milioni 70 na vijana wakiwa nusu yake, unadhani kweli CCM wataweza kuzuia mabadiliko? .. sidhani hata vyombo vya usalama vitataka ku face hiyo challenge.. ni ngumu sana aisee kuanzisha vita na watu wako wenyewe...
 
Nakubaliana na wewe, ila kwa namna mambo yanavoenda, kama katiba mpya haitapatikana ndani ya hii nchi ndani ya miaka 10 ijayo, ni ngumu sana ku guarantee kwamba hii nchi haitamwaga damu.

Fikiria taifa sasa lina watu karibu milioni 60, miaka 10 ijayo tunaweza fika milioni 70 au 80, hapo hapo kiwango cha umasikini bado ni kikubwa, halafu sehemu kubwa ya population ni vijana chini ya 30 years ambao wengi hawana ajira.... mimi naona kabisa kuna bomu ndani ya muongo mmoja unaokuja, wala sina shaka kuhusu hili.

Na triggers mojawapo ni suala la sheria na katiba mbovu, itakuwa ngumu sana kwa watanzania kuvumilia utawala mwingine wa mabavu. Never
Uko sahihi kabisa
 
Back
Top Bottom