Kuelekea UEFA champions league final

Kuelekea UEFA champions league final

Kuelekea UEFA champions league final

download.php


Madrid vs Juventus bonge la game pale UK.itakuwa fainali ngumu kweli..maana juventus itahitaji kulichukua taji ambalo waliporwa na barca 2015 na Madrid watahitaji kuweka rekodi ya kuchukua mara mbili mfululizo…

Juventus-vs-Real-Madrid.jpg


Juventus lazima watakuja na mbinu yao ya kujilinda muda mwingi wa mchezo huku mashambulizi yao yakiwategemea Mandzukic,Dybala na Higuain pia hata Cuadrado,naamini wataanza na mabeki wakati watatu (BBC) na midfielder wawili Khedira na Pjanic(ingawaje siku za karibuni wamekuwa wakipenda kutumia mabeki wawili wakati ).Kwa mfumo wa mabeki watatu wakati utawapa Real Madrid wakati mgumu sana kupata nafasi kwenye final third ya juve.Mfumo huu ni rahisi kwa juventus kuwazuia Madrid ukizingatia real marid wamekuwa wakiwatumia sana Marcelo na carvajal kuleta mipira ya cross kwa benzema na ronaldO.Pia ili kuwazuia madrid ni lazma kumnyima nafasi huyu goal scoring machine(Ronaldo),yote hii itategemea juventus kaba wataweza kushina battle la midfield..kwenye kushambulia juventus wamekuwa wakimtumia Paulo Dybala kama mtu wa kutafsiri mashambulizi yao,dybala anazunguka uwanja mzima,Dybala anafunga na ku assist,huyu ndio key player wa Juventus.
Prediksi-Skor-Juventus-vs-Real-Madrid-4-Juni-2017.jpg


Zidane atakuja na mbinu zake zile zile za kihuni kwenye game kubwa…cha kwanza huwa anajilinda na kushambulia kwa kushtukiza huku akitegemea speed ya Ronaldo benzema na winger mwingine ambaye anaweza kuwa Bale ,Isco,Rodriguez au Asensio...defense ya Madrid itaunganishwa na Casemiro ambaye yuko ki ulinzi zaidi ukilinganisha na Krose na Modric ambapo wao kazi yao ni kufanya Real Madrid inakuwa na mpira na kusambaza mipi haswa kwa Marcelo na carvajaal..

Eneo la kiungo ndilo litakalo amua hiyo game,aamini vita kali itakuwa kwenye kiungo.kwa Juventus watakuwa na kazi ya kuwazuia Kroos na Modric wasiweze kupiga pasi ambazo zitawafikia Marcelo na Carvajaal.


Kwa upande wa ulinzi real Madrid wana tatizo kiasi…goalkeeper K.navas amekuwa na makosa madogo madogo…pia wamekuwa wakiandamwa na majeraha haswa pepe,varane na Marcelo ambayo imepelekeaa Nacho Fernandez kupata nafasi ya kucheza msimu huu Ni wazi kuwa game itakuwa ya nguvu na kasi huku real Madrid wakitawala mchezo na juventus watajilinda na kushambulia kwa kushtukiza…


Ronaldo na Dybala ndio watu ambao nategemea wataamua mechi ingawaje kwenye mechi kama hizi ingawaje mchezaji huwa yeyote anaweza kuamua mechi.. Pia kwenye hii game nadhani ndipo mahali ambapo buffon na ronaldo wanatakiwa kutuonyesha nani kati yao anastahili tuzo ya mchezaji bora wa dunia japo ronaldo ana nafasi nyingine ya kuonesha uwezo wake kwenye kombe la mabara mwezi june nchini Russia

Juve wanakumbukumbu ya mwaka 1998-5-20 walipofungwa na Madrid 1-0

Katika fainali ile ambayo Juve ilipoteza ilikuwa na Zidane(Mchezaji wa Juve katika fainali ile) na kikosi kilikuwa kama ifuatavyo

View attachment 517327

Baada ya kukutana mwaka 1998 watakutana tena Katika fainali ya jumamosi hii ambapo mchezaji wa Juve wakati huko Zidane akiwa upande wa pili wa shilingi


Timu yeyote inaweza kupata ushindi katika fainali hii hivo tungojee tuone uhondo huu kutoka Cardiff,Wales

Makala imeandaliwa na Dkileo na Deadbody

Mimi Deadbody Nipo Juventus na naona fainali hii Juventus 1 VS Madrid 0

Historia itawaua REAL MADRID

Historia itawabeba na JUVENTUS

FT (1-0)
Historia ipi itakayombebe Juve? Kama 1998 alifungwa kama historia hujirudia atafungwa tena,kama ni utemi kwenye Uefa hajafikisha hata nusu ya makombe ya R.Madrid na kama bingwa mtetezi ni R. Madrid.Historia ipi ya Juve itakayombeba?
 
Historia ipi itakayombebe Juve? Kama 1998 alifungwa kama historia hujirudia atafungwa tena,kama ni utemi kwenye Uefa hajafikisha hata nusu ya makombe ya R.Madrid na kama bingwa mtetezi ni R. Madrid.Historia ipi ya Juve itakayombeba?
Kati ya real Madrid na juve nani ambae ni kibonde kwa mwenzie!?
 
Mleta Mada Kuna Kitu Umesahau..
Udhaifu wa Madrid upo kwenye beki ya kushoto Yaani Marcelo..
Ukitaka uwafunge Madrid acha wakushambulie,Marcelo atapanda kisha kabeni vizuri alafu mpeni winger wenu anaecheza upande huo...
 
Madrid atapigwa goli za chap chap alafu wabishi wa turin, watacheza mchezo wao wakihuni naposema mchezo wa kihuni kama hua unafatilia na kuitazama juve basi utakua umenielewa murua.
Juve 2-0 madrid.
 
Madrid atapigwa goli za chap chap alafu wabishi wa turin, watacheza mchezo wao wakihuni naposema mchezo wa kihuni kama hua unafatilia na kuitazama juve basi utakua umenielewa murua.
Juve 2-0 madrid.
Achana na juve,Madrid anaweza piga timu yoyote on earth.Jumamos juve anarandikwa kama alivyotandikwa 1997 na borusia Dotmand na 1998 na R. Madrid na 2003 na ndugu yake Ac Milan
 
Jumamosi itakua siku mbaya sana kwa Zidane na mashabiki wa madrid,Madrid atapigwa goli la mapema sana.

Sioni mtu wa kupenya ukuta wa chuma wa Juventus chini ya beki katili Chielini.

Kule Mbele tunamwacha mtu mrefu Mandzukic,Ramos akileta mieleka yake atakula red mapema sana.

Kibibi Kizee cha turin twende kazi
 
Back
Top Bottom