Kugonga mwamba kwa Mazungumzo kati ya Viongozi wa ACT-Wazalendo na CHADEMA kuhusu kuungana kwenye Uchaguzi Mkuu na picha halisi ya Uchaguzi Mkuu ujao

Kugonga mwamba kwa Mazungumzo kati ya Viongozi wa ACT-Wazalendo na CHADEMA kuhusu kuungana kwenye Uchaguzi Mkuu na picha halisi ya Uchaguzi Mkuu ujao

Mati Mkenda

Senior Member
Joined
Mar 4, 2018
Posts
171
Reaction score
211
Kwa muda mrefu chama cha ACT-Wazalendo kimekuwa kikiwashawishi Viongozi wa CHADEMA ili wakubaliane na wazo lao la kushirikiana au kuungana katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu. Ikumbukwe kuwa ACT-Wazalendo ndio wameonekana kuwahitaji zaidi Chadema, kuliko wao kuhitajiwa na CHADEMA.

Taarifa za kuaminika kutoka kwa mmoja wa wajumbe waliohusika kwenye mazungumzo hayo ni kuwa CHADEMA wamekataa katakata baada ya kugundua mchezo mchafu ambao ACT-Wazalendo wametaka kuucheza ili kujijenga kisiasa. CHADEMA bado wanahangaika kuuguza majeraha waliyoyapata baada ya kubadili gia angani mwaka 2015 kwa kumsajili, kumsafisha na hatimaye kumpa nafasi kubwa mtu waliyemchafua kwa muda mrefu, ambaye mwisho aliwakimbia. Lakini pia CHADEMA bado wanahangaika kujenga imani kwa wafuasi wao ambao wameonekana kufurahishwa na namna serikali ilivyotekeleza yale yote ambayo wao walikuwa wakiyalilia kwa muda mrefu, licha ya viongozi wao kubeza juhudi hizo za serikali.

Kutokana na hilo CHADEMA wamesema kila mtu afe kivyake na mchakato wa kupitisha wagombea ndani ya vyama hivyo umeanza. ACT-Wazalendo wanahaha kwa sababu wanajua kuwa mtu wanayetaka kumsimamisha kama mgombea kwa nafasi ya Urais hana mvuto mkubwa kisiasa, kwani mwaka 2015 wananchi wengi sana walimkataa kwa nguvu zote. Mtu huyo hafahamiki kabisa nje ya ukanda wa Kusini anakotokea, na ndio maana muda mwingi wamekuwa wakijinadi huko.

Wakati UKAWA ukiwa umesambaratika, vyama vingi vilivyokuwa ndani ya umoja huo vimeamua kumuunga mkono Mgombea Urais aliyepitishwa na CCM katika nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mh. John Pombe Magufuli.
 
Membe si anajisifia waziwazi kuwa ni jasusi mbobezi. Atumie girisi inayoitwa mabillioni aone kama TL hatawaongoza cdm kumlamba miguu.
 
Kila mtu ashinde mechi zake.akuna kuungana mwaka huu.
 
Kwa muda mrefu chama cha ACT-Wazalendo kimekuwa kikiwashawishi Viongozi wa Chadema ili wakubaliane na wazo lao la kushirikiana au kuungana katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu. Ikumbukwe kuwa ACT-Wazalendo ndio wameonekana kuwahitaji zaidi Chadema, kuliko wao kuhitajiwa na Chadema.

116757236_301032438003801_613182120956803509_n.jpg
 
ACT wananin cha kuunganisha na CDM nikisikia hiyo habari huwa nahisi kichefuchefu.Membe tayari kaishamezwa.Nasidhani kama ACT bila mbereko wanaouwezo wa kupata kata 5, nikupoteza muda kuungananao bora Dovutwa
 
Kila mtu ashinde mechi zake.akuna kuungana mwaka huu.
Acha hizo mambo washirikiane ila Lissu ndio awe mgombea, kura za kusini, pwani, Pemba,Kigoma tunazihitaji bado. Kuna watu wanapiga kura kwa mrengo tofauti kabisa na mafikirio yetu, kama Mama Mgwhira alipata kura , usifikir Membe atashindwa kupata hata kura laki 5/6, awamu hii tunahitaji kila kura. Jambo lamsingi waangalie namna bora yakutopoteza hata kura 1.
 
......... Chadema bado wanahangaika kuuguza majeraha waliyoyapata baada ya kubadili gia angani mwaka 2015 kwa kumsajili, kumsafisha na hatimaye kumpa nafasi kubwa mtu waliyemchafua kwa muda mrefu, ambaye mwisho aliwakimbia.

Wakati UKAWA ukiwa umesambaratika, vyama vingi vilivyokuwa ndani ya umoja huo vimeamua kumuunga mkono Mgombea Urais aliyepitishwa na CCM katika nafasi ya Urais wa JMT ambaye ni Mh. John Pombe Magufuli.

Uandishi wa kwenye laptop na tablets za Lumumba
 
I shall say again kutokuwa na dhamira ya kuweka mgombea mmoja kwa upinzani bara ni upuuzi mkubwa wenye ubinafsi ndani yake WE BETTER ALL OF US VOTE TO CCM ikiwa na maana ya kuwa HAKUNA MALENGO YA KWELI NDANI YA UPINZANI
 
ACT wananin cha kuunganisha na CDM nikisikia hiyo habari huwa nahisi kichefuchefu.Membe tayari kaishamezwa.Nasidhani kama ACT bila mbereko wanaouwezo wa kupata kata 5, nikupoteza muda kuungananao bora Dovutwa
Kata tano wakati 2015 walichukua halmsahauri nzima, na Dodoma,na Mbeya walipata diwani mmoja mmoja nafikiri na urambo pia hebu tulizen mihemko tunahitaji kura zote, waangalie namna bora yakushirikiana ila tu kwa sharti Lisu awe mgombea.
 
Kata tano wakati 2015 walichukua halmsahauri nzima, na Dodoma,na Mbeya walipata diwani mmoja mmoja nafikiri na urambo pia hebu tulizen mihemko tunahitaji kura zote, waangalie namna bora yakushirikiana ila tu kwa sharti Lisu awe mgombea.
Tunazungumzia 2020 usidhani ccm au cdm atabaki na viti vilevile lazima kuwepo kupanda na kushuka
 
Tunazungumzia 2020 usidhani ccm au cdm atabaki na viti vilevile lazima kuwepo kupanda na kushuka
Kwahio unamaana Membe akigombea hatapata kura hata laki 3?. Unaonaje hizo kura zingeenda kwa mgombea mmoja wa upinzani?.
 
Acha hizo mambo washirikiane ila Lissu ndio awe mgombea, kura za kusini, pwani, Pemba,Kigoma tunazihitaji bado. Kuna watu wanapiga kura kwa mrengo tofauti kabisa na mafikirio yetu, kama Mama Mgwhira alipata kura , usifikir Membe atashindwa kupata hata kura laki 5/6, awamu hii tunahitaji kila kura. Jambo lamsingi waangalie namna bora yakutopoteza hata kura 1.
Na ACT pia wanasema hivyo,muungane lakini mgombea awe BM.
Ngoja tuone vita vya panzi.
 
Acha hizo mambo washirikiane ila Lissu ndio awe mgombea, kura za kusini, pwani, Pemba,Kigoma tunazihitaji bado. Kuna watu wanapiga kura kwa mrengo tofauti kabisa na mafikirio yetu, kama Mama Mgwhira alipata kura , usifikir Membe atashindwa kupata hata kura laki 5/6, awamu hii tunahitaji kila kura. Jambo lamsingi waangalie namna bora yakutopoteza hata kura 1.
LMnaitaja sana kusini lkn pia mkumbuke kusini yupo kassim majaliwa, nadhan Membe ata kusini nguvu yake si ya kutisha
 
Act hiyo alikufa tu baada ya kuzaliwa
Chadema kinapumulia machine, na uchaguzi wa October kikipata viti vitano vya ubunge mnisute!
Mambo yamebadilika, mahitaji ya wananchi uchaguzi uliopita siyo Kama ya uchaguzi huu
 
Acheni kuokoteza. Kuna mambo mengi ya kiufundi kwa pande zote.

Lazima kwenye mazungumzo kuwe na win - lose situation.

Uzito wa kila upande na analysis inahitajika.

Kila upande unamuhitaji mwenzake kwa namna tofauti. Tuombe wafikie point of Resolution.


Hili la Membe na lissu litapimwa kwa hoja kwa kila upande.

Binafsi napendekeza wapige mchezo wa kombolela ili waje washtukize lala salama. Naishia hapo.
 
Back
Top Bottom