Kuelekea 2025 tutegemee drama za kutosha

Kuelekea 2025 tutegemee drama za kutosha

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Kuna maswali wanajiuliza wananchi kuhusiana na kucharuka kwa wabuge wa Bunge la CCM kwenye kikao kinachoendelea huko Dodoma.

Napenda kuwakumbusha kwamba tusiwe wasahaulifu sana tukidhani wanaongea kwa maslahi ya nchi. Tujikite kwenye msingi wa hoja zao hasa kuchunguza vyanzo vya hizo hasira feki wanazozionesha leo.

TUJIULIZE
  1. Ni Bunge lipi lilipitisha Bajeti 2022/2023 yenye miiba yote ya kuwachoma wananchi na walipakodi?
  2. Ni Bunge lipi walipitisha sheria wanazozilalamikia leo kuwa ni kandamizi?
  3. Ni Bunge lipi limekuwa linapokea ripoti za CAG na kukwepa eneo la uwajibishaji?
  4. Bunge linalalamikia ongezeko la deni la Taifa wwkati huohuo lilisimama kumuwajibisha Spika Ndugai aliyehoji kasi ya ukopaji uaipzingatia uhalisia wa uwezo wa kulipa?
Turejee kwenye medani ya uongozi
  1. Tunavuna gesi ambayo hatuna haki ya kuipangia bei ya ugavi, leo tunawalaumu vipi wananchi wanaotumia nishati mbadala nje ya gesi huku tukiwapandishia bei hata kama soko la dunia bei imeporomoka?
  2. Tumewaondoa vijana kwenye ujasiriamali kwa kuwapiga marufuku wasifanye uchuuzi kupitia vitambulisho vya ujasiriamali huku wakiambiwa watapangiwa maeneo yao (hewa). Wengi wameshindwa na wakaingia makundi ya kihalifu na wanauawa kabla hakimu hajasoma hukumu...
  3. Mikopo ya 10% za Halmashauri imekuwa haitolewi lakini CAG anaelezea katika ripoti yake kuwa pesa inaenda kwenye vikundi visivyoeleweka na haijarudishwa
  4. Serikali ambayo kimsingi hupaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, inasimamia uvunjwaji wa sheria ya vyama vingi kwa kuzuia mikutano yote huku ikiwahadaa kwa kifurushi cha muafaka kuhusu haki zao kikatiba
  5. Malalamiko ya watumiaji wa huduma za bando kuhusu wizi na uonevu unaofanywa na makampuni ya simu hayapatiwi ufumbuzi badala yake mamlaka ya mawasiliano imewekeza kununua mitambo ya kufuatilia wananchi wanaoikosoa serikali na viongozi wake.

Tutegemee drama nyingi sana kwa sababu waliotengeneza matatizo na mkwamo mkubwa tunaoupitia ndiyo hao hao wanaojifaragua kuwa wana majibu ya matatizo hayo.

Drama za kiinterehamwe
 
Huwa nashangaa hata watu wanapata wapi muda wa kufuatilia hilo bunge la majizi ya kura. Kila kinachofanywa na hilo bunge kwangu ni haramu kwani ni bunge lisilo na uhalali wa umma.
 
Kuna maswali wanajiuliza wananchi kuhusiana na kucharuka kwa wabuge wa Bunge la CCM kwenye kikao kinachoendelea huko Dodoma.

Napenda kuwakumbusha kwamba tusiwe wasahaulifu sana tukidhani wanaongea kwa maslahi ya nchi. Tujikite kwenye msingi wa hoja zao hasa kuchunguza vyanzo vya hizo hasira feki wanazozionesha leo.

TUJIULIZE
  1. Ni Bunge lipi lilipitisha Bajeti 2022/2023 yenye miiba yote ya kuwachoma wananchi na walipakodi?
  2. Ni Bunge lipi walipitisha sheria wanazozilalamikia leo kuwa ni kandamizi?
  3. Ni Bunge lipi limekuwa linapokea ripoti za CAG na kukwepa eneo la uwajibishaji?
  4. Bunge linalalamikia ongezeko la deni la Taifa wwkati huohuo lilisimama kumuwajibisha Spika Ndugai aliyehoji kasi ya ukopaji uaipzingatia uhalisia wa uwezo wa kulipa?
Turejee kwenye medani ya uongozi
  1. Tunavuna gesi ambayo hatuna haki ya kuipangia bei ya ugavi, leo tunawalaumu vipi wananchi wanaotumia nishati mbadala nje ya gesi huku tukiwapandishia bei hata kama soko la dunia bei imeporomoka?
  2. Tumewaondoa vijana kwenye ujasiriamali kwa kuwapiga marufuku wasifanye uchuuzi kupitia vitambulisho vya ujasiriamali huku wakiambiwa watapangiwa maeneo yao (hewa). Wengi wameshindwa na wakaingia makundi ya kihalifu na wanauawa kabla hakimu hajasoma hukumu...
  3. Mikopo ya 10% za Halmashauri imekuwa haitolewi lakini CAG anaelezea katika ripoti yake kuwa pesa inaenda kwenye vikundi visivyoeleweka na haijarudishwa
  4. Serikali ambayo kimsingi hupaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, inasimamia uvunjwaji wa sheria ya vyama vingi kwa kuzuia mikutano yote huku ikiwahadaa kwa kifurushi cha muafaka kuhusu haki zao kikatiba
  5. Malalamiko ya watumiaji wa huduma za bando kuhusu wizi na uonevu unaofanywa na makampuni ya simu hayapatiwi ufumbuzi badala yake mamlaka ya mawasiliano imewekeza kununua mitambo ya kufuatilia wananchi wanaoikosoa serikali na viongozi wake.

Tutegemee drama nyingi sana kwa sababu waliotengeneza matatizo na mkwamo mkubwa tunaoupitia ndiyo hao hao wanaojifaragua kuwa wana majibu ya matatizo hayo.

Drama za kiinterehamwe
Ccm ilishakufa haipo. Inatembelea kamba nyembamba sana ya Dola.
 
Huwa nashangaa hata watu wanapata wapi muda wa kufuatilia hilo bunge la majizi ya kura. Kila kinachofanywa na hilo bunge kwangu ni haramu kwani ni bunge lisilo na uhalali wa umma.
Wanashangaza sana
 
Tukifika 2025 watasimama majukwaani na kulaani kila kitu cha serikali na kuomba nafasi wakafanye rectification. After hapo pesa itatembea kwa watu wachache ili kura ziibiwe then ghafla tutawaona wakishukuru wananchi na kuendelea kujineemesha mifuko yao na vitambi
 
Kuna maswali wanajiuliza wananchi kuhusiana na kucharuka kwa wabuge wa Bunge la CCM kwenye kikao kinachoendelea huko Dodoma.

Napenda kuwakumbusha kwamba tusiwe wasahaulifu sana tukidhani wanaongea kwa maslahi ya nchi. Tujikite kwenye msingi wa hoja zao hasa kuchunguza vyanzo vya hizo hasira feki wanazozionesha leo.

Tutegemee drama nyingi sana kwa sababu waliotengeneza matatizo na mkwamo mkubwa tunaoupitia ndiyo hao hao wanaojifaragua kuwa wana majibu ya matatizo hayo.

Drama za kiinterehamwe
Hasira za waheshimiwa wabunge wetu sio hasira fake, ni hasira bonafide genuine, na sasa bunge linaanza kutimiza wajibu wake kikamilifu kuisimamia serikali.
P
 
Na hata uwajibishwaji na uwajibikaji fake tuutarajie kuanzia Sasa kuelekea 2025. Lengo ni kuwahadaa wadanganyika.
 
Hasira za waheshimiwa wabunge wetu sio hasira fake, ni hasira bonafide genuine, na sasa bunge linaanza kutimiza wajibu wake kikamilifu kuisimamia serikali.
P
Mheshimiwa, inawezekana unayoyasema.yakawa ndiyo dhahiri.

Lakini tutajuaje kuwa wapo serious wakati miaka yote hali huwa hivi kuelekea msimu wa Uchaguzi?

Hawajawahi kuwa serious na maisha yetu. Hebu fikiria Mbunge ana ajira ya miaka mitano lakini masurufu ni mengi kisha hayupo kwenye mpango wa fao la kujitoa. Wakati huo huo mfanyakazi anayekatwa kodi inayoenda kuchangia posho na mshahara wa mbunge anapiga kazi hata mpaka miaka 30 na akistaafu anapangiwa fao kiduchu tena ndundundu na fao lenyewe asilimia hamsini linatokana na makato kutoka mshahara wake.... haruhusiwi kujitoa na amepangiwa kupokea mafao kwa span ya miaka 12 mbele.... nani walipitisha hiyo sheria?

Unanithibitishia vipi kuwa hizi siyo drama wakati wabunge hao hao wanapitisha sheria za ajabu ajabu kama ile ya kumuweka spika juu ya sheria kwamba hatoshtakiwa endapo atastaafu huku akiwa ameacha madudu kibao.

Wanachokifanya ni section ya viral kwenye filamu. Lazima kuwepo na mapigano, mafarakano na hatimaye mapatano mwishoni.

Hilo ndilo lengo la filamu yetu chini ya mratibu aliyewaweka hapo
 
Hasira za waheshimiwa wabunge wetu sio hasira fake, ni hasira bonafide genuine, na sasa bunge linaanza kutimiza wajibu wake kikamilifu kuisimamia serikali.
P

Hao wabunge wangekuwa wameingia bungeni kwa uchaguzi halali wangekuwa na nguvu hiyo. Kinyume na hapo ni wachekeshaji wa mfalme.
 
Mnachushuhudia bungeni ni drama za kuelekea 2025.

CCM inacheza na akili zetu.

Wanaokwapua fedha za miradi ndo hao wasimamizi wa chaguzi ngazi za wilaya.

Hawawezi kukwapua fedha za umma bila kuanzia kamati za fedha za manispaa ambapo Wabunge ni wajumbe wa kamati hizo.

Mabaraza ya madiwani hawasimami na umma kwenye ripoti za CAG kuchukua hatua ama kutoa misimamo.


Serikali ngazi ya KATA ndipo chezo loote linapigwa hapo. Watendaji wa Kata wanaaprove miradi ambayo haina viwango ili wakandarasi walipwe. Hakuna muunganiko wa kiuwajibikaji kwenye fedha za umma kutoka Kata hadi mtaa au kijiji. Miradi yote hufanyika ngazi za mitaa au vijiji lakini kamati za mitaa hazitambuliki linapokuja suala la miradi ya umma.

Haya ndp matokeo ya kukumbatia gunia la misumari (CCM) ambayo inatuaminisha kuwa viongozi wa mitaa, vijiji na vitongoji ni lazima wawe TABULARASA.

Tuamke
Tuikatae CCM kwa vitendo hasa kupitia sanduku la kura
 
Hasira za waheshimiwa wabunge wetu sio hasira fake, ni hasira bonafide genuine, na sasa bunge linaanza kutimiza wajibu wake kikamilifu kuisimamia serikali.
P
Kauli ya sasa ya mhe Spika imezua maswali mazito.

Kama siyo kelele za Watanzania, muswada unaohusu ulinzi wa Maliasili zetu ungesomwa na kujadiliwa kidogo na kupitishwa kwa kishindo
 
Back
Top Bottom