Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Dah let's wait and see mkuu
 
Nitozwe fine kwa kosa lipi ndugu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nipo hewani mkuu
Utazimiwa soon.
Lakini itatusaidia sana kubana matumizi, haya mabando yalikuwa yanatumalizia sana hela. Tutarudi kwenye internet cafe kama zamani, nusu saa kwa wiki sh 500 tu.
Na nyumbani siyo lazima kila mmmoja awe na simu.
Yale mambo ya kila mtu ana simu nyumbani hadi housegirl na watoto wa form two fyekelea mbali.
Simu hata ya jirani itasaidia.
Binafsi hii kitu ya kukata mtandao wa wasiosajiliwa itanipunguzia matumizi ya sh 2,000 kwa siku ambayo ni kama 60,000 kwa mwezi. Hebu twende mwendo huo kwanza, usawa huu mgumu sana.
Kila changamoto ina faida zake, wazungu wanasema 'a blessing in disguise'!
 
Tarehe 20.
Inaisha saa 23:59.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kwani tarehe 21 imefika?
Si walisema mwisho ni tarehe 20/1/2020, ina maana leo bado hawajasitisha/funga mawasiliano. Ikifika saa 5.dk 59.sek 59 usiku leo, basi watafunaga kama ni kweli watafanya hivyo.

Kama kwako wamekata, basi wewe uko mbele kwa siku nzima.
 
Usiwe na shaka Ndugu, hawezi kuzifikia zote, hawana uwezo huo, unakumbuka wakati ule waliposema wanafunga simu zote ambazo hazikuwa zimethibitisha IMEI number ?!, wewe endelea na shughuli zako inaweza kuwa ni tatizo la Network.
 
Unaelewa maana ya KABLA ya tarehe 20?Leo ni 20 au?
 
Mimi nina daiwa shilingi 4900 kwenye nipige tafu..
kiukweli hii nilikuwa nataka nilipe ila nahofia laini yangu kufungwa kwasababu sijasajili kutumia alama za vidole..

Najua kuna wengine wanadaiwa songesha, Wengine M-pawa.. Wengine wamekopa airtel, halotel au tigo
Je laini zao zikifungiwa, nani atawalipa mitandao ya simu fidia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…