Kuelekea UEFA champions league final

Kuelekea UEFA champions league final

Watu wanaongea suala la historia, soka la sasa halitazami historia. Soka la sasa linatazama ufundi, mbinu n.k

Madrid beki yao sio nzuri saaaaana kutokana na majeruhu ya hapa na pale pamoja na kipa wao Navas kuwa kama Juma Kaseja.

Juventus beki yao ipo vyema, ile beki ikisema hairuhusu goli hata kwa dakika 120 inawezekana kabisa.

Natupa karata yangu kwa juventus kubeba kombe.
 
Jumamosi itakua siku mbaya sana kwa Zidane na mashabiki wa madrid,Madrid atapigwa goli la mapema sana.

Sioni mtu wa kupenya ukuta wa chuma wa Juventus chini ya beki katili Chielini.

Kule Mbele tunamwacha mtu mrefu Mandzukic,Ramos akileta mieleka yake atakula red mapema sana.

Kibibi Kizee cha turin twende kazi
Kama upo akilini mwangu vile, sijui Madrid watapata goli kwa njia gani kwa kweli.
 
Moja kati ya match ngumu sana fainali muhimu kwa Cr7 na Madrid kwa ujumla, Zidane atakuwa na kazi rahisi sana ya kupanga kikosi anawatu wengi sana wanaoweza fanya maajabu... Upande wa pili Juve hawana kingine wanachotaka zaidi ya ubingwa wa Uefa unaowasumbua kwa kipindi kirefu wakiwa na record ya kupoteza fainali Nne, Buffon anayinafasi ya mwisho ya kukamilisha record ya kuwa kipa bora zaidi ushindi wa Juve unaweza kumpatia kombe na ballon dor pia. All in all nawapa nafasi kubwa Real madrid kuchukua kombe... Final score R.Madrid 3 - Juventus 2. Hii sio ya kukosa.....
Naona Mkuu unaandika tu goli 3 kirahisi rahisi, embu angalia stats za Juve msimu huu UEFA halafu urudi tena hapa kuedit post yako.
 
Naona Mkuu unaandika tu goli 3 kirahisi rahisi, embu angalia stats za Juve msimu huu UEFA halafu urudi tena hapa kuedit post yako.
Kuanzia hatua ya mtoano,Juve karuhusu goli moja tu
 
Juventus ina beki na viungo wazuri sana wenye uwezo wa kutengeneza nafasi nyingi za kufunga. Shida ya juventus ipo kwenye kumalizia ndio tatizo hasa higuan amekuwa anapoteza nafasi nyingi sana za wazi. Real madrid wapo vizuri mbele na viungo ila alegri ni mzuri kwenye mbinu za kimchezo hivyo juventus nawapa nafasi ya kunyakua kombe
Ha ha ha ha ha ha ha eti mtu anadiriki kuwatishia Juventus kuwa viungo vya Madrid ni wazuri na wataisumbua Juve.

Kama kuwaona viungo wa Madrid wanahold mipira na kupiga pasi za hapa na pale basi kesho tutawaona wakifanya hivyo muda wote ila sio kuleta madhara kwenye ngome ya Juventus.

Ile Ngome si mchezo.
 
Afadhali carvajal karudi huwa anapiga cross murua ambazo cr7 anadukua kwa kichwa
Jamani embu tuwe serious, Ronaldo anabebwa sana na ukakamavu wake wa mwili, ni mrefu na yupp strong kweli kweli akijua yupo kwenye nafasi ya kufunga.

Hivi Mkuu, unajua ni rahisi kupiga shuti katikati ya uwanja na ukaifunga Juventus kuliko mipira ya vichwa?
 
To be honesty, kama ikitokea Madrid akashinda basi itakuwa imetokea tu, lakini kiuhalisia msimu huu UEFA hakuna timu ya kupambana na Juve na wakatoka salama. Hakuna,

"Labda itokee tu" in Sheikh Kipoozeo voice.
Unajua Mkuu, mashabiki wa ronaldo wanamihemko saaaana. Kiukweli hakuna timu ya kuipasua Juventus msimu huu, HAKUNA.

Madrid sijui hilo goli lao watalipata kwa njia ipi.
 
Narudia tena,
Sijaona team ya kumfunga Juventus kwa msimu huu.
OVER
 
Historia ipi itakayombebe Juve? Kama 1998 alifungwa kama historia hujirudia atafungwa tena,kama ni utemi kwenye Uefa hajafikisha hata nusu ya makombe ya R.Madrid na kama bingwa mtetezi ni R. Madrid.Historia ipi ya Juve itakayombeba?
Baelezee baelezee
 
Back
Top Bottom