Makoye Matale
JF-Expert Member
- May 2, 2011
- 6,491
- 2,104
Wana JF nawasalimu sana katika Jina la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Baada ya salamu hizo leo nimekuja na kamada kadogo kabisa katika hili jukwaa la lugha.
Watu wengi wamekuwa na maswali mengi, mtu anapokufa wasemeje; wengine wamekuwa wakisema 'amefariki', wengine wanasema 'amefariki dunia', kwa kuangalia makundi haya baadhi ya watu wameshindwa kufahamu hasa ni kundi lipi liko sahihi.
Nimefuatilia na kugundua kuwa: Neno 'kufariki' chanzo chake siyo 'kufa' bali ni 'faraka' yaani kuachana na ...; mfano marafiki wawili waliopendana wakaamua kuvunja urafiki basi huitwa 'wamefarakana' yaani wameachana! Hivyo basi mtu anapoishi duniani anakuwa ameambatana na dunia, pale mtu huyo anapoachana na dunia basi anakuwa 'amefarakana' na hiyo dunia au ametengana na hiyo dunia hivyo ni sahihi kusema 'amefariki dunia' na siyo kuishia tu kwamba 'amefariki' ambapo huacha swali kwamba 'kafariki nini'?
Kwa upande mwingine neno 'kufariki' linaweza kutumiwa kwa mtazamo huu: Mtu ambaye ameishi Dar es Salaam na sasa ameuhama Dar es Salaam anaenda mji mwingine; atakapokuwa ameuhama Dar es Salaam haitakuwa makosa kusema mtu huyo 'amefariki Dar es Salaam'.
Watu wengi wamekuwa na maswali mengi, mtu anapokufa wasemeje; wengine wamekuwa wakisema 'amefariki', wengine wanasema 'amefariki dunia', kwa kuangalia makundi haya baadhi ya watu wameshindwa kufahamu hasa ni kundi lipi liko sahihi.
Nimefuatilia na kugundua kuwa: Neno 'kufariki' chanzo chake siyo 'kufa' bali ni 'faraka' yaani kuachana na ...; mfano marafiki wawili waliopendana wakaamua kuvunja urafiki basi huitwa 'wamefarakana' yaani wameachana! Hivyo basi mtu anapoishi duniani anakuwa ameambatana na dunia, pale mtu huyo anapoachana na dunia basi anakuwa 'amefarakana' na hiyo dunia au ametengana na hiyo dunia hivyo ni sahihi kusema 'amefariki dunia' na siyo kuishia tu kwamba 'amefariki' ambapo huacha swali kwamba 'kafariki nini'?
Kwa upande mwingine neno 'kufariki' linaweza kutumiwa kwa mtazamo huu: Mtu ambaye ameishi Dar es Salaam na sasa ameuhama Dar es Salaam anaenda mji mwingine; atakapokuwa ameuhama Dar es Salaam haitakuwa makosa kusema mtu huyo 'amefariki Dar es Salaam'.