Kuendelea kumtaja Hayati Magufuli kwa mabaya ni upuuzi wa ajabu

We ni mpumbavu sn vp kama lissu angekuwa ni baba yako ndo kapewa ukilema ungekuja na hz pumba hz? Shaaabashii..
Kusemwa vibaya mwendazake kutaisha pale tu serikali itakapoamua kulivalia njuga suala la waovu wote waliotenda uovu wao eidha kwa kutumwa wakati wa utawala wa Magu au kujipendekeza watakapochukuliwa hatua kinyume chake mzee wa watu ataendelea kupewa makavu na hicho kuumiza mioyo ya ndugu zake kwa muda mrefu sana.
 
Unaposikia Holocaust Kwa uelewa wako huwa unaelewa nini?
 
Kama watu aina ya Makonda bado wapo mtaani wanavimba tu makalio hatutokaa kimya.

Makonda alikuwa ni sawa na Maliyamungu kwenye utawala wa Idd Amin Dada.
 
Wewe usiwapangie watu cha kuandika humu kama wewe humsemi kimpango wako. Kaa pembeni kuleee [emoji117][emoji117][emoji117][emoji117][emoji117][emoji117]
Mbona mnapanic hakuna anayetaka kuwakataza kumsema huyo Magufuli hata mkitaka na mvue nguo na kutembea uchi barabarani kwa kutia msisitizo kuwa Magufuli alikuwa muovu ni uamuzi wenu tu mie sina mamlaka ya kukuzuia, hapa tunajadiliana tu ni ipi faida ya kutumia muda mwingi kuzunguma mabaya ya Magufuli kuliko tunavyozungumzia mabaya yanayoendelea kufanya sasa na waliyo hai, sasa inaonekana wenzetu mnapanic mnaona kama tunataka kuwazuia msimseme Magufuli.

Hii inaonyesha hili suala lipo kihisia zaidi kwa maana mnachokifanya ni kupunguza hisia za hasira mnapokuwa mnamsema huyo Magufuli, na hili liko wazi maana tunaona maneno ya kumwita shetani,Ibilisi, mara mnamlaani, sijui ni kuni za moto,Mungu kaamuwa ugomvi, kafa kwa corona na maneno kibao ambayo yanaonyesha ni jinsi gani mnamchukia huyo Marehemu na si kwamba mnaeleza mapungufu yake kwa nia ya wengine kutoyarudia na ndio maana mnakuwa wakali mtu anapohoji mnachokifanya.
 
Huyu naye ni mmoja wa wale wahamiaji haramu kama alivyokuwa yule mwovu
Sasa maneno kama hayo utasema unamkosoa huyo marehemu kwa nia ya kutaka wengine wasirudie makosa? Hizo ni hasira kwa marehemu.
 
Kama watu aina ya Makonda bado wapo mtaani wanavimba tu makalio hatutokaa kimya.

Makonda alikuwa ni sawa na Maliyamungu kwenye utawala wa Idd Amin Dada.
Nyinyi endeleeni tu kumshambulia huyo marehemu ili kupunguza hasira mlizonazo kwa huyo marehemu ila tusidanganyane hapa kwamba et kwa kumsema Magufuli kwa hivyo mnavyofanya ndio mtashinikiza serikali kwa lolote.

Miaka miwili sasa Makonda yupo hajaguswa na wengine wamechaguliwa kwenye nafasi za uongozi na Samia.

Nyinyi endeleeni kuangaika na marehemu.
 
Mkuu tatizo ni kwamba katika watanzania M60 sio wote wana hasira na Magufuli hata kama Magufuli alifanya mabaya kwenye uongozi wake, msichoelewa ni kwamba mnachokifanya nyinyi hapa ni kupunguza tu hasira zenu kwa huyo marehemu na si kingine.

Mnataka wote tuamini kwamba nchi hii ilikuwa shwari tu ila Magufuli ndio kaja kuharibu, mkiambiwa mambo mengi mnayolaumu kutafanya Magufuli mbona hata huko nyuma yalifanyika, mnasema hayo elezeni nyie hamtaki kuyajadili mnataka mueleze ya Magufuli tu.
 
Hajawahi kutokea Kiongizi mwizi na muuaji kama magufuli
Sawa ila mwisho wa siku mwizi ni mwizi tu, je hao wezi wengine ambao si kama Magufuli mmewafanya nini hadi sasa? Kikwete hakuwahi kuambiwa mwizi? Je mmemfanya nini? Ndio kwanza mnamwita kuwa ni mtu mwema ndio maana hajafa.
 
Inasaidia sana kumtaja Magufuli na maovu yake na hufundisha kwa namna nyingi tu:

1. Kuwa hakuna aliye juu ya sheria
2. Kila dhulma zina mwisho wake
3. Udikteta ni mmbaya
4. Historia ndio hakimu wa wakati wote
5. Wananchi ndio mahakimu wa matendo ya viongozi
6. Haki ya mtu haipotei
7. Uongo una mwisho
8. Tuwe makini kuchagua viongozi wetu
9. Kamwe isijirudie tena! Never, never and never again people of this kind
10. Mungu hadhihakiwi!
 
Tulia we cheti feki, jumapili njoo mwanza uone MV hapa kazi tu. Inavyoshushwa ziwani.
Melikubwa kuwahi kutokea katika ziwa kwenye ukanda huu wa Africa mashariki na kati na ambayo imetengenezwa hapahapa.

Maneno yenu ya kutungatunga hayawezi kumchafua hayati Magufuli.
Fikra nakazizake zitaendelea kuwatesa mbaka mnaingia kaburini.

Nyinyi majitu hovyo sana sijui mapata faida gani kutunga uwongo juu ya Shujaa' Magufuli.
 
Tena ujinga sana kwenye hali kma ya hiii ya mfumoko wa bei mtu marehemu wa mwaka ssa tuna kwenda wa 2 bado JPM NI TOPIC NA UPUUUZ HUUU UNAUPATA KWENYE JUKWAAA LA MAXMELO JF ILA MTAAANI HALI TOFAUTI KABISA HAPO NDIO NAJIULIZA JE JF NI SEHEMU YA WAGANGA NJAAA NA WATEMBEA NA BAHASHA AU NIWAGU WANAOISHI MUHU NI WAJINGA?
 
Na wewe utakuwa na asili ya Uhutu?
Tukio la meli litapongezwa ila ukatili utalaaniwa[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Wamebanwa kwenye kona wamekosa pakutokea... Wamemgeza hayati kuwa punching bag.... Mbona tunashuhudia mengi ya hovyo yakifanuika wakati huu kuzidi hata awamu zilizopita....
 
Sawa ila mwisho wa siku mwizi ni mwizi tu, je hao wezi wengine ambao si kama Magufuli mmewafanya nini hadi sasa? Kikwete hakuwahi kuambiwa mwizi? Je mmemfanya nini? Ndio kwanza mnamwita kuwa ni mtu mwema ndio maana hajafa.
Kikwette hajaiba kitu. Ni uelewa wako finyu wa ussues
 
Unadhani toka muanze kuyasema hayo maovu ya Magufuli hadi sasa ni kwa kiasi gani watu wamejifunza katika hayo uliyoyaorodhesha? Unaweza ukaeleza ni kwa vp watu wamejifunza na si kwamba wanawaona kuwa mnafanya hivyo kupunguza hasira zenu kwa huyo marehemu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…