Kuepuka laana, tuweke tozo angalau ya Tsh. 20 kwa kila chupa ya maji ya kunywa kuwanusuru wenzetu wenye mahitaji maalum

Mkuu, katiba mpya kwenye jamii corrupt haiwezi kusaidia sana. Kwa mfano una jamii inayoamini kuwa wizi ni ujanja, katiba mpya itasaidiaje?

Katiba mpya itasaidia kwa kuwaadhibu wezi bila upendeleo kama ilivyo sasa!! Athabu zitakazotolewa kama ile Katiba ya wananchi ikipitishwa ni kwamba haitajali kama ni matoto wa Kikwete au wa Masanja wakikamatwa na NGADA wote wataadhibiwa kufuatana na sheria.
 
Ripoti ya CAG imeonesha ubadhirifu mkubwa wa hela za umma.

Kabla ya kuweka tozo mpya kwa nini watu wasiangalie mianya ya ubadhirifu iko wapi na inazibwa vipi?
 
Ndio raha ya kuwa kiongozi Tanzania.

Unafuja mapesa ila kwakua watu wananufaika na huo ufujaji hakuna kinachoendelea.

Ndio aina ya maisha ambayo jamii zetu imezikubali.

Na inaheshimu sana watu wenye fedha zenye vyanzo vya aina hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…