Kuelekea derby ya Kariakoo, Tahadhari muhimu kwa Simba!

Kuelekea derby ya Kariakoo, Tahadhari muhimu kwa Simba!

MTAZAMO

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,675
Reaction score
33,583
Wakuu,

Kipute cha Kariakoo deby kimekaribia, mimi kama shabiki wa Lunyasi nina maoni yafuatayo kuelekea siku hiyo.

1) Ubora wa Yanga ni Nabi, Nabi amefanikiwa kusumbua makocha wengi kimbinu sababu akili zao huzama kwenye wachezaji hatari kama Mayele kuliko akili ya Nabi. Kwa muda mrefu Nabi anamaliza game kipindi cha pili na makocha wameshindwa kudhibiti hilo.

2) Ubora wa viungo wa Yanga, sehemu ngumu na muhimu Yanga ni kiungo. Plan zote zinaanzia hapo na kufia hapo. Lazima uwe na viungo wenye intensity ya kutosha dakika zote ikibidi sub ili kulinda utimamu wa timu.

3) Fiston Mayele ni mchezaji hatari akiachwa peke yake maeneo hatari. Huyu akiwa maeneo mengine apewe uhuru lakini akiwa kwenye 18 lazima awe na destructive player kama Putin. Akiwa peke yake mpira ukamfikia akiwa kwenye hatari mtaufuata nyavuni.

4) Kama nilivyosema Nabi game ngumu anashinda kipindi cha pili. Sub zake na mabadiliko ya positions uwanjani kipindi cha pili lazima haraka sana yafanyiwe home work na ku switch plan. Makocha wengi wa bongo wakiona 1st half wana droo au wanaongoza wanafikiri wamekamata game kumbe kipindi cha pili Nabi ndio anacheza baada ya kujua strength and weakness za mpinzani.

Hitimisho:
Kocha Robertinho ameifunga Yanga mara mbili na amefanikiwa kwa aina ya soka alilokuwa akitumia huko. Mara nyingi anacheza direct football na double striker! Huu mfumo ni complicated kueleweka kwa mashabiki hasa wa Simba!

Kocha wa Simba ni hatari timu yake ikiwa haina mpira kuliko ikiwa na mpira! Hili imechukua muda wachezaji kumuelewa na sasa wameingia kwenye mfumo.

Kama wachezaji wakifata maelekezo yake vizuri na pia kama kocha mwenyewe akimzidi ujanja Nabi hasa kipindi cha pili basi Simba atashinda goli nyingi.

#nguvumoja
 
Huu nao uchambuzi? Kazi IPO, badala ya kugombea Simba angalau iambulie share unaongelea habari za Yanga hii kufungwa goli nyingi na Simba?

Hakuna cha kujadili hapa, maana umejitia upofu na umeikataa reality.
Naona unajenga utetezi mapema. Bila kumfunga mtani hata ubingwa haunogi shekhe [emoji23]
 
Sawa kijana wa Nabi, mwanasimba mmoja,pamoja na kujaribu kumwibia baba ujanja, kesho kutwa kwa uchache tunawachapeni.🖐️
 
Changamoto ambayo wengi wataipata kwa Yanga hii hakuna mchezajo wa kumuundia kamati. Yan akabwe Mayele sijui umzuie Aucho au Moloko hilo swala kwa Yanga halipo. Kwa sababu kila mchezaji anajituma kwa nafasi yake kwa kila anapopata nafasi.

Sasa kinachobaki ni mbinu za Nabi na hapo ndipo wengi wanaposhindwa kwa sababu unapoishia kufikiria mwenzako keshafikiria mara mbili zaidi yako. Unapofikiri umeweka mtego mwenzako keshautegua kabla hujaweka. Kuna mtu alisema usimpe nafasi ya kufikiria Nabi utaumia.

Kwa kusema hayo bado sioni nafasi ya Simba kuambulia hata sare. Ni kichapo tu hakuna namna
 
Tupate wadhamini.
Screenshot_20230412_170808_Instagram~2.jpg
 
Changamoto ambayo wengi wataipata kwa Yanga hii hakuna mchezajo wa kumuundia kamati. Yan akabwe Mayele sijui umzuie Aucho au Moloko hilo swala kwa Yanga halipo. Kwa sababu kila mchezaji anajituma kwa nafasi yake kwa kila anapopata nafasi.

Sasa kinachobaki ni mbinu za Nabi na hapo ndipo wengi wanaposhindwa kwa sababu unapoishia kufikiria mwenzako keshafikiria mara mbili zaidi yako. Unapofikiri umeweka mtego mwenzako keshautegua kabla hujaweka. Kuna mtu alisema usimpe nafasi ya kufikiria Nabi utaumia.

Kwa kusema hayo bado sioni nafasi ya Simba kuambulia hata sare. Ni kichapo tu hakuna namna
Hawa watu Simba wachunge sana.

1. Mayele
2. Joyce Lomalisa
3. Musonda
 
Bado sina sababu ya kuidharau Simba ingawa Yanga FC ndiyo iko vizuri sana kiuchezaji hata kiushindani msimu huu.

Ikumbukwe Simba hana cha kupoteza NBC PL mwaka huu, itamlazimu ijitutumue kivyovyote vile ili iifunge Yanga ipate raha.

Miaka minne mfululizo hivi karibuni ambapo Simba ilichukua makombe ya ligi kuu ilikuwa ikisumbuliwa sana na Yanga FC kimatokeo.

Derby ni derby, Wananchi tuwe neutral katika kupokea matokeo ingawa naamini Yanga itashida Jpili 16/04/2023.
 
Back
Top Bottom