Kucheleweshwa kwa Mkopo World Bank: Tumkemee Zitto Kabwe kwa pamoja

Kucheleweshwa kwa Mkopo World Bank: Tumkemee Zitto Kabwe kwa pamoja

Kalamu1,

Habari za mwaka mpya?
Zito hajasema ukweli, tangu enzi ya Mwl Nyerere hakuna mwanafunzi aliyepata mimba akaendelea kusoma, ni upotoshaji wa hali ya juu. Watanzania lazima wafahamu kwamba hata nchi kubwa kama USA au UK huwa hawakubaliani kwenye mikakati yao ya ndani lakini linapokuja swala la kitaifa wote huwa kitu kimoja.

Anayekomolewa hapa sio JPM pamoja na baraza lake la Mawaziri etc bali ni wale ambao pesa hizo za mkopo zingewasaidia. Zito pamoja na wanaharakati wenzake wasisahau kitu kimoja. Whether they exist or not Tanzania will be there. Shame on them. BTW WB wameahirisha tu uamuzi wakati wowote ule wakiona Tanzania ina-secure mkopo kutoka nchi rafiki watapiga magoti kwa JPM achukue mkopo.

(I can bet you my last nickel, hivi sasa watu wapo kazini na utasikia kuna nchi watatukopesha pesa kwa bei nafuu zaidi au hata AfDB).
 
WE MLETA MADA NI NANI ALIWAAMBIA WATZ WAFYATUE WATOTO NAYE ATAWASOMESHA? HAYA HAYANA TOFAUTI NA MAUNO YA LUGOLA MWISHOWE KUTUMBULIWA
 
Kama ni kweli kwamba barua hiyo imeandikwa na mheshimiwa Zitto, basi amekuwa muungwana sana, kwani hayo yote ndiyo yalisemwa na Jiwe katika hotuba yake ya kuwapatia kibali watanzania wawafyatue watoto kadri wawezavyo ili naye awasomeshe.

Sijaona uongo wa Mh. Zitto hapo. Wanalumumba msijaribu kupotosha ukweli wa alichokisema Meko.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa na Mimi ndo namshangaa huyu jamaa,sijui anawashwa?.
Kauli ya kufyatua watoto atawasomesha bure ilishatolewa Leo anawatetea?
 
Nashangaa Sana waafrika,Hawa wazungu hamwapendi na mnawaita mabeberu,Kama hatuwapendi na tunawachukia kwa Nini pesa zao tunazitaka?.
Kama wao Ni wabaya na pesa zao tuzione pia mbaya .
 
Habari za mwaka mpya?
Zito hajasema ukweli, tangu enzi ya Mwl Nyerere hakuna mwanafunzi aliyepata mimba akaendelea kusoma, ni upotoshaji wa hali ya juu. Watanzania lazima wafahamu kwamba hata nchi kubwa kama USA au UK huwa hawakubaliani kwenye mikakati yao ya ndani lakini linapokuja swala la kitaifa wote huwa kitu kimoja. Anayekomolewa hapa sio JPM pamoja na baraza lake la Mawaziri etc bali ni wale ambao pesa hizo za mkopo zingewasaidia. Zito pamoja na wanaharakati wenzake wasisahau kitu kimoja. Whether they exist or not Tanzania will be there. Shame on them. BTW WB wameahirisha tu uamuzi wakati wowote ule wakiona Tanzania ina-secure mkopo kutoka nchi rafiki watapiga magoti kwa JPM achukue mkopo. (I can bet you my last nickel, hivi sasa watu wapo kazini na utasikia kuna nchi watatukopesha pesa kwa bei nafuu zaidi au hata AfDB).
Mkuu Ole, ningependa sana nikujibu kwa moyo mtulivu ili unielewe ninachosema, lakini wakati huenda ukanivuruga na kukupa andiko ambalo halikunyooka kama nilivyotaka liwe.

1. Ninakubaliana nawe moja kwa moja kwamba hata enzi za Mwalimu na hadi awamu nyingine zote wasichana waliopata mimba hawakuendelea na shule. Hili ni kweli na liko wazi kwa kila mmoja wetu.

Lakini jambo hili halikuwahi kuwa kikwazo kwa wafadhiri kutoa msaada.
Hii sio kwa sababu Mh Zitto hakuwepo kuwashtaki hao viongozi wake toka enzi za Mwalimu , Mwinyi, Mkapa hadi Kikwete. Kikwete alilizungumzia hili "Kiuswahili swahili", na hakuna aliyelichukulia kwa uzito mkubwa likaishia hapo.

Sasa tofauti usiyotaka kuikubali kati ya huyu aliyepo na hao wengine ndilo tatizo. Tatizo sio Zitto.
Alivyolichukua na kulitangaza, na huku kwa upande mwingine akihimiza wanawake 'wafyatue,', 'contrast' ya ajabu sana.
Staili ya "Uwasilishaji" wa jambo, ukiambatana na hali nyingine iliyopo katika serikali yake, wewe bado huoni tofauti hiyo kubwa kati ya yeye na watangulizi wake?

Anavuta 'hisia' na 'attention' sehemu nyeti kabisa inayohitaji uangalifu mkubwa sana kuishughulikia. Hilo ni tatizo si katika jambo hili pekee, bali tumeona hata katika mambo mengine, kama ile mikataba ya madini. Mambo mazuri tunayotamani, lakini utekelezaji wake unatia ukakasi mkubwa.

Swala la hizo nchi kubwa, sikubaliani kabisa nawe hasa kwenye swala kama hili la ndani kwa ndani. Nadhani unachanganya au huna uelewa na maswala ya watu hao.
Hata hivyo, tofautisha kabisa hizo nchi na hizi zetu. Wao hawalilii misaada kama hiyo ya Benki kuu kuwasomesha watoto wao.
Usijifanye kutotambua sababu inayowafanya akina Zito waende huko kuomba msaada kama huo wa kuzuia. Ni kwa sababu hapa nyumbani hata wakilia machozi ya damu hawawezi kusikilizwa, sana sana wataishia gerezani au ya akina Lissu yanawapata. Hayo huyaoni huko uliko wewe, na bado unatoa mfano kama huo?

Unajiliwaza eti Benki wameahirisha tu, baadae watazitoa hela. Tunaomba iwe hivyo, kwa sababu funzo tayari litakuwa limewasilishwa kwenu. Kama nyinyi ni watu wenye akili kichwani hamuwezi kutojifunza chochote tokana na funzo hili.

Hata dunia itakuwa imewawashia mwanga kufahamu mapungufu yenu.

"Nchi marafiki watapiga magoti"
BTW WB wameahirisha tu uamuzi wakati wowote ule wakiona Tanzania ina-secure mkopo kutoka nchi rafiki watapiga magoti kwa JPM achukue mkopo. (I can bet you my last nickel, hivi sasa watu wapo kazini na utasikia kuna nchi watatukopesha pesa kwa bei nafuu zaidi au hata AfDB).
Hapa ndipo ninapokudharau kabisa.
Huko mwanzo tulipoanza kujibishana, kuhusi ile thamani ya shilingi ya Tanzania na dollar ya Kimarekani na kuhusu Waziri Mkuu Edward Sokoine, kidogo nilidhani wewe unao upeo kiasi fulani.
Sasa angalia mistari kama hiyo niliyoi-'quote' hapo juu!

Nadhani inanibidi nikupe pole sana.
 
Nimesoma kwa ufasaha Taarifa zilizoandikwa na Mwandishi Tom Wilson kwenye Gazeti la FINANCIAL TIMES akiwa Uingereza kuwa baadhi ya viongozi wa Jamii ya Tanzania wakiongozwa na Mbunge wa Kigoma Mjini Ndugu yangu Zitto Kabwe kuiomba Benki Kuu ya Dunia kuahirisha kuipa Tanzania Dollar Milion 500 za mkopo kwa kile kilichoelezwa kuwa kufanya hivyo ni kuwapiga kofi la uso wanawake ambao wamezuiliwa kusoma huku wakiwa na ujauzito kwenye shule za Tanzania.

Kupitia Barua iliyoandikwa na kutumwa kwenda Benki ya Dunia na Zitto Kabwe wiki iliyopita na kupokelewa na Bodi ya Benki hiyo, Zitto ameandika taarifa za uongo kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Magufuli imewanyima haki wanafunzi Wajawazito kusoma na badala yake inawahamasisha wanawake kuzaa kwa kadri ya uwezo wao ili kuongeza idadi ya Watu wa Tanzania. Nitanukuu "Excluded pregnant Girls from School and encourage women to free their ovaries to boost the country's population"

Ndugu Zitto Kabwe na washirika wake wanaamua kupotosha Hotuba za Rais kwenye maeneo tofauti tofauti kwa makusudi ili kukidhi matarajio yao.

Kuunganisha Hotuba za Mh. Rais za maeneo tofauti tofauti ili kuleta maana isiyo sahihi ili kukidhi matarajio yako ni makosa lakini pia ni dhambi.

Kupitia Barua yake Zitto Kabwe ya kushinikiza Tanzania kunyimwa fedha na Benki ya Dunia ameandika pia kuhusu fedha za kupunguza umasikini dola Milioni 450 ambazo ziliidhinishwa mwezi Septemba na benki hiyo kwa kujiridhisha kuwa Tanzania inafuata matakwa ya masharti ya fedha hizo, Zitto ameenda mbali zaidi na kuandika kuwa hakuna kilichobadilika!

Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa Mikoa ambayo Mwanafunzi wa Kike anakabiliwa na Changamoto Mbalimbali katika Masomo yake na Kwa kutambua hilo Serikali ya Tanzania kupitia mpango wa Elimu Bila malipo haukumtenga mwanafunzi wa Kike.

1. Mpango wa Elimu Bila malipo hauna Ubaguzi

Fedha za Ruzuku ya Elimu bila malipo Chini ya mwongozo uliotolewa Tar 28 Decemba 2015 umeelekeza fedha za Ruzuku kwa kila mwanafunzi wa Shule ya Msingi kuwa ni Tsh 6,000 na Sekondari Tsh 25,000 kwa kila Mwanafunzi kwa mwaka bila kujali kuwa ni wa Kiume ama wa Kike na fedha hizo zinatumwa Shuleni Moja kwa moja na kufanya kwa mwaka Serikali kutumia Tsh 12,329,791,183 kwa mwaka. Je, wasichana wetu wamenyimwa haki ya Kusoma?

2. Serikali imekuwa ikifuatilia kesi zinazohusiana na Wanafunzi wanaobebeshwa mimba na Wahusika wamekuwa wakiwajibishwa kwa Mjibu wa Sheria

Kwetu sisi ambao tumekuwa viongozi wa wananchi na kushughulika na matatizo ya wananchi wetu moja kwa moja tumekuwa tukikimbizana na watu wanaowapa mimba wanafunzi wetu na watu wanaokutwa na hatia hiyo wamekuwa wakiwajibishwa.

Kwahiyo maneno ya Zitto kuwa wasichana wenye mimba wamekuwa hawaruhusiwi kusoma na badala yake wanahamasishwa kuongeza jitihada katika kuongeza idadi ya watu Tanzania si za kweli kwani nchi inayowahamasisha wasichana kubeba mimba haiwezi kuweka sheria Kali za kuwaadhibu wanaowabebesha mimba wanafunzi wakati lengo ni kuongeza watu wa Tanzania.

3. Mfumo wa Elimu Nchini umewezeshwa kuwasaidia watu walioacha masomo kwa sababu mbalimbali ili kutimiza ndoto zao

Vituo mbalimbali vya Mitihani na Program za muda mfupi (miaka 2) inatambuliwa na Serikali ya Tanzania kwa miaka kadhaa sasa ili kuendeleza dhana ya Elimu kutokuwa na mwisho.

Ni dhahiri kwamba kama Tanzania ingekuwa inapinga mwanafunzi aliyebeba mimba kukosa haki ya kujielimisha isingetambua mifumo hii inayowarudisha watu hawa kupata haki hii ya Elimu na bado matokeo ya Mitihani yao inawawezesha kujiunga na Elimu ya Juu. Kwa hiyo si kweli kwamba wananyimwa haki ya Elimu.

4. Waziri wa Elimu ni Mwanamke.

Hili nalo pia linaweza kuwa chachu ya kuonyesha ni jinsi gani Serikali ya awamu ya 5 inadhamini mtoto wa kike kwenda shule. Mimi nimeona hivyo sijui nyie mnaonaje. Siamini kama Prof Ndalichako, mama huyu wa Kigoma anaweza kusimamia Wizara ambayo inachimbia handaki jinsia yake. Siamini pia kama Rais Magufuli anaweza kumteua mwanamke kwa lengo la kuzika matumaini ya wanawake kupata Elimu. Inahitaji kuwa na akili ya kichaa kuelewa lengo la Zitto katika kuamusha hisia za jinsia fulani kutengwa kielimu.

Mikopo na misaada inayotulazimisha kuchanganya wajawazito na wasio wajawazito hiyo inatakiwa kuangaliwa kwa macho na akili.

Mkuu wa nchi kukemea tabia za kubebesha na kubebeshwa mimba wanafunzi hapo anakuwa anatimiza wajibu wake. Tafsiri ya maneno ya Rais inayobebwa na mtu kupeleka sehemu fulani kwa lengo la kupotosha huko ni kukosa uzalendo.

Kuandika barua kwa siri kwenda kwenye taasisi ya fedha duniani kwa lengo la kudhuru nchi yako huku ukijua hauna nchi nyingine ya ahadi pia ni kiwango cha juu cha usaliti wa Utanzania wako. Ishitaki Serikali ya Tanzania kwa Watanzania wenzako na siyo kwa Mabeberu pamoja na mawakala wa Ukoloni mamboleo ambao hata hivyo uhusiano wetu na wao unatakiwa uwe wa kutumia akili sana.

Hata hivyo nimeona mrejesho wa Msemaji wa Benki ya Dunia akisema kuwa "Kutakuwa ni kutokomaa ikitokea yeye akazungumza chochote wakati Bodi ya Benki kuu ikiwa haijalitathmini jambo hilo "

Natambua matamanio ya mwanasiasa yoyote kama Zitto ni kuona Kunatokea Agenda yoyote inayoweza kusaidia Chama chake kukua na kutimiza malengo lakini napenda nimueleze kuwa Urais hautafutwi hivyo.

Siku ukiona unasaidiwa na Mataifa ya Nje kutawala Nchi ambayo mwanzoni mlipambana kwa hali zote muachwe ili muwe huru ujue ndio utakuwa mwanzo wa kuwakaribisha Wakoloni tena.

Upinzani wenye nia njema na Tanzania unajishughulisha na Watanzania wenyewe kwenye nchi yao, nenda Kusini, kasikazini Magharibi na Mashariki na kila kona zote za Tanzania, wakikuelewa watakupa Nchi. Urais wa Tanzania haupo mkononi mwa Benki kuu ya Dunia wala Ulaya.

Umewaacha Watanzania kwenye ardhi yao wakiwa wanafaidi mema ya Magufuli itakuwa ni ngumu kwao kukuelewa.

Mwambieni Zitto Serikali ya Magufuli anayoitumu vitu vingi vibaya inaendelea kumlipa Mshahara wake wa Mwezi na hajawahi kukataa hata siku moja Mshahara huo.

Najua atasema ni haki yake kulipwa lakini pia akumbuke kuwa haki hiyo inakumbukwa na Serikali ile ile anayoituhumu kwamba inavunja haki za Binadamu.

Ninasikitika sana kwamba Serikali ya awamu ya nne ilikuwa na mfumo wa kufanya kazi na Zitto lakini hii ya awamu 5 kidogo imejitenga nae kwa kiasi fulani na hivi ndivyo ameamua kuishi na Serikali hii.

Ni matumaini yangu kuwa sasa umefungua ukurasa rasmi wa kuachana na wewe kwenye vyombo vya uwakilishi.

Nchi haitafutwi hivyo.

#KigomaVoteWisely2020 #ourleaderisourproblem

Elia Fredrick Michael
Buyungu, Kakonko Kigoma
Huwa hatuna tabia ya kuwasikiliza malaya wa siasa huweza uza vyote bila mipaka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nani anaeathirika na kunyimwa huo mkopo?.. Zito sio mzalendo ni mnafiki
 
Wanabodi za jioni!

Tangu naanza kufuatilia siasa zetu!nimekuwa nikimfuatilia huyu zitto kama mjenga hoja mzuri na mwanasiasa machachari hapa nchini!

Lakini kuna baadhi ya watu wamekuwa wakimhusisha na kitengo yaani usalama wa taifa!Swali la kujiuliza kama ni mwana usalama kwanini aivue nguo serikali inayomlipa mshahara??Lengo lake ni nini?Kwenye sakata la kunyimwa mkopo nchi yetu na Benki ya Dunia zitto ana mkono!kwenye sakata la kupinga kukua kwa uchumi wetu zitto yumo!kwenye lile sakata la Richmond alikuwemo!Karibia kila jambo ambalo linaipa kibano serekali ye yumo!sasa najiuliza anakuwaje mtu wa kitengo?

Hadi sasa ndio kiongozi pekee wa upinzani ambae hana kesi mahakamani japo anaongoza kwa kutoa hoja za kupinga na kuhujumu taarifa za serikali!Je serekali inampuuza?Je hana madhara kama Lema,Mbowe?Je serekali ina furahia hoja zake?Au ameshindikana wamemshindwa?Au ana nguvu za kipekee ambazo zinamlinda kuliko mwanasiasa mwingine wa upinzani?

Ana nini huyu zitto ambacho wenzake hawana? Yeye ni nani hadi ameshiriki Benki ya Dunia isitishe mkopo wake halafu bado anadunda tu? Mbona Tundu lissu alionywa kwa maneno hadi yakamkuta makubwa?

Anaemjua Zitto ni nani atuambie maana anaonekana sio wa kawaida huyu!au ni mzimu unaoogopwa??Angekuwa Lema je? ambae aliota tu miezi minne ndani!

Wanabodi naombeni mnisaidie kumwelewa Zitto Zuberi Kabwe!!!
 
Zito ni mwanasiasa tu ni mtu wakucheza na maslahi yake akiyakosa hubuni mbinu nyingi kuhakikisha anaogopwa
Alicheza na Makapuni ya madini kisha Richmond akacheza na mabilion yalipo uswis hasa kuwatishatisha
Alijipenyeza vizuri kwa baadhi ya viongozi enzi za Jk. Sasa huyu JPM kamtema anahasira sana


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitengo uwatumia watu waliowekwa upande mwingine ili kupush agenda fulani au kuzuia dili fulani kama halina maslahi kwa taifa.

Ili kisionekane kama kimefanya kazi direct ufanya kazi indirect.

Usalama wa taifa kiufupi ndio kazi yao kubwa kuzuia wakifeli kuzuia wanavujisha dili lilivyofanyika.

pande zote hizo Zitto anaonekana.

What if zile 500$ zilitaka kutumika vibaya? kinyume na tunavyoaminishwa?
 
Zito ni mwanasiasa tu ni mtu wakucheza na maslahi yake akiyakosa hubuni mbinu nyingi kuhakikisha anaogopwa
Alicheza na Makapuni ya madini kisha Richmond akacheza na mabilion yalipo uswis hasa kuwatishatisha
Alijipenyeza vizuri kwa baadhi ya viongozi enzi za Jk. Sasa huyu JPM kamtema anahasira sana


Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa mbona hana kesi hata moja mahakamani?
 
Zitto Ni Mwanasiasa pekee aliyekosana na mungu Mbowe lakini ameshindikana kupotea, aidha kufa au kufa kisiasa .

Na Kibaya Zaidi Wafuasi Wa Mbowe Wakiwemo Wachagga na Wapare Hawajakata Tamaa Ya Kupambana Naye.

Yaani huwezi kuwakuta wanamponda Lowassa Wala Sumaye Na Kuwaita Wanatumika Na CCM.

Na Kibaya Zaidi Jamaa Anavyozidi Kufanikiwa Ndio Kabisa Wanaumia Sana Roho.
 
Back
Top Bottom