Kubagua Mwanza na Mbeya AFCON haikubaliki

Kubagua Mwanza na Mbeya AFCON haikubaliki

viwanja vinne vitatosha.
1. KWA MKAPA

2. UHURU STADIUM

3. HUO MPYA UNAOJENGWA ARUSHA

4. MPYA UTAKAOJENGWA DODOMA.

kwengine wasubiri, na wasituharakishe.
 
Hii tabia ya kubagua Mikoa ya Mbeya na Mwanza kwenye mambo ya Maendeleo naona imeanza kukita mizizi.

Wakati mikoa mingine ikipendelewa sie Mwanza na Mbeya tumekuwa wahanga wa kutengwa na Kubaguliwa kwenye masuala mbalimbali ya kimaendeleo licha ya kuwa tunastahili kwa vigezo na sio kwa kuonewa huruma.

Haiwezekani na haiingii akilini eti kubagua miji hii maarufu kwa wanamichezo na badala yake wakaipendelea miji isiyo na mashabiki wala wanamichezo ya Arusha na Dodoma.

Nasisitiza tunadai haki yetu na sio favour kwa sababu zifuatazo;

Mwanza
  • Mikoa wa pili kuchangia Pato la Taifa GDP baada ya Dar.
  • Jiji la Pili kuwa na population kubwa baada ya Dar.
  • Jiji la 3 Kuchangia Mapato ya Kikodi.
  • Uwepo wa mashabiki wa kutosha na wanamichezo.

Mbeya
  • Mikoa wa 3 kuchangia Pato la Taifa nyuma ya Dar na Mwanza.
  • Jiji la 6 Kwa idadi ya watu Tanzania.
  • Jiji la 2 Kwa Wanamichezo wengi kama timu za NBC&Championship.
  • Pamoja na mtoto Wetu Songwe ni Mkoa wa 4 Kwa mapato ya Kikodi.
View attachment 2766225
Kwa vigezo hivyo pekee tunastahili kupata kitu sio kwa upendeleo bali kwa haki.

Habari za kusema hakuna hoteli au miundombinu ya kisasa na blaa blaa kama hizo zinatokana na Serikali hii ya ccm kuchukua pesa na jasho letu kwenda kujenga Mikoa mingine kama Arusha, Dodoma, Tanga, Dar nk.

Ni aidha Serikali ianze ujenzi wa viwanja vya Kisasa kwenye miji yetu kutufuta machozi na sio lazima kwa ajili ya AFCON bali kutupa heshima yetu kwenye michezo au tumwage mboga 2025.

Hali hii haivumiliki na haikubaliki, ni wakati wa watu wa Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kusini kufanya jambo la kujitambua mwaka 2025 endapo wataziba maskio.

Ni bora kumwaga mboga sio kwa sababu tunawakubali Wapinzani bali ni kwa nia ya kukomoana kwamba tukose wote, tumechoka kutengwa na tabia hii ikiendelea ipo siku tutagawana fito.
View attachment 2766050View attachment 2766051View attachment 2766052

Angalizo: Haya ni maoni na mtizamo binafsi, yasichukuliwe kama uchochezi.Nachokonoa mada Kwa maslahi mapana ya Nchi hii na watu wa Mbeya na Mwanza.
Mwanza kuna miradi ya maendeleo mingi tu inaendelea. Kuna daraja la kukatiza ziwa, kuna upanuzi wa Airport, kuna SGR inajengwa. Arusha kuna nn kinaendelea? Wakiongea Mbeya wataeleweka.
 
Ningeishanga serekali Kama isinge Jenga na uwanja Arusha ,Arusha Ni hub na ni njia kuu za kwenda mbugani hapo Arusha patafurikaa
 
Arusha ni mji bora na uliondelea kuliko mwanza. na ni mji wenye infrastructures bora kuliko Mwanza na mbeya combined.
Mimi nilitamani iwe Arusha, Dar na Zanzibar. Hiyo mikoa mingine imekaa kushoto.
Nashangaaga mijitu mingine inaifNanisha Arusha na mijitu ya mikoo wakulima wa mbungaa
Ni vyema umewaeleza kuwa Arusha ninstrategie city
 
Kwanza kuna watu kutoka corners nyingine za Africa hawajawahi kuliona Ziwa Victoria, hii ingekuwa fursa kwao. Ingawa Arusha nayo inafaa kwa kuwa kuna vivutio wa watalii vingi.

Tatizo la Arusha nawahurumia wageni. Ule mji hauna adabu kabisa:umejaa wahuni, wasela mavi, wavuta bangi na wezi kama wote. A typically hooligan place! Wageni wetu wanaenda kuibiwa, kujeruhiwa, kupigwa vidole sehemu nyeti, kubakwa,n.k. MJI WA HOVYO SANA ULE!
Acha kuchafua mji wetu bhan
 
Game nyingi sana za maana zimechezwa Arusha, na ule mji umeandaa mashindano na events kubwa za kimataifa na watu wake wamekuwa wenyeji wa matukio mengi sana ya kimataifa na mji ule unaweza hata sasa hivi kupokea wageni wengi wa caliber ya juu.
Msifananishe Arusha na mwanza, hayo ni mambo ya humu jamiiforums siyo kiuhalisia.
Safi sna kobelo
 
Ligi kuu tanzania presons na Ihefu championship kuna mbey city,kengold, na hawa waliotoroka mbeya kwanza.

Nenda dodoma arusha tim ya mwisho kuwa ligi kuu ilikuwa kabla mwaka haujageuka kuwa namb 2. Na hwana hata habar na mipira ni kitakuwa godown la bidhaaa yaaan
Acha liwe serekali haiwazi Kama mnavyo waza
 
Kwani wanaangalia hivyo?

Acheni hizo big deal ni what will happen baada ya hayo mashindano
 
Wewe si ndio tukipindea viongozi unaleta uzwazwa...

CCM kirumba wa Mwanza ni uwanja mzuri ila umeachwa umeenda kuchukuliwa wa Arusha wenye kuhitaji ukarabati mwingi, wakati CCM kirumba ilikuwa ni pesa kidogo tu uwanja unakaa shikopa
Kwel kabisa mkuu kirumba ndy uwanja unaobeba watu wengi ukiacha mkapa
 
Wewe si ndio tukipindea viongozi unaleta uzwazwa...

CCM kirumba wa Mwanza ni uwanja mzuri ila umeachwa umeenda kuchukuliwa wa Arusha wenye kuhitaji ukarabati mwingi, wakati CCM kirumba ilikuwa ni pesa kidogo tu uwanja unakaa shikopa
Arusha unajengwa Uwanja mpya kabisa
 
Nalog off huu uzi sababu Kuna watu wameishiwa hoja wameanza kuweka fuckinchuki mihemko matabaka na fuckinbattle ya Mwanza na karusha
 
Huu upuuzi unataka kukisiri sasa ni wakati wa watu wa Mbeya na Mwanza kupaza sauti haiwezekani kila project kubwa hii mikoa inatengwa,imekua too much sasa,kama vipi tuwakatae hawa watu by 2025
 
Dar: Jiji Kuu, Jiji la Biashara.
Mwanza: Jiji Kuu la Pili la Biashara.
Arusha: Kitovu cha Utalii Tz
Dodoma: Makao Makuu ya Nchi.
Zanzibar: Kitovu cha Utalii.
Mbeya: Wanapenda sana mpira.(Moro? Kigoma? Mtwara?)

Kibiashara Dar inatosha kutuwakilisha kulingana na ufinyu wa nafasi.
Dodoma, ni Jiji Kuu andaliwa, linahitaji promotion kubwa hakukuwa na namna ya kuliacha.
Arusha kwa nafasi yake katika Utalii hakuna namna ya kutomia fursa hii kulitangaza/halina mbadala.
Zanzibar ukizingatia Umaarufu wake duniani, na nafasi yake katika Utalii, hakuna MTU angeweza kuipoka nafasi hiyo akaeleweka. (inawezekana Zanzibar na Arusha zitafurika wageni wengi kuliko miji yote itakayoshiriki Afcon EA)

Katika hizo nafasi 4, Mwanza ingeweza kuisukuma Dodoma nje, lakini unyeti wa Dodoma kwa sasa unafanya ibaki hapo.
Mbeya haina nafasi kabisa hapo kwenye orodha, labda tungekuwa na nafasi sita.

Viwanja vinahitajika sana, hata kwetu Morogoro. Ajabu viwanja vingi vinapitia Ukarabati sijawahi sikia Jamuhuri-Morogoro. Kwa heshima yetu kama mkoa katika Soka, tunahitaji kiwanja Kipya cha Kisasa-Kiegea au Lukobe, au kwenye shamba la Mkonge Tungi, kukuza mji.
 
Back
Top Bottom