Kuhujumiwa kwa Rais Samia Suluhu

Kuhujumiwa kwa Rais Samia Suluhu

Ashasembeko

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2017
Posts
225
Reaction score
910
Ni kawaida nchini kwa kila kiongozi mpya anapoingia madarakani, kuwepo kwa genge la wanufaika wa uongozi uliopita kulinda na kusukuma maslai yao. Mwinyi – kama alivyoandika kwenye kitabu chake – alisumbuliwa sana na ‘watu’ wa Nyerere, ikiwemo Nyerere mwenyewe. Mkapa hakusumbuliwa sana na hili.

Kikwete alisumbuliwa kidogo na watu wa Mkapa. Magufuli alisumbuliwa kwa sana na watu wa Kikwete ambao maslai yao kwa upana yaliguswa na walihisi kutengwa.

Kuna dalili za wazi, Rais Samia, ameaza kusumbuliwa na watu wa Hayati Magufuli, na nina hofu mpango huu una maono ya 2025. Kama umekua ukifuatilia kwa ukaribu kwenye mitandao, kila changamoto inayotokea nchini, kuna kakikundi - ambacho ukifungua profile zao - utagundua wengi hawana followers zaidi ya 10, wanacomment, mambo yanayolenga kumlaumu Samia, na “kumkumbuka” JPM kwani mambo haya “hayakuwepo” wakati wa uongozi wake. Hizi accounts kitaalamu zinaitwa bots.

Naomba tukumbushane
Matatizo Tanesco; Ni kweli kuwa matatizo ya umeme yalipungua wakati wa JPM, ila hitilafu zilikua zinajitokeza mara moja moja, ila hawa watu wana comment kana kwamba huko nyuma mambo yalikwisha kabisa. Huu ni upotoshaji wa maksudi. Mifano ya hizi hitilafu huko nyuma soma hapa, hapa na hapa.

Ujambazi; Kama ilivyo maswala ya umeme, ujambazi ulipungua kwa sana ila ulikuwepo. Soma hapa, hapa, hapa, hapa na hapa. Ipo mifano mingi, tafuteni kwenye mitandao. Ninajaribu tu kuwakumbusha maana watanzania ni hulka yetu kusahau. Kwa kuongezea wakati wa JPM ujambazi wa kihalifu ulipungua, lakini ujambazi wa kisiasa ulishamiri. Wanasiasa kupigwa risasi, wafanyabishara kutekwa, wengine kukatwa masikio, ila sisi watanzania kama kawaida ni wasahaulifu.

Sasa, anapokuja mtu kusema wakati wa JPM haya mambo hayakuwepo anakuwa na maana gani? Maana ni upotoshaji wa wazi. Ushauri wangu kwa Rais Samia, awe makini na usalama wake wa taifa na baadhi ya watu wake ndani ya uongozi.

Kuna watu wa JPM walioupata utajiri mkubwa katika uongozi wa JPM na wanajiaribu sana kutumia utajiri huo kuregain influence yao katika serikali. Kiufupi wanakujaribu na kujaribu kukukwamisha uonekana mbaya kwa watanzania.

Kama alivyofanya JPM wakati wa Kikwete, na wewe isuke team ya watu unaowaamini, hususani kwenye Usalama wa Taifa ambapo Magufuli alijaza wasukuma wake. Huyo Mkurugenzi wa Usalama unamwamini? Anafanya kazi kwa niaba yako au niaba ya genge la JPM? Najua upo karibu sana na Mabeyo, kaa nae mshauriane mnaisuka vipi usalama, hiki ndio chombo kitakachodetermine mafanikio ya uRais wako.

All the best!!
 
Kwa kuongezea wakati wa JPM ujambazi wa kihalifu ulipungua, lakini ujambazi wa kisiasa ulishamiri. Wanasiasa kupigwa risasi, wafanyabishara kutekwa, wengine kukatwa masikio, ila sisi watanzania kama kawaida ni wasahaulifu.
asante sana, looks you are very smart. Bravo
 
Sasa kama anahujumiwa Raisi kazi yake ni nini sasa, yupo pale kufanya nini, kuwa head of state is a toughest job ever. Apambane kiume, akizingua 2025 tunatembea na Chadema.
 
Labda afe au awe dhaifu sana kinyume na hapo hakuna wa kimshinda SSH. Wataruka ruka ila viti alivyokalia vina nguvu sana kikatiba.
 
Wewe umamtetea Mama wakati yeye mwenyewe keshakiri kuwa sasa hivi anaona viujambazi jambazi na viuporaji poraji vimeanza kurudi maana yake anakiri kuwa vilikuwa havipo kwa kipindi cha nyuma. Ma kamuagiza Siro kuhakikisha vinadhibitiwa. Kwa hiyo ni ukweli vilikwisha huko nyuma.
 
Waafrika mna akili za kijinga sana. Ahujumiwe na nani? Na nani amekwambia kuondoa watu na kuleta wapya ndio kunaondoa hujuma kama zipo? Mama anatakiwa kuwa mkali that's it.

Kuongoza mtu mweusi ni kazi sana. Ukicheka na nyani utavuna mabua. Eti wanufaika, wapi hao na walinufaika na nini kipindi cha JPM? Li nchi la kubadili huyu leta yule, badili huyu leta yule, miaka inaenda tu, tunazidi kuzaliana bila tija, matatizo kibao siasa imeshindwa kutatua.
 
Dogo acha ukabila, jikite kwenye mada, utakuwa Wenda wazimu kutaja kabila la ili kujustafy your narrative.

Nyuzi za kijinga kama hizi, zisakamazo makibila ya watu, huwa hazijengi. Kwa hiyo wasukuma hawafai au siyo watanzania? Idiot.
 
Na tukisema mnalihujumu hilo kundi mnaloliita la sukuma gang/wafuasi mnaowaita wa jpm ili watolewe watu fulani ambao bado wanawabania ili muachiwe msibuguziwe mpige hela vizuri je?

Mama samia ukweli ni kua jini likujualo halikuli likakumaliza. Hao wanaoitwa sukuma gang na wanaoitwa wafuasi sijui wa jpm bdo watakusaidia ktk kusonga na kupata uungwaji mkono wa wananchi ktk uongozi wako.

Hao mafisadi yanayojaribu kucheza kila rafu ili wajisogeze kwako na kina lugumi kua nao Makini sanaaaa,utageuka Mr.msoga baada ya miaka mi3 base na kuanza kupapasa papasapapasa ulichowafanyia waTZ pindi ukiulizwa umefanya mn ktk uongozi wako
 
Wewe ni mshauri UCHWARA @ujinga. Company.
Kila mjanja nchi hii amekwishaona jinsi mnavyorudi kuiba kwa kasi tokea huko mafichoni mlipokuwa.​

JamiiForums1682347556.jpg
 
Mama naona anaiga style ya JK, yeye kimya yani anawaachia tu. Tofuati yake na JK ni kwamba JK ni Master Spy na Mtaalamu wa siasa, anapiga hesabu za mbali na anapima kisha anaamua cha kufanya. Aliju kuwa Edo alikuwa anamhujumu, na alifikia kutaka kupinduliwa uenyekiti 2012 lakini alitulia. Hata ile 2015 mipango ya Edo aliijua na hata wajumbe kuimba mbele yake wanaimani na Edo alitabasamu akawatuliza akawaambia haya mkale turudi. Huyu jamaa ni Master.

Huyo Rostam anayeonekana anasumbua alishakimbia hapa alikuwa zake Dubai, karudi kipindi cha Marehemu. Alimpa onyo kwa upole kiwango cha hayo unayofanya ukiendelea unachostahili ni hiki, jama akapote kabisa.

Sasa huyu Mama yetu hata kifua cha kuhimili mambo sijui kama anacho, ana kazi sana katika uongozi wake.
Maccm majinga tu
 
Ni kawaida nchini kwa kila kiongozi mpya anapoingia madarakani, kuwepo kwa genge la wanufaika wa uongozi uliopita kulinda na kusukuma maslai yao. Mwinyi – kama alivyoandika kwenye kitabu chake...
Ambao hawaridhiki na uongozi wa mama wakafufue ile ng'ombe ije iendeleze utawala wake wa kidikteta, sisi hatukuiambia idharau corona, ilidhihaki covid afu covid ikapita nae
 
Ni kawaida nchini kwa kila kiongozi mpya anapoingia madarakani, kuwepo kwa genge la wanufaika wa uongozi uliopita kulinda na kusukuma maslai yao. Mwinyi – kama alivyoandika kwenye kitabu chake...
Hakika wewe ni MZALENDO WA DHATI.
 
Ujinga tu. Kwa hiyo mimi nikiona anazingua Madame nisiseme kisa nina Followers less than 10.
Ni haki yako kusema ikiwa SSH anazingua. Lakini kwanini usema "haya hayakuwepo wakati wa Magufuli" wakati yalitokea?
 
Mama Samia ameanza kuisuka team yake. Ndio hawa kina Hamduni na huyo Wambura aliyekuja Dar.

Kila rais wa Tanzania ni mzuri sana anapoondoka madarakani na ni wa hovyo sana anapokuwepo pale ikulu.

Ni kielelezo cha kutokujielewa kwetu kama jamii ya kitanzania, ni ile hulka ya kupenda kulalama muda wote huku tukiwa na urahisi wa kumpata mchawi wa matatizo.

Kila rais ndani kabisa ya moyo wake anataka matatizo yote ikiwezekana yatatuliwe na watu wanaowaongoza wawe na furaha maishani mwao.
 
Back
Top Bottom