Wewe huna ulijualo,si juzi tu hapa ulikua unaomba ushauri jinsi gani utaapply hiyo kozi sisi tunamshauri huyo MTU kwa sababu tupo kwenye hii kada na nafasi kwa Sasa chache..Kama unaona Kuna zahanati hizo ziko wazi na umesoma nenda kafanye kazi.
NB:Clinical officer ni kozi nzuri mno Ila Kuna Mambo hapa Kati Kati yametokea yameharibu ubora na thamani ya hii kozi.
1.Mrundikano na wa vyuo na kupunguzwa kwa vigezo vya kusoma hiyo kozi zamani ilikua DCC Ila Sasa DDD inaenda.
2.Serikali kukaa zaidi ya miaka 5 bila kuajiri Hali iliyosababisha mlundikano wa watahiniwa mtaani.
3.Vyuo vya private kufanya biashara kwenye mafunzo ya afya Hali inayofanya kuzalisha watu wengi wasiokuwa na sifa huku wale wenye sifa kuonekana wote sawa.
4.Kuongezeka kwa vyuo vinavyotoa ngazi ya digrii na kudahili watahiniwa wengi na wanaohitimu wengi pia.hivyo kufanya C.O awe wakawaida tu.
5.Kukua kwa teknolojia ambayo inamfanya daktari asiwe mtu muhimu Sana kwa asilimia fulani kwa baadhi ya magonjwa hasa Tabibu maana karibu ya magonjwa mengi watu wanayafahamu hata jinsi ya kutibu hivyo watanzania siku hizi kila mtu daktari na ukiona anaenda hospital Basi ameshindwa kujitibu.
Na nyingine nyingi ....
Kwa Sasa kozi ambazo bado Zina market kubwa kwa mtoto wa maskini ni hizi hawezi kukosa ajira Tena atakaa hospital za wilaya.
1.Nesi(hasa kwa wanawake)
2.Radiology
3.Dental
Hizo kozi MTU akishikwa Hana namna ya kukusaidia lazima apate msaada na ndio kwa Sasa Zina watu wachache 2&3.
Optemetry na Physiotherapy ni nzuri Ila hospital zinazotoa hiyo huduma ni chache utachelewa kuajirika tegemezi lako Itakua serikali Ila ukipata shavu utakaa sehemu nzuri.
Sent from my TECNO KD6 using
JamiiForums mobile app