Kuelekea mechi ya CAFCC | Simba SC dhidi ya ASEC Mimosas SC, mechi kubwa kwa timu kubwa

Kuelekea mechi ya CAFCC | Simba SC dhidi ya ASEC Mimosas SC, mechi kubwa kwa timu kubwa

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Habari Tanzania na Kote Duniani..!

Kuelekea siku ya Jumapili February 13, 2022 hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Barani Afrika CAFCC kupigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa (Mkapa Stadium), ambapo Mnyama Mkali Mwituni Simba SC anakamuana na ASEC Mimosas kutoka Ivory Coast.

Ni mchezo mkubwa kwa timu kubwa zitakapombana kutafuta matokeo chanya kwenye michuano hii ya pili kwa ukubwa baada ya CAFCL.

Neno kutoka kwa M/kiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu amesema kuwa

"Hii ni hatua kubwa na vile vile ni utamaduni wa kawaida wa Klabu ya Simba, kuweza kushiriki katika mashindano haya, kama tunakumbuka tangu historia ya mpira wenyewe katika miaka ya 70, 80, na 90 Simba SC imekuwa ikifanya vizuri na kwa kipindi cha miaka minne mitano tumekuwa na mfululizo wa kushiriki mashindano ya Kimataifa na kufikia ngazi ya makundi na ngazi ya robo fainali, na tunaamini kwa Kikosi tulichokuwa nacho mipango ya bechi la ufundi na management tutahakikisha timu yetu inafanya vizuri na kufikia hatua ya juu zaidi".

Naaam Wanasimba na mdau wa Kabumbu, maandalizi yote yanaendelea hivyo nasi ni jukumu letu kujiandaa kuhakikisha tunajitokeza kwa wingi na kushangilia mwazo mwisho huku tukishuhudia kandanda safi liliothibitishwa na CAF kutoka kwa Mkali wa Soka Nchini, Simba SC.

Karibu kwa yakayojiri kabla ya mchezo wenyewe..Usikose Ukaadithiwa.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana

============

Update;

Naibu Spika Mh. Mussa Azzan Zungu, atakuwa mgeni Rasmi kwenye mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

=========

Kocha wa Simba SC Pablo Franco amesifu uwezo wa wapinzani wao ASEC Mimosas huku akisema timu hiyo ipo vizuri kwenye mipira ya kutengwa.

Naye Kocha wa ASEC Mimosas Julien Chevalier amekimwagia sifa uwezo wa Simba SC huku akitanabaisha kuwa timu hiyo inapenda mashindano makubwa.
 
Nina kawoga flani.. lakini nikikumbuka Simba kwa mkapa Ni hatari..napata amani
Sio Simba hii. Nikikumbuka Galaxy walivyofanya, imani inanitoka kabisa.

Wachezaji wetu wa Simba wa sasa waliunajisi uwanja wa Mkapa kwa kuruhusu kufungwa bao tatu na kutupwa nje ya CCL

Kabda ya hapo Watanzania tulijua na wapinzani wetu kutoka nje ya nchi nao walijua kua Kwa Mkapa mbele ya Lunyasi SSC haponi mtu

Kocha wa Ahly Mosimane katika hafla ya kupanga draw ya CCL alisema anafarijika maana this time hawatakwenda kwa Tanzania(kucheza na Simba kwa Mkapa)

Hebu vijana wetu wauchukulie serious mchezo huu. Asec Mimosas hatujawahi kuwafunga ndani wala nje na kumbukumbu ya Sekou Bamba bado tunayo alivyotuua pale Shamba la Bibi. Ila siku zimebadikika na lolote linawezkana. Tukapambane
 
Kuwa na amani mkuu, Simba ashapitia mechi ngumu kama hizi.

ASEC Mimosas wenyewe wanajua kwamba wana kazi moja kubwa mbele ya Simba SC.
Ngoja wengine tufanye kuaga maiti, nitatia neno baada ya mechi. Ila kuweka kumbukumbu sawa ukiachana na mechi ya Galaxy, mechi ya Simba vs Red arrows pengine tungeona matokeo ya tofauti kama uwanja usingejaa maji. Mechi ya jumapili kuna wachezaji pia watakosekana akiwepo Chama
 
Simba wachezaji wengi hawapo ,Kibu , Morison ,Mugalu ,Lwanga na Dilunga nao njia panda .

Dah sina imani na mechi hii naona mambo yatakuwa magumu sana
Lwanga ameshakuwa yupo vizuri..Ni jukumu la Kocha Pablo kuaamua kumpanga.
 
Hebu vijana wetu wauchukulie serious mchezo huu. Asec Mimosas hatujawahi kuwafunga ndani wala nje na kumbukumbu ya Sekou Bamba bado tunayo alivyotuua pale Shamba la Bibi. Ila siku zimebadikika na lolote linawezkana. Tukapambane
Ni namna ya kutuongopea au huna data kamili na au umepoteza kumbukumbu kwa.. katika michezo miwili tuliokutana nayo kwa mara ya mwisho mimosa aliumia hapa nyumbani kwa goli moja kwa bila(1-0).... marudiano kule kwao simba aliumia goli 4-3
 
Simba wachezaji wengi hawapo ,Kibu , Morison ,Mugalu ,Lwanga na Dilunga nao njia panda .

Dah sina imani na mechi hii naona mambo yatakuwa magumu sana
Mkuu pengine mnarejesha zile vimbinu mbinu vyenu vya kumfanya hata Bocco akabadilika kuwa kama Lionel Messi. Si umeona watu wameingia king kwa kuhisi Chama na Luis ni wachezaji wa hatari sana kumbe ni power bank za kwa Mkapa pekee ndio zimewasaidia saivi wanastuka kuwa kumbe walisajili magalasa wanatamani kuwarejeshea magalasa yenu.
 
Ni namna ya kutuongopea au huna data kamili na au umepoteza kumbukumbu kwa.. katika michezo miwili tuliokutana nayo kwa mara ya mwisho mimosa aliumia hapa nyumbani kwa goli moja kwa bila(1-0).... marudiano kule kwao simba aliumia goli 4-3
Ngajapo,

Simba haijawahi kuifunga Asec Mimosas. Na kama unavyosema ni kweli kwamba eti Simba ilishinda hapa 1-0 na ikapoteza marudiano Abidjan 4-3 Simba si wangekua wamesonga mbele kwa faida ya goli la ugenini?

Maana ingekua wamepata magoli matatu ugenini!!!!
 
Ngajapo,

Simba haijawahi kuifunga Asec Mimosas. Na kama unavyosema ni kweli kwamba eti Simba ilishinda hapa 1-0 na ikapoteza marudiano Abidjan 4-3 Simba si wangekua wamesonga mbele kwa faida ya goli la ugenini?

Maana ingekua wamepata magoli matatu ugenini!!!!
We mwana simba mwenzetu je unakumbuka CAF group stage ya mwaka 2003 kipindi icho magroup ni mawili na timu ni 8 ambayo kama robo final ya sasa?

Kundi liliisha

1Ismaily
2.Enyimba
3.Simba
4. Asec

Simba alimaliza na points 7 alishinda dhidi ya Asec na enyimba mechi ya Ismaily refa alikataa goli halali la simba hapa shamba la bibi

Kule Ivory coast Asec waliifunga simba 4-3 tena kuna mda simba walikua mbele kwa goli 3-2 , had dakika za mwisho Ndio wakachomoa na kuongeza goli la 4
 
Ivory Coast ni ndugu zetu kabisa, pia mwalimu alisema Afrika ni moja. Pia nikukumbuka vile Sekou Bamba alivyokimbiza wakati ule, nashawishika kusema ASEC MEMOSA hoyeeeee.
 
We mwana simba mwenzetu je unakumbuka CAF group stage ya mwaka 2003 kipindi icho magroup ni mawili na timu ni 8 ambayo kama robo final ya sasa?

Kundi liliisha

1Ismaily
2.Enyimba
3.Simba
4. Asec

Simba alimaliza na points 7 alishinda dhidi ya Asec na enyimba mechi ya Ismaily refa alikataa goli halali la simba hapa shamba la bibi

Kule Ivory coast Asec waliifunga simba 4-3 tena kuna mda simba walikua mbele kwa goli 3-2 , had dakika za mwisho Ndio wakachomoa na kuongeza goli la 4
Nimekumbuka Lunyasi mwenzangu, nimekumbuka sasa. Tulinyimwa goli la kichwa cha ama Emmanuel Gabriel Mwakyusa au Joseph Golota eti ofside

Ile .echi ya Ivory Coast tuliitupa wenyewe. Nimekumbuka mkuu wangu. Samahani
 
We mwana simba mwenzetu je unakumbuka CAF group stage ya mwaka 2003 kipindi icho magroup ni mawili na timu ni 8 ambayo kama robo final ya sasa?

Kundi liliisha

1Ismaily
2.Enyimba
3.Simba
4. Asec

Simba alimaliza na points 7 alishinda dhidi ya Asec na enyimba mechi ya Ismaily refa alikataa goli halali la simba hapa shamba la bibi

Kule Ivory coast Asec waliifunga simba 4-3 tena kuna mda simba walikua mbele kwa goli 3-2 , had dakika za mwisho Ndio wakachomoa na kuongeza goli la 4
mkumbushe anaishi kwa kukariri
 
Back
Top Bottom