Kuagiza gari hadi kulipia kodi ya bandari

Kuagiza gari hadi kulipia kodi ya bandari

Premij canoon

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2018
Posts
1,203
Reaction score
2,771
Habari wakuu. Bila shaka nyote ni wazima na mishe mishe zinaendelea kama kawaida. Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu uagizaji wa magari.

Internet imerahisisha sana shughuli za binadamu, leo hii mtu unaweza kuagiza chochote kupitia mtandao tu. Kumekuwa wimbi kubwa la madalali wanaojihusisha na biashara ya uagizaji magari na wameweka utaratibu wa kulipa kwa awamu na wao wanatumia mtandao huo huo ambao yeyote anaweza kuutumia na ukaagiza gari yako (wameona fursa na wanaitumia vizuri, pongezi kwao)

Shida au changamoto ambayo inatukwamisha wengi ikiwemo na mimi ni zile hesabu za TRA kama ushuru na tozo za bandari ambazo kwa fununu kadhaa nilizopata ni kuwa tozo zote za gari husika zimewekwa mwenye site ya TRA, ambapo yeyote anaweza kukamilisha na akaitoa gari yake bila kupitia mtu wa katikati.

Naomba kwa yeyote mwenye ufahamu juu ya haya basi atupe ABC's za kufanya ili kukamilisha zoezi lote kuanzia kuagiza hadi ushuru na kulitoa gari lako bandarini ili wengi ambao hatufahamu nasi tuweze kufahamu. Nafahamu JF ni jukwaa kubwa lenye wataalamu wa fani za kila aina na natumaini watajitokeza watu wenye uzoefu wa hili. Natanguliza shukraan.

Nawasilisha.
 
Suala la kuagiza gari nje kwa njia ya mtandao ni rahisi sana kama utatumia makampuni yanayotambulika kama Beforward, SBT Japan, Autocom Japan, Autorec na mengineyo.

Ingia kwenye moja ya makampuni hayo, tafuta gari unalotaka. Ukilipata, tambua bei yake kwa CIF (gharama za gari hadi linafika bandarini Dar). Baada ya hapo, ingia kwenye website ya TRA ( Used Motor Vehicle Valuation System - Used Motor Vehicle Valuation System ) itakupa mwogozo jinsi ya kuingiza taarifa za hilo gari, mwisho unabofya 'calculate', unapata jumla ya ushuru unaotakiwa.

Ni ngumu kukufundisha kila kitu hapa. Utaweza kwa kujizoeza kufanya haya niliyokuelekeza.

NB: hakikisha ukifungua na kupata ushuru wa gari, kwenye hizo hesabu za TRA, angalia kitu kinaitwa customs value CIF (hii ni kama bei elekezi ya hilo gari). Hakikisha bei ya gari (CIF), haizidi hiyo customs value CIF ya TRA. Ikiizidi, jua utalipa kodi kubwa zaidi.
 
Kuongezea alichokiandika ilonga inabidi uelewe utaratibu na hatua zifuatazo.

1. Kuchagua aina ya gari mtandaoni, hii inajumuisha kujua jumla ya gharama za gari pamoja na kulisafirisha hadi bandari husika uliyopo.

2. Kufanya hayo malipo kwa kampuni husika inayouza magari. Hadi hapo unatakiwa iwe umeshafamu makadirio ya gharama za kodi unazotakiwa kuzilipia. Hii ni kwa msaada wa tovuti ya TRA.

3. Gari ikishapakiwa, unatumiwa documents za gari yako. Unaziingiza kwenye mfumo wa TRA meli ikishafika unapatiwa mskadirio ya kodi unaenda kulipia bank.

4. Ukimalizana na TRA, unaenda hatua ya mwisho ya kulipia gharama za matumizi ya bandari na yozo zake. ( Hapa kama umetumia waksla/agent anaweza kukamilisha zoezi lote hadi gari kutoka akajumlishia na gharama za uwakala)

Baada ya hapo ni kujimwambafai ila hatujaongelea Bima.
 
Suala la kuagiza gari nje kwa njia ya mtandao ni rahisi sana kama utatumia makampuni yanayotambulika kama Beforward, SBT Japan, Autocom Japan, Autorec na mengineyo.

Ingia kwenye moja ya makampuni hayo, tafuta gari unalotaka. Ukilipata, tambua bei yake kwa CIF (gharama za gari hadi linafika bandarini Dar). Baada ya hapo, ingia kwenye website ya TRA ( Used Motor Vehicle Valuation System - Used Motor Vehicle Valuation System ) itakupa mwogozo jinsi ya kuingiza taarifa za hilo gari, mwisho unabofya 'calculate', unapata jumla ya ushuru unaotakiwa.

Ni ngumu kukufundisha kila kitu hapa. Utaweza kwa kujizoeza kufanya haya niliyokuelekeza.

NB: hakikisha ukifungua na kupata ushuru wa gari, kwenye hizo hesabu za TRA, angalia kitu kinaitwa customs value CIF (hii ni kama bei elekezi ya hilo gari). Hakikisha bei ya gari (CIF), haizidi hiyo customs value CIF ya TRA. Ikiizidi, jua utalipa kodi kubwa zaidi.

IMG_7423.JPG


Naomba kuuliza hapa kidogo mkuu.. Bei halisi ni hio yenye rangi nyekundu au kijani?
 
View attachment 1250252

Naomba kuuliza hapa kidogo mkuu.. Bei halisi ni hio yenye rangi nyekundu au kijani?
Ni hiyo nyekundu (CIF). Kwenye website ya SBT Japan nadhani wanaiita CRF kama sijakosea. Hiyo inajumuisha gharama zote (bei ya gari, shipment, insurance, na inspection)za kulifikisha gari bandarini kabla hujalipa ushuru TRA.
 
Kuongezea alichokiandika ilonga inabidi uelewe utaratibu na hatua zifuatazo.

1. Kuchagua aina ya gari mtandaoni, hii inajumuisha kujua jumla ya gharama za gari poja na kulisafirisha hadi bandari husika uliyopo.

2. Kufanya hayo malipo kwa kampuni husika inayouza magari. Hadi hapo unatakiwa iwe umeshafam makadirio ya gharama za kodi unazotakiwa kuzilipia. Hii ni kwa msaada wa tovuti ya TRA.

3. Gari ikishapakiwa, unatumiwa documents za gari yako. Unaziingiza kwenye mfumo wa TRA meli ikishafika unapatiwa mskadirio ya kodi unaenda kulipia bank.

4. Ukimalizana na TRA, unaenda hatua ya mwisho ya kulipia gharama za matumizi ya bandari na yozo zake. ( Hapa kama umetumia waksla/agent anaweza kukamilisha zoezi lote hadi gari kutoka akajumlishia na gharama za uwakala)

Baada ya hapo ni kujimwambafai ila hatujaongelea Bima.

Asante mkuu kea kushare ila naomba kuuliza tena...

2. kufanya malipo kea kampuni husika inayouza gari. je haya malipo nayafanyia kwa bjua gani?

3. Gari ikishapakiwa kwenue meli ntatumia documents za gari yangu. JE hizi document zitatumea kwa EMAIL ?

4. hivi nikishamalizana na TRA kuna malipo mengine tena ya bandari? inamaana ile kodi ya TRA haihusiki na bandari?

Ni hayo tu mkuu
 
Asante mkuu kea kushare ila naomba kuuliza tena...

2. kufanya malipo kea kampuni husika inayouza gari. je haya malipo nayafanyia kwa bjua gani?

3. Gari ikishapakiwa kwenue meli ntatumia documents za gari yangu. JE hizi document zitatumea kwa EMAIL ?

4. hivi nikishamalizana na TRA kuna malipo mengine tena ya bandari? inamaana ile kodi ya TRA haihusiki na bandari?

Ni hayo tu mkuu


Malipo unaenda kulipia Bank kiasi sawa na bei ya gari CIF. Hapo watakutumia Proforma Invoice ndio iwe kiambatanisho cha kukusaidia kufanya malipo.

Gari ikishapakiwa kwenye meli inamaana jina la hiyo meli litakua tayari linajulikana, gari imeshafanyiwa ukaguzi, unaweza kuifuatilia meli kwenye mtandao safari yake hadi siku inatia nanga na kushusha mzigo. Documents wanakutumia softcopy kwa email lakini original nazo zinatumwa kwa DHL au kampuni yeyote ya kutuma vifurushi kwa njia haraka.

Bandari (TPA) na TRA ni vitu viwili tofauti.
TRA watashughulikia kodi zote na usajili wa kari yako. Baada ya kumalizana na TRA, mfumo utaruhusu mchakato wa kuruhusu gari itoke kukupa makadirio ya kiasi unachotakiwa kuwalipa bandari ili gari yako itoke. Lakini mara nyingi hapa gharama sio kubwa sana.
 
Na kwa mfano ukiwatumia beforward wanakipengele cha clearance inamaana hutadeal na watu wa TPA si ndio?

Uko sahihi, ukishalipia kodi zote na usajili. Beforward watamalizana na TPA na kuitoa gari yako.

Watakupa invoice ukalipe jumla ya gharama zao na zile za TPA.

Hapo utakabidhiwa gari yako ikiwa na namba zake kila kitu.
 
Back
Top Bottom