Kuanzia 2015 Tanzania itatawaliwa "kidikteta" Ukweli huu hapa

Kwa taarifa yako huyo Lowassa huko cdm alivamia treni kwa mbele. Baada ya uchaguzi wa 2010, cdm ndio chama kilichofanya kazi ya kisiasa kuliko chama chochote cha kisiasa. Ndio chama kilichoanzisha operations nyingi za kisiasa zilizopandisha hamasa za kisiasa hapa nchini. Watu walijiandikisha kwa wingi kupiga kura tena kwa hasira licha ya vikwazo vingi, wakijua fika ccm watamchagua Lowassa kuwa mgombea wao ili wamchinjie mbali. Umesahau neno vitambulisho vya kura kuitwa vichinjio?

Wakati hamasa hiyo ikiwa juu, Lowassa alikuwa ccm, na Magufuli alikuwa hajajua kuwa atakuwa mgombea kupitia ccm. Au unataka kusema hamasa ya uchaguzi ule ilikuja baada ya Lowassa na Magufuli kuwa wagombea wa hivyo vyama? Hiyo ni intro tu ya ukweli, ukitaka nitakupa zaidi ukweli ambao usingependa ufahamike. Ukweli huu ni nje ya upotoshaji uliojaa kichwani mwako.
 
Mwamba ulipiga mulemule!
 
Kweli wewe inaonesha hutumii kichwa chako vizuri kuchakata mambo. Sasa kuanzia leo utambue ya kuwa Lowasa ndiye aliyekuwa kiongozi mwenye mvuto na anakubalika na wanachi kuliko mwanasiasa yeyote yule pamoja na chadema kutumika kumchafua lakini mzee wa watu hakuchafuka ndio kwanza alizidi kupedwa, na ndio maana alipokatwa nchi iliingia ukiwa kama vile kuna msiba wa kitaifa ila matumaini yaliibuka baada ya Mbowe kumchukua mzee na ndio maana alipata kura zaidi ya million sita wakati chadema hata wanachama million tatu hawana. Mzee alikuwa anamvuto wa kisiasa, ukiwa na mvuto wa kisiasa unaweza usifanye mambo makubwa lakini ukaoendwa tu.

Tabia mliyonayo yakuchafua viongozi wa ccm hamkomi, na hata siku za nyuma mlijikita kumchafua Makonda lakini ndo kwanza jamaa anazidi kupendwa, kwenye hili mjitafakari sana.

JPM yeye wananchi ni kama walifanyiwa surprise sio kwamba alikuwa ni dhaifu ila hakuwa kuonesha nia ya kugombea urais huko nyuma ila mwamba alipendwa sana kwa kazi zake na maamuzi magumu na makini na hakutaka kucheka na kima kabisa.
 
Nimecheka kwa nguvu, kama Lowasa alipendwa hadi kupata kura 6m akiwa na miezi miwili ndani ya cdm, je alileta kura ngapi akiwa na miaka miwili ndani ya cdm? Kama alikuwa na nguvu hizo kwanini hakwenda TLP ili tuone hizo nguvu zake? Halafu Lowassa alichafuliwa, kwani alikuwa na usafi gani, ama kuchukiwa na cdm ndio akawa msafi?

Magufuli alipendwa, ikawaje chini ya utawala wake ndio tukawa tunashuhudia chaguzi za kihayawani zaidi? Huyo Makonda kwangu sina hata la kumuongelea maana najua ni muhalifu kama wahalifu wengine.
 
Ni dhahiri wewe hujui hata unachokitaka kutoka kwa mtawala yeyote zaidi hasa unachotaka wewe ni kuona chadema inatoa Rais. Ulipaswa ubishane na mfia chama mwenzako kwa bahati mbaya mimi ni mtu mwenye fikra huru, sio mfia chama.

Ninachoangalia mimi kwa kiongozi ni namna gani anafanya mambo yenye maslahi kwa kwa taifa ni sio kuongea ongea tu halafu taifa halisongi mbele. Kwa wewe endelea kuwa mtumwa wa vyama vya siasa badala ya kuwa mtumwa wa taifa lako.

Kinachowaponza nyie huko chadema ni kuwa mtu akiwa na fikra huru na akatoa maoni yake tofauti na wakuu wake mnamuona msaliti na ndio maana enzi za JPM wenye fikra huru wengi walihama. Tofauti wenzenu wa ccm ukiangalia chama Chao ni kama kuna makundi mawili yenye upinzani wa ndani kwa ndani lakini huwezi wasikia wakiitana majina ya wasaliti na wakiwa na jambo lao lenye maslahi kwa wananchi au chama wanakuwa pamoja.
 
Ni kweli sijui ninachokotaka, maana ww ndio mwenye muongozo wa nini mtu anatakiwa akitake😂

Ww unaangalia kiongozi analifanyia nini taifa, mimi ninaangalia taifa linatakiwa liongozwe vipi kufikia maendeleo yake, na hii ni kupitia katiba yenye meno, na sio katiba ya kumfanya rais mungu mtu.

Huko ccm ukihama wanakusifia ili tuone kama wanaheshimu mwenye mawazo tofauti? Tuanze na Ndugai nini kilimkuta toka kwa wanaccm baada ya kutoa maoni yasiyomfurahisha mwenyekiti wa ccm? Mpina huko bungeni, ni nani wamemsagia kunguni hadi kutolewa bungeni? Au maslahi ya taifa kwako ni yapi zaidi ya hayo aliyosimamia Mpina? Ama huo umoja wa ccm kwenye maslahi ya taifa ni upi unaongelea boss? Hebu kaa kimya maana huna jipya.

Unajifanya sio mfia vyama, lakini unaisifia ccm sijui ina umoja kwenye maslahi ya taifa, nimekupa na mifano halisi kuwa hujui usemalo. Hapo huo ufia chama unadhani ni hadi uukiri, hata michango yako inaonyesha ni mfia chama usiyejiamini.
 
Nani kakuambia anatatizo na Mpina? Watu kama kina Mpina ndio tunao wataka. Leo hii unajadai kumuona Mpina Shujaa, sasa Mpina na JPM wanatofauti gani. Ndio maana nasema wewe ni mfia chama na hujui nini unataka Ndugai ni mara Ngapi umemtukana humu hasa akiwa Spika na aliyekuambia ana tatizo na Ndugai ni nani?. Leo hii unazungumzia katiba mpya kwa akili yako unadhani katiba ndio inaleta maendeleo? Katiba mnayodai nyie ni kwa maslahi ya kisiasa na si vinginevyo. Weka fact hapa nikuelewe ni vipi katiba inaleta maendeleo. Katiba yetu sio mbovu kama mnavyodai na ndio maana JPM alifanyia nchi mambo makubwa kupitia katiba hii hii. Hakuna kiongozi angependa kuwa na katiba inayehatarisha usalama wa cheo chake au kesho yake na ndio maana mpaka Leo mmeshindwa kuheshimu katiba ya chama chenu, sasa mtaweza heshimu katiba ya nchi ninyi ikiwa mtu mmoja anakuwa kiongozi milele.
 
Acha uchafuzi wa lugha. Wewe huna fikra huru bali ni mateka wa fikra za CCM. Yaani ni msukule mfuata bendera
 
Katiba hii imepitwa na wakati. Hivi kichwa kina makamasi tu!! Sidhani kama una akili. Sasa unamsfia Magufuli ambaye alikuwa anavunja Katiba kila siku! Magufuli alikuwa DIKTETA, akanyamazisha bunge na kutuachia bunge la chama kimoja, akaitisha mahakama, akanyamazisha vyombo vya habari.

Mbaya zaidi alikuwa anateka na kuua wapinzani. Alikuwa anachukia matajiri. Mtu yule hafai hata kuwa Mwenyekiti wa kijiji kwa namna ya roho ya kimaskini
 
Wapi umeona namsifia Mpina? Mimi nimekuonyesha huko ccm hakuna umoja huo unaosema wanao kwenye masuala ya kitaifa. Huyo Mpina na Ndugai nimekupa mifano yu, lakini sina popote ninapomuona ni shujaa. Naona unanipotezea muda kwa kuniwekea mazdhana yako ambayo siwajibiki nayo.

Maendeleo ni wajibu wa kiongozi au chama kinachokusanya kodi, na wala sio hisani ya rais. Ninapozungumzia katiba bora ni pamoja na kumfanya rais awajibike kwa wananchi, na wala asidhani anapaswa kuleta maendeleo kwa kusujudiwa. Ww ndio unaamini kwenye watu sio kwenye mifumo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…