Kufunga ndoa kwangu kumeniondolea marafiki wengi

Kufunga ndoa kwangu kumeniondolea marafiki wengi

Pole sana mkuu,
Hii michango inaleta uhasama sana kimsingi tu naona bora nisichangishe maana kuidai hio michango ni shughuli kweli kweli
Tatizo linakuja tukianzia hapo kwenye mentality ya kudai michango.

Tumefanya michango kama aina fulani ya social insurance.

Unamchangia mtu ukitegemea na yeye atakuchangia, kitu ambacho si lazima.

Mchango unatakiwa uwe kama zawadi, unachangia ukijua huyu anaweza kunichangia au anaweza asinichangie, after all, hatujui kesho yake itakuwaje. Hatujui hata kama atakuwa hai.

Unqtakiwa ujue kuwa mimi nahitaji kuwa na uwezo wa kufanikisha shughuli yangu either way.

Sasa, tatizo letu tumefanya michango kuwa ni uwekezaji, ukiwekeza unahitaji kurudishiwa, na usiporudishiwa inakuwa ugomvi.

Hapo ndipo naona imefika wakati tuachane na michango ya harusi. Kama mtu anataka kutoa zawadi, atie zawadi tu.

Michango inaleta pressure sana.

Imagine umeomba watu michango wakatoa watu wengi sana hela nyingi sana.

Hilo linamanisha nini?

Kwamba na wewe itakubidi utoe hela nyingi sana kuchangia harusi za watu wengi sana?

Kama huna?

Hatuoni hapo tunatengeneza tatizo?
 
Tatizo linakuja tukianzia hapo kwenye mentality ya kudai michango.

Tumefanya michango kama aina fulani ya social insurance.

Unamchangia mtu ukitegemea na yeye atakuchangia, kitu ambacho si lazima.

Mchango unatakiwa uwe kama zawadi, unachangia ukijua huyu anaweza kunichangia au anaweza asinichangie, after all, hatujui kesho yake itakuwaje. Hatujui hata kama atakuwa hai.

Unqtakiwa ujue kuwa mimi nahitaji kuwa na uwezo wa kufanikisha shughuli yangu either way.

Sasa, tatizo letu tumefanya michango kuwa ni uwekezaji, ukiwekeza unahitaji kurudishiwa, na usiporudishiwa inakuwa ugomvi.

Hapo ndipo naona imefika wakati tuachane na michango ya harusi. Kama mtu anataka kutoa zawadi, atie zawadi tu.

Michango inaleta pressure sana.

Imagine umeomba watu michango wakatoa watu wengi sana hela nyingi sana.

Hilo linamanisha nini?

Kwamba na wewe itakubidi utoe hela nyingi sana kuchangia harusi za watu wengi sana?

Kama huna?

Hatuoni hapo tunatengeneza tatizo?
Ndio balaa na sahizi usipochanga watu wanakuhesabia gap tu! Ikifika muda unahitaji huoni mtu kuchanga unaona bora ukaushe tu.
 
Vijana wa sasa, nimegundua kujikweza na kutaka kufanya harusi kubwa kuliko uwezo wao ndio kinacho wagharimu.

Lets say “Ukioa kimya kimya kuna ubaya gani” ukitoka zako kufunga ndoa kanisani alika ndugu wa karibu wa pande zote mbili na marafiki wachache nendeni sehemu tulivu kwa gharama zako binafsi wapige chakula na vinywaji hadi watambae na uhakika ulitenga milioni tano zinatosha kabisa kuwachachafya, baada ya hapo beba mke wako nendeni mkajenge familia.

Mambo ya kutaka kuwekwa instagram page za ma MC maarafu ndio zinawaponza, mbona miaka yetu tulioa huko vijijini ni wali na nyama ya ng’ombe na mziki mambo yanaisha na leo tupo imara katika ndoa tofouti na hawa wanaofunga ndoa kwa gharama kubwa kisha wanaishia kuacha ndani ya miaka michache.
Nakubaliana nawe sana.

Watu wanatengeneza tatizo wenyewe, halafu wanalalamika.
 
Nakubaliana nawe sana.

Watu wanatengeneza tatizo wenyewe, halafu wanalalamika.
Vijana wengi baada ya harusi huwa wana stress sana kitu ambacho nilikuja kugundua wengi wao huwa na madeni si chini ya milioni kumi (10) maana huwa wanakopa kunogesha harusi.

Sasa huwa najiuliza zile basic course za uchumi wanazojifunza chuo huwa zinawasaidia nini, maana hiyo milioni kumi angeitumia kufungua mradi mdogo si ungemsaidia kwa kiasi fulani kusukuma maisha kuliko kuichoma yote kufurahisha walimwengu.
 
Vijana wengi baada ya harusi huwa wana stress sana kitu ambacho nilikuja kugundua wengi wao huwa na madeni si chini ya milioni kumi (10) maana huwa wanakopa kunogesha harusi.

Sasa huwa najiuliza zile basic course za uchumi wanazojifunza chuo huwa zinawasaidia nini, maana hiyo milioni kumi angeitumia kufungua mradi mdogo si ungemsaidia kwa kiasi fulani kusukuma maisha kuliko kuichoma yote kufurahisha walimwengu.
Kuna mashindano ya kijinga sana, kuna kujionesha na ufahari wa kipuuzi sana.

Wakati ukumbi wa Mlimani City unafunguliwa, kuna jamaa alikuwa anataka kuwa mtu wa kwanza kanisani kwao kufanya harusi hapo.

Wakati uwezo hana.

Akakopa sehemu milioni tano za kufanikisha shughuli.

Mpaka leo hajarudisha na hana haya kasahau kuwa alikopa anaenda kuomba kukopa zaidi. Kisa kakopa mtu wa familia anaona poa tu.

Wakati gharama za harusi yake kama angefanyia biashara angeweza kuwa mbali saa hizi.

Na hata kama asingefanya biashara, angeweza kuepuka harusi ya gharama na kukopa hela ambazo hakurudisha.

Watu wanakopa hela nyingi, kwa shughuli ya ufahari wa siku moja tu, kisha wanaurudia umasikini wao.
 
Mnapotaka kuoa msitegemee michango ya ndugu/rafiki ifanikishe sherehe zenu jipangeni, msilaumu watu kila mtu ana mipango yake ya maisha.
 
hii ni tamaduni yetu tuliikuta na tunaiendeleza ingawa watu hapa wanajifanya kuikandia but still wanachanga kwa wengine kama walivyochangiwa wao kwenye zao,kitendo cha kutokuchangiwa kisikukatishe tamaa ndotulivyo tunapenda kupokea kuliko kutoa ilimradi ushawafahamu we deal na wanaodeal na mambo yako wengine piga chini
 
Nilikua na washkaji wengi kabla ya kufunga ndoa na ndugu wengi nilikua nawachangia sana kwenye misiba na harusi lakini Mimi nilivotangaza ndoa wakaniunga mkono muda ulipofika nikipiga cm wana hawapokei wala kujibu text

Nikakausha nikakomaa likapita saivi wengine wanaishia kuview status WhatsApp tu na wengine tukionana wanajikanyaga tu

Nimeamua saivi nitachangia misiba tu Teena ila ya moja kwa moja cjui kipaimara harusi cjui nini mwisho na Nina list ya walionichangia ndo nataka tu kuwarudishia michango yao baasi

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Hii ndio shida ya kufanya jambo ukategemea michango ya watu,watu ukiwategemea watakudisapoint vibaya vibaya.

Andaa bajeti yako kwamba weka akilini jambo fulani utalifanya mwenyewe mwanzo mwisho andaa bajeti itakuwa bei gani weka kila kitu pahala pake,kama muda mdogo sogeza mbele siku ili upate uhuru wa kufanya jambo lako mwenyewe,wakitokea wa kukupush basi unaweka pembeni hiyo pesa unafanyia mambo mengine hakuna ulichopoteza.

Ukishamaliza kufanya mwenyewe kila kitu umegharamia mwenyewe hujamsumbua mtu then usiweke kinyomgo na ambao hawajakuchangia,wana shuda wasaidie huna waambie hauna,huu ndio ubinadamu hatuwezi kuishi kwa visasi utaona kila mtu mbaya.

Wema ni ule ambao unaufanya pasi na nia ya kumlipa mtu alichokufanyia.
Na deni ni kumfanyia mtu mfano wa alichokufanyia wewe

Wengi wetu hatufanyi wema wa kuchangia harusi bali tunalipa madeni kwa sababu walituchangia na wao tunawachangia,haya sio maisha.
 
Hii ndio shida ya kufanya jambo ukategemea michango ya watu,watu ukiwategemea watakudisapoint vibaya vibaya.

Andaa bajeti yako kwamba weka akilini jambo fulani utalifanya mwenyewe mwanzo mwisho andaa bajeti itakuwa bei gani weka kila kitu pahala pake,kama muda mdogo sogeza mbele siku ili upate uhuru wa kufanya jambo lako mwenyewe,wakitokea wa kukupush basi unaweka pembeni hiyo pesa unafanyia mambo mengine hakuna ulichopoteza.

Ukishamaliza kufanya mwenyewe kila kitu umegharamia mwenyewe hujamsumbua mtu then usiweke kinyomgo na ambao hawajakuchangia,wana shuda wasaidie huna waambie hauna,huu ndio ubinadamu hatuwezi kuishi kwa visasi utaona kila mtu mbaya.

Wema ni ule ambao unaufanya pasi na nia ya kumlipa mtu alichokufanyia.
Na deni ni kumfanyia mtu mfano wa alichokufanyia wewe

Wengi wetu hatufanyi wema wa kuchangia harusi bali tunalipa madeni kwa sababu walituchangia na wao tunawachangia,haya sio maisha.
Nakubaliana na ww mkuu [emoji109][emoji115]
 
hii ni tamaduni yetu tuliikuta na tunaiendeleza ingawa watu hapa wanajifanya kuikandia but still wanachanga kwa wengine kama walivyochangiwa wao kwenye zao,kitendo cha kutokuchangiwa kisikukatishe tamaa ndotulivyo tunapenda kupokea kuliko kutoa ilimradi ushawafahamu we deal na wanaodeal na mambo yako wengine piga chini
Kwa hivyo ukikuta jamii ina utamaduni wa kula baadhi ya watoto wanaozaliwa, utakubali utamaduni huo na kusema huu ni utamaduni wetu tumeukuta na tunauendeleza?

Jambo linakubaliwa au kukataliwa kwa sababu ya uzuri /ubaya wake? Au kwa sababu ni utamaduni tu umezoeleka?
 
Kwa hivyo ukikuta jamii ina utamaduni wa kula baadhi ya watoto wanaozaliwa, utakubali utamaduni huo na kusema huu ni utamaduni wetu tumeukuta na tunauendeleza?
mangapi unayafanya na yanaimpact neg kwenye jamii mkuu?haya mnayoyakataa leo in reality ndotunayoyaishi hata wewe ulitokea kwenye hii michango,tunaishi kwa kutegemeana hakuna aliyekamilika kwenye kila kiyu ndomana tuna michango mbalimbali
 
mangapi unayafanya na yanaimpact neg kwenye jamii mkuu?haya mnayoyakataa leo in reality ndotunayoyaishi hata wewe ulitokea kwenye hii michango,tunaishi kwa kutegemeana hakuna aliyekamilika kwenye kila kiyu ndomana tuna michango mbalimbali
Hujajibu swali nililokuuliza na ulilojibu sijakuuliza.

Ukikuta kwenu kuna utamaduni wa kula mavi na wewe utakubali kula mavi kwa sababu ni utamaduni wa kwenu unauendeleza?

Hatuwezi kujiongeza na kukataa tamaduni fulani zilizopitwa na wakati?
 
Ndoa ni tatizo binafsi la mtu ingependeza kila alibe be kivyake vyake hasa ukizingatia ni tatizo la kutengeneza halijaja automatically.

Mambo ya kuchangishana ni kutiana umasikini
 
Hujajibu swali nililokuuliza na ulilojibu sijakuuliza.

Ukikuta kwenu kuna utamaduni wa kula mavi na wewe utakubali kula mavi kwa sababu ni utamaduni wa kwenu unauendeleza?

Hatuwezi kujiongeza na kukataa tamaduni fulani zilizopitwa na wakati?
hilo jibu liko wazi mkuu kama wanakula mavi ma me ntakula afu tafuta mifano iliyo hai kuliko kufananisha vitu vibaya just to justify your point
 
Usipaniki jamaa..ndio maisha ya watanzania wamejaa unafiki..siku ukiwaambia unataka kuoa watakupa saport..siku ukiomba mchango wote huwaoni.
Ukipata changia wala usiwe na kinyongo.
Zen kingine mimi naona ni muhimu kujipanga tu mapema kama una jambo lako usitegemee wanadamu watakuangusha.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Sure kabisa
 
hilo jibu liko wazi mkuu kama wanakula mavi ma me ntakula afu tafuta mifano iliyo hai kuliko kufananisha vitu vibaya just to justify your point
Umesema suala la kuendeleza utamaduni bila kujadili uzuri au ubaya wa utamaduni.

Kama unaweza kula mavi kwa sababu ni utamaduni wenu tu, sina cha kujadiliana nawe zaidi.

Nikijadiliana nawe zaidi unaweza kuniambukiza kipindupindu cha akili buree.
 
Habari za kuchangishana kwenye harusi na misiba ni habari za ujima.

Tutengeneze uchumi utakaowezesha watu kugharamia harusi na mazishi yao wenyewe.Ikibidi hata kwa bima maalum za maisha na mifuko maalum ya kuweka akiba za harusi.

Kama mtu anaamua kutoa iwe zawadi kwenye harusi au kusaidia familia vitu vikubwa kwenye misiba.

Naelewa hali ilivyo, na kwamba haya mambo labda yanahitajika kwa sasa, na kwamba yameonekana kama sehemu ya utamaduni, lakini, kimsingi, ni maishabfulani ya kijima yanayojiondoa katika kujitegemea.

Pia, kwenye harusi watubwengi wanaendekeza harusi kubwa zenye gharama sana wakati hawananuwezo wa kiuchumi kuzi support harusi hizo na kuishi maisha yaliyo sawa na harusi hizo. Na gharama hii inabebwa na michango.

Michqngo ya harusi inakuwa mingi kuliko michango ya shughuli za maendeleo.

Utasikia sana watu wanachangishana harusi, lakini husikii watu wakichangishana hivyo kwenye biashara au kusoma.

Hii ni dalili ya jamii inayoendekeza kubembea badala ya kufanya kazi.

Tufikie wakati iwe nibjambo la aibu mtu kuhitaji kuchangiwa ili kufanikisha harusi yake.

Ikibidi vijana, kama wanatakanharusi za kifahari, waanze kuweka akiba tangu wadogo.

Mbona nyumba watu wanajenga bila kuchangiwa na jamii?

Sasa hivi tunatengeneza mpaka uhasama kwa sababu ya michango ya harusi, urafiki unakwisha kwa sababu ya michango ya harusi.

Mbona zamani watu walifanya harusi simole sana na ndoa zilidumu vizuri tu?

Kwani ni lazima kufanya harusi zenye gharama kubwa sana?

Ni jambo la kuhuzunisha sana.
Hii comment yako naenda kuiwekea lamination kabisa
 
Back
Top Bottom