Kuhujumiwa kwa Rais Samia Suluhu

Kuhujumiwa kwa Rais Samia Suluhu

Nashangaa unashauri kwa maswali. Kwa maana nyingine huna uhakika na unacho kiwashauri.

Siku nyingine ukitaka kushauri kuwa na uhakika.
 
Rais Samia bado ana nafasi kubwa ya kujipanga,ushauri wangu takeoff yake siipendi,asiruhusu nguvu iliokuwepo kushuka,inachotakiwa aongeze nguvu juu ya nguvu iliokuwepo ili aepukane na lawama kuwa ana fail,hii ni inamuharibia sana,kiasi cha kuonekana kuwa kwake mwanamke ni tatizo,bado ninaamini uwezo anao ila tu awe makini na wanaojaribu kushusha uwezo wake kwa maslahi yao binafsi...
 
Kwaiyo unataka kutuaminisha Nini Yani kwamba hao majambazi Kuna mtu anawatuma kwamba Kuna watu wameambiwa wakahujumu Umeme?
 
Taasisi imara zingeondoa na kuzuia matatizo mengi sana ya nchi hii kwa muda mrefu na endelevu.
 
Ujinga mtupu ,umbea na kujipendekeza. Si ajabu umepata upeo wa kujieleza kwenye awamu ya tano tuliokulia kwenye awamu kadhaa ya nchi hii tunafahamu awamu ya tano ilivyofanya. Awamu hii ya sita inaelekea kufanana fanana Nan awamu ya nne na tunapinga kurudi huko. Anyway kuna some points ila ni chache na hauonyeshi reality badala ya ushabiki Nan kujipendekeza.
 
Usalama wa taifa taasisi inayotakiwa kuwa flexible na kutokuwa katika genge la utawala uliopita. Naomba waingilir kati kusambaratisha jitihada zozote za magengr haya ya kihuni!!
 
Wewe unachuki na wasukuma tu na kundi lako,na wala haitakusaidia.Unadai wasukuma walijazwa na mwendazake hivyo ashauriane na Mabeyo,kwani Mabeyo ni mgogo? Si naye ni msukuma?.Eti asimwamini Mkurugenzi wa TISS kisa aliteuliwa na JPM, vipi hao mawaziri wote aliowakuta na anaendelea nao si waliteuliwa na JPM? Mshauri nao awaondoe wote.
unapofanya propaganda ya kuwachukia na kuwatenga wasukuma unajua madhara yake au kubwabwaja tu? Unajua maana yake anawabagua wasukuma wote mikoa ya Tabora, Shinyanga, Geita, Simiyu,Mwanza, na wasukuma wote waliosambaa Tanzania nzima maana ndo kabila lenye watu wengi na wamesambaa kuliko makabila yote Tanzania.
chuki mnazoeneza kwa wasukuma ni kumchonganisha rais wetu na kanda ya ziwa madhara yake mtayaona huko mbele.
Kuna mawaziri,wakuu wa mikoa,wilaya,wakurugenzi,wakuu wa taasisi nk ni wasukuma mnataka awatoe wote siyo.
unachokifanya ni kumpotosha rais kwa maslahi yenu huku mkijua madhara ya huko mbele ni makubwa zaidi.
 
Mimi nachomuomba mama yetu Rais wetu apunguze mikwara na awe mkali kwa vitendo na atimue watumishi wanao mkwamisha, watendaji wameshaanza kumchukulia poa, mama ana malengo mazuri sana kwa taifa mipango yake ni thabiti
 
Mama naona anaiga style ya JK, yeye kimya yani anawaachia tu. Tofuati yake na JK ni kwamba JK ni Master Spy na Mtaalamu wa siasa, anapiga hesabu za mbali na anapima kisha anaamua cha kufanya. Aliju kuwa Edo alikuwa anamhujumu, na alifikia kutaka kupinduliwa uenyekiti 2012 lakini alitulia. Hata ile 2015 mipango ya Edo aliijua na hata wajumbe kuimba mbele yake wanaimani na Edo alitabasamu akawatuliza akawaambia haya mkale turudi. Huyu jamaa ni Master.

Huyo Rostam anayeonekana anasumbua alishakimbia hapa alikuwa zake Dubai, karudi kipindi cha Marehemu. Alimpa onyo kwa upole kiwango cha hayo unayofanya ukiendelea unachostahili ni hiki, jama akapote kabisa.

Sasa huyu Mama yetu hata kifua cha kuhimili mambo sijui kama anacho, ana kazi sana katika uongozi wake.
Kabisa
 
Na tukisema mnalihujumu hilo kundi mnaloliita la sukuma gang/wafuasi mnaowaita wa jpm ili watolewe watu fulani ambao bado wanawabania ili muachiwe msibuguziwe mpige hela vizuri je?



Mama samia ukweli ni kua jini likujualo halikuli likakumaliza,
Hao wanaoitwa sukuma gang na wanaoitwa wafuasi sijui wa jpm bdo watakusaidia ktk kusonga na kupata uungwaji mkono wa wananchi ktk uongozi wako,Hao mafisadi yanayojaribu kucheza kila rafu ili wajisogeze kwako na kina lugumi kua nao Makini sanaaaa,utageuka Mr.msoga baada ya miaka mi3 base na kuanza kupapasa papasapapasa ulichowafanyia waTZ pindi ukiulizwa umefanya mn ktk uongozi wako
Kabisa
 
Wewe umamtetea Mama wakati yeye mwenyewe keshakiri kuwa sasa hivi anaona viujambazi jambazi na viuporaji poraji vimeanza kurudi maana yake anakiri kuwa vilikuwa havipo kwa kipindi cha nyuma. Ma kamuagiza Siro kuhakikisha vinadhibitiwa. Kwa hiyo ni ukweli vilikwisha huko nyuma.
Wakati wa JPM utoaji wa habari ulidhibitiwa na matukio mengi yalipita bila kuripotiwa.
 
Ujinga mtupu ,umbea na kujipendekeza. Si ajabu umepata upeo wa kujieleza kwenye awamu ya tano tuliokulia kwenye awamu kadhaa ya nchi hii tunafahamu awamu ya tano ilivyofanya. Awamu hii ya sita inaelekea kufanana fanana Nan awamu ya nne na tunapinga kurudi huko. Anyway kuna some points ila ni chache na hauonyeshi reality badala ya ushabiki Nan kujipendekeza.
Mataga mpaka mje mstuke jamaa hatunae tena 2030 hii hapa paap!!!
 
Huo ni mtazamo wako na wewe.

Kwa hiyo tusiingiliane. Uhuru wa maoni
Ndio maana nikasema Rais SSH akizingua una haki (uhuru) wa kusema. Ninachokusihi usiseme lisilo la kweli, au we unaonaje?
 
Back
Top Bottom