Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Umeambiwa muda ni mpaka tarehe 20/jan/2020 saa 23;00 pm ndio mwisho sasa wewe mapema yote hii umejilipua mwana hebu tuliza mzuka huo. subiri muda ulio semwa ufike ndo uanze kuchokonoa watu wako ukiona hawapatikani ujue ndio kumekucha. hapo unaweza kuanza kulialia
 
Kama umesajili line yako na bado unasubiri taarifa confirmation au bado hujasajili naona baadhi yetu tumeanza kuonja joto la kuzimiwa mtandao.

Si mimi hata jamaa yangu hapo Dar hapatikani, nimetumia njia mbadala kwa kupitia jamaa wa ofisini kwake ndipo akaniambia yupo ofisini.

Sijaelewa kama ndiyo wamefanya yao au wanatest mitambo, mdau huko ulipo vipi upo hewani?
mwisho ni saa 6 usiku leo ndugu!!
 
Watanzania hata mkipewa miaka 10. hamtasajili. Mko hivyo. Kulalamika. Mnaibiwa. Lakini Leo Ona mnakotokea. So stupid. Ningekuwa mchina. Ningesema. Kweli mnaonewa. Ila tunajuana. Wabongo.
Mtanzania Embu soma nilichoandika. Kuna sehemu nimesema muda uongezwe? Binafsi naona Hakuna sababu ya kuwa na deadline, kwani kuna emmergency gani?

Ukiweka utaratibu mtu akipoteza line lazima arenew kwa alama za vidole, mtu akipata tatizo either ni mpesa au tigopesa au yoyote ili ahudumiwe lazima arenew kwa vidole, line mpya zote lazima urenew kwa vidole, mtu akitakata kuhamisha fedha kwa njia ya simu kuanzia lets say laki tano ili uwe na access basi lazima urenew yaani unaweka vibarier barier vingi vingi utashangaa in two years kila mtu kajisajili kwa vidole.

Mbona wakati simu za mkononi zinaingia watu hawakupewa deadline ya kuwa na line na leo hii watu karibu wote wanazo?

Unless kuna emmergency hakuna sababu ya kuzima simu maana tumekaa miaka mingi bila kusajiliwa why leo in short time iwe ni lazima umesajiliwa?

Ndio ni lazima kutii mamlaka ila pia tuwe na tabia ya kujiuliza why? Tukiwa watu wa kujiuliza ni kwanini hili jambo lipo hivi tutatengeneza kizazi kizuri cha ushauri kwa viongozi wetu badala ya kuwa kama mifugo.
 
Ni kweli mkuu kuna watu vichwa vyao ni makasha ya kuifadhia upumbavu wao,tulio wengi hasa mkoa wa manyara,hususani wilaya zake watu wengi walisha kamilisha taratibu zote mpaka kupiga picha,tangu mwezi wa nane mwaka Jana havijatoka kitambulisho wala namba mpaka Leo yaani hii serikali dah!?
Pole
 
Uliambiwa usajili laini yako kabla ya tarehe 20 January,leo ni tarehe ngapi,nakwanini uwe hewani hadi saa hizi wakati ni tarehe 20,ingekuwa walisema sajili laini yako kabla ya tarehe 21 wewe ambaye hujasajili usingeshangaa kuwepo hewani hadi saa hizi.

Kuna kitu,siyo bure,endapo upo hewani hadi muda huu,wakati hukutakiwa kuwepo.
KABLA na siyo BAADA.
 
Serikali imetengeneza tatizo hawakujua kwamba chombo chao NIDA hakina uwezo na uweledi matokeo yake nguvu kazi ya taifa inapotea kwenye mifoleni isiyo na maana.
Badala ya kutatua matatizo ya wananchi hawa wana create problems. Likiisha hili watabuni kero nyingine kwa wananchi.
 
Kama umesajili line yako na bado unasubiri taarifa confirmation au bado hujasajili naona baadhi yetu tumeanza kuonja joto la kuzimiwa mtandao.

Si mimi hata jamaa yangu hapo Dar hapatikani, nimetumia njia mbadala kwa kupitia jamaa wa ofisini kwake ndipo akaniambia yupo ofisini.

Sijaelewa kama ndiyo wamefanya yao au wanatest mitambo, mdau huko ulipo vipi upo hewani?
Nadhani wanazima leo saa sita usiku mkuu ndo itakuwa siku ya mwisho kati ya zile siku 20 alizotoa mheshimiwa Rais.
 
Back
Top Bottom