Kubomoka kwa daraja la Kiyegeya: Meneja Tanroads Morogoro arudishwa Wizarani

Kubomoka kwa daraja la Kiyegeya: Meneja Tanroads Morogoro arudishwa Wizarani

Awamu Hii Ya Tano
Inajitahidi Sana Mpaka Mheshimiwa PM Ametoa Pole Toka Kwa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
PM kumwajibisha mtendaji ni hatua nzuri. Lipo tatizo vishimo vidogo ambavyo hata kwa dharula vingezibwa kwa garama ndogo moram wakijipanga, vinakaa miezi, vinagarimu uharibifu magari, ajali na vifo. Tanroad waweke hotline ktk mabango yao tuwajuze.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivyo vishimo ni kero balaah, mwaka mzima vinakaa bila kuzibwa
 
Tanroads mkishirikiana na jeshi la polisi undeni haraka Road patrol and rescue department itakayokuwa na tawi kila mkoa na kazi yake kuu ni kufanya daily road patrol kuangalia road traffics, road damages, na road safety kiujumla Tanzania nzima, uokozi wote kwenye ajali za barabarani utafanywa mara moja na hii department, magari mabovu yote lazima immediately yaondolewa na hawa jamaa, barabara mbovu zinazohitaji matengenezo ya haraka wapewe hawa jamaa.

Kila mkoa kupitia hizo Road patrol departments unatakiwa uwe na vitendea kazi vifuatavyo, Mobile crane tatu ( 40tons, 60tons na 200tons), Breakdowns za kutosha, Low beds x 2, wheel loaders,Excavators, lighting plants, load signs, load blocks na ambulance kadhaa. Team lazima iwe na helicopters hata mbili na zipaki headquarter na inapotokea zinahitajika popote pale ziende haraka.

Dunia inakwenda kasi sana.
 
Ukija na mawazo mbadala unakumbwa na figisu Kama alizokumbana nazo kamishna jenerali wa zimamoto aliyepita, afande Thobias Andengenye!
Ni vyema wakawa creative na pia wafuate taratibu katika kufikisha mawazo yao. Tusiwe waoga kuja na mawazo mbadala, na pia tusisahau kufuata taratibu.
 
HAPO nilikwama kwenye basi ...nilifanya mawasiliano TANROADs kuomba waruhusu Mabasi kubadilishana Abiria (kufaulisha) yanayotokea Moro/Dar yachukue abiria waliotoka Mwanza/Dodoma..na kugeuka... Hawakuzingatia ushauri huu. Japo kuna njia watembea kwa muguu wanavuka. Mabasi mengi walitafutia abiria wao Usafiri ng'ambo kasoro baadhi walioendelea kuhold ikiwemo KIDIA ONE. hapo kuna watoto wadogo wapo tokea jumatatu...wanahitaji msaada.

Hebu tueleze; TANROADS wanahusikaje na mabasi kubadilishana abiria pande mbili za barabara?
 
Huyo anayejiita waziri mkuu amekubuhu kuchukua hatua zenye ombwe la uongozi...!! Shame on him!
 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD), mkoa wa Morogoro, Mhandisi Godwin Andalwisye arejeshwe wizarani na nafasi yake ijazwe na mtu mwingine mara moja baada ya kuzembea kutimiza wajibu wake.

Uamuzi huo umekuja baada ya kiongozi huyo kushindwa kufanya ukaguzi wa usalama wa madaraja yaliyoko kwenye mkoa wake na kubaini kama kuna daraja linamatatizo hali iliyosababisha daraja la Kiyegeya lililopo eneo la Gairo ambalo linaunganisha mkoa wa Morogoro na Dodoma kuvunjika.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo(Jumatano, Machi 4, 2020) baada ya kutembelea eneo hilo na kukagua ukarabati ili kurejesha mawasiliano ya barabara. Waziri Mkuu ameshuhudia mrundikano wa magari na abiria hali ambayo haikumfurahisha.

“Hivi unajua udhahifu wako ni kwa sababu hukufanya ukaguzi kuona kama daraja limejaa mchanga au uchafu ambao umesababisha kipenyo cha kupitisha maji kuwa kidogo na maji yakalazimika kupanda juu hali ambayo ilisababisha daraja hili kusombwa na maji.”

Amesema wakati njia hiyo inarekebishwa itengenezwe njia nyingine ya muda ili kuweza kupitisha magari na kisha Serikali itachukua hatua baada ya kubaini nini kimesababisha.

Ili kuharakisha kazi hiyo inakamilika kwa haraka, Waziri Mkuu ameagiza Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isack Kamwelwe, Katibu Mkuu wa wizara hiyo pamoja na wahandisi wote wa TANROAD mkoa wa Morogoro na Dodoma leo wakutane kwenye eneo la tukio na wahakikishe kuanzia kesho (Alhamisi, Machi 5, 2020) njia hiyo iwe imefunguka.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema atawasiliana na Mkuu wa Majeshi, Generali Venance Mabeyo ili aweze kupata msaada wa wanajeshi ili waongeze nguvu katika kuhakikisha kwamba mawasialaino yanarejea kwa haraka.

Akiwapa pole madereva na watumiaji wengine wa barabara waliokwama katika eneo hilo, Waziri Mkuu amesema “Nimetumwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuja kuwapa pole na kuwahakikisha kwamba Serikali inafanya kila linalowezekana ili kuifungua barabara hii.”
Asante sana waziri Mkuu Majaliwa. Hivyo ndivyo inavyotakiwa ku react. Ukiendelea hivyo Ticket yako iko wazi ya wewe kumrithi Rais Magufuli 2025.

Tanzania inahitaji viongozi wanao yaona matatizo na kutumia mamlaka yao kukabiliana nayo mara moja. Watanzania hawahitaji viongozi wanao piga piga porojo. Nyakati za porojo na kusameheana kwa makosa ya kijinga zimepita, sasa ni nyakati za ku take action.

Hongera sana waziri mkuu, hongera sana. Mungu akujalie na azidi kukupa ujasiri wa kuchukua maamuzi mazito. Thank you![emoji120]

Kitengo ambacho mimi kwa hisia zangu, mtanisamehe kama nitakuwa sipo "up to date", ni wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Sina uhakika kama Mh. Engineer Kamwelwe analitambua hilo. Nina uhakika maovu mengi ya utekelezaji mbovu wa miradi ya barabara kama hii na ujenzi wa majengo inawezekana unasababishwa na watu wenye mamlaka wizarani.

Mimi binafsi sina imani kubwa sana na Waziri Kamwelwe. Inawezekana akawa yuko vizuri katika fani yake, lakini katika usimamizi na ufuatiliaji wa watumishi anao waongoza sidhani kama yuko vizuri. Naona kama bado anatumia zile njia za zamani katika kuwasimamia watendaji wa chini yake.

Kwanini hachukui mifano ya mawaziri wenzake kama Waziri Kalemani, Kigwangalla, Lukuvi, Jafo, Biteko, Hasungwa na Naibu waziri wake Bashe, Prof. Mbarawa, Prof. Mpango, Ummy Mwalim na Prof. Kabudi?Watanzania hatuna budi kujivunia hawa mawaziri wetu. Haya ni mejembe yetu. Hapa Rais hakufanya kosa kuwateua. Shukran za thati zimwendee Rais wetu na majembe yetu. Mungu awabariki na kuwajalia katika majukumu yenu ya kulivusha Taifa letu kwenye uchumi wa kati 2025. Nawapenda sana na ninaimani na nyie.[emoji120]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kikosi kazi yaani gang ikiiiongozwa na Myampala kama sikosei,eti watawala weusi wakafuta cheo na kikosi kazi sababu ya neno Mnyampala kwa sababu nyepesi tu.
Mkoloni ametuachia mambo mengi mazuri lakini sisi kazi yetu ni kuvuruga tu.Tumevuruga elimu,tumevuruga ushirika,tumevuruga kilimo ,tumevuruga siasa,hata kuvuruga East African Common Services.
Malkia alimwambia Nyerere (tunaemwabudu) kuwa "hamuwezi kujitawala" miubishi yake ona sasa!!
 
Kwani anajenga kwa mshahara wake huyo Meneja?

Watumbuaji wa hao Mamenej ndio wahusika wanaipaswa kupeleka fedha za ujenzi n ukarabati
Awamu ya tano mameneja wa TANROADS hawagusagwi kabisaaaa,hongera baba majaliwa kwa kudubutu kumngoa huyo wa morogoro.huku geita na kule serengeti ,kahama,mameneja wa TANROADS wamelala barabara ni mbovu mno mno,Ile inayotoka geita kwenda kahama ni mbovu haipitiki na imekaa maji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom