Kuchukua mkopo benki na kujengea nyumba ni jambo jema lakini hasara yake ni kubwa

Kuchukua mkopo benki na kujengea nyumba ni jambo jema lakini hasara yake ni kubwa

Kulipa kodi 400000 kuna reflect kipato chako. Maisha ya sasa vijana tunavipato vidogo. Ukiwa na uwezo wa kulipa hiyo kodi, ni bora ukope ili pesa uliyotakiwa kulipa kodi ifanye marejesho.
Nakubaliana na wewe kabisa, unalipa kodi laki 400,000 kwa mwezi, unashindwa nini kukopa na marejesho yakawa hiyo gharama ya kodi unayolipa kila mwezi?
 
Kama ni mwajiriwa hasa wa serikali, unatake home ya tsh. mil.1.2- 2. na unalipa kodi ya pango ya tsh.250000 - 400000. Nakushauri kopa na hicho kiwango unacholipa kodi kwa mwezi ndo kiwe marejesho ya mkopo bank, utanishukuru baadae. Hata kama unamshahara mkubwa, kundunduliza fedha eti upate ya kutosha kujenga huku tayari unamajukumu mengi ni uongo, utajenga nyumba ukiwa umezeeka na unakaribia kustaafu.
 
Mikopo tunayokopa benki hapa nchini Tanzania zina riba kubwa sana kitu ambacho hufanya watanzania wengi kutofaidika sana na mikopo hiyo. Kwani kuna benki hutoza riba zenye faida ya asilimia 18%-23%.

Watanzania tulio wengi tukishachukua mikopo hiyo hukimbilia kuninua uwanja na kuanza kujenga nyumba, kisha huishi maisha ya shida sana kwa kipindi cha miaka minne mpk mitano. Wapo wengine hukimbilia kununua gari ili waonekane hapa mjini lakini hata uwanja hawana, mikopo hiyo ya benk ina mambo sana.

Wazo la kukimbilia kujenga nyumba kwa kutumia mkopo ni kujitengenezea maisha ya dhiki sana kwani makato huwa makubwa na kufanya kila siku kukimbizana na madeni yasiyoisha. Ushauri wangu na maoni yangu kama unataka kujenga au kununua gari ni bora ujiwekee mkakati binafsi unaweza amua kila mwezi kujiwekea kiasi fulani ambacho unatumia kwaajiri ya ujenzi, utafanya hivyo bila riba wala hasara yeyote.

Mikopo ya benki ni yakuwekeza katika biashara na ili ziongeze kipato na biashara hiyo irudishe mkopo huo yenyewe bila we kuathiri mapato ya kazi yako.

Kuweka pesa kila mwezi au kila sikunkutokana na maingizo yako inawezekana, kikubwa ni uamuzi thabiti na kujiwekea malengo na kuhakikisha unayafikia malengo yako.

Huu ni ushauri na maoni yangu jinsi ninavyoona namna ya kutumia mkopo wa benk kwa faida, lakini hata kama mtu akajenga nyumba ya biashara ni sahihi lakini nyumba ya kuishi ni safi sana lakini kuna hasara kubwa ndani yake.
Unadhani wanaochukua mikopo hawapendi kujiwea akiba? 😆😆😂.

Huo ujasiri ni wa wachache sana.
 
Umesema vema sana,,,na ushahidi nauona kwa watu kadhaa wanaonizunguka.. Ila ni vzr kukopa ukazalisha kuliko kukopa ukajenge,,, mm hua nakopa tena sana tu ila sikop kama sina hela,nikitaka kununua kitu labda cha 5m. Nahakikisha hiyo hela ninayo,then naenda kukopa ile ile 5m,baadae nanunua nachotaka then ile hela niliyonayo naiweka kwenye mzunguko inalipa deni,,sijawah kujuta kutumia njia hii
Mimi Kukopa sijawahi kwanza naogopa mikopo ila ni bingwa wa.ubahili na saving,Huwa nasevu 60% ya kipato change.
 
Kama ni mwajiriwa hasa wa serikali, unatake home ya tsh. mil.1.2- 2. na unalipa kodi ya pango ya tsh.250000 - 400000. Nakushauri kopa na hicho kiwango unacholipa kodi kwa mwezi ndo kiwe marejesho ya mkopo bank, utanishukuru baadae. Hata kama unamshahara mkubwa, kundunduliza fedha eti upate ya kutosha kujenga huku tayari unamajukumu mengi ni uongo, utajenga nyumba ukiwa umezeeka na unakaribia kustaafu.
Kiujumla kama una salary take home ya hicho kiasi Kukopa ni bora maana unaweza pata pesa nyingi ya kufanyia masuala yako kuliko kudunduliza kwa saving.
 
Ni mawazo mazuri lakini ardhi siku hizi ni gharama sana, kama wewe ni mwajiriwa na kazini kidogo una ka position, unalipwa milioni 2 kwa mwezi. mpaka zifike nyumbani una 1.4. hapo hujalipa pango unapokaa, gharama za maisha ya kila siku, hujawasaidia wazazi na hapo kati kati watoto wa shangazi pia wamekuja kuomba msaada wa MRI scan ya mama yao.

Unataka kununua kiwanja, kwa hadhi yako maeneo unayotaka kuishi waliowahi wanauza kuanzia milioni 40, kuwa maelewano inafika 35 mpaka 30. Ni lini utaweka pesa hiyo? Ni kheri uchukue mkopo uanze kujenga hata banda, unaweza kumaliza ujenzi mkopo ukiisha.
Watu wa Dar mna tabu na maisha magumu Sana yaani kiwanja mil.40? Ni City centre au residential plots za kawaida?
 
Kuna jamaa yangu ana nyumba 5 mpaka ss kutokana na mikopo,

Mwanzon alikuwaga anajenga then aksihamaliza boma anakopa na kufanya finishing then anapangisha, mkopo ukiisha anafanya the same. mwaka jana amekopa 50M/5yrs akamaliza ujenzi wa nyumba within 3month na kuipangisha. Anasema kwa kusaidia na nyumba nyingine mkopo wake utaisha after 3/3.5yeras instead ya 5 years

Hivi sasa anajidunduliza atafute eneo kubwa aje kujenga nyumba 3 houses kwa mikopo hiyo hiyo ( kwa dhamana ya one house plus salary yake)

Advantage aliyonayo ni kuwa anakopa kutumia mshahara then makato ya salary plus kodi ya hizo nyumba ndo zinamsaidia kulipa.

Sofar naona yuko vzr, kama anapata 1.2M/month na i think its a good business model
Salary ikiweza kukudhamini kupata hizo 50 basi atakuwa na kaposition au ni senior staff..

Lakini salary za Kukopa sijui mil 2-5 kwangu ni useless kama unaishi mjini maana tija yake ni ndogo ila kwa walio Vijijini kwenye kilimo inawatoa fasta.
 
Kuna mdada moja alikuwa anatufundisha fom 5 alitokea uswizi alituuliza kila moja malengo na ndoto zetu za badaye wengi wetu walikua wanasema nikimalize niajiliwe kisha nioe -nijenge nyumba yangua ys kuisihi na nininie gari langi la kutembela.yule dada alishangaa sana kwanza akauliza kwa nini wengi wenu ndoto zenu zinafanana na akashangaa akauliza kwani huku ni rahisi kujenga hadi kila mtu anataka awe na nyumba??
Hamna aliyesema anataka aanzishe kampuni,hamna aliyesema anataka kuwa mwanasiasa,hamna aliyesema anataka aanzishe mradi fulani aajili watu kwa kweli yule dada alishangaa sana!
Urahisi wetu unatokana na upatikanaji wa kiwanja,tofauti na Ulaya ardhi ni ishu ila kwenye materials za ujenzi ni simple.

Pia si unajua no regulations tunajenga kiholela na tunajenga vibanda sio nyumba za standards
 
We yaelekea bado una panga au unaishi kwenye nyymba ya baba yako, ya urithi ama unaishi ukweni. Huwezi jenga nyumba Kia kudunduliza ili zijae ndo uanze ujenzi, hiyo itakuwa ni kukosa akili labda kama unaishi kwa wakwezo. Ndo maana nikasema we hujui kujenga ilivokuwa kazi kubwa ukizingatia gharama za ujenzi zinapanda kila mwaka. Huwezi mfananisha mtu anaekopa pesa akajenge na anaekopa pesa akafanyie biashara. Hao watu wana malengo tofauti na furaha yao ni kuona malengo yao yanafanyika. Hebu jaribu kujifikirisha kidogo Kia mtu aliekopa pesa miaka 5 ilopita na kujenga nyumba na yule aliedunduluza tangia wakati huo ili aanze ujenzi mwaka huu. Anglia bei za vifaa na gharama za wakati huo na sasa. Bei ya kiwanja miaka 5ilopita na bei ya sasa. Kumbuka katika kufikia malengo yako huwezi epuka risk. Angalia nyakati hizi za Magu ambapo Niagara nyingi zimeanguka na watu kujinyonga kwa kushindwa kilipa marejesho benki. Kopa ili kutimiza ndoto zako na sio blablaa za vijiweni. Hakuna raha na faida kama kuishi kwenye nyumba ya jasho lako we na mkeo na wato wako. Zaidi ya hapo ni utumwa ambao kila siku inakubidi umwombe Maulana akunasue.
Kudunduliza ni majanga, gharama za maisha zinaongezeka kiasi kwamba huwezi sema natafuta milioni 10 nije kujenga 2025 .
 
Nenda Wizara ya Ardhi gorofa ya 9, utapata maelezo yote, lazima uwe mfanyakazi wa UMMA. Ni 2% interest only, kuna benefits nyingi sana kwa wafanya kazi!
Ukijenga kwa mkopo wa mortgage ni nafuu kuliko mkopo wa commercial banks.
 
Kusema unadunduliza ela ya kununua Gari au kununua kiwanja ni kitu kigumu kidogo coz utapatwa na mahitaji mengine ambayo utatumia hiyo hiyo ela unayosema unadunduliza

Cha msingi ni kutokuwa na source of income moja tu, ili uweze kufanya mambo yako kwa wakati,pia Saccos ni nzuri maana zina riba ndogo sana

Bank wacha wakopeshane wenyewe tu unaweza kufa siku si zako
Inategemea na taasisi uliko,mimi ni junior staff kwenye taasisi x na uwezo wangu wa kudunduliza kwenye salary na posho unanipa Kati ya mil.8-10 kwa mwaka so naweza ku skip mikopo kwa sababu pia naiogopa..
 
Mikopo tunayokopa benki hapa nchini Tanzania zina riba kubwa sana kitu ambacho hufanya watanzania wengi kutofaidika sana na mikopo hiyo. Kwani kuna benki hutoza riba zenye faida ya asilimia 18%-23%.

Watanzania tulio wengi tukishachukua mikopo hiyo hukimbilia kuninua uwanja na kuanza kujenga nyumba, kisha huishi maisha ya shida sana kwa kipindi cha miaka minne mpk mitano. Wapo wengine hukimbilia kununua gari ili waonekane hapa mjini lakini hata uwanja hawana, mikopo hiyo ya benk ina mambo sana.

Wazo la kukimbilia kujenga nyumba kwa kutumia mkopo ni kujitengenezea maisha ya dhiki sana kwani makato huwa makubwa na kufanya kila siku kukimbizana na madeni yasiyoisha. Ushauri wangu na maoni yangu kama unataka kujenga au kununua gari ni bora ujiwekee mkakati binafsi unaweza amua kila mwezi kujiwekea kiasi fulani ambacho unatumia kwaajiri ya ujenzi, utafanya hivyo bila riba wala hasara yeyote.

Mikopo ya benki ni yakuwekeza katika biashara na ili ziongeze kipato na biashara hiyo irudishe mkopo huo yenyewe bila we kuathiri mapato ya kazi yako.

Kuweka pesa kila mwezi au kila sikunkutokana na maingizo yako inawezekana, kikubwa ni uamuzi thabiti na kujiwekea malengo na kuhakikisha unayafikia malengo yako.

Huu ni ushauri na maoni yangu jinsi ninavyoona namna ya kutumia mkopo wa benk kwa faida, lakini hata kama mtu akajenga nyumba ya biashara ni sahihi lakini nyumba ya kuishi ni safi sana lakini kuna hasara kubwa ndani yake.
Unatak kujenga hoja gani ? Kuwa mfumo wa mortgage haufai Tz?
 
Wadanganye wenzio nimekopa nimejenga kanyumba kangu na kausafiri kangu navimba tu mjini sidaiwi na mtu zaidi ya benki na Wala sijali na siwazi halafu silingi Wala Nini majirani wananionea tamaa kopa Fanya Mambo ya maana usishinde bar[emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nyie pigeni kalele tutakutana uzeen maisha ni nyumba.kama uko single endelea kupanga lakin Kama upo double napita miaka 3 unakuja huku unatembea labda huwe hanisi.
Nyumban ni furaha
Nyumba Ni comfortable
Nyumba Ni heshima ya ndoa
Nyumba inaokoa gharama zisizo na lazima.
Kijana wew fuata mkumbo utaamuka jua limeshazama.
Miaka 3 mi nne kitu gani?? Wewe una skill ya kurun biashara itakayotoa faida ya nondo 50@ 27000/= cement alreast mifuko 150@ 16000/= bado kiwanja....
Acha uzembe kopa ujenge upate heshima ya ndoa
 
Kiujumla kama una salary take home ya hicho kiasi Kukopa ni bora maana unaweza pata pesa nyingi ya kufanyia masuala yako kuliko kudunduliza kwa saving.
"...maana unaweza pata pesa nyingi ya kufanyia masuala yako ...." Ss hapo pesa itatoka wap? mana utakua na kaz mbili marejesho + kodi that's means utaendelea kujibana tena sana.

Sijui... Labda mm cjui hesab lakin nachokiona km unaweza kulipa deni la mkopo kwa MSHAHARA WAKO that's means unaweza kujenga bila hata kuhitaji huo MKOPO (kwa kuptia savings / kudunduliza) bila kua na stress za marejesho, cjui naeleweka hapo?!.
 
"...maana unaweza pata pesa nyingi ya kufanyia masuala yako ...." Ss hapo pesa itatoka wap? mana utakua na kaz mbili marejesho + kodi that's means utaendelea kujibana tena sana.

Sijui... Labda mm cjui hesab lakin nachokiona km unaweza kulipa deni la mkopo kwa MSHAHARA WAKO that's means unaweza kujenga bila hata kuhitaji huo MKOPO (kwa kuptia savings / kudunduliza) bila kua na stress za marejesho, cjui naeleweka hapo?!.
Utajenga plus biashara afu faida utatumia kufanya marejesho,kula na kukuza biashara.

Tunaamini kwamba biashara yenye mtaji mkubwa/mzunguko mkubwa ina returns kubwa pia.
 
Kuna tofauti kati ya biashara na uwekezaji

Japo zote zinahusu capital na revenues.

I prefer uwekezaji coz ninakuwa huru kufanya michakato mingine ,my money works for me while i ain't around.

Siku za mwanzo uwekezaji una returns ndogo ila kadri siku zinavyozidi kwenda value inaongezeaka na returns pia zinakuwa

Anko wangu mmoja alinunua kiwanja mbezi beach miaka ile ya 90 sidhani hata milioni moja ilifika.

Akajenga nyumba nzur ya kisasa nikikadiria kwa bei wakati upe labda aound 50-60m ila leo nyumba ilipo hapo mbezi beach akitaka aiuze hakosi around 500m

Alichofanya kaivunja vunja na kwa staili ya kupangisha chumba sebule jiko choo cha ndani.

Wapangaji wanapagombea wanalipa advance kabisa anakunja kila unit 600k kwa mwezi ana katoa unit 6 pale maana lilikuwa jumba kubwa na lote limejaa

Yeye kahamia bunju huko alijenga ingine.zamani


Ndani ya miaka 3-4 anakula faida tu akiwa havuji jasho akiwa kalala usingizi au anakunywa wine home kwake

3.6m per month sio ndoho
 
Back
Top Bottom