Elections 2015 Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...

Elections 2015 Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...

Halafu bila aibu eti wanakuja kutuomba kura! Hivi wanatuonaje?
Wapinzani wanavyotuona ndivyo CCM inavyotuona na inavyotuchukulia, na sisi wananchi tunaendelea kufanya vile vile kila baada ya miaka mitano, ni unachukua... unaweka ... waa!.
P
 
Mkuu JokaKuu , mimi ni katika wale tulioingia enzi zile za chama kimoja, we had no options you have to join it, hivyo tulipoanza mfumo wa vyama vingi, we had options lakini ukweli ni kuwa chama kwa maana halisi ya chama, chama ni kimoja tuu, the one and only CCM! .
Mimi kozi mwana mandanda, kulala njaa kupenda, sivizii makombo, ni kama kuku tuu wa kienyeji, nachakura.
P

..Ccm ni Mwenyekiti na genge lake la watu wachache.

..Nyinyi wengine mpo kuwezesha ufisadi, unyama, au ukatili wao.
 
..Ccm ni Mwenyekiti na genge lake la watu wachache.

..Nyinyi wengine mpo kuwezesha ufisadi, unyama, au ukatili wao.
Hapana!, CCM sio watu, sio Mwenyekiti na viongozi na wanachama, CCM ni ideology institution, ndio maana mtashangaa sana kuhusu mgombea urais wa CCM 2025!, umdhanie ndiye, siye!, soma HII
P
 
Wapinzani wanavyotuona ndivyo CCM inavyotuona na inavyotuchukulia, na sisi wananchi tunaendelea kufanya vile vile kila baada ya miaka mitano, ni unachukua... unaweka ... waa!.
P
Asante sana kwa kuvunja mlima huu wa theluji! Wapinzani wasijione wao ni special kwa wananchi!
 
CHADEMA wakijipanga vizuri watazoa kura nyingi sana hasa kura za Wabunge.
 
Wanabodi,

6. Kwa sasa, angalau Chadema, kupitia M4C, imeshagundua adui halisi anayewakosesha ushindi ni nani!, na sasa imejielekeza kwa wananchi wa grassroots level ambao ndio wenye maamuzi ya mwisho na wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu, hivyo concentration ikiwekwa kwenye "changing the mindset" ya wenye maamuzi, kuacha kuchagua kwa mazoea tuu, bali kuchagua kwa sababu yaani making informed decisions, Wananchi, watafunguka macho na akili, na hawatakuwa na sababu tena ya kuendelea kuichagua CCM!.

7. Ili hili liwezekane, wapinzani wasiwe ni watu wa kulalamika na kulaumu tuu kuhusu CCM, bali sasa wajikite kueleza where CCM does wrong, lakini wao wakiingia, watafanya nini tofauti na CCM, na ukichagua upinzani kitabadilisha nini, ili wale wanaoichagua CCM kwa mazoea tuu, wapate sababu za msingi za kutoichagua CCM na kuwachagua wapinzani. Yaani Wapinzani wawape Watanzania reasons za not kuchagua CCM na sio kuibadili tuu badala ya kuichagua CCM waichague Chadema for what?.

8. Mara baada ya uchaguzi wa 2010 na mafanikio makubwa upande wa Chadema, kwenye ile mada yangu ya CCM Imechokwa, CHADEMA Haijajipanga! niliwaeleza Chadema kuwa wao na wapinzani wengine wote bado wako kiuana harakati zaidi, yaani vyama vya kiuana harakati, bado hawajipanga mkao wa kichama tawala tayari kwa kushika dola, lakini kwa kwa sasa kupitia M4C, Chadema wanaonyesha dalili za kujipanga japo bado wanakabiliwa na madhaifu haya na yale, yakiwemo, lile koti la ukanda, udini, ukabila na ubinafsi wa "umimi" etc.

16. Suppose 2015, Watanzania tutakuwa Milioni 50 wenye sifa za kupiga kura ni milioni 30, hawa wote wakihamasishwa kujiandikisha na kujitokeza kupiga kura, mgombea wa CCM atajipatia kura zao zile milioni 5 za wanachama wao kwa mujibu wa tovuti ya CCM, halafu hizo kura milioni 25 zimuangukie mgombea wa upinzani, hata NEC ya CCM, wachakachue vipi, there will be no way out!, hivyo adui yetu mkubwa sio CCM, bali ni Watanzania wanaipigia kura CCM! na Watanzania wengi zaidi ambao hawajiandikishi na hata wakijiandikisha hawajitokezi kupiga kura!. The magic ni uhamasishaji na reaching out kuwafikia!.

17. Sasa ili kuwafikia Watanzania wote -haswa hawa grassroots level na kuwaamsha waliolala, Chadema haiwezi kuwafikia Watanzania wote kwa kutegemea maandamano na mikutano ya hadhara na mass media za wengine. Chadema lazima wawe na mass media yake ambayo ita propagate the message of "changing the mindset" ya Watanzania. Chadema wana all the resource kumiliki media yake lakini very unfortunately they are myopic, hawana vision ya kuona mbali kuangalia nje ya box and see a bigger picture. Hawajui kupanga priorities zao. Bei ya gari moja tuu la M4C linatosha kununua transmitter ya Digital ya redio na TV and convert chumba kimoja pale Ufipa into a modern studio! na kuwa na YouTube Channel yake ya live stream na active interactive social media pages, Chadema bila media yake, ni kutwanga maji kwenye kinu! CCM ina media yake na TV yake ya TBCCM, radio zake na magazeti yake, Chadema bila media yake, ikulu wataendelea kuisikia tuu kwenye bomba, 2015 ni CCM tena! .

Wasalaam.

Paskali


NB. Paskali, sasa ni mwanachama, mfuasi na mshabiki wa chama fulani cha siasa, in fact ni kada!. Lakini ni kada Mzalendo contemporary mwenye kutanguliza mbele utaifa na maslahi ya taifa ndio maana licha ya kuwa kada wa chama kingine bado anawashauri vyama vingine the right thing to do.
Tangu lini wewe umetaka Chadema iingie Ikulu?

Amandla...
Mkuu Fundi Mchundo a.k.a Fundi Utumbo Fundi Mchundo ,
Unaweza kusema the motives behind bandiko hili?.
P
 
Mkuu Fundi Mchundo a.k.a Fundi Utumbo Fundi Mchundo ,
Unaweza kusema the motives behind bandiko hili?.
P
Undumila kuwili? Opportunist? Baada ya hapo ukatangaza kwa sauti kubwa kuwa wewe ni kada wa CCM. Hauwezi kuwa kada halafu ukataka mgombea wa urais wa chama chako ashindwe.

Mimi naamini kabisa kuwa mnatambua timu ya Mbowe na Lissu inatishia hegemony ya CCM. Dawa ni kuivunja kwa sababu mnajua taika kuwa Lissu bila structure aliyojenga Mbowe hatafika mbali. Hawa wapambe wa kwenye mtandao watamuacha solemba mambo yakipamba moto. Na CCM itaendelea kupeta.

Amandla...
 
Undumila kuwili? Opportunist?
Naomba kuheshimu mawazo yako.
Baada ya hapo ukatangaza kwa sauti kubwa kuwa wewe ni kada wa CCM.
Ni kweli kabisa mimi ni kada wa CCM ila ni kada Mzalendo, kwangu ni Taifa kwanza, chama baadae, na hili nimelisema wazi hata nilipoomba kuingia Bungeni nilisema wazi, kwanini nataka kwenda Bungeni, na nakwenda kufanya nini
View: https://youtu.be/Qr6j25jFGyI?feature=shared
Hauwezi kuwa kada halafu ukataka mgombea wa chama chako ashindwe.
Kwenye wanachama wa chama cha siasa kuna wanachama mashabiki, wanachama wafuasi na wanachama waumini.

Wanachama mashabiki ni kama mashabiki wa Simba na Yanga, hao ni wakereketwa huwaambiii kitu kuhusu chama chao, ukiwauliza sababu hawana, hawa CCM ikisimamisha jiwe, wanalichagua.

Wanachama waumini,ni wale wenye imani na chama,chama kikiwaletea ujinga wa kuwasimanishia mtu wa hovyo, wanakitosa,na kumchagua mgombea wa opposition!。 Hivi ndivyo alivyofanya Baba wa taifa ile 1995。

Hivyo CCM ilipotuletea ujinga nilihamashisha wana CCM, tuukatae ujinga tuchague the opposition Kinondoni na Siha, tusikubali ujinga huu! hata Mwl. Nyerere alikataa ujinga wa CCM, 1995 akachagua upinzani!

Hivyo hata kwenye urais,CCM ikimsimamisha mgombea asie na uwezo,halafu the opposition wakamsimamisha mgombea safi, Waranzania tunaitosa CCM na kuchagua the opposition!。
P
 
Kuna uzalendo na uzalendo. Ukimpigia debe mpinzani ashinde ubunge nitakuelewa. Lakini sio aingie Ikulu. Nitakuamini tu pale utakapotangaza wazi wazi kuwa huna imani na uongozi wa chama chako kwa sasa hivi.

Amandla...
 
Kuna uzalendo na uzalendo. Ukimpigia debe mpinzani ashinde ubunge nitakuelewa. Lakini sio aingie Ikulu. Nitakuamini tu pale utakapotangaza wazi wazi kuwa huna imani na uongozi wa chama chako kwa sasa hivi.

Amandla...
Kwanza kwenye freedom of expression sio lazima kila mtu kutangaza chaguo lake ndio maana kura ni siri.

Uzuri wangu mimi ni mkweli na muwazi sana, msimamo wangu kuhusu 2025 uko kwenye mada HII

Ila pia nimemtumia ujumbe from time to time kama
Hapa Magufuli alikuwa na kibali kikafutwa! Rais ni kibali, anajitambua? Je, tumsaidie atimize matakwa ya kibali chake ili kisifutwe, au tumuachie mwenyewe?

Na hapa Kuna Kitu Rais Samia Amekisema Kuhusu Kurejea Kizimkazi “Post 2025”. Nashauri na Nasisitiza Wenye Uwezo Kusaidia, Tumsaidie Kumshauri Ukweli!
Na hapa Pongezi Spika Dkt. Tulia umeonesha uwezo na unaweza! Je, tumshauri Dada Mkubwa, ikimpendeza, ampishe Dada Mdogo kwenye lile jambo letu?
P
 
Back
Top Bottom