hivi kumbe mazungumzo yote kwenye zile threads unakuwa uko serious>?? kama ni hivyo naomba unisamehe sana. Siipendi hii sifa. nilifikiri ni sehemu ya kutaniana hapa jamvini pamoja na kujifunza.
Ila kama ndo umeona hivyo, kwa kweli sijapendezwa na hiyo sifa..unisamehe sana. Samahani kwa yote!
Swali langu lilikua Na huo UPENDO ukikosekana?
. . . . . . . . . kila mmoja anaweza akapata mwenza mwingine wa nje ya ndoa na akazaa nae kutokana na utengano wao . . . . . .
Labda kama ni ndoa ya kiislam, kiserikali ama kipagani. Kama ni ndoa ya kikristo hakuna kuachana hata hiyo 'kisheria' waliyoisema wachangiaji wengine hapo juu. Mkioana ndio 'ntolee hiyo', labda mmoja wenu afe. Au pengine uamue kubadili dini!
Hivi mkuu tushukulie umeoa ukiwa na miaka 26 ndowa yenu haikudum hata mtoto hakujaliwa kupata inakuwaje na hamruhusiwi kuowa tena mpaka afe mmojawenu na hafi mpaka unaanza kupinda mgongo itakuwaje hapo?
We unauliza swali ambalo majibu hayatakusaidia, ulipaswa kutuuliza kama unataka kuolewa na mtu mwenye ndoa au kuoa mke wa mtu unataka tukusaidia kisheria utaratibu unakuwaje. Sasa umejua hawajaachana ni mke au mume inakusaidia nini? Maswali ya huyu ni mbuzi au kondoo wakati unaona hayasaidii.
sheriia ni ile ile, ukikaa na binti kwa miezi mitatu ni mke, na ukitengana na mke au mume nonstop for 3 month hakuna ndoa hapo.
Aunt we kula kwa raha zako, kikubwa jua msimamo wa mwenzio. asiwe kigeugeu.
sheriia ni ile ile, ukikaa na binti kwa miezi mitatu ni mke, na ukitengana na mke au mume nonstop for 3 month hakuna ndoa hapo.
Aunt we kula kwa raha zako, kikubwa jua msimamo wa mwenzio. asiwe kigeugeu.
Sasa kwanini waishie kutengana kama wanataka kua na watu wengine?Si waachane kabisa!!!
Nadhani Mkuu ameelezea kwa namna nyingine ambayo nafikiri umeelewa.
Mimi pengine sijakuambia ya kwamba nilikuwa naongelea ndoa za kikristo ambazo sisi wakristo tunasema KILICHOUNGANISHWA NA MUNGU BINADAMU HAWEZI KUKITENGANISHA. Kwa kifupi, kwenye ndoa ya kikristo hakuna kuvunja ndoa, ni kifo tu pengine na kubadili dini. Kwa ndoa hizo za aina nyingine sina mchango maana sizijui zilivyo.
So here it is dear....
Mathayo 19 kwanzia mwanzo Yesu anaongelea jinsi ambavyo kilichounganishwa na Mungu mwanadamu asikitenganishe....ila mstari wa 9 unasema :Nami nawaambia ninyi,Kila mtu atakae mwacha mkewe isipokua ni kwasababu ya uasherati akaoa mwingine, azini, naye amuoae yule aliyeacha azini.
Kumbukumbu la torati 24:1-2 inasema....Mtu akiisha twaa mke kwa kumuoa, asipopata kibali machoni mwake kwa kua ameona neno ovu kwake na amwandikie hati ya kumwacha, akamtilie mkononi mwake na kumtoa katika nyumba yake.Naye akiisha kuondoka katika nyumba yake ana ruhusa kwenda akawa mke wa mtu mwingine.
Zipo sehemu nyingine zinazoongelea hivi vitabu viwili vinaelezea vizuri zaidi!!Alafu kote wanasema kwamba imeruhusiwa kwasababu ya ugumu wa moyo wa mwanadamu!!
Lizzy na hayo ndo makosa makubwa sana ambayo huwa tunayafanya.X anaachana na Y kisha hawaendi mahakamani kuomba talaka.X anavuta kimwana mpya anaishi naye.Jamii nzima inawatambua kuwa ni 'mke' na 'mme'.Wanazaa watoto,wanalea na wakati huo huo wanafungua biashara wanajenga ,mradi maisha yanakuwa muruuuwa. Siku ya siku tena ghafla bin vuu mme ndee presha anadondoka chini na kurudi kwa muumba wake.Pekua pekua makabrasha mzee hakuacha mirathi.Hapo ngoma inogile maana so called ex-wife atatinga msibani na cheti chake cha ndoa, utake usitake yeye na wanae watarithi kila kitu na huyu aliyetafuta mali na marehemu ataambulia sifuri na wanae,law is an ass,mambo ya sheria hayo! Ushauri wa bure njemba/dem akikuzengua tafuta makaratasi kabisaa mahakamani,ikitokea baby come back hakuna kizuizi kaoaneni upya kwa DC.
Lizzy.... run away fast... they are tracking each other .... ni hatari sana couple za aina hiyo, jamaa akikukuta atajua kuwa wewe ndio kududumtu, ulikuwa benhind their separation. Do not be a victim...
Hivi kin'asti ukitokewa na mlugluga hana kitu inakuwaje hana mali lakini anaweza kuwa na mapenzi ya kweli kama mimi
Hahahhahaha.....Okada bwana!!</p>
<p>Owkey ngoja nichape mwendo fastaaaaa!