Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Umejuaje? Ninachojua hawana uwezo huo. Nawashangaa watu wanaoenda kupoteza muda wao kusimama kwenye misururu mirefu eti kutafuta namba ya nida ili kusajili line za simu! Sipangi mstari na nitawasiliana nipendavyo, na nitaenda kusajili nikiwa na muda.
Hivi la simu fake liliishia wapi ? Ni kweli hawawezi zima kwa mara moja. Nadhani itakuwa chache chache.
 
Dah pole sana mkuu. me nakumbuka nilijiandika tar 31/12/2017 nikakaa week 2 tu nikaenda kufata hard copy yangu nikaipata. Nadhani hicho kipindi watu wengi walikuwa wameshakata tamaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa wamefunga message inaingia kivipi?

Nahisi kutakuwa kuna flag inawekwa kwa namba ambayo inayo na isiyo na usajili...

Kwa ambayo haina usajili hiyo flag ikiwa activated ina trigger SMS center itume huo ujumbe kabla ya kuwa barred...

Kwa hiyo mtiririko utakuwa activate XXX flag >>trigger SMSC to send SMS >> deactivate from system (barr)
 
TCRA imeeleza kuwa haitazima line zote ambazo hazijasajiliwa kwa wakati mmoja, bali wataanza kuzima taratibu.

Watawazimia wale wenye vitambulisho na namba za NIDA ila hawajasajili, sababu hawa hawana sababu za kutowafanya wasisajili.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani line ikizimwa inakuwaje?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo kutoka 2014-2019 ulikosa ila wengine walipata mfano mimi nilichelewa sikujiandikisha mapema ila nilikomaa mpaka nikapata kitambulisho tukubali tu tulizembea sana japo kwa sasa tunajisahau mno na kuona serikali haiwezi kufanya chochote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usalama wa watanzania ni wao waamue wenyewe hatima yao, yaani yaanzishwe maandamano taifa zima hadi vijijini ili kumtoa huyu Dikteta mshamba na katili na CCM yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii offer na mimi nimeipata but nime-doubt kitu kimoja,ikitokea nimepoteza line kisha nikahitaji kuirudisha kama huyu aliyenisajilia hajawa karibu bado mitihani itakuwa ile ile tu cos hatutegemei kama binadam kuwa karibu muda wote kuna kuhama eneo,kifo nk so nilichoamua acha wafunge line {ninazo tatu} nitarudi zama za mawe kwa muda halafu kama kufuatilia nitaanza pale NIDA foleni itakapoisha pia watakapoboresha huduma zao.

Siyo jambo jepesi mtu kufunga shughuli zako kwa muda zaidi ya siku tatu kwenda kupanga foleni usiyotegemea kupata unachokitegemea na hii nimeapa sitafanya na kama kufunga acha wafunge.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Aisee! mmeanza kupona magonjwa yenu ya akili mmoja mmoja hadi mtapona wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie mnao sema TCRA hawawezi kuzima line za simu lazima mtakuwa mmesha sajili msituchongee sisi tafadhali, hivi mna mchokoza nani?????.

Kweli wabongo NYOSO.

TCRA mnaweza kuzima simuzetu wakuu achaneni na hawa wahuni please,please please.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…