kichongeochuma
JF-Expert Member
- Jan 21, 2024
- 1,669
- 2,864
Nimekuja mbio nikijua MAGAMBA MATATU kaja na jambo jipya kuelekwa 2025 😒
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tisi nakuona unasaka Umbea ukashtue wanao watutimbie.JPM hakuwahi kuwa dikteta
ukitaka kumuua umbwa mpe jina bayaJPM hakuwahi kuwa dikteta
Kwa taarifa yako huyo Lowassa huko cdm alivamia treni kwa mbele. Baada ya uchaguzi wa 2010, cdm ndio chama kilichofanya kazi ya kisiasa kuliko chama chochote cha kisiasa. Ndio chama kilichoanzisha operations nyingi za kisiasa zilizopandisha hamasa za kisiasa hapa nchini. Watu walijiandikisha kwa wingi kupiga kura tena kwa hasira licha ya vikwazo vingi, wakijua fika ccm watamchagua Lowassa kuwa mgombea wao ili wamchinjie mbali. Umesahau neno vitambulisho vya kura kuitwa vichinjio?Umeandika mambo mengi sijaona ukimtaja Lowasa na hiyo ndiyo tabia yenu ninyi wafia vyama haijalishi mpo chama gani, muwe unaheshimu mchango wa watu. Uchaguzi wa 2015 ni dhahiri ulikuwa ni wa watu wawili wenye ushawishi na wala haukuwa na ushindani wa kivyama. JMP alivutia wapiga kura kutokana na record yake ya utendaji, Lowasa alivutia wapiga kura kutokana na umaarufu wake so usileta fact za uongo humu kuwa Chadema au ccm ilivutia wapiga kura. Wapiga kura wanavutiwa na aina ya wagombea na sio vyama vya siasa japo navyo vina nafasi yake kiasi fulani.
Mahaba niue.JPM hakuwahi kuwa dikteta
Unaamini udikiteta ni kile ukichosoma shule yako ya KATA shule unaenda na Ufagio..Choo cha shimo.Huujui udikteta kaa kimya kula bata uwezavyo.kama umeiona awamu ya tano ndio ya kidikteta rudi shule kasome uelewe vzr then njoo utuandikie tena, CCM ndio hii bado inatuongoza.
Mwamba ulipiga mulemule!Kwa nini nimeamua kusema hivi? Kuna mambo matano (5) makuu yananilazimisha kusema kuwa:
"Tanzania itatawaliwa kidikteta"Ni vigumu sana kwa mtu asiyeona mbali kunielewa kirahisi na pia ni rahisi sana kwa anayependa demokrasia kunibeza na kuniona kama naota.
1. Kwanza kuna uwezekano mkubwa Rais ajaye ataingia madarakani kwa utata nikimaanisha kutakuwa na mizengwe katika utoaji wa matokeo kwani hali halisi inajionesha wazi kuwa kuna mvutano mkubwa wa vyama viwili na hakuna kinachokubali kuwa kimeshindwa ki-haki.Endapo mgombea wa chama tawala akashinda basi chama kikuu cha upinzani kitatumia nguvu ya umma ili kupata sapoti wakati aliyejiona kashinda kwa haki atakimbilia ikulu na kushawishi dola kulinda ushindi wake kadri wawezavyo.Tukumbuke yaliyozikumba nchi za :LIBYA, IVORY COAST, LIBERIA, NIGERIA, ZIMBABWE, KENYA, VISIWA VYA COMORO, MISRI na TUNISIA.
2. Pili ni ahadi atakazozitoa hususani zile za kushughulikia "MAFISADI". Ili kupambana na aliyekuzidi kifedha lazima uchukue fedha zake kwa nguvu hivyo atataifisha mali za waliosemekana ni wahujumu uchumi au mafisadi. Akiwa yupo kwenye hali hiyo lazima watamwinda hivyo itamgharimu kuwa dikteta katika kupambana na mafisadi ikiwa ni pamoja na kunyonga baadhi yao ili kuweka fundisho. Pia atajikuta analipa kisasi cha mateso yote yaliyompata katika harakati za kuingia ikulu.
3.Suala zima la maendeleo haliendani na kuwapa watu uhuru wa kukaa mijini na kuendeleza masuala kama ya kupiga debe, kutembeza vitu mijini, kuuza na kula madawa ya kulevya, polisi wa barabarani kupokea rushwa, maafisa wa TRA kusamehe kodi na kutoa vibali kwa njia za panya, viongozi wa serikali kutumia ofisi zao kama kampuni zao! Yote haya yatasababisha rais ajaye awe dikteta na mkatili kwa wazembe wote wanaokwamisha matarajio yake, ikiwa ni pamoja na kuwafurutisha vijana wote mijini na kuwafukuza kazi wazembe wote.
4. Suala zima la ushawishi wa dini, endapo ataegemea dini moja basi atajikuta yupo kwenye wakati mgumu kwani atajikuta amegeuka gafla na kuwa adui wa dini nyingine hivyo kujikuta akichukua maamuzi ya kibabe ili kukabiliana na upinzani kutoka dini fulani. Suala kujiunga na dini ya mashetani au "FREEMASONS" litakuwa jambo la kawaida na watu wengi wenye kupinga serikali watatoweka na wasijulikane wapo wapi.
5.Ushawishi wa nchi za magharibi; hili nalo ni tatizo ambalo nitafanya nchi isitawalike endapo Rais ajae ataamua kufuata matwakwa ya raia wake kwenye masuala la uwekezaji, ajira, ugawaji wa ardhi, kodi, na utaifishaji wa mali za umma kama viwanda, mashamba makubwa, n.k.na endapo atawageuka wananchi na kusikiliza matakwa ya nchi za magharibi basi atajikuta amepitisha sera ya ndoa za jinsia moja, biashara haramu ya siaha, urutubishaji wa nyuklia. Hali hii itapelekea wanachi waanze kumchukia na atajikuta anatumia nguvu za dola kulazimisha wananchi wakubali sera zake.
Pia kuna mambo mengine kama kuibuka vyama vya siasa vyenye nguvu vinavyotaka kumtoa madarakani kwa nguvu na atajikuta akiwasweka rumande wapinzani wengi ambapo itachafua hali ya hewa ya nchi. Pia utata wa mgawanyiko wa wabunge maana kuna kila dalili vyama viwili vyenye ushindani kugawana sehemu kubwa ya idadi ya wabunge na hivyo kumlazimisha Rais kuwa na wakati mgumu wa kuvunja bunge zaidi ya mara moja kwenye kipindi cha miaka mitano.
Pia suala la ajira litaendelea kutesa nchi na ongezeko la wasomi itakuwa pia tatizo hivyo itamlazimu kutumia sheria kali na za kibabe ili kuendesha utawala wake.
Vyombo mbalimbali vitanyimwa uhuru wa kutoa mawazo yao hii itapelekea vyombo vya habari vya magharibi kumuulika nchi na hivyo hali kuwa mbaya zaidi.
Swali la kujiuliza, Rais ajaye atakuwa nani ?
Ni vigumu kupata jibu la moja kwa moja ingawa watu wengi wanatazamia kuona sura mojawapo kati ya hizi:
- Zito Kabwe,
.
- Dr. Willbrod Slaa,
- Dr. Asha Rose Migiro,
- Edward Lowassa.
- Samwel Sitta
- Prof. Ibrahim Lipumba.
- Bernad Membe, na
- John Pombe Magufuli
Kwanini Watanzania wengi wanategemea kati ya watu hawa mmoja wapo atakuwa Rais wa Tanzania mwaka 2015?
Jibu kubwa na la msingi ni suala zima la uwajibikaji na kujituma.
Kwanini nasema hivyo?
Ukiangalia sura zote ni watu wachapa kazi, wanajituma na wenye maamuzi magumu kwa masuala nyeti ya nchi. Ingawa kila mmoja ana mapungufu yake lakini ukweli bado unabaki pale pale wanauwezo mkubwa wa kulifikisha taifa pale Watanzania wanapotaka ikiwa watatekeleza majukumu yao ipasavyo.
Bado suala la wapinzani kuungana na kumsimamisha mgombea mmoja litakuwa ni ndoto. Kwanza utofauti wa sera na mawazo yao vinakinzana. Pia kuna suala zima la itikadi ya chama na mitazamo. Wapinzani wamejifunza mengi kutoka kwa jirani zao Kenya. Hivyo hawapo tayari kuungana na kuanza kung'ang'aniana madaraka ni bora kila mmoja ashiriki kwa nguvu zake na ashinde kwa nguvu zake.
NigaragazeMahaba niue.
Kweli wewe inaonesha hutumii kichwa chako vizuri kuchakata mambo. Sasa kuanzia leo utambue ya kuwa Lowasa ndiye aliyekuwa kiongozi mwenye mvuto na anakubalika na wanachi kuliko mwanasiasa yeyote yule pamoja na chadema kutumika kumchafua lakini mzee wa watu hakuchafuka ndio kwanza alizidi kupedwa, na ndio maana alipokatwa nchi iliingia ukiwa kama vile kuna msiba wa kitaifa ila matumaini yaliibuka baada ya Mbowe kumchukua mzee na ndio maana alipata kura zaidi ya million sita wakati chadema hata wanachama million tatu hawana. Mzee alikuwa anamvuto wa kisiasa, ukiwa na mvuto wa kisiasa unaweza usifanye mambo makubwa lakini ukaoendwa tu.Kwa taarifa yako huyo Lowassa huko cdm alivamia treni kwa mbele. Baada ya uchaguzi wa 2010, cdm ndio chama kilichofanya kazi ya kisiasa kuliko chama chochote cha kisiasa. Ndio chama kilichoanzisha operations nyingi za kisiasa zilizopandisha hamasa za kisiasa hapa nchini. Watu walijiandikisha kwa wingi kupiga kura tena kwa hasira licha ya vikwazo vingi, wakijua fika ccm watamchagua Lowassa kuwa mgombea wao ili wamchinjie mbali. Umesahau neno vitambulisho vya kura kuitwa vichinjio?
Wakati hamasa hiyo ikiwa juu, Lowassa alikuwa ccm, na Magufuli alikuwa hajajua kuwa atakuwa mgombea kupitia ccm. Au unataka kusema hamasa ya uchaguzi ule ilikuja baada ya Lowassa na Magufuli kuwa wagombea wa hivyo vyama? Hiyo ni intro tu ya ukweli, ukitaka nitakupa zaidi ukweli ambao usingependa ufahamike. Ukweli huu ni nje ya upotoshaji uliojaa kichwani mwako.
Nimecheka kwa nguvu, kama Lowasa alipendwa hadi kupata kura 6m akiwa na miezi miwili ndani ya cdm, je alileta kura ngapi akiwa na miaka miwili ndani ya cdm? Kama alikuwa na nguvu hizo kwanini hakwenda TLP ili tuone hizo nguvu zake? Halafu Lowassa alichafuliwa, kwani alikuwa na usafi gani, ama kuchukiwa na cdm ndio akawa msafi?Kweli wewe inaonesha hutumii kichwa chako vizuri kuchakata mambo. Sasa kuanzia leo utambue ya kuwa Lowasa ndiye aliyekuwa kiongozi mwenye mvuto na anakubalika na wanachi kuliko mwanasiasa yeyote yule pamoja na chadema kutumika kumchafua lakini mzee wa watu hakuchafuka ndio kwanza alizidi kupedwa, na ndio maana alipokatwa nchi iliingia ukiwa kama vile kuna msiba wa kitaifa ila matumaini yaliibuka baada ya Mbowe kumchukua mzee na ndio maana alipata kura zaidi ya million sita wakati chadema hata wanachama million tatu hawana. Mzee alikuwa anamvuto wa kisiasa, ukiwa na mvuto wa kisiasa unaweza usifanye mambo makubwa lakini ukaoendwa tu.
Tabia mliyonayo yakuchafua viongozi wa ccm hamkomi, na hata siku za nyuma mlijikita kumchafua Makonda lakini ndo kwanza jamaa anazidi kupendwa, kwenye hili mjitafakari sana.
JPM yeye wananchi ni kama walifanyiwa surprise sio kwamba alikuwa ni dhaifu ila hakuwa kuonesha nia ya kugombea urais huko nyuma ila mwamba alipendwa sana kwa kazi zake na maamuzi magumu na makini na hakutaka kucheka na kima kabisa.
Ni dhahiri wewe hujui hata unachokitaka kutoka kwa mtawala yeyote zaidi hasa unachotaka wewe ni kuona chadema inatoa Rais. Ulipaswa ubishane na mfia chama mwenzako kwa bahati mbaya mimi ni mtu mwenye fikra huru, sio mfia chama.Nimecheka kwa nguvu, kama Lowasa alipendwa hadi kupata kura 6m akiwa na miezi miwili ndani ya cdm, je alileta kura ngapi akiwa na miaka miwili ndani ya cdm? Kama alikuwa na nguvu hizo kwanini hakwenda TLP ili tuone hizo nguvu zake? Halafu Lowassa alichafuliwa, kwani alikuwa na usafi gani, ama kuchukiwa na cdm ndio akawa msafi?
Magufuli alipendwa, ikawaje chini ya utawala wake ndio tukawa tunashuhudia chaguzi za kihayawani zaidi? Huyo Makonda kwangu sina hata la kumuongelea maana najua ni muhalifu kama wahalifu wengine.
Ni kweli sijui ninachokotaka, maana ww ndio mwenye muongozo wa nini mtu anatakiwa akitake😂Ni dhahiri wewe hujui hata unachokitaka kutoka kwa mtawala yeyote zaidi hasa unachotaka wewe ni kuona chadema inatoa Rais. Ulipaswa ubishane na mfia chama mwenzako kwa bahati mbaya mimi ni mtu mwenye fikra huru, sio mfia chama.
Ninachoangalia mimi kwa kiongozi ni namna gani anafanya mambo yenye maslahi kwa kwa taifa ni sio kuongea ongea tu halafu taifa halisongi mbele. Kwa wewe endelea kuwa mtumwa wa vyama vya siasa badala ya kuwa mtumwa wa taifa lako.
Kinachowaponza nyie huko chadema ni kuwa mtu akiwa na fikra huru na akatoa maoni yake tofauti na wakuu wake mnamuona msaliti na ndio maana enzi za JPM wenye fikra huru wengi walihama. Tofauti wenzenu wa ccm ukiangalia chama Chao ni kama kuna makundi mawili yenye upinzani wa ndani kwa ndani lakini huwezi wasikia wakiitana majina ya wasaliti na wakiwa na jambo lao lenye maslahi kwa wananchi au chama wanakuwa pamoja.
Nani kakuambia anatatizo na Mpina? Watu kama kina Mpina ndio tunao wataka. Leo hii unajadai kumuona Mpina Shujaa, sasa Mpina na JPM wanatofauti gani. Ndio maana nasema wewe ni mfia chama na hujui nini unataka Ndugai ni mara Ngapi umemtukana humu hasa akiwa Spika na aliyekuambia ana tatizo na Ndugai ni nani?. Leo hii unazungumzia katiba mpya kwa akili yako unadhani katiba ndio inaleta maendeleo? Katiba mnayodai nyie ni kwa maslahi ya kisiasa na si vinginevyo. Weka fact hapa nikuelewe ni vipi katiba inaleta maendeleo. Katiba yetu sio mbovu kama mnavyodai na ndio maana JPM alifanyia nchi mambo makubwa kupitia katiba hii hii. Hakuna kiongozi angependa kuwa na katiba inayehatarisha usalama wa cheo chake au kesho yake na ndio maana mpaka Leo mmeshindwa kuheshimu katiba ya chama chenu, sasa mtaweza heshimu katiba ya nchi ninyi ikiwa mtu mmoja anakuwa kiongozi milele.Ni kweli sijui ninachokotaka, maana ww ndio mwenye muongozo wa nini mtu anatakiwa akitake😂
Ww unaangalia kiongozi analifanyia nini taifa, mimi ninaangalia taifa linatakiwa liongozwe vipi kufikia maendeleo yake, na hii ni kupitia katiba yenye meno, na sio katiba ya kumfanya rais mungu mtu.
Huko ccm ukihama wanakusifia ili tuone kama wanaheshimu mwenye mawazo tofauti? Tuanze na Ndugai nini kilimkuta toka kwa wanaccm baada ya kutoa maoni yasiyomfurahisha mwenyekiti wa ccm? Mpina huko bungeni, ni nani wamemsagia kunguni hadi kutolewa bungeni? Au maslahi ya taifa kwako ni yapi zaidi ya hayo aliyosimamia Mpina? Ama huo umoja wa ccm kwenye maslahi ya taifa ni upi unaongelea boss? Hebu kaa kimya maana huna jipya.
Unajifanya sio mfia vyama, lakini unaisifia ccm sijui ina umoja kwenye maslahi ya taifa, nimekupa na mifano halisi kuwa hujui usemalo. Hapo huo ufia chama unadhani ni hadi uukiri, hata michango yako inaonyesha ni mfia chama usiyejiamini.
Acha uchafuzi wa lugha. Wewe huna fikra huru bali ni mateka wa fikra za CCM. Yaani ni msukule mfuata benderaNi dhahiri wewe hujui hata unachokitaka kutoka kwa mtawala yeyote zaidi hasa unachotaka wewe ni kuona chadema inatoa Rais. Ulipaswa ubishane na mfia chama mwenzako kwa bahati mbaya mimi ni mtu mwenye fikra huru, sio mfia chama.
Ninachoangalia mimi kwa kiongozi ni namna gani anafanya mambo yenye maslahi kwa kwa taifa ni sio kuongea ongea tu halafu taifa halisongi mbele. Kwa wewe endelea kuwa mtumwa wa vyama vya siasa badala ya kuwa mtumwa wa taifa lako.
Kinachowaponza nyie huko chadema ni kuwa mtu akiwa na fikra huru na akatoa maoni yake tofauti na wakuu wake mnamuona msaliti na ndio maana enzi za JPM wenye fikra huru wengi walihama. Tofauti wenzenu wa ccm ukiangalia chama Chao ni kama kuna makundi mawili yenye upinzani wa ndani kwa ndani lakini huwezi wasikia wakiitana majina ya wasaliti na wakiwa na jambo lao lenye maslahi kwa wananchi au chama wanakuwa pamoja.
Katiba hii imepitwa na wakati. Hivi kichwa kina makamasi tu!! Sidhani kama una akili. Sasa unamsfia Magufuli ambaye alikuwa anavunja Katiba kila siku! Magufuli alikuwa DIKTETA, akanyamazisha bunge na kutuachia bunge la chama kimoja, akaitisha mahakama, akanyamazisha vyombo vya habari.Nani kakuambia anatatizo na Mpina? Watu kama kina Mpina ndio tunao wataka. Leo hii unajadai kumuona Mpina Shujaa, sasa Mpina na JPM wanatofauti gani. Ndio maana nasema wewe ni mfia chama na hujui nini unataka Ndugai ni mara Ngapi umemtukana humu hasa akiwa Spika na aliyekuambia ana tatizo na Ndugai ni nani?. Leo hii unazungumzia katiba mpya kwa akili yako unadhani katiba ndio inaleta maendeleo? Katiba mnayodai nyie ni kwa maslahi ya kisiasa na si vinginevyo. Weka fact hapa nikuelewe ni vipi katiba inaleta maendeleo. Katiba yetu sio mbovu kama mnavyodai na ndio maana JPM alifanyia nchi mambo makubwa kupitia katiba hii hii. Hakuna kiongozi angependa kuwa na katiba inayehatarisha usalama wa cheo chake au kesho yake na ndio maana mpaka Leo mmeshindwa kuheshimu katiba ya chama chenu, sasa mtaweza heshimu katiba ya nchi ninyi ikiwa mtu mmoja anakuwa kiongozi milele.
Wapi umeona namsifia Mpina? Mimi nimekuonyesha huko ccm hakuna umoja huo unaosema wanao kwenye masuala ya kitaifa. Huyo Mpina na Ndugai nimekupa mifano yu, lakini sina popote ninapomuona ni shujaa. Naona unanipotezea muda kwa kuniwekea mazdhana yako ambayo siwajibiki nayo.Nani kakuambia anatatizo na Mpina? Watu kama kina Mpina ndio tunao wataka. Leo hii unajadai kumuona Mpina Shujaa, sasa Mpina na JPM wanatofauti gani. Ndio maana nasema wewe ni mfia chama na hujui nini unataka Ndugai ni mara Ngapi umemtukana humu hasa akiwa Spika na aliyekuambia ana tatizo na Ndugai ni nani?. Leo hii unazungumzia katiba mpya kwa akili yako unadhani katiba ndio inaleta maendeleo? Katiba mnayodai nyie ni kwa maslahi ya kisiasa na si vinginevyo. Weka fact hapa nikuelewe ni vipi katiba inaleta maendeleo. Katiba yetu sio mbovu kama mnavyodai na ndio maana JPM alifanyia nchi mambo makubwa kupitia katiba hii hii. Hakuna kiongozi angependa kuwa na katiba inayehatarisha usalama wa cheo chake au kesho yake na ndio maana mpaka Leo mmeshindwa kuheshimu katiba ya chama chenu, sasa mtaweza heshimu katiba ya nchi ninyi ikiwa mtu mmoja anakuwa kiongozi milele.