Kuhatarisha usalama wa Taifa? Give me a Break!



hahahaha......akiingia huko lazima nimpotezee....mambo ya kuhamishiana majukumu watoto wa kiume siyafagilii kabisa yani....ila nadhani dogo yupo kizalendo zaidi
 

Asante sana Derimto.....umejibu maswali mengi......sasa maswali mengine...

1. mtu akitaka kufanya kazi na hawa jamaa anaaply wapi?
2. hivi hizi nembo zao zipo online?....kuna mtu yeyote mwenye hiyo nembo atupostie hapa?.......kwa mfano ukienda wikipedia nembo ya CIA ipo pale kwenye page yao.
3. watu wengi wamejibu kuwa kufanya kazi na hawa watu hailipi kifedha.....wanasahau kuwa wengine ni wazalendo tu, na pia kufanya kazi nao unaweza kuwa Under Cover...ukawa unafanya kazi Voda na unalipwa mshahara kama wafanyakazi wengine
 

sasa ulivyoandika hivyo "Senior" wako kama yupo JF na akaisoma hii si atajua we ni nani?......au?
 
Umetoa hoja nzuri sana. I was curious pia kujua hili dubwasha likoje maana naona kama vile hawapo ilihali tunaangamizwa kiuchumi na watu waliotuibia kura.....

...I am impressed mkuu....

Very patriotic shekhe. Ninasoma mpaka nasisimka kiujasiri kutaka kuonesha umwamba kwenye kulinda maslahi ya nchi.

Hoja yako hii naiita ya karne maana imejibu maswali yangu mengi sana.
Najua wapo watakaobeza (kwa sababu zao) ila majibu ya DERIMTO yamefungua ukurasa mpya kuhusu kuifahamu hii taasisi moyo wa taifa. ingawa kiuhalisia wanabaniwa sana kufanya shughuli zao lakini kwa sehemu wanaoesha wanajali huku wakipuuzwa na viongozi wetu....
 
kazi yao ni kuhakikisha taifa lipo salama! hahaha!
 
Wakati nasoma hii itaarifa kwanza ilikuwa inanivutia sana kulingana na wachangiaji wake kuelezea kwa hisia kali, binafsi nilikuwa sifahamu kitu chochot kama ilivyoelezwa hapa, lakini nilikuwa nawajua na bado nawajua baadhi ya watu ambao wanafanya kazi huko.

Jambo la pili ambalo pia limenisisimua ni jinsi pia kunavyotokea baadhi ya vifo vya watu ambao wanaonekana kwenda tofauti na serikali, hapa pameniumiza sana mfano Prof Mwaikusa, hapa umenikuna sana mtoa mada, nimejisikia kutoipenda hii kazi kwa mana hata ipo siku utaambiwa nenda kaamue fulani.

Jambo jingine ni kwamba wakati nasoma habari hii ni kama vile nilikuwa naangalia filamu fulani hivi, mana nilivuta taswira iliyonipeleka kuona baadhi ya matukio ambayo wachangiaji wameweka hapa. Sitofautishi sana habari hii na zile simulizi za Willy Gamba kama wadau mtakuwa mnamkumbuka. Binafsi nimefurahi lakini pia nimeingiwa na woga juu ya haya yaliyoelezwa.
 
Nilitalikua natoa baadhi ya mambo machache baada ya chifunanga kutaka ufafanuzi ambao utamwezesha mtu kuomba kazi huko lakini inavyoonekana bado watu wengi hawajaridhika labda nijaribu kujibu na kufafanua baadhi ya mambo kidogo sana ili tuelewane angalau kwa sehemu fulani.

Hii kazi mara nyingi kwa hapa kwetu siwahi kuona watu matangazo na watu wakaomba kazi kama kazi zingine zilivyo mara nyingi wao ndiyo mara nyingi hufuata mtu ambaye wataona ana tabia na uwezo wanaoutaka wao kwa mahali husika yaani wanapotaka kwenda kumtumia na hapo wataendelea kuangalia uwezo wako unaweza kubadilika na mazingira husika kwa haraka kiasi gani na kukutumia kwa kazi kubwa zaidi ya mwanzo.

Kwa hapa kwetu Tanzania miaka ya nyuma kulikuwa na JKT. Na ulikuwa mfumo mzuri sana wa watu kuonyesha vipaji vyao mbalimbali na kama ilivyo kawaida UC. Wengi wamejaa kila mahali na hasa kwenye sehemu muhimu na hapo waliangalia uwezo wa mtu bila kujali ni mtoto wa nani na kwao wana uwezo mkubwa wa kifedha namna gani na hatimaye mtu unapewa taarifa tena bila kumjua mtu aliyekupendekeza wewe kuingia kwenye kazi hiyo na mfumo mara nyingi unatumiwa zaidi na nchi kama Israel kumuandaa ofisa yeyote kuingia idara yao ya ujasusi (Mossad) ambapo hata makao makuu ya Mossad hayajulikani na watu wengi tofauti na nchi nyingi za magharibi.

Kwa sasa kama unataka kujiunga ni vizuri kuwa karibu na hao wanausalama wa ukweli wanaofahamika kila kona za mtaa na kumpelekea habari za umbea hasa zinazowahusu viongozi na vigogo vya serikali na hasa zinazopendelea serikali iliyoko madarakani hata kama inafanya vibaya utawekwa kwenye list yao maana HONGO KUBWA YA KAZI KWENYE HII IDARA NI TAARIFA HATA KAMA NI ZA UMBEA WA JIRANI YAKO TU maana hakuna kazi nyingi za kuweka busy zaidi ya usalama wa viongozi hao watano na ndiyo maana wakipelekwa mikoa ambayo hao viongozi hawafiki mara kwa mara wanaishia kulalamika tu kuwa wanafanya kazi za ccm

Kuna watu wanataka kujua nembo za TISS Na kama wanaweza kupata kwenye web. Naomba ikumbukwe kwamba hapa kwetu pamoja na kwamba idara hii inasakamwa sana bado kuna wazee na watu bora kabisa tena wanajua nini maana ya idara ya ujasusi tofauti na sasa ambapo wamejaa huko watoto wa vigogo wengi ambao kama alivyosema mchangiaji mmoja kuwa wanatumia vyeo vibaya na kutongozea mademu na kutishia watu ili waogopwe na watu pamoja na baadhi ya maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama.

UC. Wengi wanatakiwa kuwa na bidii na akili binafsi za kuzaliwa za kuweza kubuni mambo kwa ufanisi zaidi ya akili za kawaida ili kulinda cover yake isijulikane kwa namna yoyote ile na kuandika report na ikumbukwe kuwa yeye anapoandika report siyo kazi yake kuifuatilia kama imefanyiwa kazi au laa na unaweza kuona wakatumwa hata watu wengine wanne zaidi kwa nyakati tofauti ili kujiridhisha na taarifa uliyopeleka ina ukweli kiasi gani ingawa siku hizi hii imepungua na majungu ni makubwa inaangaliwa report yako imependelea upande gani yaani anaangalia wewe unawazaje kwa kutumia (W) ya mwisho yaani Why? Na hapo ndipo unajikuta unasota bench muda mrefu na wenzako wakienda mbali na kufaidi kodi za nchi hii.

Napenda Pia kumjibu mwana jamii mwenzangu Pelosi kuwa hapa ni jamvini tunachangia na kama wewe ni mwanausalama ninakukera nisamehe (come and get me kwenye JF)ingawa najua kwako hii ni taarifa itakayokunyanyua sana kama hauna kazi ya kufanya na mahali pa kupata taarifa muhimu za ulinzi na usalama wa nchi yako zinazolimaliza Taifa hili changa kwa kuficha ukweli halisi na kureport umbea kama huu unaopata huku ndani nenda kaziprint peleka report kwa wakubwa wako utasifiwa na kujihakikishia kazi milele MAANA SERIKALI HII HAITAONDOKA MADARAKANI na huu ni baadhi ya ukweli kidogo tu ninao ufahamu kuhusu idara hii kwa nje tu maana Idara hii ni kubwa na imeagwanyika sehemu mbalimbali kulingana na kazi husika.

H/W Yako ni hii nenda kamuulize Mabere Marando wa Chadema kwa nini siku ile bungeni alipokua anaomba uspika hakuzitaja sifa na uzoefu wake kiundani kama alivyofanya Anna Makinda na je alikorofishana nini na hayati Mwl.Nyerere?

Pia nilipenda kumjibu mwana jamii ambaye aliuliza swali na kutaka kujiridhisha maana yeye ni mlipa kodi ni haki yake kujua japo kwa nje tu hii idara maana kuna watu wengi wamenyanyasika kijinsia na kudhulumiwa na watu wanaotumia vibaya jina la hii Idara kwa manufaa yao binafsi na kutaka waogopwe tu na jambo hili limeshawawi kunikuta mwenyewe nilitishiwa na mtu ambaye anamfahamu mtu wa Idara hii nikawa mpole na baada ya kujipanga vyema nikamtokea kihalisi kifupi ilikuwa na mvuto na yule bwana alikimbia jiji sijawahi kumwona mpaka leo hivyo basi kuna mamluki wengi sana mtaani wanajidai ni wana usalama kama wewe na kila mtu anamjua kitu ambacho siyo sawasawa hasa UC. Mimi mwenyewe hakuna mtu kwetu anayenijua kiundani kuanzia Baba, Mama, na ndugu mpaka hata majirani isipokua mke wangu tu ndiye aliyenishitukia na hana uhakika wa kutosha.

Am just talking coz. am tired and pecdoff. with this corrapt.Gov. Na ninamatumaini iko siku itakwishwa na watumishi wa umma waadilifu watalitumikia Taifa hili kwa haki na ukweli bila kuogopa aina ya watu fulani wenye uwezo wa kifedha au madaraka zaidi ya kuangalia masilahi ya mwananchi wa kawaida na mali zao.

Kwa kumalizia ni kuwa kazi hii kama ikifuatwa misingi yake kama ilivyowekwa ni ya heshima lakini haimfanyi muhusika kupata upendeleo wa aina yoyote na mara nyingi kama ni mfuata maadili mzuri utawanguliza wananchi wako na masilahi ya Taifa kwanza na wewe kupata haki hiyo wa mwisho na usio kuwa bwana mkubwa fulani na kuwanyanyasa wananchi wa kawaida.

NB: VIONGOZI BORA, WATUMISHI NA WANYAKAZI BORA NA WAADILIFU WAKO NA WANA UWEZO MKUBWA SANA WA KULITUMIKIA TAIFA HILI ILA MAZINGIRA YALIYOKO NI HATARISHI ZAIDI KWA MAISHA YAO YA MBELE HAWAJAPATA NAFASI YA KUONYESHA UWEZO WAO.
 
sasa ulivyoandika hivyo "Senior" wako kama yupo JF na akaisoma hii si atajua we ni nani?......au?

Ni marehemu muda mrefu sana uliopita hata hakushudia kilichotokea baadaye Mungu ailaze roho yake pema mzee yule mzalendo wa kweli ambaye hakuwahi kuwa kibaraka wa kiongozi yeyote.
 
Heshima kwako Mkuu Derimto,

Mkuu nimesoma mabandiko yako yote nimeridhika unachoandika unakijua vyema na pengine hatuna budi kuisifu JF kwani faida tunayoipata ni kubwa mno.

Kuna kijana mmoja akifanya kazi agency ya serekali si idara ya usalama baba yake alikuwa akiongoza kurugenzi moja TISS[jina naliifadhi] alifariki kabla JK hajawa rais zikliuwepo fununu angekuwa Boss wa TISS.JK na makamu wa rais walishiriki shughuli za mazishi ya huyo kigogo wa TISS. Kilichonishangaza kijana wake aliacha kazi kwa kisingizio cha kujishughulisha na biashara, nilikuja kubaini hakusema kweli kipindi cha marais wa EAC wanasaini itifaki ya soko la pamoja nikakumbana naye kwenye misafara ya wakubwa kapiga sunglass nikajua jamaa kajiunga na TISS kupitia mgongo wa baba yake.
 

Nimekupata mkuu, na nimesoma baadhi ya vitu nimepiga tiki we uko sehemu fulani! kama ulivosema si kazi ya kujivunia kwa mtu mwenye akili timamu ....kutokana na mazingira ya kikazi Tanzania yetu yalivyo.
 
:yield::yield::yield:....Demrito you deserve..:yield::yield::yield::yield:
 
Pia, kuna rafiki yangu mmoja anataka kufanya kazi Usalama wa Taifa, kuna jinsi ya ku apply? (wapi, lini, kivipi, etc etc)......au ndio "you don't find us, we'll find you?"
kwa bongo mkuu hakuna jinsi ya ku-apply! wakikutaka watakutafita wao wenyeweeeeeeeeeee.....ila hiyo kazi mmmh, you have to do what they want and not what you want! Ukikiuka, you are finished! I bet you better be in a top position (big fish) but if you are going to be a small fish mmmh, too bad! They will use you!
 
wadau.....asanteni kwa michango......nyongeza mbili:

1. kama kuapply ni wao ndio wanakutafuta, ni obvious ni ndugu na jamaa ndio watakuwa wanafanya hivyo.....kwa sababu leo hii mi nikiwa natafuta mtu anayejua kupiga gitaa, nitawauliza watu ninaowafahamu na najua shangazi yangu ataniambia kuwa binamu yangu anapiga gitaa.....ndio maana mwisho wa siku inaonekana kama wanaarijiana kindugu....kumbe inawezekana ikawa hawana jinsi yakuwaona wengine wenye vipaji kama huyu rafiki yangu anayetaka kazi huko....mi nadhani ingekuwa vizuri wangeweka jinsi ya kuadvertise nafasi za kazi.....hata wasipospecify ni kazi gani, ila wangeweka kama sehemu kwamba....kama mtu anataka kufanya kazi TISS basi aende sehemu fulani akaapply....ila kupata kazi au kukosa ni siri ya TISS na muombaji.

2. Hivi kazi ya TISS ni kulinda viongozi na kuua watu tu?......hakuna kazi ya kumanage systems fulani?.....hakuna kazi ya kufanya mahesabu fulani?.....hakuna kazi ya kutengeneza vitu fulani?......yaani TISS ni kulinda na kuua tu?.......mi nadhani usalama wa taifa ni zaidi ya hayo mambo mawili tu......hebu wadau nisaidieni?
 

Kazi ya Usala wa Taifa haiombwi km nyingine. Kinachofanyika ni watu wenyewe wa usalama kufanya recruitment kutoka vyanzo mbalimbali, hususan katika vyuo vya elimu ya juu.

Taarifa na wasifu wa mtarajiwa hufanyiwa utafiti wa kina kabla ya mmoja wao kuwa na direct contact na mtarajiwa. wanaobahatika kupita mchujo wa awali huandaliwa mafunzo. Kinachozingatiwa mwanzo ni intelligence ya mtu, uadilifu na msimamo wake katika mambo ya msingi husuan ya jamii, mapenzi yake kwa taifa lake.

Na kwa vile kazi hiyo ina matawi lukuki basi hata recruitment inafanyika kutegemea mahitaji husika...Lakini good command katika fani yoyote ni kigezo muhimu kwani Hata kazi ya usalama wa taifa essentially inahusu ukusanyaji wa taarifa ( intelligence gathering), uchambuzi wa taarifa zilizokusanywa ( analysis), na enterpreters of the intelligence gathered). Ndio maana kuna watu wanaoitwa majina km informers, data collectors, analysers, undercovers na hata majasusi (spies), ambao hutumwa kazi nje ya mipaka ya nchi.
 
hahahaha......akiingia huko lazima nimpotezee....mambo ya kuhamishiana majukumu watoto wa kiume siyafagilii kabisa yani....ila nadhani dogo yupo kizalendo zaidi

uzalendo au dormant mind?
 
Kazi ya Usalama wa Taifa pia imegawika katika mafungu haya:
1. Kulinda Viongozi Wakuu- Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, na Viongozi wa staafu wa ngazi hizo, (pamoja na kulinda viongozi wakuu wa UWT km mkurugenzi wake mkuu).
2. Kukusanya taarifa za usalama kwa lengo la kujua mood ya wananchi kuhusiana na kila tukio linalotokea ama lisilotokea nchini ili kuiwezesha serikali kufanya maamuzi sahihi, na mara zote kulinda maslahi ya taifa.
3. Kutafuta intelligensia kutoka nje ya mipaka zenye kuiwezesha nchi kujua siri za ndani za nchi nyingine, rafiki ama shindani, ama hasimu, ili ziweze kuisaidia kufikia maamuzi sahihi (informed decisions) kuhusiana na mambo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
 

Mimi sioni sababu ya kumkatisha tamaa ya kuapply Usalma wa Taifa kama ni kazi ilio katika damu yake. Binadamu hutakiwi kuyakimbia matatizo bali kuyakabili. Pengine akiingia Usalama wa Taifa atakuwa ni mmoja wa wazalendo tunaowahitaji. Anayejua namna ya kupata kazi huko amsaidie.
 
KAKA NIMEKUBALI MAMBO YAKO,YANA UKWELI MWINGI NA yanasaidia kuelewa baadhi ya mambo AMBAYO KUFAHAMIKA KWAKE SIO HATARI KWA USALAMA WA NCHI. KAMA KUNA MTU ANADHANI KWA TAARIFA HIZO AMWPATA TAARIFA NYETI ZA UC, AMEKOSEA SAANA. 90% YA HABARI INAYOPATIKANA BURE VALIDITY YAKE NI 10% NA 10% YA HABARI INAYOPATIKANA KWA JASHO VALIDTY YAKE NI MORE THAN 90%. SIMAANISHI KUWA ULICHOSEMA SIO VALID BALI KUJUA UNDANI WA UC KUPITIA TAARIFA YAKO NI 10%.
 
Tanzania ina majasusi ambao kazi yao ni kuchumia tumbo wala sio kujali maslahi ya watz. Kazi yao kubwa ni pamoja na kuiba kura,kuiba rasilimali za taifa na kusema ni siri kubwa, kulinda wanasiasa wa ccm, kuiba mali ya umma
:A S angry:
 
Majukumu ya Idara ya Usalama wa Taifa yako wazi nenda kwenye google andika Tanzania intelligence and security service Act imetoa majibu ya maswali yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…