Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
katika nchi za wenzetu kama marekani, mnaweza kugombea nafasi moja lakini baada ya Uchaguzi, wagombea wote wanaheshimiana, aliyeshindwa anamtambua aliyeshinda na aliyeshinda vile vile anamheshimu aliyeshindwa. Ndiyo maana Obama alimheshimu mama klintoni na kumpa cheo kikubwa sana serikalini kwake. Walifanya hivyo pia marais kama Kennedy aliyemteua Johnson kuwa makamu wake, na Rais Reagan alimteua George Bush (sr) kuwa makamu wake.

Tatizo la kwetu, mkigombea wawili, baada uchaguzi yule aliyeshinda anafanya kila liwezekanalo kummaliza mpinzani wake kisiasa, yaani uchaguzi unageuka kuwa ugomvi wa kudumu. Hapo ndipo ninapoona tatizo kwa CHADEMA
 
wengi tuwagumu kuombana radhi...

hajaomba radhi amewacheza shere kina zitto baada ya kugundua plan b ya wazee wenye chama itafanya kazi vizuri.

Kama anataka aandike kwenye gazeti lake kesho ili wajumbe wa chadema wasome.ukimkosea mtu kwenye gazeti muombe radhi huko huko hapa jf hakuna wajumbe wengi wa mkutano mkuu wa chadema.

Kifupi chadema wamekwisha mwaga maji.kama wazee wanamtaka mbowe wangewanunua wajumbe na kumshinda zitto kwenye uchaguzi,lakini madudu haya waliyoyafanya yatawaumbua sana na kina kitila wanajuta kwenda huko.moyoni mwao wanahisi hawaaminiwi na wenye chama.

Hakuna kitu kibaya mtu kufanya kazi mahala ukawa huna amani na hushirikishwi rasmi.kibanda amekwisha walebal kuwa ni wajinga na mamluki hiyo haitoki.seleli kelele zake kakosa madaraka kwenye mtandao,sitta uwaziri mkuu,hapa chadema imetengeneza kina seleli wake.inakuwa vigumu kuwarudisha kundini.
 
http://www.ippmedia.com/frontend/index.php?m=54
owenya%281%29.jpg

Lucy Owenya.

Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo na mtoto wake, Lucy Owenya, wamechaguliwa bila kupingwa kukiongoza chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Kilimanjaro kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Ndesamburo alichaguliwa tena kukiongoza chama hicho mkoani hapa baada ya kuibuka na ushindi wa kura
49 kati ya 50 za wajumbe wa mkutano huo wakati mtoto wake, Lucy, aliibuka na ushindi wa idadi ya kura kama hizo katika uchaguzi mkuu uliofanyika jana mjini hapa.

Katika uchaguzi huo,
Basil Lema, alichaguliwa kuwa Katibu wa chama hicho huku Deogratius Munishi, akichaguliwa kuongoza Baraza la Vijana wa chama hicho na Seranus Mushi alichaguliwa kuongoza Baraza la Wazee wa chama hicho.

Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Ndesamburo alisema ushindi wake ni ishara kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwamba bado anakubalika na kamwe hata katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu hapo mwakani, atajitahidi kutetea kwa udi na uvumba kiti chake cha ubunge.

Alisema anashangazwa na propaganda za viongozi wa CCM ambao wamekuwa wakidai kuwa yeye ni mzee na hivyo hatagombea tena kiti cha ubunge Jimbo la Moshi Mjini jambo ambalo si la kweli.

"Eti wanasema mimi ni mzee, kibabu nimechoka sitagombea tena ubunge...Huo ni uzushi wao na ushindi wangu wa leo ni indiketa ya kwamba uchaguzi mkuu ujao nitatetea jimbo langu na kumbwaga mgombea wa CCM,” alisisitiza Ndesamburo.

Naye Lucy Owenya ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) akizungumza na waandishi wa habari baada ya ushindi huo, alitoa wito kwa wanawake mkoani Kilimanjaro kujitokeza kwa wingi na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Owenya alisema wanawake hawana budi kuacha woga wa kuwania nafasi za uongozi kuanzia serikali za mitaa, madiwani na hata ubunge ili kuweza kufikisha uwakilishi wa asilimia asilimia 50 bungeni na halmashauri.





CHANZO:

Ndesamburo na Mtoto wake hawakuwa na wapinzani kama itakavyokuwa kwa Mbowe hatakuwa na Mpinzani.

kingine wagombea wote ni wachagga kwani Kilimanjaro si kuna wapare pia?
 
I'm speechless kwa haya yanayotokea Chadema...Bado tuna safari ndefu mno kufikia Demokrasia ya kweli....Kwa mwendo huu bado tutakuwa na taabu sana ya kuing'oa CCM!!
 
Baada ya kufikiri kwa makini, nimegundua kuwa kumbe CHADEMA kuna matatizo makubwa ambayo sisi tulioko nje hatuyajui. Wakati CHADEMA mnapandishiana, ndipo CCM inapata nafasi ya kutia propasganda, na hata kuyeyushilia mbali skendo za ufisadi ambazo zimekuwa zinaibuliwa na CHADEMA hao hao: Pakacha kuvuja ndiyo nafuu kwa mchukuzi.

Marehemu Wangwe waliwahi kuonyesha kuwa kuna mfukuto ndani ya CHADEMA lakini akatangulia kabla wengi hatujayajua sawasawa. Sasa hili la Zito kugombea Uenyekiti dhidi ya mwenyekiti wake wa sasa linaashiria kuwa kweli kuna mpasuko ndani ya CHADEMA, na kama kweli kuna kikundi kinachomzuia asigombee basi kumekucha.
 
Inaonekana Zitto akuwasiliana na Freeman kabla ya kuchukua form, mawasiliano kama haya hayaitajiki CCM kutokana na ukubwa wake, lakini kwa chama kama CHADEMA ambacho mihimili yake ni Freeman, Slaa na Zitto ni lazima wawasiliane kabla ya hayo maamuzi. Ndiyo ni demokrasia lakini inaonekana kuna vita ya chini chini kati ya Freeman na Zitto..

Usemi wa Zitto kwamba Freeman arudishe form ili kukinusuru chama ni dhairi kwamba hakubaliani na mwenyekiti wake na kunakurukupushani kati ya hao wawili.

Sidhani kama Kibanda angeweza kumshambulia Zitto bila kujua kuwa kuna mvutano kati ya Zitto na Freeman.....

Tupo pamoja
 
Habari zilizotufikia punde zinasema kijana wetu MH mbunge Bw zitto kabwe,,..amejitoa katika kinyangiro cha uchaguzi ...akihitimisha msuguano uliopo mh DK SILAA amekiri kupokea barua rasmi kutoka kwa Mh KABWE ikijieleza sababu za kujitoa kinyanganyiro.............

Bado najiuliza ni kweli zitto mwanasiasa ama msanii wa siasa...tuwaachie wenyewe...akizungumza na redio one leo Dk silaa amekiri kupokea barua hiyo na kusema aliandika kwa ridhaa yake bila ya kushurutiwa na mtu yoyote...akiitaja sababu ya kuendelea kuleta mshikamano wa kisiasa.......kama kweli huyu bwana atanisamehe kwa kumuita msanii wa siasa ambae hana msimamo thabiti....na hivyo tusishangae siku atakapotangaza kuamua kwenda CCM.....
 
Dah,hii kali...Kila ninapofikiri kuwa tumepiga hatua katika siasa za bongo najikuta kuwa the real events proves me wrong!!Yaani inachosha sana,no wonder when it comes to voting,Tanzanians opts for ZIMWI WALIJUALO.Kwani hawa wengine hawatabiriki.I doubt the way CHADEMA wanavyolitafsiri neno Demokrasia.
 
mkuu hiyo ndio demokrasia halisi alitufundisha nyerere kipindi cha uchaguzi ....muulizwe malecela sababu za kujitoa was simple democracy....

ukiona mwenzio anataka kukupiga tumboni muwahi shingoni.....hiyo ndio demo ya bongo
 
nimesoma thread za zitto mpaka nimechoka......nasapoti uyu bwana kweli yawezekana alikuwa na nia ya kutafuta umaarufu baada ya kujazwa na mafisadi
 
Upinzani wa KWELI utatokea CCM.Period.
 
Wana JF si kawaida yangu kuandika sanasana na imenilazimu leo... Tangu zamani niliamini kuwa CHADEMA kinaweza kuwa chama cha 'Demokrasia' na daima kitaruhusu 'Demokrasia' kuchukua mkondo wake lakini tunapoelekea inaelekea sivyo.

Naam, nazungumzia kikao kilichofanyika leo na 'wazee' wa CHADEMA kuanza 'kumshinikiza' Zitto Kabwe kuondoa jina katika kinyang'anyiro cha Uenyekiti.

Ndiyo, nilikuwa sioni sababu ya Zitto kugombea mwanzoni lakini kwakuwa alishaweka jina nilitarajia atapewa nafasi kuweza kudhihirisha kuwa demokrasia imeweza kuchukua mkondo wake ndani ya CHADEMA.

Nasisitiza, napinga kwa sana njia hii inayotumika kuhakikisha Freeman anabaki mgombea pekee, inawezekana kwa maslahi ya chama chenu mmefanya hivyo kukinusuru chama (kama mnavyodhania) lakini binafsi (si msimamo wa JF) naamini ndio mnakizika chama... Bado mna muda, mwacheni Zitto agombee na akishindwa ashindwe kidemokrasia...

Kama ni kuondoa basi wote wawili (Zitto na Freeman) waondoe majina na ifikiriwe namna mpya.

Katika hili, mmechemsha!

Mkuu, mimi nahisi what you want inatakiwa itokee CCM sio kwenye vyama ya upinzani kwa Tanzania kwa sasa. Give them a brake.

CHADEMA = Slaa, Zitto, Mbowe, Tundu, Ndesapesa. Naamini bila hawa CHADEMA isingekuwa hapa hasa Dr. Slaa. Hata mtoto mdogo hapa Runzewe anamjua. Kutokana na kauwezo wangu wa kuangalia mambo nahisi kuna mgogoro kati ya either Slaa VS Zitto or Mbowe Vs Zitto au Slaa and Mbowe Vs Zitto. Kibanda amejaribu kuprove hili. Nahii ni hatari sana katika stage hii ambayo kila mtu amekata tamaa. Ikitokea hii basi we are done. KAMA KWELI ZITTO ALICHUKUWA FORM BILA HATA YA KUWASILIANA NA SLAA BASI. TUMEKWISHA, NIMEISHA.

Kama ikiwezekana Slaa kugombea uenyekiti would be much better but kitendo cha kuchukua form ilhali kama wanajua kuwa ndo wahimili wa chama basi kuna tatizo na linapaswa kushulikiwa.

I would be happy if Dr. Kitila kugombea kuliko figure hizi 2 ambazo zinaonyesha something is wrong na hata kama wakinyamaza but wenye nao walishaona siku mingi tu. Ila mkae mje na mbinu mpya maana akina Makamba wanagonga glass za wine.

Ni mbaya sana kufananisha haya mazingira ya siasa za Tanzania na siasa za pale US. Hata za Kenya na Tanzania haiwezekani. Hata Tarime na Bunda. Hata Moshi mjini na vijijini. Mfano mdogo tu, jana nilifika kichochoro huku Runzewe (karibu na mgodi wa Tulawaka, barabara ya kwenda Bukoba) wakawa wanajadili suala la Zitto na Mbowe wote kuwania uenyekiti. Hili limewapa shida watz wengi mno.

Sisi tulio wachache wenye uwezo wa kuangalia nini kinafanyika kule. Tuendelee tu kuwapa maarifa hawa walio mbele yetu. Ipo siku we will get there.
 
huyu mh Zitto kama msanii flani niliwahi kusoma kuwa hatagombea ubunge tena, lkn bdae akageuka, na inavyo onekana kwa hatua aliyofikia ya kujitoa naanza kupata hofu labda alitaka kuuza chama kama angeshinda ila alipoona amestukiwa ameamua kujitoa. Ila hofu yangu wasije waka mCHACHA WANGWE kama atakuwa hana msimamo
 
I would be happy if Dr. Kitila kugombea kuliko figure hizi 2 ambazo zinaonyesha something is wrong na hata kama wakinyamaza but wenye nao walishaona siku mingi tu. Ila mkae mje na mbinu mpya maana akina Makamba wanagonga glass za wine.
Basi na Freeman achomoe jina!
 
Unajua nyie wadanganyika ni wagumu kuelewa. Sisi tulishawaona zamani hiki chama cha watu wachache na cha kikabila kinachoongozwa na DJ.

Tuliwaambia zamani sana ila hamkusikia, sasa yanatokea ndo mnashtuka.

Ila ndo kawaida yetu wabongo, kuamka wakati rasilimali zimeshaenda.
 
huyu mh Zitto kama msanii flani niliwahi kusoma kuwa hatagombea ubunge tena, lkn bdae akageuka, na inavyo onekana kwa hatua aliyofikia ya kujitoa naanza kupata hofu labda alitaka kuuza chama kama angeshinda ila alipoona amestukiwa ameamua kujitoa. Ila hofu yangu wasije waka mCHACHA WANGWE kama atakuwa hana msimamo

Wewe tafakari kwanza.

Zitto kaitwa na wenye chama akaambiwa aondoe jina lake.

Wangwe kwa kuwa hakuwa na shule nzuri mlimdharau na kumuundia umbea kuwa alipewa rushwa na migodi...Sasa Zitto.

Hapa tatizo ni MBOWE Disco Joker
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom