Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Jamani! Ninajua kila mmoja hana haki ya kutoa maoni lakini pia wengine wana haki ya kuvumilia maoni yake ( i mean siyo haki kusikiliza na kukubaliana na maoni ya kila anayetoa).
Maoni ya Malaria Sugu tuna haki ya kuyavumilia.
Mimi kiwango cha uvumilia wa stupidy opnions of Malaria sugu basi!!!!

Kama mnaweza dont comment anything on his posts.......ataondoka mwenyewe kutafuta mkondo wa mafisadi wenzake!!
 
Na taarifa ya NEC ya leo unapingana nayo pia? Kwanza Shimbo aelewe akiua tu mtanzania ni sawa na kujielekezea bunduki yeye mwenyewe. Ni mwanajeshi gani atakubali kuua mama yake, baba yake, mjomba wake, binamu yake, mtoto wake. Ategemee kugeukwa tu!!!!!!
 

Rais mtarajiwa wa CCM wa 2015 Membe huyo...
 
Kama kweli JK anatarajiwa kushinda uchaguzi ambao ni huru na wa haki sasa majeshi ni ya nini? Membe ni vyema akoisoma vizuri katiba yetu Ibara ya 148 kabla ya kupiga domo. Chini ya Ibara hiyo jeshi halinamamlaka ya mambo ya ndani ya nchi kabisa kwa hiyo Jk anchofanya ni kukiuka katiba na hili linatosha kwa wapigakura kutomchagua.
 
President Jakaya Kikwete, 60, is expected to win re-election easily for a second and final term, but faces a growing challenge from the opposition Chadema party's candidate Willibrod Slaa.

Membe anayo matokeo tayari ya nini sasa kwenda kwenye uchaguzi???????
 
HUUUUU SIOOOOOOOO UNGWANA HATA KIDOGOOOOOOO>SUBIRI MATOKEO YATANGAZWE NDIO ASEME>
MEMBE UTASHANGAA masikio yatawasha utakachosikia.
 
mEMBE MKURUPUKAJI, mi namuona ni mwana siasa wa kizazi cha nyuma kidogo, anapenda sana kujikweza.
 
Kwa bahati mbaya sana Membe ni mmoja wa wale wanaounyemelea urais kwa mgongo wa CCM mwaka 2015. Kauli zake zitakuja kumrudi na zitampa tabu sana kuzitetea, kwa wakati huo JK atakuwa anakimbizia mafao yake. Time will tell. Membe you will live with your satatement for long long time to come. It will backfire you.
 
Wewe malaria sugu ni Mpumbavu.

Mod, kwanini usitoe onyo kwa hawa watu wanaomshambulia mtu badala ya kushambulia hoja yake? Hivi JF tunashindwa kujibu hoja bila kumshutumu mtoa hoja? MS wewe endelea na hoja, anayejibu hoja mjibu hoja yake, anayetukana achana naye!! JF hatuna uhuru wa maoni bila uhuru wa matusi. Tuna safari ndefu hadi kukubaliana kutofautiana bila kukushifiana!!
 
watanzania "tutapewa" na kulazimishiwa "watawala" na siyo viongozi hadi lini?
Itanishangaza vibaya kama jinamizi hili la membe kuwa rais litatimia kuwa kweli.

Mpaka pale tutakapotembea kwa miguu hadi ikulu ya magogoni na kuwatia pingu wezi na majambazi wanaofilisi nchi yetu.
 
Polisi yafafanua tamko lao na Shimbo




Na Romana Mallya



14th October 2010



B-pepe




Chapa




Maoni









Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Abdulrahman Shimbo.



Jeshi la polisi limefafanua kuhusu kauli iliyotolewa hivi karibuni na vyombo vya ulinzi na usalama kuhusu namna vilivyojipanga kufanikisha uchaguzi mkuu, na kusema kuwa kauli hiyo haikulenga kutishia wananchi bali kuimarisha amani kwenye kampeni, wakati wa uchaguzi na baada.
Mkuu wa jeshi hilo IGP, Said Mwema, alitoa ufafanuzi huo jana baada ya baadhi ya viongozi wa siasa na wa dini kuilalamikia kauli hiyo kuwa imelenga kuwatisha Watanzania.
Viongozi hao wa dini na wanasiasa walitoa malalamiko hayo katika mkutano uliofanyika jana jijini Dar es Salaam uliolenga kujadili kuhusu masuala ya amani, usalama na utulivu wakati wa uchaguzi na baada.
Mkutano huo uliwakutanisha viongozi hao, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na jeshi la polisi ambapo kwa pamoja waliweka maazimio 11 yatakayowawezesha kila mmoja na nafasi yake kuielimisha jamii.
Katika mkutano huo, baadhi ya viongozi hao walitoa malalamiko kuwa, kauli iliyotolewa na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Abdulrahman Shimbo, ililenga kutishia umma wa Watanzania.
Mwema akijibu malalamiko hayo alisema kuwa, tamko hilo halikuwa na nia wala mpango wa kuitishia jamii, bali lilimaanisha kuwa, vyombo hivyo vya ulinzi kila kimoja kwa nafasi yake vihakikishe kuwa vinalinda amani.
“JWTZ kwa nafasi yake itahakikisha amani inaendelea kuimarishwa vile vile, jeshi langu siku hiyo tutaingia mitaani kutekeleza hilo, lakini kauli hiyo haikumaanisha JWTZ watafanya kazi zetu, hofu imetokana baada ya yule aliyetoa tamko kuwa JWTZ,” alisema.
Alisema vyombo vya dola kote duniani huwa na mbinu na mikakati ya ulinzi.
“Hapa kwetu vyombo vya usalama huwa tunakutana kila mwezi kujadili jinsi ya kuimarisha ulinzi hasa kutokana na kukua kwa teknologia ya mawasiliano, kuna masuala ya ugaidi, pia kipindi hiki kumejitokeza ujumbe mfupi unaotumwa kwenye simu unaotishia umwagaji damu na kuchochea vurugu, hivyo lazima vyombo vya usalama tufanye kazi kukabiliana navyo,” alisema.
Baadhi ya maazimio yaliyofikiwa wadau hao viongozi wa dini waendelee kuelimisha amani na utulivu vyombo vya habari kuhakikisha mambo ya amani na utulivu yanapewa kipaumbele.




CHANZO: NIPASHE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…