Uchaguzi 2020 Kuambiwa kwamba si Raia wa Tanzania, ni kashfa kubwa kwa Tundu Lissu na familia yake

Uchaguzi 2020 Kuambiwa kwamba si Raia wa Tanzania, ni kashfa kubwa kwa Tundu Lissu na familia yake

Mzee wa lupaso alituwekea dereva feki dereva kanjanja abiria wamegutuka wameingizwa Chaka miba.
 
Hiyo ni mbinu ya kijinga na chafu ya Serikali ya Awamu hii iliyotumika sana miaka 5 iliyopita ikiwa na nia ya kuwanyanazisha wapinzani au wakosoaji lakini mara nyingi imeshindikana kwa kukosa ushaidi. Wananchi wengi sana wanaishi nchini passport zao zikiwa zinashikiliwa na Serikali kwa madai kuwa watu hao si Raia na uchunguzi utaendelea miaka baadaye kimyakimya hurudishiwa passport zao lengo likiwa limetimia lakini wahusika wakiwa wamepoteza kila kitu. Wameona anakuja vibaya kwa upande wao kwenye kampeni wanatafuta njia ya kumuengua kwa kutumia kila mbinu chafu kama hiyo pia ameitwa afike mbele ya kamati ya maadili kujibu tuhuma zisizowekwa bayana. Toka kampeni zianze wamekuwa wakimshutumu kuwa anatumia lugha za matusi lakini hakuna anayetaja matusi hayo na lini na nani anatukanwa. Mwezi mmoja wa kampeni imekwisha salama waelewa wanafurahi lakini wa upande wa pili hawapendi kuona yanayoendelea wanaanza kutumia vyombo vya dola kufanya chokochoko ili kupunguza au kusitisha kabisa kasi ya kampeni ya Mgombea wa Upinzani. Mgombea wa Upinzani anakubalika sana na wananchi na Serikali inachofanya kujaribu kumuengue ili mgombea wao apite kwa urahisi ni hatari sana inaweza ikaleta machafuko yakashindikana kuzimwa. Mpaka sasa Polisi wamefanya kazi nzuri sana kwa kutokuelekea upande mmoja kama ilivyo kawaida yao ingawa wachache imewagharimu na tunawapa pole na kuwaomba waendelee kulinda raia na mali zao. Mh. Lissu unaifahamu sana Serikali hii na wa Serikalini keep your distance but never surrender you are the only hope. Wishing you all the best as you face Pharaoh!

Hawawezi faulu Hilo October maamuzi ni mawili kurudi Chato au kwenda the Hague achague kipi rahisi kwake.
 
Nchi hii tuna watu wa ajabu sana na mtaji wa CCM bado ni propaganda kama hizi za mabeberu, kibaraka na siku hizi za ushoga.

Nimewahi kumsikia mtu mzima ninayemuheshimu akikubaliana na tuhuma kama hizi dhidi ya Lissu.

Mwingine niliwahi kumsikia akiniambia eti waliompiga risasi Lissu hawakuwa na nia ya kumuua.

Kumkomboa Mtanzania kutahitaji nguvu ya ziada.
Inahitaji nguvu ya mabavu kumtoa mtanzania kwenye utumwa wa upumbavu na mawazo
 
Mbelgiji amekuja kuhakikisha amani yetu inaondoka yaani yeye kila akisimama jukwaani hana kauli za amani ni Shari tu,

Mara ooh patachimbika,

Kitaeleweka,

Tutaingia barabarani,

Tutawapeleka ICC.

Huyu mtu ana matatizo sio bure.
Atawapa stroke kweli, Mungu wa haki yupo!!!
 
Mkuu wala siyo ajabu yeyote naye dai haki na kutishia uwepo wa CCM huwa anapewa tuhuma hizo.
Na hio imewaathiri sana wakazi wa mikoa ya Kigoma, Kagera na Mara ambao mitazamo yao inapingana na ile ya chama tawala. Kumbuka yaliyompata askofu Severine Niwemugizi wa jimbo la Rulenge Ngara, alipokosoa utawala huu akaambiwa apeleke credentials za kuonesha uraia wake.
 
Kuhisiwa pekee kwamba yeye na familia yake si raia tena wa Tanzania kwa hakika si jambo la kupuuzwa na kwanza na yeye Tundu na pia vyombo vya Dola.

Tundu Lissu anapaswa mara moja alitolee ufafanuzi suala hilo na tena kwa ushahidi.

Pili vyombo vya Dola vimchunguze Tundu Lissu kama ni kweli si Mtanzania tena ili mara moja hatua stahiki zichukuliwe.
Niliwahi kutoa Uzi wangu.Nikiomba Tindu Lissu ,ajibu hii tuhumu ,hapa JF.Kwani naamini yupo.Kwa kuambiwa kuwa si RAIA.Ili kuweka mambo sawa.Baada ya Katambi kudai hivyo.Na Lissu kukaa kimya.Lakin MODS waliondoa Uzi huo Mara moja.So kuelewa kwanini walifanya hivyo.
 
Mbelgiji amekuja kuhakikisha amani yetu inaondoka yaani yeye kila akisimama jukwaani hana kauli za amani ni Shari tu,

Mara ooh patachimbika,

Kitaeleweka,

Tutaingia barabarani,

Tutawapeleka ICC.

Huyu mtu ana matatizo sio bure.
Huyu katumwa na Mungu kuja kutukomboa Watanzania kutoka mikononi mwa wakolini weusi(ccm). Pia Jiwe katumwa na Mungu kuiua ccm

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
sio kashfa ni porojo za kisiasa ambazo hazimsaidii mtanzania maskini
 
Huu uzi unakiri kwamba serikali ya magufuli ni dhaifu katika nyanja mbalimbali ikiwemo intelijensia. Mbali na kutojua nani anaua watanzabia coco beach intelijensia yake hainaweza kubaini mhamiaji haramu hadi kapewa nafasi ya kuombea urais. Shame!!
 
Hata kama angekuwa ameseek asylum bado ni Mtanzania..mataga jiandaeni kisaikolojia 28/10
 
Back
Top Bottom