Kuchelewa Kuoa hakukufanyi ufanikiwe au uwe na unafuu wa Maisha

Kuchelewa Kuoa hakukufanyi ufanikiwe au uwe na unafuu wa Maisha

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
KUCHELEWA KUOA HAKUKUFANYI UFANIKIWE AU UWE NA UNAFUU WA MAISHA!

Anaandika Robert Heriel.

Kwa kijana isipungue miaka 25 wala isizidi 33. OA mapema. Usikawie. Hakuna kitu kizuri kwenye maisha Kama Familia yako. Wewe, Mkeo na watoto.
Chelewa kupata yote usichelewe kuoa au kuolewa. Lazima itakusumbua sehemu Fulani Huko mbele.

Miaka 28-30 ndio miaka mizuri ya kupata Mke na kupata mtoto.

Usije jifanganya kuwa utaoa mambo yakiwa MAZURI, hakuna mambo mazuri kwenye maisha Kama kufanya Jambo Kwa wakati.

Kuna wakati wa kuoa
Kuna wakati wa Kulea.
Kuna wakati wa Kula pension
Hatimaye wakati wa Kifo.

Wengi unaowaona waliowafanikiwa kwenye maisha ya sasa hivi hawakuchelewa kuoa, walioa wakiwa na hali ngumu, lakini hawakujali.

Hakuna Jambo zuri Kama kumhudumia Mkeo na watoto ukiwa kijana mwenye NGUVU.
Sio unasubiri uzee ambao kimsingi unaanzia miaka 40 ndio Uoe.

Madhara ya kuchelewa kuoa utayaona kwenye malezi ya watoto wako.
Utayaona Kwa Mkeo kushindwa kummudu,
Na Kama ukishindwa kabisa kimaisha ndio utakuwaa kwenye hatari kubwa Sana na kubaki kuwalaumu wanawake na watoto wako.

OA hata Kama umepanga chumba kimoja
OA hata Kama unashindwa kulipa Kodi
OA hata Kama hujui kesho utakula nini.

Ilimradi uoe mwanamke unayefanana naye.

Usioe mwanamke mwenye ndoto kubwa ambayo anataka itimie hivi karibuni. Utashindwa, muache aolewe na waliokwisha kufikia ndoto hizo.

Usiyaogope maisha ingawaje yanaogopesha.

Usioe Kwa sababu unaona unauwezo wa kumhudumia Mwanamke na mtoto.
OA umri ukifika, OA ukiwa na nguvu, umri wa miaka 25-33 uwe umeoa.

Umri wa 20-30 uwe na walau mtoto mmoja au wawili.

Maisha hatahitaji kusubiri.
Usijilaumu Kwa lolote sio kosa lako wala la wazazi wako. Ndio mfumo wa maisha upo hivyo.
OA mapema bila kujali mazingira yanaruhusu au laa.

Usiige familia Tajiri, HAO wanachelewa kuoa na pengine kupata watoto Kwa sababu wanaurithi Kwa watoto wao.

Sasa wewe usiwaige.

OA mapema!


Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
DAR ES SALAAM
 
Vijana wa Zama hizi unakuta mtu anasubiri Jambo ambalo hajui linakuja lini.

Ati ataoa siku mambo hakikaa Sawa.

Kwa uzoefu wangu mambo hayawi Sawa mpaka siku tukienda kuzimu
Kwa hali halisi ya mahusiano ilivyo kuowa si lazima.

Ukiona wewe umefikia umri wa kuowa owa aubolewa.


Ona hii, huyu alikuwa anataka kuowa.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linawashikilia Watu wawili wanaodaiwa kula njama na baadaye kumuua Mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Barke Pesa Rashid (30) mkazi wa Ilala Utete Jijini Dar es salaam kisa madai ya kwamba Mwanamke huyo aligharamiwa na Mwanaume hadi kumpangishia nyumba lakini akawa na Wanaume wengine.

"Tukio hilo limetokea January Mosi,2022 Tabata Segerea kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Maridadi ambako tarehe hiyo Mtuhumiwa wa kwanza Mwanaume, Jonsiner Bounser( 34), Mkazi wa Segerea Kalabash Pub alifanya mipango ya mapenzi na Mwanamke aliyemuua baada ya kula njama na Mtuhumiwa mwingine wa pili aliyekamatwa Mwanaume anayeitwa White (33) Mfanyabiashara ya Lori la kuzolea taka Mkazi wa Tabata Segerea"

"Mwanamke huyo alikabwa shingo mpaka kupoteza maisha akiwa katika nyumba hiyo ya kulala wageni, Bounser alikodiwa na White kwa malipo ya Tsh.Milioni 1.7 ili amtongoze na baadaye aende kumuua Mwanamke huyo kwa madai kuwa White alimgharamia sana na kumpangishia nyumba lakini Mwanamke huyo ana Wanaume wengine"

"Bounser amekiri kupewa Tsh. Milioni 1.2 kwa nyakati tofauti kabla na baada ya kutekeleza mauaji hayo na kwamba alikuwa bado anadai Tsh. Laki tano kwa White kwa mauaji ya Mwanamke huyo, uchunguzi wa tukio hilo unakamilishwa na watafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo" ——— Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam
#MillardAyoUPDATES
 
Kwa hali halisi ya mahusiano ilivyo kuowa si lazima.

Ukiona wewe umefikia umri wa kuowa owa aubolewa.


Ona hii, huyu alikuwa anataka kuowa.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linawashikilia Watu wawili wanaodaiwa kula njama na baadaye kumuua Mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Barke Pesa Rashid (30) mkazi wa Ilala Utete Jijini Dar es salaam kisa madai ya kwamba Mwanamke huyo aligharamiwa na Mwanaume hadi kumpangishia nyumba lakini akawa na Wanaume wengine.

"Tukio hilo limetokea January Mosi,2022 Tabata Segerea kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Maridadi ambako tarehe hiyo Mtuhumiwa wa kwanza Mwanaume, Jonsiner Bounser( 34), Mkazi wa Segerea Kalabash Pub alifanya mipango ya mapenzi na Mwanamke aliyemuua baada ya kula njama na Mtuhumiwa mwingine wa pili aliyekamatwa Mwanaume anayeitwa White (33) Mfanyabiashara ya Lori la kuzolea taka Mkazi wa Tabata Segerea"

"Mwanamke huyo alikabwa shingo mpaka kupoteza maisha akiwa katika nyumba hiyo ya kulala wageni, Bounser alikodiwa na White kwa malipo ya Tsh.Milioni 1.7 ili amtongoze na baadaye aende kumuua Mwanamke huyo kwa madai kuwa White alimgharamia sana na kumpangishia nyumba lakini Mwanamke huyo ana Wanaume wengine"

"Bounser amekiri kupewa Tsh. Milioni 1.2 kwa nyakati tofauti kabla na baada ya kutekeleza mauaji hayo na kwamba alikuwa bado anadai Tsh. Laki tano kwa White kwa mauaji ya Mwanamke huyo, uchunguzi wa tukio hilo unakamilishwa na watafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo" ——— Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam
#MillardAyoUPDATES


Kwenye maisha ogopa Ukichaa na uchizi.

Ukichaa ni ugonjwa wa Akili(biological)
Uchizi ni ulozi wa Shetani(spiritually) unaokufanya ufanye mambo ya kishetani.

Hata usipooa au ukioa ukipatwa na moja ya hayo hapo juu umekwisha
 
KUOA SIO LAZIMA NA SIO DHAMBI... OA UKIWA TAYARI NA USIOE KWA KUFUATA MKUMBO...

NDOA NI TAASISI NYINGINE KABISA....!


Kuoa sio lazima Kwa maiti au ambaye mwili hau-function.

Lakini kuoa ni lazima ikiwa mtu yupo Hai na Afya njema.ili asizini.

Lakini kusema kuoa/kuolewa sio lazima wakati mtu anazini ni Dalili ya ushetani
 
Kuoa sio lazima Kwa maiti au ambaye mwili hau-function.

Lakini kuoa ni lazima ikiwa mtu yupo Hai na Afya njema.ili asizini.

Lakini kusema kuoa/kuolewa sio lazima wakati mtu anazini ni Dalili ya ushetani
KWA HIYO UNATAKA KUNIAMBIA WATU WOTE AMBAO MIILI YAO IKO VIZURI HAPA DUNIANI WAMEOA?

UNALAZIMISHA WATU KUOA KWA KIGEZO KIPI?

KUTOKUOA SIO DHAMBI NASISITIZA NA SIO USHETANI
 
Picha linaanza nakula Mlo mmoja Kwa siku ,nalala kwenye box ....

Unataka niongeze mtu mwingine wa kumhudumia ....uko sawa kweli ...


Mbaya zaidi wanawake wanakuwa tegemezi .....

Wanaume siku hizi hatuoi mapema kwa sababu hata hao wanawake hawana mapenzi ,wanatafuta unafuu wa maisha ,ndio maana kutwa kuimba mwanamke anahitaji huduma ,kuhudumiwa akiwa kwenye ndoa ....


Sasa Mimi kijana nianze kulea mtoto wa mtu na kujipa majukumu ya mzazi wake wakati wazazi wake wapo ?...

Huo ndio mwanzo wa vijana kuogopa kuoa ....
 
KWA HIYO UNATAKA KUNIAMBIA WATU WOTE AMBAO MIILI YAO IKO VIZURI HAPA DUNIANI WAMEOA?

UNALAZIMISHA WATU KUOA KWA KIGEZO KIPI?

KUTOKUOA SIO DHAMBI NASISITIZA NA SIO USHETANI


Kama Mwili hauwaki tamaa usioe.

Lakini sio unasema kuoa sio lazima na wakati huo huo unalala na wanawake Kwa zinaa
 
Picha linaanza nakula Mlo mmoja Kwa siku ,nalala kwenye box ....

Unataka niongeze mtu mwingine wa kumhudumia ....uko sawa kweli ...


Mbaya zaidi wanawake wanakuwa tegemezi .....

Wanaume siku hizi hatuoi mapema kwa sababu hata hao wanawake hawana mapenzi ,wanatafuta unafuu wa maisha ,ndio maana kutwa kuimba mwanamke anahitaji huduma ,kuhudumiwa akiwa kwenye ndoa ....


Sasa Mimi kijana nianze kulea mtoto wa mtu na kujipa majukumu ya mzazi wake wakati wazazi wake wapo ?...

Huo ndio mwanzo wa vijana kuogopa kuoa ....


😀😀😀😀
 
kuoa si lazima wala hiayari ni maamuzi ya mtu akiona inampendeza kwa sisi introvert kuoa ni kama tunajinyima furaha ,
Kuish na mtu inahitaji moyo eti kuwa na watoto ni muhimu kwa 22-30 age kuoa ni uko mbeleni
Introvert sio [emoji2][emoji2],
Umenikumbusha uzi mmoja humu unatuponda maintrovert wa kibonho
 
Back
Top Bottom