Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Zitto ataweza?

Maswali Magumu: Na Ansbert Ngurumo
Source: Tanzania Daima

NIMEFARIJIKA kusikia na kusoma kwamba Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ameamua kugombea uenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa shinikizo la wapambe, si kwa hiari yake; kwani maswali ya awali niliyokuwa najiuliza niliposikia anagombea uenyekiti, si kama ana weza au la.

Nilitaka kujua Zitto ana haraka gani, na kama anagombea kwa uamuzi wake binafsi au kwa shinikizo la watu wengine; na kama ni kweli, ni kina nani.

Nilitaka kujua pia kama anajua athari ya uamuzi wake huo kwa muda mfupi na mrefu kwenye chama chake na yeye binafsi.

Vile vile, nilitaka kujua kama chama chake kilichomtambua, kikamlea na kumfunda kisiasa kimemwandaa kugombea nafasi hiyo au anakwenda kama ‘mgombea binafsi’ ndani ya chama.

Lakini kwa sababu ameshajibu swali moja hapo juu, na kwa kuwa bado yapo maswali mengi yanaulizwa juu yake, hasa kwa kuwa ameibua mjadala kitaifa, nimeona leo niandike makala hii kumlinda na kumsaidia kama mdogo wangu, msomi mwenzangu, mwanaharakati mwenzangu, kijana mwenzangu na rafiki yangu; na kwa kuwa mimi na Zitto tuna mengi tunayokubaliana na kutofautiana.

Zitto amethubutu kufanya kile ambacho vijana wengi wa umri wake wanaogopa kufanya. Anajaribu kuutumia umaarufu wake karama yake na mvuto wake wa kisiasa vikiwa bado juu ili asonge mbele na kujijenga kisiasa.

Tumzuie? Tumruhusu? Tumpinge? Tumuunge mkono? Tumshabikie? Tumshauri au tumwache? Tumjali au tumpuuze? Je, tuna uwezo wa kufanya lolote miongoni mwa hayo hapo juu?

Jambo moja liko wazi.

Kila anayemjadili Zitto leo, si tu kwamba anamjadili Mbunge wa CHADEMA, bali anamjadili pia mbunge wa taifa.

Uamuzi aliochukua na athari au hatima yake vina mwangwi mkubwa kitaifa.

Kwa sababu hiyo, hatuwezi kumpuuza Zitto. Na mimi nitajaribu kufanya nitakaloweza katika hayo niliyoyataja hapo juu.

Bahati nzuri kuna walionitangulia. Rafiki yangu mwingine, ambaye pia ni rafiki ya Zitto, Absalom Kibanda, katika safu yake ya Tuendako, wiki hii, amemsema sana mbunge huyo katika kile alichokiita ‘anguko la Zitto.’

Mimi nitajadili anguko la CHADEMA. Lakini kabla ya kwenda mbali, hatuna budi kujiuliza: Nani angependa na kushabikia anguko la Zitto au la CHADEMA? Kwa manufaa gani? Je, kuna watu wanaomwandalia Zitto na kumsindikiza katika anguko lake au la chama chake? Je, anguko la Zitto ni kuupata au kuukosa uenyekiti wa CHADEMA? Je, Zitto kuupata au kuukosa uenyekiti wa CHADEMA ni heri kwa Tanzania?

Maswali ni mengi, lakini lipo hili ambalo Kibanda amelidokeza katika makala yake, akalichochea na kulifafanua zaidi katika barua pepe kwa umma; la kusema Zitto anatumiwa na CCM bila kujua ili kuivuruga na kuibomoa CHADEMA, mithili ya NCCR-Mageuzi na CUF.

Nataka kumtetea Zitto kidogo. Naamini kwamba hatumiwi na CCM bila kujua. Kwangu mimi, Zitto ameshavuka viwango vya kutumiwa bila kujua. Zitto ni mjanja vya kutosha, kiasi kwamba akiamua kutumika, atafanya hivyo kwa hiari yake.

Kwa vyovyote vile, Zitto anajua analofanya. Hivyo, wanaomlaumu na wanaomtetea wasizunguke mbuyu; waseme kile wanachokusudia kusema. Wamwambie.

Kama wanakerwa na vikao vya siri anavyofanya na vigogo kadhaa wa CCM, waseme; na watutajie majina. Kama ni Joseph Sinde Warioba au Dk. Ahmed Salim au Rostam Azizi au Edward Lowassa au Rais Jakaya Kikwete au Lawrence Masha au William Ngeleja; waseme wazi.

Kilicho wazi ni kwamba Zitto anajaribu kujenga himaya yake kisiasa ndani na nje ya CHADEMA. Wakati mwingine anajisikia fahari kuzungukwa na kushauriwa na vigogo kama hao.

Katika umri wake mdogo, anaona heshima na fahari ya pekee kupata joto na ushauri wa vigogo kama hao, hata kama baadhi yao hawana majina mazuri kisiasa na kijamii. Kwake, kisiasa, anaona kama anawekeza kwa malengo ya muda mrefu.

Maana kinachozungumzwa sasa ni kwamba mojawapo ya ajenda za Zitto kuutaka uenyekiti ni ahadi aliyopewa na baadhi ya vigogo wa CCM kwamba wanatamani kujiengua na kujiunga na CHADEMA iwapo tu, ataweza kumwangusha Freeman Mbowe katika nafasi ya uenyekiti.

Uongo wanaotumia ni kwamba wakishajimega kutoka CCM wataiwezesha CHADEMA kupata wabunge wengi mwaka 2010, na hata kuipa uwezekano wa kuwa na waziri mkuu kutoka chama cha upinzani.

Lakini hapa kuna mambo mawili. Zitto anajua kuwa mwaka 2005, chama chake kilikuwa na mpango kama huo wa kuwashawishi watu maarufu kutoka CCM wajiunge na CHADEMA kwa malengo hayo hayo.

Na mmoja wa watu waliokuwa wanawindwa katika hatua za awali kabisa ni Jakaya Kikwete na kundi lake, wakati wanamtandao wakiwa hawana uhakika wa mtu wao kupitishwa katika vikao vya CCM kutokana na tuhuma walizojua zinamwandama mtu wao, lakini pia kutokana na hujuma za kisiasa kutoka kwa vigogo kama Philip Mangula, Benjamin Mkapa, John Malecela, Frederick Sumaye na wengine ambao walikuwa wameshikilia chama na serikali; huku pia ukiwapo woga na hofu juu ya Dk. Salim Ahmed Salim.

Wanamtandao walikuwa tayari kuhama kama wangekataliwa CCM, na chama walichotaka kukimbilia ni CHADEMA.

Zitto mwenyewe anakumbuka jitihada zake za kuwanasa wanasiasa wa aina ya Zakia Meghji zilivyoshindikana, hasa baada ya yeye mwenyewe kutoboa siri hiyo kwa vyombo vya habari.

Na kikubwa zaidi, waliweza kutumia vema mbinu zao chafu, wakapenya katika kinyang’anyiro na kumpitisha mtu wao. Wakaanza mkakati na wakala yamini kumshughulikia Mbowe kisiasa na kibiashara, wakijua kuwa nguvu yake inategemewa sana kuikuza CHADEMA, na kwamba wakifanikiwa kumdhoofisha Mbowe, CHADEMA itadhoofika pia na kuwapisha kirahisi mwaka 2010.

Tunajua mbinu walizokuwa wanatumia, na tumeshuhudia wakifurukuta tangu mwaka 2007; lakini wameshindwa kwa sababu CHADEMA imekuwa na watu shupavu na mahiri, huku ufisadi wa wanamtandao ukichangia kuwamaliza ‘makabakaba’ na kusaidia harakati za kuwabana.

Zitto amekuwa mmoja wa mashujaa katika vita dhidi ya ufisadi, lakini akiwa mkweli atatuambia bila kificho kuwa watu wale wale waliokuja kufahamika baadaye kuwa mafisadi, ndio waliokuwa wanaomba CHADEMA iwape nafasi walipokuwa hawajaipata CCM.

Kwa hiyo, kupata kwao nafasi katika CCM ndio ulikuwa wokovu wa CHADEMA, maana leo hii ndiyo ingekuwa inashambuliwa kwa ufisadi kama wanamtandao wangejiunga nayo, hata kama wasingefaulu kushika madaraka.

Ndiyo maana wengi wetu tunatarajia kwamba Zitto angepaswa kuwa mwangalifu sana anapoletewa masharti ya namna hii na vigogo wa CCM wanaomuahidi kujiunga CHADEMA kwa kishindo iwapo atamuondoa Mbowe.

Hili ni sharti lenye hila; na woga wao kwa Mbowe unapaswa utumiwe kama nguvu ya CHADEMA dhidi ya CCM, na sifa ya ziada ya kiuongozi ya Mbowe.

Wana CCM hawawezi kuwachagulia wana CHADEMA kiongozi bora. Na kama kweli wanamtuma Zitto (ingawa yeye amekanusha) wanajua wanachokitaka.

Pili, Zitto na wapambe wake wanapaswa wajue kuwa nguvu na uhai wa CHADEMA haviwezi kutoka CCM. Na kama ikitokea hivyo, vigogo wa CCM wakameguka na kujiunga CHADEMA, hilo ndilo litakuwa anguko la kwanza la CHADEMA.

Sababu ni moja. Baadhi ya hao wanaoionea ‘huruma’ CHADEMA kwa staili hiyo, ni makapi ya kisiasa huko waliko. Siamini kama ni jambo jema kutarajia kuijenga CHADEMA kwa kutumia makapi ya CCM.

Wanaotaka kuijenga CHADEMA bora wawekeze katika damu mpya, kizazi kipya kisicho na mawaa ya ufisadi.

Kazi ile ile iliyofanyika kuwatambua kina Zitto, John Mnyika, John Mrema, Halima Mdee, Mhonga Ruhwanya na vijana wengine wengi wanaoendelea kuchangamsha siasa za CHADEMA na kuchochea harakati, iendelee kufanyika kuendeleza kazi nzuri iliyokwishaanza chini ya uongozi wa sasa wa kina Mbowe, Dk. Willibrod Slaa na Zitto mwenyewe.

Kwa hiyo, kama makundi haya ya wana CCM yanamwaminisha Zitto kwamba njia pekee ya kuijenga CHADEMA ni kumwondoa Mbowe, kumweka Zitto na kuwaruhusu wao kujiunga, Watanzania wanaoona mbali watamuonya yeye na watu wake kwamba sasa wanavuka mipaka ya demokrasia, wanajiingiza katika uhujumu, usaliti na uhaini ambao unamfanya Zitto sasa aanze kuwashambulia viongozi wenzake kwa maamuzi yaliyofanyika ndani ya vikao halali (kwa mfano kuhusu kuwasimamisha watu uanachama au kuwafukuza kabisa), wakati naye alishiriki, tena kama kiongozi mwandamizi wa chama.

Na jambo hili linazua hoja kwamba labda akifanikiwa kuwa mwenyekiti hatachukua hatua zozote dhidi ya wazembe, wasaliti, mafisadi na watovu wa nidhamu ndani ya chama.

Ikumbukwe kuwa ni vigumu Zitto kukiri kuwa anatumiwa na CCM. Inawezekana watu wanamuonea tu kwa sababu ya hisia, lakini ninavyokumbuka mimi tuhuma hizi zimetokana na mambo kadhaa.

CCM wanaogopa nguvu ya CHADEMA; na wanatafuta pa kupumulia, baada ya kuthubutu na kushindwa kwa miaka mitatu mfululizo.

Wanadhani wakifanikiwa kuwapambanisha vigogo wa chama unaweza kuwa mwanya wa kujenga ufa ndani ya chama na wao kupona.

Wanahofia umaarufu wa Zitto unaweza kuwadhuru wasipokuwa karibu naye. Njia rahisi wanayodhani inaweza kumlainisha ni kukiri umaarufu wake, kuutambua na kumfanya ajisahau, alewe umaarufu wake, wamtumie.

Ndiyo maana Zitto alipojisahau akaanza kutetea ununuzi wa mitambo ya Dowans, akidhani umaarufu wake ungeweza kubadili mjadala wa kitaifa na upepo wa kisiasa, wapambanaji wenzake walimsikitikia sana, na tuhuma za waziwazi zikaanza kurushwa dhidi yake kwamba ‘kuna waliomharibu.’

Hata leo, kauli yake kuhusu Dowans imemjeruhi sana kisiasa, hasa inapochangiwa na kile wachunguzi wanachokiita vikao vyake vya siri na wabaya wa CHADEMA. Na kama baadhi yao ndio wanaojitokeza leo kumshabikia na kumpongeza hadharani kwa hiki anachofanya, ni vigumu kuzuia hisia za wananchi dhidi yake. Itamchukua muda mrefu kujisafisha.

Na katika siku za hivi karibuni, Zitto amesikika akizungumza katika Radio Sauti ya Ujerumani akidai kwamba tofauti ya msingi kati yake na Mbowe katika kinyang’anyiro cha uenyekiti ni kwamba ‘Mbowe ni bepari, Zitto ni mjamaa!’

Lakini Zitto anajua kuliko wengi wetu kuwa kiitikadi CHADEMA haijawahi kuwa chama cha kijamaa.

Anajua kuwa watu pekee wanaojidai kuwa na itikadi ya ujamaa hapa nchini ni CCM, ingawa nao wanaishi kwa siasa za ubepari wenye ulemavu.

Katiba ya CHADEMA, ambayo Zitto ameshiriki kuiandika upya mwaka 2006, akiwa mbunge na kiongozi mwandamizi, inaeleza vema itikadi ya chama chake. Miaka mitatu baadaye, Zitto amegeuka na kuwa mjamaa katika chama cha kibepari? Lipi limemsibu Zitto?

Zaidi ya hayo, Zitto amepata bahati ya kukosolewa na vyombo vya habari visivyomilikuwa na CCM, huku akisifiwa na kupongezwa na kupewa moyo na vyombo vya CCM au vinavyomilikiwa na makada wa CCM.

Ikumbukwe pia katika migogoro mingine iliyopita ya uongozi ndani ya CHADEMA, ya kweli na ya kupandikizwa, vyombo hivyo hivyo vilikuwa vinawaunga mkono na kuwashabikia waliojitokeza kuisumbua CHADEMA au Mbowe.

Hii si neema ya kisiasa kwa Zitto. Wana CCM wanamsifu makusudi ili kumchafulia jina mbele ya wana CHADEMA na wananchi wengine waliomwamini kwa muda mrefu, ili baada ya muda naye awe kapi la kisiasa kama wao.

Sisi wengine tungependa kumzuia asiende huko – kama atasikiliza. Vinginevyo, iwapo atakifikisha chama chake katika unyonge, udhalili na hatimaye kifo kama kilichowakuta NCCR-Mageuzi, au kama hataki kujikumbusha jinsi CCM ilivyoisambaratisha CUF, anaweza kuchagua kutumia ubishi na umaarufu kukuza haiba yake kisiasa na kuua taswira ya taasisi iliyomlea na kumkuza.

Nimekuwa nafuatilia wanasiasa wanaompongeza. Ni vyama vya NCCR-Mageuzi, CUF na TLP; vile vile ambavyo vimeshughulikiwa na CCM, na baadaye vimekuwa katika ushindani na wivu dhidi ya CHADEMA, ambayo inakua, vyenyewe vinafifia, kiasi cha kuathiri hata ushirikiano wa kisiasa uliokuwa umeanzishwa.

Hizi ndizo pongezi anazotafuta Zitto? Anazihitaji? Anapochanganya hizi na za CCM, anapata jawabu gani?

Kwa elimu na uzeofu wake, Zitto anapaswa kuelewa kwa nini watu wanapigia kelele uamuzi wake wa kugombea uenyekiti sasa, katika mazingira haya, na kwa staili aliyoamua kutumia.

Watanzania hawako tayari kumsamehe binadamu yeyote atakayeshiriki kwa kujituma au kutumiwa kudhoofisha nguvu iliyopo sasa ya CHADEMA Bara na CUF Visiwani. Na kama yupo, asiwe Zitto.

Ni haki yake kugombea na kuongoza. Lakini lazima atumie busara inayomlinda yeye na taasisi yake. Nyota yake kisiasa bado ni changa na inawaka. Hana sababu ya kujiingiza katika jitihada za kuizima mapema hivi.

CHADEMA inaweza kumwandaa Zitto kuwa kiongozi mkubwa kitaifa baadaye, iwapo atakubali kufanya kazi na viongozi wenzake na kujijenga pole pole.

Naamini kwamba hata Mbowe asingefika hapo alipo kama angekurupuka au kama angegombea kwa mbinu zinazotiliwa shaka, na katika mazingira kama haya ya sasa. Tungemshauri kama tunavyofanya kwa Zitto leo.

Hata hivyo, ninapotafakari mbinu alizotumia Zitto, nafika mahali nadhani Zitto hajadhamiria kushinda, bali anataka kumtikisa Mbowe na chama, kuleta msisimko wa kitaifa kuhusu uchaguzi ndani ya CHADEMA, kujenga hisia na ufuasi wa hapo baadaye, ili atakapokuwa amefuzu, na chama kiko tayari, iwe rahisi kwake kupitishwa, kugombea na kushinda.

Kwa sasa naona anatumia njia ile ile iliyotumiwa na Jakaya Kikwete kuusaka urais mwaka 1995, ambao aliupata baada ya miaka 10 ya kujijenga, kujitangaza na ‘kukua kidogo.’

Tuombe tu kwamba umaarufu uambatane na uwezo; maana kama alivyosema Kibanda, ya Augustine Mrema na Kikwete yametufundisha ukweli kwamba kuna tofauti kati ya kutoa hotuba nzuri, kuhamasisha umma na kuwa kiongozi.

Navijua CHADEMA na CCM; nawajua vizuri Mbowe na Zitto. Najua uwezo na udhaifu wao, na sababu ya CCM kuiogopa CHADEMA ya Mbowe.

Kama CCM wamehangaika kwa miaka mitatu mfululizo wakashindwa, na kama wataweza kuibomoa CHADEMA hii kabla ya Uchaguzi Mkuu 2010, ibilisi awape nini!

Si lazima wamwangushe Zitto, maana anaweza kujikwaa, au hata akaanguka na kusimama pale pale alipo au akasimamia pengine. Lakini iwapo CHADEMA itaanguka haitaamka; na itatuchukua muda mrefu sana kupata nguvu nyingine na uwanja wa mapambano; walau si kabla ya 2010.

Wasioona anguko la CHADEMA katika mpambano wa Zitto na Mbowe, waendelee kutafakari, na wajiulize sababu za ushabiki wa wazi wa wabaya wa CHADEMA katika pongezi wanazompa Zitto.

Natambua kuwa Zitto amefanya kazi nzuri bungeni na majukwaani. Aendelee kuifanya, maana anaiweza, na taifa linamhitaji kuelekea 2015 akiwa na viongozi wenzake waandamizi wa CHADEMA.
 
Sad indeed, CHADEMA wametuangusha sana, ktk hali kama hii ni vema Mbowe akaondoa jina lake, hapo nitaweza kurudisha imani yangu kwa CHADEMA. Woga wa kupambana kidemokrasia ni woga unaojenga udikteta. Bado tupo mbali kuliko tunavyofikiria.
Demokrasia na ushindani ndiyo njia pekee yakupata uongozi au kiongozi bora kuachiana uongozi ndiyo chanzo cha kupata viongozi dhaifu sioni kama Mbowe anajiamini aogope kugombea kwa Zitto na kuacha kura zichukue mkondo wake.Kama Zitto atajitoa kumwachia Mbowe litakua doa kubwa kwa CHADEMA na mwanzo wa wananchi kupoteza imani kwa chama hiki kwani wananchi watashindwa kuitofautisha CHADEMA NA CCM.Wazee wa CHADEMA mnapashwa kuliangalia hili kwa makini.MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Kichefu chefu kitupu, yaani naona kama akili zinataka kuruka vile dah...... sasa naona zama za kuendelea kutawaliwa na ccm mpaka nitakapoingia kaburini ndo zinaendelea kushamiri, na hapa ndo ccm itakapotumia mpasuko huu kuuangusha upinzani na wakapata ushindi wa kishindo 2010. Eee Mola tuangalie viumbe wako tunavyochezewa sinema mchana kweupeee
 
Kwakweli NJAA ni mbaya sana. Njaa inaharibu Ueledi na inauwa shule ya mtu.

Bwana Ansbert Ngurumo kama ulikuwa na nia nzuri na Zitto basi ungeelezea pia kuwa Mbowe anagawa chama na nini unashauri kuhhusu Mbowe.

WEWE Ansbert Ngurumo UMELIPIWA ADA YA SHULE na Mbowe. Chochote utakachosema humu kwa mshindani wa Mbowe ni CONFLICT OF INTEREST.

Jamani hawa waandishi wa Tanzania daima mi naomba pass mark zao za secondari O and A level. Isije kuwa wamefeli huko na kudandia vyuo vya Royal journalism college na kufadhiliwa na kupata degrees.

Seriously nina wa doubt sana.

Yona Bin Sira alisema: Ficha upumbavu wako ila usifiche hekima yako
 
Sijui lakini ninahisi kama bwana Ansbert Ngurumo hautofautiani sana na Issa Mnali wa magazeti ya UDAKU bongo.

Unapoongelea Zitto kukutana na wana CCM kwa siri..ulitaka ukiwa Chadema ukienda kuonana na Fairplayer basi utangaze?!... typical udaku style

Hongera DJ, fedha zako zanafanya kazi, naona umegeuka kuwa manji wa Ze comedy (Tanzania daima), tofauti yako ni kuwa unaimiliki.

Hongera sana
 
owenya%281%29.jpg

Lucy Owenya.

Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo na mtoto wake, Lucy Owenya, wamechaguliwa bila kupingwa kukiongoza chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Kilimanjaro kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Ndesamburo alichaguliwa tena kukiongoza chama hicho mkoani hapa baada ya kuibuka na ushindi wa kura
49 kati ya 50 za wajumbe wa mkutano huo wakati mtoto wake, Lucy, aliibuka na ushindi wa idadi ya kura kama hizo katika uchaguzi mkuu uliofanyika jana mjini hapa.

Katika uchaguzi huo,
Basil Lema, alichaguliwa kuwa Katibu wa chama hicho huku Deogratius Munishi, akichaguliwa kuongoza Baraza la Vijana wa chama hicho na Seranus Mushi alichaguliwa kuongoza Baraza la Wazee wa chama hicho.

Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Ndesamburo alisema ushindi wake ni ishara kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwamba bado anakubalika na kamwe hata katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu hapo mwakani, atajitahidi kutetea kwa udi na uvumba kiti chake cha ubunge.

Alisema anashangazwa na propaganda za viongozi wa CCM ambao wamekuwa wakidai kuwa yeye ni mzee na hivyo hatagombea tena kiti cha ubunge Jimbo la Moshi Mjini jambo ambalo si la kweli.

"Eti wanasema mimi ni mzee, kibabu nimechoka sitagombea tena ubunge...Huo ni uzushi wao na ushindi wangu wa leo ni indiketa ya kwamba uchaguzi mkuu ujao nitatetea jimbo langu na kumbwaga mgombea wa CCM," alisisitiza Ndesamburo.

Naye Lucy Owenya ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) akizungumza na waandishi wa habari baada ya ushindi huo, alitoa wito kwa wanawake mkoani Kilimanjaro kujitokeza kwa wingi na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Owenya alisema wanawake hawana budi kuacha woga wa kuwania nafasi za uongozi kuanzia serikali za mitaa, madiwani na hata ubunge ili kuweza kufikisha uwakilishi wa asilimia asilimia 50 bungeni na halmashauri.





CHANZO:

Ndesamburo na Mtoto wake hawakuwa na wapinzani kama itakavyokuwa kwa Mbowe hatakuwa na Mpinzani.

kingine wagombea wote ni wachagga kwani Kilimanjaro si kuna wapare pia?


Kitilla,

Rafiki yangu nakuwambiaga kila siku humu. Tulia kwa sasa, tafakari...chukua hatua.

Mnyika,

Ukiona mwenzio ana....na wewe......... najua una akili za kupima. Tutaftane baada ya uchaguzi.
 
CHADEMA: Chama Cha DEMOKRSASIA na MAENDELEO

Huu ndiyo msingi mama wa Chama kama wanataka waeleweke ni chama cha namna hiyo. Kabla hawajafanya maamuzi yote kwa kivuli cha UMOJA wa CHAMA wakumbuke CHADEMA inasimamia nini ukiondoa individuals. I hope CHADEMA wanataka kujenga TAASISI huru na si UFALME.

Then kama ni hivyo wajiulize: DEMOKRASIA YA KWELI NI NINI?
Na MAENDELEO YA KWELI NI NINI?

Then si vibaya kujifunza kutoka USA ilikuwaje The CLINTONS magiant wa Chama wakapambana na The OBAMAS na je kwa kufanya hivyo walikigawa chama?
 
Ndio maana naona itakuwa ngumu kwa vyama vya upinzani kutoa suluhisho mbadala la kusuasua kwa CCM. Kuna watu vyama vya upinzani ni kama NGO zao
 
CHADEMA: Chama Cha DEMOKRSASIA na MAENDELEO

Huu ndiyo msingi mama wa Chama kama wanataka waeleweke ni chama cha namna hiyo. Kabla hawajafanya maamuzi yote kwa kivuli cha UMOJA wa CHAMA wakumbuke CHADEMA inasimamia nini ukiondoa individuals. I hope CHADEMA wanataka kujenga TAASISI huru na si UFALME.

Then kama ni hivyo wajiulize: DEMOKRASIA YA KWELI NI NINI?
Na MAENDELEO YA KWELI NI NINI?

Then si vibaya kujifunza kutoka USA ilikuwaje The CLINTONS magiant wa Chama wakapambana na The OBAMAS na je kwa kufanya hivyo walikigawa chama?

Wakati nipo University nilidhani ninaweza kuhamamia chuo kingine kama vile wakati nipo primary kumbe sio.......

Misingi ya siasa yetu haifanani naya kimarekani. I would compare technologies in technical issues but not politics base. DCI inaweza kazi kama FBI but sio sio rahisi CHADEMA kufanya kama DEMO.
 
Last edited:
Wakati nipo University nilidhani ninaweza kuhamamia chuo kingine kama vile wakati nipo primary kumbe sio.......


  • Misingi ya siasa yetu haifanani naya kimarekani. I would compare technologies in technical issues but not politics base. I wish DCI ifanye kazi kama FBI but sio sio rahisi CHADEMA kufanya kama DEMO.

Unajua kwanini? mi najua kwanini
 
Ndio maana naona itakuwa ngumu kwa vyama vya upinzani kutoa suluhisho mbadala la kusuasua kwa CCM. Kuna watu vyama vya upinzani ni kama NGO zao

This situation of political parties in this country is heartbreaking!!!

A few weeks ago we were discussing CCM and their kitchen mess, now its CHADEMA and their domestic unrest, not long ago were looking at CUF cobwebs!!

For once, can our country live without politics???

WAKUBWA WA CHADEMA MZE SLAA, DOGO ZITTO, CLASSMATE KITILA, KAMANDA MBOWE, WEWE LWAKATARE ULIYEENDA CHADEMA NA ZOGO LIMEANZA [i dont mean you are the cause]; etc.... You re members here and sadly your silence allows speculation and rumour mongering, which in turn, is detrimental to all ya....

JUST COME UP WITH SOMETHING AND YOU WILL SHELF YOUR OWN PARTY AND PERSONALITY FROM BEING UNDRESSED BY GREAT THINKERS

MAGAZETI NAYO SASA YAMEANZA KUCHUKUA HUMU HABARI NA KUCHAPISHA, DO NOT ALLOW TABLOIDS TO GET STORIES BY YOUR SILENCE... IF YOU TRUST MTANZANIA DAIMA ALONE, MMEKOSEA KWANI COVERAGE YAKE BADO

COME UP AND OUT AND CLEAR THIS MESS YOURSELVES

SLAA UNA BUSARA SANA HEBU TUONE KWA HILI, SOMETIMES I WONDER IF POLITICIANS ARE THE MOST UNRELIABLE THINGS ON EARTH.... PROBABLY RIGHT!!!

 

This situation of political parties in this country is heartbreaking!!!

A few weeks ago we were discussing CCM and their kitchen mess, now its CHADEMA and their domestic unrest, not long ago were looking at CUF cobwebs!!

For once, can our country live without politics???

WAKUBWA WA CHADEMA MZE SLAA, DOGO ZITTO, CLASSMATE KITILA, KAMANDA MBOWE, WEWE LWAKATARE ULIYEENDA CHADEMA NA ZOGO LIMEANZA [i dont mean you are the cause]; etc.... You re members here and sadly your silence allows speculation and rumour mongering, which in turn, is detrimental to all ya....

JUST COME UP WITH SOMETHING AND YOU WILL SHELF YOUR OWN PARTY AND PERSONALITY FROM BEING UNDRESSED BY GREAT THINKERS

MAGAZETI NAYO SASA YAMEANZA KUCHUKUA HUMU HABARI NA KUCHAPISHA, DO NOT ALLOW TABLOIDS TO GET STORIES BY YOUR SILENCE... IF YOU TRUST MTANZANIA DAIMA ALONE, MMEKOSEA KWANI COVERAGE YAKE BADO

COME UP AND OUT AND CLEAR THIS MESS YOURSELVES

SLAA UNA BUSARA SANA HEBU TUONE KWA HILI, SOMETIMES I WONDER IF POLITICIANS ARE THE MOST UNRELIABLE THINGS ON EARTH.... PROBABLY RIGHT!!!


Pole kwa kuchelewa kuona haya. Siku nyingine tukiwaambia basi mfikirie mara mbili mbili!
 
Hivi hawa CHADEMA wanaelekea wapi, au na wao wanataka kuwa kaCCM walivyomundia Sitta tume, wamuache Zitto, tumuone jinsi gani anavyokubalika.
 
Hivi hawa CHADEMA wanaelekea wapi,? au na wao wanataka kuwa kama CCM walivyomuundia Sitta tume, wamuache Zitto, tumuone jinsi gani anavyokubalika.
 
Pole kwa kuchelewa kuona haya. Siku nyingine tukiwaambia basi mfikirie mara mbili mbili!

Mkubwa, haya yako wazi, lakini ni kama unapouguza mgonjwa; huwa haukati tamaa-- inakuja imani kwamba aliye mahututi ataamka tu na kutembea, ni mpaka pale anapokata roho ndio unapata akili na kuanza kupanga nyumba ili wageni waje kuzika nk.

Its sad pale ambapo hata walio second class [or third class] katika siasa wanaanza kuonyesha kucha zao changa!!!!

I WISH I COULD SEE CCM EXECS WANAVYOKATA WINE KWA FURAHA.... ADUI YAKO MUOMBEE NJAA
 
Jamani Chadema, sidhani kama mnatambua ni kwa jinsi gani mmejishushia hadhi na imani kwa hili. Mimi nilivyoona asubuhi ya leo sikuamini kama ni Chadema ninayoifikiria! Wengi wanaamini nyie mnademokrasia ya kweli lakini kumbe wale wale.

Mimi sina chama ila kwa Muda mrefu nimekuwa nikifikiria kujiunga na Chadema but I better dont, sivyo mnavyoonekana.

Mbowe ni nani hadi asipingwe!!!!!??? kama anakubalika ndani ya chama wacha aende na akishinda hata Zitto atakubali na mshikamano utaongezeka.

Kweli CCM leo lazima wanywe mvinyo wa furaha. Nadhani hatuna chama cha kweli cha demokrasia TZ hiii, ni usanii na siasa maslahi zimetawala.

Mmeniharibia J2 yangu leo Nyie Chadema
 
[/LIST]
Unajua kwanini? mi najua kwanini

Mfumo siasa na Imani alionijengea baba yangu ambaye nae alijengewa na CCM ambayo haikumuelewa Mwalimu J. K Nyerere ambae alikuwa anatamani siku moja tuishi kama scand countries. Yaani nchi yenye ustawi, ila wajanja walikuwa wengi. Watu wamekata tamaa maana kila wanaposhika pabaya, ukijaribu kufikiria ya kesho unatamani CCM iondoke lakini akumbuka hajajenga nyumba hana gari anatamani CCM mwishoni tunatamani nafasi zetu tusilimishe kwa umjuae au kwa ndugu ili kuhakikisha kuwa mirija haikatiki.

Kuna jamaa kaniacha hoi ofisini " Nilifikiria mtu kama Zitto ataweza kuandaa maisha ya baadae kwa watoto wangu. sio kwa kunipa hela ila kwa kutengeneza platform ilio fair for everybody. Kitendo cha mtazamo wangu kwake na yeye leo kuanza kwenye kule juu nimepoteza imani yangu kwani kwa vision yake can not be implemented now may be 2015 na angetumia muda mwingi kutafuta Zittos badala ya kwenda huko. Maana atakosana tu na watu na labda awe dikteta".

Bado natafakari suala la DOWANS, Kujitoa na kurudi tena kuwania ubunge na hili la mwenyekiti.

Kimsingi sijawahi kukutana wala kuongea na Zitto, namwona tu magazetini, JF but sisi wafuasi wake tunapata shida kumsafisha kuhusu suala la Dowans. Siasa mtaji wake ni watu, Kumbuka kupigiwa makofi sio umaarufu.

Nafikiri Zitto hao washauri wako inabidi uwasaili, la sivyo tutarudi zidumu fikra za mwenyekiti hapa.
 
Haya ndo yale tulosema chadema ni bado saana, mlisema sana kuhusu Cuf lkn wakati safari anachukua form pamoja na yule jamaa mwengine,ambapo LIpumba alipata wapinzani wawili ktk nafasi ya uenyekiti,alichotamka Lipumba ni kwamba kila mwanachama ana hakki ya kugombea nafasi anayoitaka na itakuwa uzuri zaidi wakijitokeza kwa wingi,na Lipumba akampongeza sana Pr safari kwa kuchukua form,sasa hichi ndio chama cha democrasia...

Leo tunayaona haya, MIMI NAAMINI CHADEMA HAKIPO KWA AJILI YA KUIONG'OA CCM NA SABABU ZA MSINGI NINAZO,miongoni mwa hizo ndo hiyo inaanza kujitokeza. USHAURI WANGU KWA CHADEMA ILI WARUDISHE IMANI KWA WANACHAMA WAKE,WAMWACHE KAMANDA WETU ZITTO AGOMBEE,NA KAMA ASIGOMBEE BASI WASIKILIZE MANENO YA MKUU WANGU INVISIBLE KUWA NA MBOWE NAE ATOKE ULINGONI. KILA LA KHERI CHADEMA.
 
Lunyungu, ndo maana nimesisitiza kuwa "Bado wana muda". Kufikia kesho wawe wamefanya maamuzi ambayo yatabadili hali hii... Nimemwona Kitila mitaa hii, naona amekosa usemi kabisa!

Hii inaweza kupelekea wazalendo kadhaa kuanzisha chama kipya cha siasa... Kama hawaamini wafanye kosa kipindi hiki waone.
Ndugu yangu Invisible tutaishia kuwa na vyama vingapi? wabanane humo humo!
 
kibanda umeshinda kweli ngoma ya mtoto/kijana haikeshi zitto kawa kama arsenal ya wenger.
Kanda 2 ya Arsenal yametoka wapi tena?Man U mnaringia ushindi wa kubebwa na refa?umemsikia Mzee Wenger leo akiongea? na hiyo penalty aliyonyimwa Eboue hukuiona? Man U hovyooooo kazi kuhonga marefa,mafisadi wakubwa nyie,tena nna hasira usinikumbushe ya jana nisije nikakutoa utumbo,tuongelee premialigi ya Zitto na Mbowe!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom