Kubagua Mwanza na Mbeya AFCON haikubaliki

Kubagua Mwanza na Mbeya AFCON haikubaliki

Na sisi wakazi wa Mkoa wa Pwani tunasikitika ni kwanini wapeleke Dodoma na Arusha badala ya Pwani hasa Kibaha, Chalinze au Bagamoyo
Mkoa wa Pwani umemezwa na Mkoa wa dar es salaam Bora wangeufanya kuwa mkoa mmoja tu
 
Seriously mkuu mkoa wa Mwanza una underestimate kiasi hicho 😯.
Hii blunder haina utetezi wowote wenye mashiko.
Mkuu
Mwanza hakuna uwanja wa kukidhi vigezo.
Mwanza hakuna hotel. Naomba utaje hotel zenye hadhi ya kuchukua wachezaji kwa group Zima.
 
Mkuu
Mwanza hakuna uwanja wa kukidhi vigezo.
Mwanza hakuna hotel. Naomba utaje hotel zenye hadhi ya kuchukua wachezaji kwa group Zima.
Malaika, Goldcrest, Wag hill, Pigeon, Ryan's bay, Tilapia kwa uchache hizi sio hoteli!?

Halafu mada sio kwamba hakuna uwanja wa kukidhi ni kujenga uwanja.
 
Malaika, Goldcrest, Wag hill, Pigeon, Ryan's bay, Tilapia kwa uchache hizi sio hoteli!?

Halafu mada sio kwamba hakuna uwanja wa kukidhi ni kujenga uwanja.
Sasa hizo sini sawa na pallson hotel Yani haziwezi kidhi vigezo vya kimataifa
 
Haha na hapa sindo mtakufa watu wa Mbeya na Mwanza ChoiceVariable Kitombile Mikdad
Screenshot_20231001-071106.jpg
 
Wewe umesoma hapo na kuelewa nini?

Labda Mwanza ndio hawana hizo Barabara za njia 4 ila sio Kwa Mbeya.
Njia nne zipo, Dar, dodoma, arusha, Ilemela, mbeya, iringa, singida, moshi n.k lakini jiji la pili kwa ukubwa Tanzania halina kabisa barabara za njia nne, hii hatari sana...hii nchi ngumu sana, sijui tuliikosea nini asee.
 
Njia nne zipo, Dar, dodoma, arusha, Ilemela, mbeya, iringa, singida, moshi n.k lakini jiji la pili kwa ukubwa Tanzania halina kabisa barabara za njia nne, hii hatari sana...hii nchi ngumu sana, sijui tuliikosea nini asee.
Iringa hawana
 
Kwa AFCON sababu za kuichagua Arusha ziko nyingi ila the obsvious one ni kuwa AFCON inachezwa Kenya UG na TZ sasa Arusha ni karibu kwenda Nairobi so mashabiki wanaweza kuja Arusha kuangalia mechi kisha masaa kadhaa wakarud Nairobi au hata kuja dar

Arusha na Dom Pia sio mbali ukizingatia Dom ni central so umbal wa Dom na Arusha na Dom na Dar umepishana kdg ni safar ya siku moja tu

Sasa wapeleke Match Mbeya hv umeona hizo logistic za shabiki kutoka Nairob had Mbeya

Na kwa mashabiki UG watapitia Nairob kuja Dar au dom au Arusha maana safar itakuwa fupi kuliko akisema aje Dar au Dom kupitia route ya Kagera mwanza
 
Umenena mkuu, katika vigezo vya kuzingatiwa ili uwanja uwe umekidhi vigezo vya michezo ya kimataifa ni pamoja na kuwa na hoteli za kutosha za kitalii karibu na uwanja huo, hili ndio limesababisha Arusha kupewa nafasi
Dodoma kuna hoteli gani hapo?
 
Mkuu
Mwanza hakuna uwanja wa kukidhi vigezo.
Mwanza hakuna hotel. Naomba utaje hotel zenye hadhi ya kuchukua wachezaji kwa group Zima.
Arusha mna hotel gani za maana,taja na mm nikutajie acha kukaririshwa
 
Arusha mna hotel gani za maana,taja na mm nikutajie acha kukaririshwa
Hotel za maana hapo Arusha mjini hazifiki hata 10,pia hizo mnasema nyota tano zipo ngapi hapo na hotel nzuri kidogo zipo huko maporini mbugani ngorongoro,,kinachobaki ni bla bla bla tu
 
Hii tabia ya kubagua Mikoa ya Mbeya na Mwanza kwenye mambo ya Maendeleo naona imeanza kukita mizizi.

Wakati mikoa mingine ikipendelewa sie Mwanza na Mbeya tumekuwa wahanga wa kutengwa na Kubaguliwa kwenye masuala mbalimbali ya kimaendeleo licha ya kuwa tunastahili kwa vigezo na sio kwa kuonewa huruma.

Haiwezekani na haiingii akilini eti kubagua miji hii maarufu kwa wanamichezo na badala yake wakaipendelea miji isiyo na mashabiki wala wanamichezo ya Arusha na Dodoma.

Nasisitiza tunadai haki yetu na sio favour kwa sababu zifuatazo;

Mwanza
  • Mikoa wa pili kuchangia Pato la Taifa GDP baada ya Dar.
  • Jiji la Pili kuwa na population kubwa baada ya Dar.
  • Jiji la 3 Kuchangia Mapato ya Kikodi.
  • Uwepo wa mashabiki wa kutosha na wanamichezo.

Mbeya
  • Mikoa wa 3 kuchangia Pato la Taifa nyuma ya Dar na Mwanza.
  • Jiji la 6 Kwa idadi ya watu Tanzania.
  • Jiji la 2 Kwa Wanamichezo wengi kama timu za NBC&Championship.
  • Pamoja na mtoto Wetu Songwe ni Mkoa wa 4 Kwa mapato ya Kikodi.
View attachment 2766225
Kwa vigezo hivyo pekee tunastahili kupata kitu sio kwa upendeleo bali kwa haki.

Habari za kusema hakuna hoteli au miundombinu ya kisasa na blaa blaa kama hizo zinatokana na Serikali hii ya ccm kuchukua pesa na jasho letu kwenda kujenga Mikoa mingine kama Arusha, Dodoma, Tanga, Dar nk.

Ni aidha Serikali ianze ujenzi wa viwanja vya Kisasa kwenye miji yetu kutufuta machozi na sio lazima kwa ajili ya AFCON bali kutupa heshima yetu kwenye michezo au tumwage mboga 2025.

Hali hii haivumiliki na haikubaliki, ni wakati wa watu wa Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kusini kufanya jambo la kujitambua mwaka 2025 endapo wataziba maskio.

Ni bora kumwaga mboga sio kwa sababu tunawakubali Wapinzani bali ni kwa nia ya kukomoana kwamba tukose wote, tumechoka kutengwa na tabia hii ikiendelea ipo siku tutagawana fito.
View attachment 2766050View attachment 2766051View attachment 2766052

Angalizo: Haya ni maoni na mtizamo binafsi, yasichukuliwe kama uchochezi.Nachokonoa mada Kwa maslahi mapana ya Nchi hii na watu wa Mbeya na Mwanza.
Kwani kwenye hili mama haupigi mwingi?
 
Back
Top Bottom