Krismasi za kukumbuka (sad memories)

Krismasi za kukumbuka (sad memories)

Simulizi ya pili
Hii ni 1994. Nimefanya Kazi kwa mtu kule SABASABA mpaka tar.20.. Nikaambiwa mshahara tar 23.. Kumbe tajiri kajipanga kuondoka tar 22.. Nafika kwake tar 23 naambiwa kaondoka jana kwenda mkoani😭 sikuwa na pesa kabisa
Aliyenikoa ni bibi mmoja aliyekuwa anauza maji pale SABASABA (sikuwahi kumlipa wema wake ule) alinipa shiLingi 5000 ilikuwa kubwa sana kipindi Hicho
Sasa ni tarehe 23 natakiwa kusafiri tar 24 kwenda kijijini kwa ajili ya Xmas
Basi kujiongeza nikapata mchongo wa maembe huko Chanika Mvuti
Nikafanikiwa kupata 20 ya mkopo mahali.. Nikawa na 25 sasa.. Nikaenda zangu Mvuti
In short mpaka saa tatu usiku nilikuwa Buguruni na tenga langu la maembe nikiwa nimeshatumiq kama elfu 22 hivi gharama zote na matarajio ni kupata 45 hivi
Ugeni kwenye biashara jambo baya sana.. Nikaambiwa yale maembe yangu yanaweza kununuliwa kwa jumla elfu 25 tuu ama sivyo nikomae mwenyewe niuze mojamoja
Baada ya mabishano ya muda mrefu nikashindwa mimi inabidi nikubaliane nao
Sheshe likaja kwenye kuyamwaga chini yakaguliwe😭😭😭
1. Nilichomekewa maembe mabovu almost robo tenga
2. Waliweka majani mengi chini ya tenga..
Niliambulia Shilingi elfu 9000.tuu.

Hii sasa ndo ilikuwa komesha .
😤😢🤔
 
Daaaa! Nakumbuka miaka ya 2000 mwanzoni krismasi ndio inafika, mimi ni muajiriwa mahali fulani kipindi hicho. Halafu ndani naishi na mwanamke japo si wa ndoa na tuna mtoto mmoja. Sikukuu inafika sina kitu mfukoni na kazini hatujalipwa.

Sasa wife anasisitiza tununue chochote hata ikiwezekana tukope. Nikiangalia sioni shehemu ya kukopa. Nikamwambia wife kakope kwa mangi maharagwe tu leo tutakula tusubiri sikukuu ya mwaka mpya nitajipanga. Wife Kagoma hadi ikawa kelele ndani. Mara karopoka leo sili (mimi) na wala hapiki chochote.

Kumbe bwana mama mwenye nyumba alikuwa anasikiliza tu. Nilikuwa nimepanga nyumba tunaishi na mwenye nyumba nyumba moja kasoro vyumba tu, si unajua uswahilini.

Nikachukulia mzaha nikatulia ndani nacheki TV chaneli kama zote nabadili tu, sina ramani kabisa ya kutoka siku hiyo. Basi bwana mama mwenye nyumba kwa huruma zake kumbe kapika na ziada. Mida ya saa nane mchana nasikia anamwita wife. Hapo ni kwamba dogo (mtoto wetu) kakotogewa uji mchache asubuhi na mimi hata sikutaka kuuonja. Ndani kuna unga, mchele, viazi mviringo dagaa na mafuta ya kupikia. Mkaa upo na gesi tulikuwa nayo, kwa hiyo ilikuwa ni maamuzi tu ya wife kupika.

Wife katoka kwenda chumba cha mama mwenye nyumba, sikujua kaitiwa nini. Masikio hayana pazia bwana. Nikasikia akamwambia wife: NILISIKIA MABISHANO YENU NA MUMEO. KWA BAHATI MIMI NINA NAFASI KIDOGO NIMEAMUA NIONGEZE CHAKULA ILI NA NYIE MPATE JAPO SIKUKUU IENDE VIZIRI. LETA VYOMBO UPAKUE CHAKUALA HIKI HAPO KAMA UNAVYOONA.

Mara wife yuko ndani anachukua hotpot na mabakuli. Kaelekea kwa mwenye nyumba na baada ya mda karudi na pilau kuku, ndizi za kupika na kachumbari. Kaweka mezani wala hakunusemesha. Nami nikachuna tu. Kamwita dogo akasogea kampakulia chakuala, mimi nimekomaa na TV kama kipofu vile.

Kwa kweli nilijisikia aibu sana sana. Kuzuga nikajifanya naenda dukani kununua soda (nilichukua matupu manne). Sikupita kwa mangi nikala chocho nikatikeza mtaa wa pili. Nikaelekea kwa mshikaji wangu, yeye alikuwa bachela, hajaoa. Bahati nikamkuta nae kachili tu. Nikampa stori nzima.

Mwanangu akasononeka sana. Kaanza kunikumbusha mambo ya longi mara ooooo, huyo demu wako usingezaa nae tulukwambia sio wife material unaona sasa... Tukapiga stori pale za kutosha. Kumbe mwenzangu asubuhi kapiga zake supu hana shida.

Ikabidi nijikaze kiume, tena ukizingatia niko na mwana. Nikampa live sina hata jero na kazini hatujalipwa, tena sijala. Mwana akanielewa. Akasema kuhusu wife shauri yake... Akanitoa tukaenda kupiga kitimoto choma bwana... Baada ya hapo gambe likaanza hadi saa tano usiku nakumbuka nyumbani. Hapo simu nilizima ttka mchana. Kurudi home wife kafungua mlango mimi direct kitandani hakuna neno hata moja. Kesho yake wife anaomba msamaha. Nikaona isiwe tabu ni maisha tu nikammsamehe.
Alizingua tuu huyo na msosi upo ndani,

Saa hz nimegonga ugali dagaa hapa sina wasiwasi mimi....

Kufatisha sikukuu kama nipo childhood hpn aseeh.....
 
Acha tu mkuu. Yaani kula ugali dagaa sikukuu inaonekana dhambi au mateso fulani
kaka nimetoka kula hapa kwani nimeulizwa? Hapana nimesema mwenyewe

Miaka hii 20+ siwezi kwenda kwa mtu na kuanza kujichekesha mara hivi mara vile, siwezi wana bajeti zao....

Nasubiri jioni ifike nikale chochote ninachomudu basi maisha yaendelee mkuu,

Sipo kwenye nafasi ya kumfurahisha yeyote kisa ni sikukuu au la...
 
Kuna Christmas moja niliilia kwenye kota za police, sitosahau. Ilikuwa napenda sana kwenda kusherekea Christmas na mwaka mpya kwa bibi ifakara. Sasa kipindi hicho hakuna usafiri zaidi ya train ya tazara. Hakuna barabara za kueleweka dar-ifakara unaweza hata tumia wiki kwa gari. Tar 24 nikapandishwa train nakumbuka nilikuwa mdogo saana ila kuna mtu nilikabidhiwa anishushe ifakara pale nitapokelewa na bibi. Sijui nilijichanganya vipi nikapoteana naye kwenye train, na safari ilikuwa usiku. Chuma imetembeeaa, kumbe nimepitiliza kituo nikaja kuuliza kumbe tumeshapita kama vituo vitatu nyuma almost 80kms, usiku kama wa saa saba. Abilia wakamwambia TTE, anishushe sehemu inaitwa mngeta. Ni giza sijawahi ona mvua inanyesha. Nimeshikilia mikate ambayo nilimbebea bibi.
Kile kisehemu ni mji mdogo sana, train ilivyoondoka watu wote wakapotea nikabaki nimekaa karibu na ofisi ya mizigo nalia tu. Akaja askari mmoja sijui wa tazara yule, nikamuelezeaa. Akanichukua akanipeleka kwake nalia tu hata kula sili, nimekumbatia mikate yangu. Simu hakuna ikabidi kesho yake wakatumia zile simu za tazara kupiga ifakara wakaunganisha na simu za posta, ndo nikaongea na bibi hiyo ilikuwa next day jioni. Watoto wakawa wamenizunguka wananishangaa tu nimepotea.
Nilikataa kula chakula chao nilikula tu mkate kidogo, jioni wakanipeleka kanisani (catholic) lipo milimani hivi. Kule nilibahatika kuna gari ya mapadre lilikuwa linaenda ifakara kesho yake.
Nilifika kwa bibi nimechoka sana na mikate imeharibika. Ile Christmas ilikuwa ya mateso sana kwangu
Hadi huruma
 
kaka nimetoka kula hapa kwani nimeulizwa? Hapana nimesema mwenyewe

Miaka hii 20+ siwezi kwenda kwa mtu na kuanza kujichekesha mara hivi mara vile, siwezi wana bajeti zao....

Nasubiri jioni ifike nikale chochote ninachomudu basi maisha yaendelee mkuu,

Sipo kwenye nafasi ya kumfurahisha yeyote kisa ni sikukuu au la...
Umekua.Ingekuwa siku zile za utotoni ungemvunja mtu mguu kwa kilio cha kulilia ubwabwa.
 
Christmas ya 2006, niko ugenini kwa jamaa zangu flani,mchana ukapita empty halijarushwa,kufika jioni bado naona kimya na ndio kwanza mke wa jamaa kalala zake chumbani tu,ikabidi nijiongeza nikazama kwa mama ntilie nikajitetea na chapati maharage afu nikakausha,baadae kwenye saa 2 usiku ndo mwenyeji wangu akanichana kuwa wamezinguana na mkewe hivyo mkewe kagoma kupika,nikamwambia haina neno tukazama chimbo na jamaa tukapiga mdudu then tukarudi home kwa jamaa kila mtu akaenda kulala.
 
Christmas ya 2006, niko ugenini kwa jamaa zangu flani,mchana ukapita empty halijarushwa,kufika jioni bado naona kimya na ndio kwanza mke wa jamaa kalala zake chumbani tu,ikabidi nijiongeza nikazama kwa mama ntilie nikajitetea na chapati maharage afu nikakausha,baadae kwenye saa 2 usiku ndo mwenyeji wangu akanichana kuwa wamezinguana na mkewe hivyo mkewe kagoma kupika,nikamwambia haina neno tukazama chimbo na jamaa tukapiga mdudu then tukarudi home kwa jamaa kila mtu akaenda kulala.
Kimyakimya halafu kibabe sana😀💪🏿💪🏿💪🏿
 
Alizingua tuu huyo na msosi upo ndani,

Saa hz nimegonga ugali dagaa hapa sina wasiwasi mimi....

Kufatisha sikukuu kama nipo childhood hpn aseeh.....
Ni katika kufurahi tu mkuu, wala sio kama unafanya utoto.

Mimi huwa nafurahi sana sikukuu inikute niko kwetu, home watoto ni wengi, watoto ni chachu/chachandu/kachumbari ya sikukuu yoyote.
Bila watoto sidhani kama sikukuu zitanoga.

Mwaka huu nipo kama Poor Brain tu, sina furaha, naangalua tu videos nazotumiwa toka home wanavyoenjoy, mnyama kachinjwa, nyomi la kuzidi watoto, watu wazima mpaka wazee.
 
Simulizi ya pili
Hii ni 1994. Nimefanya Kazi kwa mtu kule SABASABA mpaka tar.20.. Nikaambiwa mshahara tar 23.. Kumbe tajiri kajipanga kuondoka tar 22.. Nafika kwake tar 23 naambiwa kaondoka jana kwenda mkoani😭 sikuwa na pesa kabisa
Aliyenikoa ni bibi mmoja aliyekuwa anauza maji pale SABASABA (sikuwahi kumlipa wema wake ule) alinipa shiLingi 5000 ilikuwa kubwa sana kipindi Hicho
Sasa ni tarehe 23 natakiwa kusafiri tar 24 kwenda kijijini kwa ajili ya Xmas
Basi kujiongeza nikapata mchongo wa maembe huko Chanika Mvuti
Nikafanikiwa kupata 20 ya mkopo mahali.. Nikawa na 25 sasa.. Nikaenda zangu Mvuti
In short mpaka saa tatu usiku nilikuwa Buguruni na tenga langu la maembe nikiwa nimeshatumiq kama elfu 22 hivi gharama zote na matarajio ni kupata 45 hivi
Ugeni kwenye biashara jambo baya sana.. Nikaambiwa yale maembe yangu yanaweza kununuliwa kwa jumla elfu 25 tuu ama sivyo nikomae mwenyewe niuze mojamoja
Baada ya mabishano ya muda mrefu nikashindwa mimi inabidi nikubaliane nao
Sheshe likaja kwenye kuyamwaga chini yakaguliwe😭😭😭
1. Nilichomekewa maembe mabovu almost robo tenga
2. Waliweka majani mengi chini ya tenga..
Niliambulia Shilingi elfu 9000.tuu.
Bibi muuza maji akakupa 5000. Mwka 1994.
 
Back
Top Bottom