Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

N i beki gani yule wa timu gani aliyetaka kusababisha goli kipindi cha kwanza? 1- kwanza alitoa pasi fyongo kwa kipa 2- aliokoa fyongo pia ni mwamba ulisaidia
 
Nawapongeza maana wameonyesha ukomo wa uwezo wao.

wanazidi kutupa tafakari ili tuone kama tunaweza kusonga mbele kwenye soka au tuwekeze mabilioni kwenye drafti, au netboli au mbio.

hongereni kwa kutolewa, binafsi nimetambua juhudi zenu, tuelekeze nguvu WC Qatar.
 
tutatupia viwili kipindi cha kwanza kuanzia dk 10 na 30... baada ya hapo ni kuziia mwanzo mwenga... kipindi cha pili tutamalizia goli letu la mwisho na kufunga idadi ya magoli matatu bila.... ili tukija tupokelewe ikulu
daaah
 
Teh, CCM ndiyo wanapanga kikosi?
CCM ndiyo wanachagua wachezaji?
CCM ndiyo kocha wa timu?
Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya timu na chama tawala. Haiwezekani leo kisha uone wanakaribia kushinda unatoka mil 50 eti ziwasaidie. Wakati tunamatatizo lukuki ya kutatua
 
Imefika wakati sasa sisi wazanzibar mtuamini sasa tukaipige hio ngome.

Ukabila na utaifa ukae pembeni.
 
Viongozi wa TFF tuondoleeni hiyo takataka... hana nia njema na Timu yetu

Ni dhahiri kabisa huyu kocha hatutakii mema sisi watanzania, ambao ni mashabiki wa timu yetu ya Taifa..
Mechi na cape verde alipanga kikosi kibovu tukafungwa.. karudi nyumbani karekebisha kikosi tukashinda..
Leo amekuja kurudia yaleyale.. baada ya kupanga kikosi cha ushindi yeye anapanga kikosi cha majaribio

Huyu kocha hatufai atimuliwe arudi kwao kuuza nyanya
 
Unabwabwaja sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…